< เปฺรริตา: 27 >
1 ชลปเถนาสฺมากมฺ อิโตลิยาเทศํ ปฺรติ ยาตฺรายำ นิศฺจิตายำ สตฺยำ เต ยูลิยนามฺโน มหาราชสฺย สํฆาตานฺตรฺคตสฺย เสนาปเต: สมีเป เปาลํ ตทนฺยานฺ กตินยชนำศฺจ สมารฺปยนฺฯ
Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho “Kikosi cha Augusto.”
2 วยมฺ อาทฺรามุตฺตียํ โปตเมกมฺ อารุหฺย อาศิยาเทศสฺย ตฏสมีเปน ยาตุํ มตึ กฺฤตฺวา ลงฺครมฺ อุตฺถาปฺย โปตมฺ อโมจยาม; มากิทนิยาเทศสฺถถิษลนีกีนิวาสฺยาริสฺตารฺขนามา กศฺจิทฺ ชโน'สฺมาภิ: สารฺทฺธมฺ อาสีตฺฯ
Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonika, alikuwa pamoja nasi.
3 ปรสฺมินฺ ทิวเส 'สฺมาภิ: สีโทนฺนคเร โปเต ลาคิเต ตตฺร ยูลิย: เสนาปติ: เปาลํ ปฺรติ เสาชนฺยํ ปฺรทรฺถฺย สานฺตฺวนารฺถํ พนฺธุพานฺธวานฺ อุปยาตุมฺ อนุชชฺเญาฯ
Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
4 ตสฺมาตฺ โปเต โมจิเต สติ สมฺมุขวาโย: สมฺภวาทฺ วยํ กุโปฺรปทฺวีปสฺย ตีรสมีเปน คตวนฺต: ฯ
Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi.
5 กิลิกิยายา: ปามฺผูลิยายาศฺจ สมุทฺรสฺย ปารํ คตฺวา ลูกิยาเทศานฺตรฺคตํ มุรานครมฺ อุปาติษฺฐามฯ
Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
6 ตตฺสฺถานาทฺ อิตาลิยาเทศํ คจฺฉติ ย: สิกนฺทริยานครสฺย โปตสฺตํ ตตฺร ปฺราปฺย ศตเสนาปติสฺตํ โปตมฺ อสฺมานฺ อาโรหยตฺฯ
Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani.
7 ตต: ปรํ พหูนิ ทินานิ ศไน: ศไน: รฺคตฺวา กฺนีทปารฺโศฺวปสฺถฺติ: ปูรฺวฺวํ ปฺรติกูเลน ปวเนน วยํ สลฺโมนฺยา: สมฺมุขมฺ อุปสฺถาย กฺรีตฺยุปทฺวีปสฺย ตีรสมีเปน คตวนฺต: ฯ
Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
8 กษฺเฏน ตมุตฺตีรฺยฺย ลาเสยานครสฺยาธ: สุนฺทรนามกํ ขาตมฺ อุปาติษฺฐามฯ
Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo “Bandari Nzuri”, karibu na mji wa Lasea.
9 อิตฺถํ พหุติถ: กาโล ยาปิต อุปวาสทินญฺจาตีตํ, ตตฺการณาตฺ เนาวรฺตฺมนิ ภยงฺกเร สติ เปาโล วินเยน กถิตวานฺ,
Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo:
10 เห มเหจฺฉา อหํ นิศฺจยํ ชานามิ ยาตฺรายามสฺยามฺ อสฺมากํ เกฺลศา พหูนามปจยาศฺจ ภวิษฺยนฺติ, เต เกวลํ โปตสามคฺโรฺยริติ นหิ, กินฺตฺวสฺมากํ ปฺราณานามปิฯ
“Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu.”
11 ตทา ศตเสนาปติ: เปาโลกฺตวากฺยโตปิ กรฺณธารสฺย โปตวณิชศฺจ วากฺยํ พหุมํสฺตฯ
Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
12 ตตฺ ขาตํ ศีตกาเล วาสารฺหสฺถานํ น ตสฺมาทฺ อวาจีปฺรตีโจรฺทิโศ: กฺรีตฺยา: ไผนีกิยขาตํ ยาตุํ ยทิ ศกฺนุวนฺตสฺตรฺหิ ตตฺร ศีตกาลํ ยาปยิตุํ ปฺราเยณ สรฺเวฺว มนฺตฺรยามาสุ: ฯ
Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
13 ตต: ปรํ ทกฺษิณวายุ รฺมนฺทํ วหตีติ วิโลกฺย นิชาภิปฺรายสฺย สิทฺเธ: สุโยโค ภวตีติ พุทฺธฺวา โปตํ โมจยิตฺวา กฺรีตฺยุปทฺวีปสฺย ตีรสมีเปน จลิตวนฺต: ฯ
Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakang'oa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete.
14 กินฺตฺวลฺปกฺษณาตฺ ปรเมว อุรกฺลุโทนฺนามา ปฺรติกูล: ปฺรจณฺโฑ วายุ รฺวหนฺ โปเต'ลคีตฺ
Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao “Upepo wa Kaskazi” ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
15 ตสฺยาภิมุขํ คนฺตุมฺ โปตสฺยาศกฺตตฺวาทฺ วยํ วายุนา สฺวยํ นีตา: ฯ
Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo.
16 อนนฺตรํ เกฺลาทีนามฺน อุปทฺวีปสฺย กูลสมีเปน โปตํ คมยิตฺวา พหุนา กษฺเฏน กฺษุทฺรนาวมฺ อรกฺษามฯ
Kisiwa kimoja kiitwacho Kanda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
17 เต ตามารุหฺย รชฺชฺจา โปตสฺยาโธภาคมฺ อพธฺนนฺ ตทนนฺตรํ เจตฺ โปโต ไสกเต ลคตีติ ภยาทฺ วาตวสนานฺยโมจยนฺ ตต: โปโต วายุนา จาลิต: ฯ
Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libya. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
18 กินฺตุ กฺรมโศ วาโย: ปฺรพลตฺวาตฺ โปโต โทลายมาโน'ภวตฺ ปรสฺมินฺ ทิวเส โปตสฺถานิ กติปยานิ ทฺรวฺยาณิ โตเย นิกฺษิปฺตานิฯ
Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli.
19 ตฺฤตียทิวเส วยํ สฺวหไสฺต: โปตสชฺชนทฺรวฺยาณิ นิกฺษิปฺตวนฺต: ฯ
Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
20 ตโต พหุทินานิ ยาวตฺ สูรฺยฺยนกฺษตฺราทีนิ สมาจฺฉนฺนานิ ตโต 'ตีว วาตฺยาคมาทฺ อสฺมากํ ปฺราณรกฺษายา: กาปิ ปฺรตฺยาศา นาติษฺฐตฺฯ
Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
21 พหุทิเนษุ โลไกรนาหาเรณ ยาปิเตษุ สรฺเวฺวษำ สากฺษตฺ เปาลสฺติษฺฐนฺ อกถยตฺ, เห มเหจฺฉา: กฺรีตฺยุปทฺวีปาตฺ โปตํ น โมจยิตุมฺ อหํ ปูรฺวฺวํ ยทฺ อวทํ ตทฺคฺรหณํ ยุษฺมากมฺ อุจิตมฺ อาสีตฺ ตถา กฺฤเต ยุษฺมากมฺ เอษา วิปทฺ เอโษ'ปจยศฺจ นาฆฏิเษฺยตามฺฯ
Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, “Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
22 กินฺตุ สามฺปฺรตํ ยุษฺมานฺ วินีย พฺรวีมฺยหํ, ยูยํ น กฺษุภฺยต ยุษฺมากมฺ เอกสฺยาปิ ปฺราณิโน หานิ รฺน ภวิษฺยติ, เกวลสฺย โปตสฺย หานิ รฺภวิษฺยติฯ
Lakini sasa ninawaombeni muwe na moyo; hakuna hata mmoja wenu atakayepoteza maisha yake; meli tu ndiyo itakayopotea.
23 ยโต ยเสฺยศฺวรสฺย โลโก'หํ ยญฺจาหํ ปริจรามิ ตทีย เอโก ทูโต โหฺย ราเตฺรา มมานฺติเก ติษฺฐนฺ กถิตวานฺ,
Kwa maana jana usiku malaika wa yule Mungu ambaye mimi ni wake na ambaye mimi ninamwabudu alinitokea,
24 เห เปาล มา ไภษี: ไกสรสฺย สมฺมุเข ตฺวโยปสฺถาตวฺยํ; ตไวตานฺ สงฺคิโน โลกานฺ อีศฺวรสฺตุภฺยํ ทตฺตวานฺฯ
akaniambia: Paulo usiogope! Ni lazima utasimama mbele ya Kaisari; naye Mungu, kwa wema wake, amekufadhili kwa kuwaokoa wote wanaosafiri nawe wasiangamie.
25 อเตอว เห มเหจฺฉา ยูยํ สฺถิรมนโส ภวต มหฺยํ ยา กถากถิ สาวศฺยํ ฆฏิษฺยเต มไมตาทฺฤศี วิศฺวาส อีศฺวเร วิทฺยเต,
Hivyo, waheshimiwa, jipeni moyo! Maana ninamwamini Mungu kwamba itakuwa sawa kama nilivyoambiwa.
26 กินฺตุ กสฺยจิทฺ อุปทฺวีปโสฺยปริ ปติตวฺยมฺ อสฺมาภิ: ฯ
Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani.”
27 ตต: ปรมฺ อาทฺริยาสมุเทฺร โปตสฺตไถว โทลายมาน: สนฺ อิตสฺตโต คจฺฉนฺ จตุรฺทศทิวสสฺย ราเตฺร รฺทฺวิตียปฺรหรสมเย กสฺยจิตฺ สฺถลสฺย สมีปมุปติษฺฐตีติ โปตียโลกา อนฺวมนฺยนฺตฯ
Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huku katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
28 ตตเสฺต ชลํ ปริมาย ตตฺร วึศติ รฺวฺยามา ชลานีติ ชฺญาตวนฺต: ฯ กิญฺจิทฺทูรํ คตฺวา ปุนรปิ ชลํ ปริมิตวนฺต: ฯ ตตฺร ปญฺจทศ วฺยามา ชลานิ ทฺฤษฺฏฺวา
Hivyo walitafuta kina cha bahari kwa kuteremsha kamba iliyokuwa imefungiwa kitu kizito, wakapata kina cha mita arobaini. Baadaye wakapima tena wakapata mita thelathini.
29 เจตฺ ปาษาเณ ลคตีติ ภยาตฺ โปตสฺย ปศฺจาทฺภาคตศฺจตุโร ลงฺครานฺ นิกฺษิปฺย ทิวากรมฺ อเปกฺษฺย สรฺเวฺว สฺถิตวนฺต: ฯ
Kwa sababu ya kuogopa kukwama kwenye miamba, waliteremsha nanga nne nyuma ya meli; wakaomba kuche upesi.
30 กินฺตุ โปตียโลกา: โปตาคฺรภาเค ลงฺครนิกฺเษปํ ฉลํ กฺฤตฺวา ชลเธา กฺษุทฺรนาวมฺ อวโรหฺย ปลายิตุมฺ อเจษฺฏนฺตฯ
Wanamaji walitaka kutoroka, na walikwisha kuteremsha ule mtumbwi majini, wakijisingizia kwamba wanakwenda kuteremsha nanga upande wa mbele wa meli.
31 ตต: เปาล: เสนาปตเย ไสนฺยคณาย จ กถิตวานฺ, เอเต ยทิ โปตมเธฺย น ติษฺฐนฺติ ตรฺหิ ยุษฺมากํ รกฺษณํ น ศกฺยํฯ
Lakini Paulo alimwambia yule ofisa wa jeshi na askari wake, “Kama wanamaji hawa hawabaki ndani ya meli, hamtaokoka.”
32 ตทา เสนาคโณ รชฺชูนฺ ฉิตฺวา นาวํ ชเล ปติตุมฺ อททาตฺฯ
Hapo wale askari walizikata kamba zilizokuwa zimeshikilia ule mtumbwi, wakauacha uchukuliwe na maji.
33 ปฺรภาตสมเย เปาล: สรฺวฺวานฺ ชนานฺ โภชนารฺถํ ปฺรารฺถฺย วฺยาหรตฺ, อทฺย จตุรฺทศทินานิ ยาวทฺ ยูยมฺ อเปกฺษมานา อนาหารา: กาลมฺ อยาปยต กิมปิ นาภุํคฺธํฯ
Karibu na alfajiri, Paulo aliwahimiza wote wale chakula: “Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika mashaka na bila kula; hamjala kitu chochote.
34 อโต วินเย'หํ ภกฺษฺยํ ภุชฺยตำ ตโต ยุษฺมากํ มงฺคลํ ภวิษฺยติ, ยุษฺมากํ กสฺยจิชฺชนสฺย ศิรส: เกไศโกปิ น นํกฺษฺยติฯ
Basi, ninawasihi mle chakula kwa maana mnakihitaji ili mweze kuendelea kuishi. Maana hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.”
35 อิติ วฺยาหฺฤตฺย เปาลํ ปูปํ คฺฤหีเตฺวศฺวรํ ธนฺยํ ภาษมาณสฺตํ ภํกฺตฺวา โภกฺตุมฺ อารพฺธวานฺฯ
Baada ya kusema hivyo, Paulo alichukua mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, akaanza kula.
36 อนนฺตรํ สรฺเวฺว จ สุสฺถิรา: สนฺต: ขาทฺยานิ ปรฺปฺยคฺฤหฺลนฺฯ
Hapo wote wakapata moyo, nao pia wakala chakula.
37 อสฺมากํ โปเต ษฏฺสปฺตตฺยธิกศตทฺวยโลกา อาสนฺฯ
Jumla tulikuwa watu mia mbili na sabini na sita katika meli.
38 สรฺเวฺวษุ โลเกษุ ยเถษฺฏํ ภุกฺตวตฺสุ โปตสฺถนฺ โคธูมานฺ ชลเธา นิกฺษิปฺย ไต: โปตสฺย ภาโร ลฆูกฺฤต: ฯ
Baada ya kila mmoja kula chakula cha kutosha, walipunguza uzito wa meli kwa kutupa nafaka baharini.
39 ทิเน ชาเต'ปิ ส โก เทศ อิติ ตทา น ปรฺยฺยจียต; กินฺตุ ตตฺร สมตฏมฺ เอกํ ขาตํ ทฺฤษฺฏฺวา ยทิ ศกฺนุมสฺตรฺหิ วยํ ตสฺยาภฺยนฺตรํ โปตํ คมยาม อิติ มตึ กฺฤตฺวา เต ลงฺครานฺ ฉิตฺตฺวา ชลเธา ตฺยกฺตวนฺต: ฯ
Kulipokucha, wanamaji hawakuweza kuitambua nchi ile, ila waliona ghuba moja yenye ufuko; wakaamua kutia nanga huko kama ikiwezekana.
40 ตถา กรฺณพนฺธนํ โมจยิตฺวา ปฺรธานํ วาตวสนมฺ อุตฺโตลฺย ตีรสมีปํ คตวนฺต: ฯ
Hivyo walikata nanga na kuziacha baharini, na wakati huohuo wakazifungua kamba zilizokuwa zimeufunga usukani, kisha wakatweka tanga moja mbele kushika upepo, wakaelekea ufukoni.
41 กินฺตุ ทฺวโย: สมุทฺรโย: สงฺคมสฺถาเน ไสกโตปริ โปเต นิกฺษิปฺเต 'คฺรภาเค พาธิเต ปศฺจาทฺภาเค ปฺรพลตรงฺโค'ลคตฺ เตน โปโต ภคฺน: ฯ
Lakini walifika mahali ambapo mikondo miwili ya bahari hukutana, na meli ikakwama. Sehemu ya mbele ilikuwa imezama mchangani bila kutikisika. Sehemu ya nyuma ya meli ilianza kuvunjika vipandevipande kwa mapigo ya nguvu ya mawimbi.
42 ตสฺมาทฺ พนฺทยศฺเจทฺ พาหุภิสฺตรนฺต: ปลายนฺเต อิตฺยาศงฺกยา เสนาคณสฺตานฺ หนฺตุมฺ อมนฺตฺรยตฺ;
Askari walitaka kuwaua wafungwa wote kwa kuogopa kwamba wangeogelea hadi pwani na kutoroka.
43 กินฺตุ ศตเสนาปติ: เปาลํ รกฺษิตุํ ปฺรยตฺนํ กฺฤตฺวา ตานฺ ตจฺเจษฺฏายา นิวรฺตฺย อิตฺยาทิษฺฏวานฺ, เย พาหุตรณํ ชานนฺติ เต'เคฺร โปฺรลฺลมฺปฺย สมุเทฺร ปติตฺวา พาหุภิสฺตีรฺตฺตฺวา กูลํ ยานฺตุฯ
Lakini kwa vile yule ofisajeshi alitaka kumwokoa Paulo, aliwazuia wasifanye hivyo. Aliamuru wale waliojua kuogelea waruke kutoka melini na kuogelea hadi pwani,
44 อปรมฺ อวศิษฺฏา ชนา: กาษฺฐํ โปตียํ ทฺรวฺยํ วา เยน ยตฺ ปฺราปฺยเต ตทวลมฺพฺย ยานฺตุ; อิตฺถํ สรฺเวฺว ภูมึ ปฺราปฺย ปฺราไณ รฺชีวิตา: ฯ
na wengine wafuate wakijishikilia kwenye mbao au kwenye vipande vya meli iliyovunjika. Ndivyo sisi sote tulivyofika salama pwani.