< ཡོཧནཿ 12 >

1 ནིསྟཱརོཏྶཝཱཏ྄ པཱུཪྻྭཾ དིནཥཊྐེ སྠིཏེ ཡཱིཤུ ཪྻཾ པྲམཱིཏམ྄ ཨིལིཡཱསརཾ ཤྨཤཱནཱད྄ ཨུདསྠཱཔརཏ྄ ཏསྱ ནིཝཱསསྠཱནཾ བཻཐནིཡཱགྲཱམམ྄ ཨཱགཙྪཏ྄།
Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alikwenda Bethania mahali ambako Lazaro aliyekuwa amefufuliwa na Yesu alikuwa anaishi.
2 ཏཏྲ ཏདརྠཾ རཛནྱཱཾ བྷོཛྱེ ཀྲྀཏེ མརྠཱ པཪྻྱཝེཥཡད྄ ཨིལིཡཱསར྄ ཙ ཏསྱ སངྒིབྷིཿ སཱརྡྡྷཾ བྷོཛནཱསན ཨུཔཱཝིཤཏ྄།
Wakaandaa karamu kwa heshima ya Yesu. Martha akawahudumia wakati Lazaro alikuwa miongoni mwa waliokaa mezani pamoja na Yesu.
3 ཏདཱ མརིཡམ྄ ཨརྡྡྷསེཊཀཾ བཧུམཱུལྱཾ ཛཊཱམཱཾསཱིཡཾ ཏཻལམ྄ ཨཱནཱིཡ ཡཱིཤོཤྩརཎཡོ རྨརྡྡཡིཏྭཱ ནིཛཀེཤ རྨཱརྵྚུམ྄ ཨཱརབྷཏ; ཏདཱ ཏཻལསྱ པརིམལེན གྲྀཧམ྄ ཨཱམོདིཏམ྄ ཨབྷཝཏ྄།
Kisha Maria akachukua chupa ya painti moja yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa, akayamimina miguuni mwa Yesu na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba nzima ikajaa harufu nzuri ya manukato.
4 ཡཿ ཤིམོནཿ པུཏྲ རིཥྐརིཡོཏཱིཡོ ཡིཧཱུདཱནཱམཱ ཡཱིཤུཾ པརཀརེཥུ སམརྤཡིཥྱཏི ས ཤིཥྱསྟདཱ ཀཐིཏཝཱན྄,
Ndipo Yuda Iskariote mwana wa Simoni, mmoja wa wale wanafunzi ambaye ndiye angemsaliti Yesu, akasema,
5 ཨེཏཏྟཻལཾ ཏྲིབྷིཿ ཤཏཻ རྨུདྲཱཔདཻ ཪྻིཀྲཱིཏཾ སད྄ དརིདྲེབྷྱཿ ཀུཏོ ནཱདཱིཡཏ?
“Kwa nini manukato haya hayakuuzwa kwa dinari 300 na fedha hizo wakapewa maskini?”
6 ས དརིདྲལོཀཱརྠམ྄ ཨཙིནྟཡད྄ ཨིཏི ན, ཀིནྟུ ས ཙཽར ཨེཝཾ ཏནྣིཀཊེ མུདྲཱསམྤུཊཀསྠིཏྱཱ ཏནྨདྷྱེ ཡདཏིཥྛཏ྄ ཏདཔཱཧརཏ྄ ཏསྨཱཏ྄ ཀཱརཎཱད྄ ཨིམཱཾ ཀཐཱམཀཐཡཏ྄།
Yuda alisema hivi si kwa kuwa aliwajali maskini, bali kwa kuwa alikuwa mwizi, kwani ndiye alikuwa akitunza mfuko wa fedha akawa anaiba kile kilichowekwa humo.
7 ཏདཱ ཡཱིཤུརཀཐཡད྄ ཨེནཱཾ མཱ ཝཱརཡ སཱ མམ ཤྨཤཱནསྠཱཔནདིནཱརྠཾ ཏདརཀྵཡཏ྄།
Yesu akasema, “Mwacheni. Aliyanunua manukato hayo ili ayaweke kwa ajili ya siku ya maziko yangu.
8 དརིདྲཱ ཡུཥྨཱཀཾ སནྣིདྷཽ སཪྻྭདཱ ཏིཥྛནྟི ཀིནྟྭཧཾ སཪྻྭདཱ ཡུཥྨཱཀཾ སནྣིདྷཽ ན ཏིཥྛཱམི།
Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.”
9 ཏཏཿ པརཾ ཡཱིཤུསྟཏྲཱསྟཱིཏི ཝཱརྟྟཱཾ ཤྲུཏྭཱ བཧཝོ ཡིཧཱུདཱིཡཱསྟཾ ཤྨཤཱནཱདུཏྠཱཔིཏམ྄ ཨིལིཡཱསརཉྩ དྲཥྚུཾ ཏཏ྄ སྠཱནམ྄ ཨཱགཙྪན།
Umati mkubwa wa Wayahudi walipojua kwamba Yesu alikuwa huko Bethania, walikuja si tu kwa ajili ya Yesu, lakini pia kumwona Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua.
10 ཏདཱ པྲདྷཱནཡཱཛཀཱསྟམ྄ ཨིལིཡཱསརམཔི སཾཧརྟྟུམ྄ ཨམནྟྲཡན྄;
Kwa hiyo viongozi wa makuhani wakafanya mpango wa kumuua Lazaro pia,
11 ཡཏསྟེན བཧཝོ ཡིཧཱུདཱིཡཱ གཏྭཱ ཡཱིཤཽ ཝྱཤྭསན྄།
kwa kuwa kutokana na habari za kufufuliwa kwake Wayahudi wengi walikuwa wanamwendea Yesu na kumwamini.
12 ཨནནྟརཾ ཡཱིཤུ ཪྻིརཱུཤཱལམ྄ ནགརམ྄ ཨཱགཙྪཏཱིཏི ཝཱརྟྟཱཾ ཤྲུཏྭཱ པརེ྅ཧནི ཨུཏྶཝཱགཏཱ བཧཝོ ལོཀཱཿ
Siku iliyofuata umati mkubwa uliokuwa umekuja kwenye Sikukuu walisikia kwamba Yesu angekuja Yerusalemu.
13 ཁརྫྫཱུརཔཏྲཱདྱཱནཱིཡ ཏཾ སཱཀྵཱཏ྄ ཀརྟྟུཾ བཧིརཱགཏྱ ཛཡ ཛཡེཏི ཝཱཙཾ པྲོཙྩཻ ཪྻཀྟུམ྄ ཨཱརབྷནྟ, ཨིསྲཱཡེལོ ཡོ རཱཛཱ པརམེཤྭརསྱ ནཱམྣཱགཙྪཏི ས དྷནྱཿ།
Basi wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki, huku wakipaza sauti wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amebarikiwa Mfalme wa Israeli!”
14 ཏདཱ "ཧེ སིཡོནཿ ཀནྱེ མཱ བྷཻཥཱིཿ པཤྱཱཡཾ ཏཝ རཱཛཱ གརྡྡབྷཤཱཝཀམ྄ ཨཱརུཧྱཱགཙྪཏི"
Yesu akamkuta mwana-punda akampanda, kama ilivyoandikwa,
15 ཨིཏི ཤཱསྟྲཱིཡཝཙནཱནུསཱརེཎ ཡཱིཤུརེཀཾ ཡུཝགརྡྡབྷཾ པྲཱཔྱ ཏདུཔཪྻྱཱརོཧཏ྄།
“Usiogope, Ewe binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda!”
16 ཨསྱཱཿ གྷཊནཱཡཱསྟཱཏྤཪྻྱཾ ཤིཥྱཱཿ པྲཐམཾ ནཱབུདྷྱནྟ, ཀིནྟུ ཡཱིཤཽ མཧིམཱནཾ པྲཱཔྟེ སཏི ཝཱཀྱམིདཾ ཏསྨིན ཨཀཐྱཏ ལོཀཱཤྩ ཏམྤྲཏཱིཏྠམ྄ ཨཀུཪྻྭན྄ ཨིཏི ཏེ སྨྲྀཏཝནྟཿ།
Wanafunzi wake Yesu mwanzoni hawakuelewa mambo haya, lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka kuwa mambo haya yalikuwa yameandikwa kwa ajili yake na alitendewa yeye.
17 ས ཨིལིཡཱསརཾ ཤྨཤཱནཱད྄ ཨཱགནྟུམ྄ ཨཱཧྭཏཝཱན྄ ཤྨཤཱནཱཉྩ ཨུདསྠཱཔཡད྄ ཡེ ཡེ ལོཀཱསྟཏྐརྨྱ སཱཀྵཱད྄ ཨཔཤྱན྄ ཏེ པྲམཱཎཾ དཱཏུམ྄ ཨཱརབྷནྟ།
Wale waliokuwepo wakati Yesu alipomwita Lazaro kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu, waliendelea kushuhudia.
18 ས ཨེཏཱདྲྀཤམ྄ ཨདྦྷུཏཾ ཀརྨྨཀརོཏ྄ ཏསྱ ཛནཤྲུཏེ རློཀཱསྟཾ སཱཀྵཱཏ྄ ཀརྟྟུམ྄ ཨཱགཙྪན྄།
Ni kwa sababu pia walikuwa wamesikia kwamba alikuwa ametenda muujiza huu ndiyo maana umati wa watu ukaenda kumlaki.
19 ཏཏཿ ཕིརཱུཤིནཿ པརསྤརཾ ཝཀྟུམ྄ ཨཱརབྷནྟ ཡུཥྨཱཀཾ སཪྻྭཱཤྩེཥྚཱ ཝྲྀཐཱ ཛཱཏཱཿ, ཨིཏི ཀིཾ ཡཱུཡཾ ན བུདྷྱདྷྭེ? པཤྱཏ སཪྻྭེ ལོཀཱསྟསྱ པཤྩཱདྭརྟྟིནོབྷཝན྄།
Hivyo Mafarisayo walipoona hayo wakaambiana, “Mnaona, hamwezi kufanya lolote. Angalieni, ulimwengu wote unamfuata yeye!”
20 བྷཛནཾ ཀརྟྟུམ྄ ཨུཏྶཝཱགཏཱནཱཾ ལོཀཱནཱཾ ཀཏིཔཡཱ ཛནཱ ཨནྱདེཤཱིཡཱ ཨཱསན྄,
Basi palikuwa Wayunani fulani miongoni mwa wale waliokuwa wamekwenda kuabudu wakati wa Sikukuu.
21 ཏེ གཱལཱིལཱིཡབཻཏྶཻདཱནིཝཱསིནཿ ཕིལིཔསྱ སམཱིཔམ྄ ཨཱགཏྱ ཝྱཱཧརན྄ ཧེ མཧེཙྪ ཝཡཾ ཡཱིཤུཾ དྲཥྚུམ྄ ཨིཙྪཱམཿ།
Hawa wakamjia Filipo, ambaye alikuwa mwenyeji wa Bethsaida huko Galilaya, wakiwa na ombi. Wakamwambia, “Tungependa kumwona Yesu.”
22 ཏཏཿ ཕིལིཔོ གཏྭཱ ཨཱནྡྲིཡམ྄ ཨཝདཏ྄ པཤྩཱད྄ ཨཱནྡྲིཡཕིལིཔཽ ཡཱིཤཝེ ཝཱརྟྟཱམ྄ ཨཀཐཡཏཱཾ།
Filipo akaenda akamweleza Andrea, nao wote wawili wakamwambia Yesu.
23 ཏདཱ ཡཱིཤུཿ པྲཏྱུདིཏཝཱན྄ མཱནཝསུཏསྱ མཧིམཔྲཱཔྟིསམཡ ཨུཔསྠིཏཿ།
Yesu akawajibu, “Saa imewadia ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.
24 ཨཧཾ ཡུཥྨཱནཏིཡཐཱརྠཾ ཝདཱམི, དྷཱནྱབཱིཛཾ མྲྀཏྟིཀཱཡཱཾ པཏིཏྭཱ ཡདི ན མྲྀཡཏེ ཏརྷྱེཀཱཀཱི ཏིཥྛཏི ཀིནྟུ ཡདི མྲྀཡཏེ ཏརྷི བཧུགུཎཾ ཕལཾ ཕལཏི།
Amin, amin nawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka ardhini na kufa, hubakia kama mbegu peke yake. Lakini ikifa huzaa mbegu nyingi.
25 ཡོ ཛནེ ནིཛཔྲཱཎཱན྄ པྲིཡཱན྄ ཛཱནཱཏི ས ཏཱན྄ ཧཱརཡིཥྱཏི ཀིནྟུ ཡེ ཛན ཨིཧལོཀེ ནིཛཔྲཱཎཱན྄ ཨཔྲིཡཱན྄ ཛཱནཱཏི སེནནྟཱཡུཿ པྲཱཔྟུཾ ཏཱན྄ རཀྵིཥྱཏི། (aiōnios g166)
Mtu yeyote anayependa maisha yake atayapoteza, naye ayachukiaye maisha yake katika ulimwengu huu atayaokoa hata kwa uzima wa milele. (aiōnios g166)
26 ཀཤྩིད྄ ཡདི མམ སེཝཀོ བྷཝིཏུཾ ཝཱཉྪཏི ཏརྷི ས མམ པཤྩཱདྒཱམཱི བྷཝཏུ, ཏསྨཱད྄ ཨཧཾ ཡཏྲ ཏིཥྛཱམི མམ སེཝཀེཔི ཏཏྲ སྠཱསྱཏི; ཡོ ཛནོ མཱཾ སེཝཏེ མམ པིཏཱཔི ཏཾ སམྨཾསྱཏེ།
Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate, nami mahali nilipo ndipo mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu akinitumikia, Baba yangu atamheshimu.
27 སཱམྤྲཏཾ མམ པྲཱཎཱ ཝྱཱཀུལཱ བྷཝནྟི, ཏསྨཱད྄ ཧེ པིཏར ཨེཏསྨཱཏ྄ སམཡཱན྄ མཱཾ རཀྵ, ཨིཏྱཧཾ ཀིཾ པྲཱརྠཡིཥྱེ? ཀིནྟྭཧམ྄ ཨེཏཏྶམཡཱརྠམ྄ ཨཝཏཱིརྞཝཱན྄།
“Sasa roho yangu imefadhaika sana. Niseme nini? ‘Baba, niokoe katika saa hii.’ Lakini ni kwa kusudi hili nimeufikia wakati huu.
28 ཧེ པིཏ: སྭནཱམྣོ མཧིམཱནཾ པྲཀཱཤཡ; ཏནཻཝ སྭནཱམྣོ མཧིམཱནམ྄ ཨཧཾ པྲཱཀཱཤཡཾ པུནརཔི པྲཀཱཤཡིཥྱཱམི, ཨེཥཱ གགཎཱིཡཱ ཝཱཎཱི ཏསྨིན྄ སམཡེ྅ཛཱཡཏ།
Baba, litukuze jina lako.” Ndipo ikaja sauti kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.”
29 ཏཙྴྲུཏྭཱ སམཱིཔསྠལོཀཱནཱཾ ཀེཙིད྄ ཨཝདན྄ མེགྷོ྅གརྫཱིཏ྄, ཀེཙིད྄ ཨཝདན྄ སྭརྒཱིཡདཱུཏོ྅ནེན སཧ ཀཐཱམཙཀཐཏ྄།
Ule umati wa watu uliokuwa mahali pale uliisikia nao ukasema, “Hiyo ni sauti ya radi,” wengine wakasema, “Malaika ameongea naye.”
30 ཏདཱ ཡཱིཤུཿ པྲཏྱཝཱདཱིཏ྄, མདརྠཾ ཤབྡོཡཾ ནཱབྷཱུཏ྄ ཡུཥྨདརྠམེཝཱབྷཱུཏ྄།
Yesu akawaambia, “Sauti hii imesikika kwa faida yenu, wala si kwa faida yangu.
31 ཨདྷུནཱ ཛགཏོསྱ ཝིཙཱར: སམྤཏྶྱཏེ, ཨདྷུནཱསྱ ཛགཏ: པཏཱི རཱཛྱཱཏ྄ ཙྱོཥྱཏི།
Sasa ni saa ya hukumu kwa ajili ya ulimwengu huu, sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.
32 ཡདྱཨཱི པྲྀཐིཝྱཱ ཨཱུརྡྭྭེ པྲོཏྠཱཔིཏོསྨི ཏརྷི སཪྻྭཱན྄ མཱནཝཱན྄ སྭསམཱིཔམ྄ ཨཱཀརྵིཥྱཱམི།
Lakini mimi, nikiinuliwa kutoka nchi, nitawavuta watu wote waje kwangu.”
33 ཀཐཾ ཏསྱ མྲྀཏི རྦྷཝིཥྱཏི, ཨེཏད྄ བོདྷཡིཏུཾ ས ཨིམཱཾ ཀཐཱམ྄ ཨཀཐཡཏ྄།
Yesu aliyasema haya akionyesha ni kifo gani atakachokufa.
34 ཏདཱ ལོཀཱ ཨཀཐཡན྄ སོབྷིཥིཀྟཿ སཪྻྭདཱ ཏིཥྛཏཱིཏི ཝྱཝསྠཱགྲནྠེ ཤྲུཏམ྄ ཨསྨཱབྷིཿ, ཏརྷི མནུཥྱཔུཏྲཿ པྲོཏྠཱཔིཏོ བྷཝིཥྱཏཱིཏི ཝཱཀྱཾ ཀཐཾ ཝདསི? མནུཥྱཔུཏྲོཡཾ ཀཿ? (aiōn g165)
Ule umati wa watu ukapiga kelele ukasema, “Tumesikia kutoka Sheria kwamba ‘Kristo adumu milele,’ wewe wawezaje kusema, ‘Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu’? Huyu ‘Mwana wa Adamu’ ni nani?” (aiōn g165)
35 ཏདཱ ཡཱིཤུརཀཐཱཡད྄ ཡུཥྨཱབྷིཿ སཱརྡྡྷམ྄ ཨལྤདིནཱནི ཛྱོཏིརཱསྟེ, ཡཐཱ ཡུཥྨཱན྄ ཨནྡྷཀཱརོ ནཱཙྪཱདཡཏི ཏདརྠཾ ཡཱཝཏྐཱལཾ ཡུཥྨཱབྷིཿ སཱརྡྡྷཾ ཛྱོཏིསྟིཥྛཏི ཏཱཝཏྐཱལཾ གཙྪཏ; ཡོ ཛནོ྅ནྡྷཀཱརེ གཙྪཏི ས ཀུཏྲ ཡཱཏཱིཏི ན ཛཱནཱཏི།
Ndipo Yesu akawaambia, “Bado kitambo kidogo nuru ingalipo pamoja nanyi. Enendeni maadamu mna nuru, msije mkakumbwa na giza. Mtu anayetembea gizani hajui anakokwenda.
36 ཨཏཨེཝ ཡཱཝཏྐཱལཾ ཡུཥྨཱཀཾ ནིཀཊེ ཛྱོཏིརཱསྟེ ཏཱཝཏྐཱལཾ ཛྱོཏཱིརཱུཔསནྟཱནཱ བྷཝིཏུཾ ཛྱོཏིཥི ཝིཤྭསིཏ; ཨིམཱཾ ཀཐཱཾ ཀཐཡིཏྭཱ ཡཱིཤུཿ པྲསྠཱཡ ཏེབྷྱཿ སྭཾ གུཔྟཝཱན྄།
Wekeni tumaini lenu katika nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Baada ya kusema haya, Yesu aliondoka, akajificha wasimwone.
37 ཡདྱཔི ཡཱིཤུསྟེཥཱཾ སམཀྵམ྄ ཨེཏཱཝདཱཤྩཪྻྱཀརྨྨཱཎི ཀྲྀཏཝཱན྄ ཏཐཱཔི ཏེ ཏསྨིན྄ ན ཝྱཤྭསན྄།
Hata baada ya Yesu kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini.
38 ཨཏཨེཝ ཀཿ པྲཏྱེཏི སུསཾཝཱདཾ པརེཤཱསྨཏ྄ པྲཙཱརིཏཾ? པྲཀཱཤཏེ པརེཤསྱ ཧསྟཿ ཀསྱ ཙ སནྣིདྷཽ? ཡིཤཡིཡབྷཝིཥྱདྭཱདིནཱ ཡདེཏད྄ ཝཱཀྱམུཀྟཾ ཏཏ྄ སཕལམ྄ ཨབྷཝཏ྄།
Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?”
39 ཏེ པྲཏྱེཏུཾ ནཱཤནྐུཝན྄ ཏསྨིན྄ ཡིཤཡིཡབྷཝིཥྱདྭཱདི པུནརཝཱདཱིད྄,
Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine:
40 ཡདཱ, "ཏེ ནཡནཻ རྣ པཤྱནྟི བུདྡྷིབྷིཤྩ ན བུདྷྱནྟེ ཏཻ རྨནཿསུ པརིཝརྟྟིཏེཥུ ཙ ཏཱནཧཾ ཡཐཱ སྭསྠཱན྄ ན ཀརོམི ཏཐཱ ས ཏེཥཱཾ ལོཙནཱནྱནྡྷཱནི ཀྲྀཏྭཱ ཏེཥཱམནྟཿཀརཎཱནི གཱཌྷཱནི ཀརིཥྱཏི། "
“Amewafanya vipofu, na kuifanya mioyo yao kuwa migumu, ili wasiweze kuona kwa macho yao, wala kuelewa kwa mioyo yao, wasije wakageuka nami nikawaponya.”
41 ཡིཤཡིཡོ ཡདཱ ཡཱིཤོ རྨཧིམཱནཾ ཝིལོཀྱ ཏསྨིན྄ ཀཐཱམཀཐཡཏ྄ ཏདཱ བྷཝིཥྱདྭཱཀྱམ྄ ཨཱིདྲྀཤཾ པྲཀཱཤཡཏ྄།
Isaya alisema haya alipoona utukufu wa Yesu na kunena habari zake.
42 ཏཐཱཔྱདྷིཔཏིནཱཾ བཧཝསྟསྨིན྄ པྲཏྱཱཡན྄། ཀིནྟུ ཕིརཱུཤིནསྟཱན྄ བྷཛནགྲྀཧཱད྄ དཱུརཱིཀུཪྻྭནྟཱིཏི བྷཡཱཏ྄ ཏེ ཏཾ ན སྭཱིཀྲྀཏཝནྟཿ།
Lakini wengi miongoni mwa viongozi wa Wayahudi walimwamini, lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakukiri waziwazi kwa maana waliogopa kufukuzwa katika masinagogi.
43 ཡཏ ཨཱིཤྭརསྱ པྲཤཾསཱཏོ མཱནཝཱནཱཾ པྲཤཾསཱཡཱཾ ཏེ྅པྲིཡནྟ།
Wao walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
44 ཏདཱ ཡཱིཤུརུཙྩཻཿཀཱརམ྄ ཨཀཐཡད྄ ཡོ ཛནོ མཡི ཝིཤྭསིཏི ས ཀེཝལེ མཡི ཝིཤྭསིཏཱིཏི ན, ས མཏྤྲེརཀེ྅པི ཝིཤྭསིཏི།
Yesu akapaza sauti akasema, “Yeyote aniaminiye, haniamini mimi peke yangu, bali yeye aliyenituma.
45 ཡོ ཛནོ མཱཾ པཤྱཏི ས མཏྤྲེརཀམཔི པཤྱཏི།
Yeyote anionaye mimi, amemwona yeye aliyenituma.
46 ཡོ ཛནོ མཱཾ པྲཏྱེཏི ས ཡཐཱནྡྷཀཱརེ ན ཏིཥྛཏི ཏདརྠམ྄ ཨཧཾ ཛྱོཏིཿསྭརཱུཔོ བྷཱུཏྭཱ ཛགཏྱསྨིན྄ ཨཝཏཱིརྞཝཱན྄།
Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni, ili kwamba kila mtu aniaminiye asibaki gizani.
47 མམ ཀཐཱཾ ཤྲུཏྭཱ ཡདི ཀཤྩིན྄ ན ཝིཤྭསིཏི ཏརྷི ཏམཧཾ དོཥིཎཾ ན ཀརོམི, ཡཏོ ཧེཏོ རྫགཏོ ཛནཱནཱཾ དོཥཱན྄ ནིཤྩིཏཱན྄ ཀརྟྟུཾ ནཱགཏྱ ཏཱན྄ པརིཙཱཏུམ྄ ཨཱགཏོསྨི།
“Mimi simhukumu mtu yeyote anayesikia maneno yangu na asiyatii, kwa maana sikuja kuuhukumu ulimwengu, bali kuuokoa.
48 ཡཿ ཀཤྩིན྄ མཱཾ ན ཤྲདྡྷཱཡ མམ ཀཐཾ ན གྲྀཧླཱཏི, ཨནྱསྟཾ དོཥིཎཾ ཀརིཥྱཏི ཝསྟུཏསྟུ ཡཱཾ ཀཐཱམཧམ྄ ཨཙཀཐཾ སཱ ཀཐཱ ཙརམེ྅ནྷི ཏཾ དོཥིཎཾ ཀརིཥྱཏི།
Yuko amhukumuye yeye anikataaye mimi na kutokuyapokea maneno yangu, yaani, yale maneno niliyosema yenyewe yatamhukumu siku ya mwisho.
49 ཡཏོ ཧེཏོརཧཾ སྭཏཿ ཀིམཔི ན ཀཐཡཱམི, ཀིཾ ཀིཾ མཡཱ ཀཐཡིཏཝྱཾ ཀིཾ སམུཔདེཥྚཝྱཉྩ ཨིཏི མཏྤྲེརཡིཏཱ པིཏཱ མཱམཱཛྙཱཔཡཏ྄།
Kwa maana sisemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba aliyenituma aliniamuru ni nini cha kusema na jinsi ya kukisema.
50 ཏསྱ སཱཛྙཱ ཨནནྟཱཡུརིཏྱཧཾ ཛཱནཱམི, ཨཏཨེཝཱཧཾ ཡཏ྄ ཀཐཡཱམི ཏཏ྄ པིཏཱ ཡཐཱཛྙཱཔཡཏ྄ ཏཐཻཝ ཀཐཡཱམྱཧམ྄། (aiōnios g166)
Nami ninajua amri zake huongoza hadi kwenye uzima wa milele. Hivyo lolote nisemalo, ndilo lile Baba aliloniambia niseme.” (aiōnios g166)

< ཡོཧནཿ 12 >