< ยากูพ: 3 >

1 เห มม ภฺราตร: , ศิกฺษไกรสฺมาภิ รฺคุรุตรทณฺโฑ ลปฺสฺยต อิติ ชฺญาตฺวา ยูยมฺ อเนเก ศิกฺษกา มา ภวตฯ
Ndugu zangu, msiwe walimu wengi, kwa maana mnafahamu kwamba sisi tufundishao tutahukumiwa vikali zaidi.
2 ยต: สรฺเวฺว วยํ พหุวิษเยษุ สฺขลาม: , ย: กศฺจิทฺ วาเกฺย น สฺขลติ ส สิทฺธปุรุษ: กฺฤตฺสฺนํ วศีกรฺตฺตุํ สมรฺถศฺจาสฺติฯ
Sisi sote tunajikwaa katika mambo mengi. Ikiwa mtu yeyote hakosei kamwe katika yale anayosema, yeye ni mkamilifu, naye anaweza kuuzuia pia na mwili wake wote.
3 ปศฺยต วยมฺ อศฺวานฺ วศีกรฺตฺตุํ เตษำ วกฺเตฺรษุ ขลีนานฺ นิธาย เตษำ กฺฤตฺสฺนํ ศรีรมฺ อนุวรฺตฺตยาม: ฯ
Tunapotia lijamu kwenye vinywa vya farasi ili kuwafanya watutii, tunaweza kuigeuza miili yao yote.
4 ปศฺยต เย โปตา อตีว พฺฤหทาการา: ปฺรจณฺฑวาไตศฺจ จาลิตาเสฺต'ปิ กรฺณธารสฺย มโน'ภิมตาทฺ อติกฺษุเทฺรณ กรฺเณน วาญฺฉิตํ สฺถานํ ปฺรตฺยนุวรฺตฺตนฺเตฯ
Au angalia pia meli, ingawa ni kubwa sana, nazo huchukuliwa na upepo mkali, lakini hugeuzwa kwa usukani mdogo sana, kokote anakotaka nahodha.
5 ตทฺวทฺ รสนาปิ กฺษุทฺรตรางฺคํ สนฺตี ทรฺปวากฺยานิ ภาษเตฯ ปศฺย กีทฺฤงฺมหารณฺยํ ทหฺยเต 'เลฺปน วหฺนินาฯ
Vivyo hivyo ulimi ni kiungo kidogo sana katika mwili, lakini hujivuna majivuno makuu. Fikirini jinsi moto mdogo unavyoweza kuteketeza msitu mkubwa!
6 รสนาปิ ภเวทฺ วหฺนิรธรฺมฺมรูปปิษฺฏเปฯ อสฺมทงฺเคษุ รสนา ตาทฺฤศํ สนฺติษฺฐติ สา กฺฤตฺสฺนํ เทหํ กลงฺกยติ สฺฤษฺฏิรถสฺย จกฺรํ ปฺรชฺวลยติ นรกานเลน ชฺวลติ จฯ (Geenna g1067)
Ulimi pia ni moto, ndio ulimwengu wa uovu kati ya viungo vya mwili. Ulimi huutia mwili wote wa mtu unajisi na kuuwasha moto mfumo mzima wa maisha yake, nao wenyewe huchomwa moto wa jehanamu. (Geenna g1067)
7 ปศุปกฺษฺยุโรคชลจราณำ สรฺเวฺวษำ สฺวภาโว ทมยิตุํ ศกฺยเต มานุษิกสฺวภาเวน ทมยาญฺจเกฺร จฯ
Kwa maana kila aina ya wanyama, ndege, wanyama watambaao na viumbe vya baharini vinafugika na vimefugwa na binadamu,
8 กินฺตุ มานวานำ เกนาปิ ชิหฺวา ทมยิตุํ น ศกฺยเต สา น นิวารฺยฺยมฺ อนิษฺฏํ หลาหลวิเษณ ปูรฺณา จฯ
lakini hakuna mtu awezaye kuufuga ulimi. Ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.
9 ตยา วยํ ปิตรมฺ อีศฺวรํ ธนฺยํ วทาม: , ตยา เจศฺวรสฺย สาทฺฤเศฺย สฺฤษฺฏานฺ มานวานฺ ศปาม: ฯ
Kwa ulimi tunamhimidi Bwana, yaani Baba yetu, na kwa huo twawalaani watu walioumbwa kwa mfano wa Mungu.
10 เอกสฺมาทฺ วทนาทฺ ธนฺยวาทศาเปา นิรฺคจฺฉต: ฯ เห มม ภฺราตร: , เอตาทฺฤศํ น กรฺตฺตวฺยํฯ
Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haistahili kuwa hivyo.
11 ปฺรสฺรวณ: กิมฺ เอกสฺมาตฺ ฉิทฺราตฺ มิษฺฏํ ติกฺตญฺจ โตยํ นิรฺคมยติ?
Je, chemchemi yaweza kutoa katika tundu moja maji matamu na maji ya chumvi?
12 เห มม ภฺราตร: , อุฑุมฺพรตรุ: กึ ชิตผลานิ ทฺรากฺษาลตา วา กิมฺ อุฑุมฺพรผลานิ ผลิตุํ ศกฺโนติ? ตทฺวทฺ เอก: ปฺรสฺรวโณ ลวณมิษฺเฏ โตเย นิรฺคมยิตุํ น ศกฺโนติฯ
Je, ndugu zangu, mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Wala chemchemi ya maji ya chumvi haiwezi kutoa maji matamu.
13 ยุษฺมากํ มเธฺย ชฺญานี สุโพธศฺจ ก อาเสฺต? ตสฺย กรฺมฺมาณิ ชฺญานมูลกมฺฤทุตายุกฺตานีติ สทาจาราตฺ ส ปฺรมาณยตุฯ
Ni nani aliye na hekima na ufahamu miongoni mwenu? Basi na aionyeshe hiyo kwa maisha yake mema na kwa matendo yake yaliyotendwa kwa unyenyekevu utokanao na hekima.
14 กินฺตุ ยุษฺมทนฺต: กรณมเธฺย ยทิ ติกฺเตรฺษฺยา วิวาเทจฺฉา จ วิทฺยเต ตรฺหิ สตฺยมตสฺย วิรุทฺธํ น ศฺลาฆธฺวํ นจานฺฤตํ กถยตฯ
Lakini ikiwa mna wivu na ni wenye chuki na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu kwa ajili ya hayo wala msiikatae kweli.
15 ตาทฺฤศํ ชฺญานมฺ อูรฺทฺธฺวาทฺ อาคตํ นหิ กินฺตุ ปารฺถิวํ ศรีริ เภาติกญฺจฯ
Hekima ya namna hiyo haishuki kutoka mbinguni, bali ni ya kidunia, isiyo ya kiroho, na ya kishetani.
16 ยโต เหโตรีรฺษฺยา วิวาเทจฺฉา จ ยตฺร เวเทฺยเต ตไตฺรว กลห: สรฺวฺวํ ทุษฺกฺฤตญฺจ วิทฺยเตฯ
Kwa maana panapokuwa na wivu na ubinafsi, ndipo penye machafuko na uovu wa kila namna.
17 กินฺตูรฺทฺธฺวาทฺ อาคตํ ยตฺ ชฺญานํ ตตฺ ปฺรถมํ ศุจิ ตต: ปรํ ศานฺตํ กฺษานฺตมฺ อาศุสนฺเธยํ ทยาทิสตฺผไล: ปริปูรฺณมฺ อสนฺทิคฺธํ นิษฺกปฏญฺจ ภวติฯ
Lakini hekima itokayo mbinguni kwanza ni safi, kisha inapenda amani, tena ni ya upole, iliyo tayari kusikiliza wengine kwa unyenyekevu, iliyojaa huruma na matunda mema, isiyopendelea mtu, tena isiyokuwa na unafiki.
18 ศานฺตฺยาจาริภิ: ศานฺตฺยา ธรฺมฺมผลํ โรปฺยเตฯ
Mavuno ya haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani.

< ยากูพ: 3 >