< มถิ: 14 >

1 ตทานีํ ราชา เหโรทฺ ยีโศ รฺยศ: ศฺรุตฺวา นิชทาเสยานฺ ชคาทฺ,
Wakati huo, Mfalme Herode, mtawala wa Galilaya, alisikia habari za Yesu,
2 เอษ มชฺชยิตา โยหนฺ, ปฺรมิเตภยสฺตโสฺยตฺถานาตฺ เตเนตฺถมทฺภุตํ กรฺมฺม ปฺรกาศฺยเตฯ
akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji; amefufuka kutoka kwa wafu! Hii ndiyo sababu nguvu za kutenda miujiza zinafanya kazi ndani yake.”
3 ปุรา เหโรทฺ นิชภฺราตุ: ผิลิโป ชายายา เหโรทียายา อนุโรธาทฺ โยหนํ ธารยิตฺวา พทฺธา การายำ สฺถาปิตวานฺฯ
Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga na kumweka gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake,
4 ยโต โยหนฺ อุกฺตวานฺ, เอตฺสยา: สํคฺรโห ภวโต โนจิต: ฯ
kwa kuwa Yohana alikuwa amemwambia Herode: “Si halali kwako kuwa na huyo mwanamke.”
5 ตสฺมาตฺ นฺฤปติสฺตํ หนฺตุมิจฺฉนฺนปิ โลเกโภฺย วิภยาญฺจการ; ยต: สรฺเวฺว โยหนํ ภวิษฺยทฺวาทินํ เมนิเรฯ
Herode alitaka sana kumuua Yohana, lakini akaogopa watu, kwa maana walimtambua kuwa ni nabii.
6 กินฺตุ เหโรโท ชนฺมาหียมห อุปสฺถิเต เหโรทียายา ทุหิตา เตษำ สมกฺษํ นฺฤติตฺวา เหโรทมปฺรีณฺยตฺฯ
Katika siku ya kuadhimisha sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti wa Herodia alicheza mbele ya watu waliohudhuria, akamfurahisha sana Herode,
7 ตสฺมาตฺ ภูปติ: ศปถํ กุรฺวฺวนฺ อิติ ปฺรตฺยชฺญาสีตฺ, ตฺวยา ยทฺ ยาจฺยเต, ตเทวาหํ ทาสฺยามิฯ
kiasi kwamba aliahidi kwa kiapo kumpa huyo binti chochote angeomba.
8 สา กุมารี สฺวียมาตุ: ศิกฺษำ ลพฺธา พภาเษ, มชฺชยิตุโรฺยหน อุตฺตมางฺคํ ภาชเน สมานีย มหฺยํ วิศฺราณยฯ
Huyo binti, akiwa amechochewa na mama yake, akasema, “Nipe kichwa cha Yohana Mbatizaji kwenye sinia.”
9 ตโต ราชา ศุโศจ, กินฺตุ โภชนาโยปวิศตำ สงฺคินำ สฺวกฺฤตศปถสฺย จานุโรธาตฺ ตตฺ ปฺรทาตุม อาทิเทศฯ
Mfalme akasikitika, lakini kwa sababu ya viapo alivyoapa mbele ya wageni, akaamuru kwamba apatiwe ombi lake.
10 ปศฺจาตฺ การำ ปฺรติ นรํ ปฺรหิตฺย โยหน อุตฺตมางฺคํ ฉิตฺตฺวา
Hivyo akaagiza Yohana Mbatizaji akatwe kichwa mle gerezani.
11 ตตฺ ภาชน อานายฺย ตไสฺย กุมารฺไยฺย วฺยศฺราณยตฺ, ตต: สา สฺวชนนฺยา: สมีปํ ตนฺนินายฯ
Kichwa chake kikaletwa kwenye sinia, akapewa yule binti, naye akampelekea mama yake.
12 ปศฺจาตฺ โยหน: ศิษฺยา อาคตฺย กายํ นีตฺวา ศฺมศาเน สฺถาปยามาสุสฺตโต ยีโศ: สนฺนิธึ วฺรชิตฺวา ตทฺวารฺตฺตำ พภาษิเรฯ
Wanafunzi wa Yohana wakaja na kuuchukua mwili wake kwenda kuuzika. Kisha wakaenda wakamwambia Yesu.
13 อนนฺตรํ ยีศุริติ นิศภฺย นาวา นิรฺชนสฺถานมฺ เอกากี คตวานฺ, ปศฺจาตฺ มานวาสฺตตฺ ศฺรุตฺวา นานานคเรภฺย อาคตฺย ปไทสฺตตฺปศฺจาทฺ อียุ: ฯ
Yesu aliposikia yaliyokuwa yametukia, aliondoka kwa chombo akaenda mahali pasipo na watu ili awe peke yake. Lakini watu walipopata habari, wakamfuata kwa miguu kupitia nchi kavu kutoka miji.
14 ตทานีํ ยีศุ รฺพหิราคตฺย มหานฺตํ ชนนิวหํ นิรีกฺษฺย เตษุ การุณิก: มนฺ เตษำ ปีฑิตชนานฺ นิรามยานฺ จการฯ
Yesu alipofika kando ya bahari, aliona makutano makubwa ya watu, akawahurumia na akawaponya wagonjwa wao.
15 ตต: ปรํ สนฺธฺยายำ ศิษฺยาสฺตทนฺติกมาคตฺย กถยาญฺจกฺรุ: , อิทํ นิรฺชนสฺถานํ เวลาปฺยวสนฺนา; ตสฺมาตฺ มนุชานฺ สฺวสฺวคฺรามํ คนฺตุํ สฺวารฺถํ ภกฺษฺยาณิ เกฺรตุญฺจ ภวานฺ ตานฺ วิสฺฤชตุฯ
Ilipofika jioni, wanafunzi wake walienda kwake, wakamwambia, “Mahali hapa ni nyikani, na muda sasa umekwisha. Waage makutano ili waende zao vijijini wakajinunulie chakula.”
16 กินฺตุ ยีศุสฺตานวาทีตฺ, เตษำ คมเน ปฺรโยชนํ นาสฺติ, ยูยเมว ตานฺ โภชยตฯ
Yesu akawaambia, “Hakuna sababu ya wao kuondoka. Ninyi wapeni chakula.”
17 ตทา เต ปฺรตฺยวทนฺ, อสฺมากมตฺร ปูปปญฺจกํ มีนทฺวยญฺจาเสฺตฯ
Wakamjibu, “Tuna mikate mitano na samaki wawili tu.”
18 ตทานีํ เตโนกฺตํ ตานิ มทนฺติกมานยตฯ
Akawaambia, “Nileteeni hivyo vitu hapa.”
19 อนนฺตรํ ส มนุชานฺ ยวโสปรฺยฺยุปเวษฺฏุมฺ อาชฺญาปยามาส; อปร ตตฺ ปูปปญฺจกํ มีนทฺวยญฺจ คฺฤหฺลนฺ สฺวรฺคํ ปฺรติ นิรีกฺเษฺยศฺวรียคุณานฺ อนูทฺย ภํกฺตฺวา ศิเษฺยโภฺย ทตฺตวานฺ, ศิษฺยาศฺจ โลเกโภฺย ททุ: ฯ
Yesu akaagiza makutano wakae chini kwenye nyasi. Akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akainua macho yake akatazama mbinguni, akavibariki na kuimega ile mikate. Kisha akawapa wanafunzi, nao wanafunzi wakawagawia makutano.
20 ตต: สรฺเวฺว ภุกฺตฺวา ปริตฺฤปฺตวนฺต: , ตตสฺตทวศิษฺฏภกฺไษฺย: ปูรฺณานฺ ทฺวาทศฑลกานฺ คฺฤหีตวนฺต: ฯ
Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
21 เต โภกฺตาร: สฺตฺรีรฺพาลกำศฺจ วิหาย ปฺราเยณ ปญฺจ สหสฺราณิ ปุมำส อาสนฺฯ
Idadi ya watu waliokula walikuwa wanaume wapatao 5,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
22 ตทนนฺตรํ ยีศุ โรฺลกานำ วิสรฺชนกาเล ศิษฺยานฺ ตรณิมาโรฒุํ สฺวาเคฺร ปารํ ยาตุญฺจ คาฒมาทิษฺฏวานฺฯ
Mara Yesu akawaambia wanafunzi wake waingie kwenye mashua watangulie kwenda ngʼambo ya bahari, wakati yeye alikuwa akiwaaga wale makutano.
23 ตโต โลเกษุ วิสฺฤษฺเฏษุ ส วิวิกฺเต ปฺรารฺถยิตุํ คิริเมกํ คตฺวา สนฺธฺยำ ยาวตฺ ตไตฺรกากี สฺถิตวานฺฯ
Baada ya kuwaaga, akaenda zake mlimani peke yake kuomba. Jioni ilipofika, Yesu alikuwa huko peke yake.
24 กินฺตุ ตทานีํ สมฺมุขวาตตฺวาตฺ สริตฺปเต รฺมเธฺย ตรงฺไคสฺตรณิรฺโทลายมานาภวตฺฯ
Wakati huo ile mashua ilikuwa mbali kutoka nchi kavu ikisukwasukwa na mawimbi, kwa sababu upepo ulikuwa wa mbisho.
25 ตทา ส ยามินฺยาศฺจตุรฺถปฺรหเร ปทฺภฺยำ วฺรชนฺ เตษามนฺติกํ คตวานฺฯ
Wakati wa zamu ya nne ya usiku, Yesu akawaendea wanafunzi wake akiwa anatembea juu ya maji.
26 กินฺตุ ศิษฺยาสฺตํ สาคโรปริ วฺรชนฺตํ วิโลกฺย สมุทฺวิคฺนา ชคทุ: , เอษ ภูต อิติ ศงฺกมานา อุจฺไจ: ศพฺทายาญฺจกฺริเร จฯ
Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji, waliingiwa na hofu kuu, wakasema, “Ni mzimu.” Wakapiga yowe kwa kuogopa.
27 ตไทว ยีศุสฺตานวทตฺ, สุสฺถิรา ภวต, มา ไภษฺฏ, เอโษ'หมฺฯ
Lakini mara Yesu akasema nao, akawaambia, “Jipeni moyo! Ni mimi. Msiogope.”
28 ตต: ปิตร อิตฺยุกฺตวานฺ, เห ปฺรโภ, ยทิ ภวาเนว, ตรฺหิ มำ ภวตฺสมีปํ ยาตุมาชฺญาปยตุฯ
Petro akamjibu, “Bwana, ikiwa ni wewe, niambie nije kwako nikitembea juu ya maji.”
29 ตต: เตนาทิษฺฏ: ปิตรสฺตรณิโต'วรุหฺย ยีเศรนฺติกํ ปฺราปฺตุํ โตโยปริ ววฺราชฯ
Yesu akamwambia, “Njoo.” Basi Petro akatoka kwenye chombo, akatembea juu ya maji kumwelekea Yesu.
30 กินฺตุ ปฺรจณฺฑํ ปวนํ วิโลกฺย ภยาตฺ โตเย มํกฺตุมฺ อาเรเภ, ตสฺมาทฺ อุจฺไจ: ศพฺทายมาน: กถิตวานฺ, เห ปฺรโภ, มามวตุฯ
Lakini alipoona upepo mkali aliingiwa na hofu, naye akaanza kuzama, huku akipiga kelele, “Bwana, niokoe!”
31 ยีศุสฺตตฺกฺษณาตฺ กรํ ปฺรสารฺยฺย ตํ ธรนฺ อุกฺตวานฺ, ห โสฺตกปฺรตฺยยินฺ ตฺวํ กุต: สมเศถา: ?
Mara Yesu akaunyoosha mkono wake na kumshika, akamwambia, “Wewe mwenye imani haba, kwa nini uliona shaka?”
32 อนนฺตรํ ตโยสฺตรณิมารูฒโย: ปวโน นิววฺฤเตฯ
Nao walipoingia ndani ya mashua, upepo ukakoma.
33 ตทานีํ เย ตรณฺยามาสนฺ, ต อาคตฺย ตํ ปฺรณภฺย กถิตวนฺต: , ยถารฺถสฺตฺวเมเวศฺวรสุต: ฯ
Ndipo wote waliokuwa ndani ya ile mashua wakamwabudu Yesu, wakisema, “Hakika, wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
34 อนนฺตรํ ปารํ ปฺราปฺย เต คิเนษรนฺนามกํ นครมุปตสฺถุ: ,
Walipokwisha kuvuka, wakafika nchi ya Genesareti.
35 ตทา ตตฺรตฺยา ชนา ยีศุํ ปริจีย ตทฺเทศฺสฺย จตุรฺทิโศ วารฺตฺตำ ปฺรหิตฺย ยตฺร ยาวนฺต: ปีฑิตา อาสนฺ, ตาวเตอว ตทนฺติกมานยามาสุ: ฯ
Watu wa eneo lile walipomtambua Yesu, walipeleka habari sehemu zote za jirani. Watu wakamletea wagonjwa wao wote,
36 อปรํ ตทียวสนสฺย คฺรนฺถิมาตฺรํ สฺปฺรษฺฏุํ วินีย ยาวนฺโต ชนาสฺตตฺ สฺปรฺศํ จกฺริเร, เต สรฺวฺเวอว นิรามยา พภูวุ: ฯ
wakamsihi awaruhusu wagonjwa waguse tu pindo la vazi lake, nao wote waliomgusa, wakaponywa.

< มถิ: 14 >