< mathiḥ 26 >
1 yīśuretān prastāvān samāpya śiṣyānūce,
Yesu alipomaliza kusema hayo yote, akawaambia wanafunzi wake,
2 yuṣmābhi rjñātaṁ dinadvayāt paraṁ nistāramaha upasthāsyati, tatra manujasutaḥ kruśena hantuṁ parakareṣu samarpiṣyate|
“Kama mnavyojua, baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili asulubiwe.”
3 tataḥ paraṁ pradhānayājakādhyāpakaprāñcaḥ kiyaphānāmno mahāyājakasyāṭṭālikāyāṁ militvā
Basi viongozi wa makuhani na wazee wa watu wakakusanyika katika jumba la utawala la kuhani mkuu, jina lake Kayafa.
4 kenopāyena yīśuṁ dhṛtvā hantuṁ śaknuyuriti mantrayāñcakruḥ|
Wakafanya shauri ili kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
5 kintu tairuktaṁ mahakāle na dharttavyaḥ, dhṛte prajānāṁ kalahena bhavituṁ śakyate|
Lakini wakasema, “Isiwe wakati wa Sikukuu, kusitokee ghasia miongoni mwa watu.”
6 tato baithaniyāpure śimonākhyasya kuṣṭhino veśmani yīśau tiṣṭhati
Yesu alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,
7 kācana yoṣā śvetopalabhājanena mahārghyaṁ sugandhi tailamānīya bhojanāyopaviśatastasya śirobhyaṣecat|
naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa; akayamimina kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani kula chakula.
8 kintu tadālokya tacchiṣyaiḥ kupitairuktaṁ, kuta itthamapavyayate?
Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?
9 cedidaṁ vyakreṣyata, tarhi bhūrimūlyaṁ prāpya daridrebhyo vyatāriṣyata|
Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”
10 yīśunā tadavagatya te samuditāḥ, yoṣāmenāṁ kuto duḥkhinīṁ kurutha, sā māṁ prati sādhu karmmākārṣīt|
Yesu, akijua jambo hili, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye amenitendea jambo zuri sana.
11 yuṣmākamaṁ samīpe daridrāḥ satatamevāsate, kintu yuṣmākamantikehaṁ nāse satataṁ|
Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
12 sā mama kāyopari sugandhitailaṁ siktvā mama śmaśānadānakarmmākārṣīt|
Alipomiminia haya manukato kwenye mwili wangu, amefanya hivyo ili kuniandaa kwa ajili ya maziko yangu.
13 atohaṁ yuṣmān tathyaṁ vadāmi sarvvasmin jagati yatra yatraiṣa susamācāraḥ pracāriṣyate, tatra tatraitasyā nāryyāḥ smaraṇārtham karmmedaṁ pracāriṣyate|
Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo hii Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
14 tato dvādaśaśiṣyāṇām īṣkariyotīyayihūdānāmaka ekaḥ śiṣyaḥ pradhānayājakānāmantikaṁ gatvā kathitavān,
Kisha mmojawapo wa wale kumi na wawili, aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda kwa viongozi wa makuhani
15 yadi yuṣmākaṁ kareṣu yīśuṁ samarpayāmi, tarhi kiṁ dāsyatha? tadānīṁ te tasmai triṁśanmudrā dātuṁ sthirīkṛtavantaḥ|
na kuuliza, “Mtanipa nini nikimtia Yesu mikononi mwenu?” Wakamlipa vipande thelathini vya fedha.
16 sa tadārabhya taṁ parakareṣu samarpayituṁ suyogaṁ ceṣṭitavān|
Tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu.
17 anantaraṁ kiṇvaśūnyapūpaparvvaṇaḥ prathamehni śiṣyā yīśum upagatya papracchuḥ bhavatkṛte kutra vayaṁ nistāramahabhojyam āyojayiṣyāmaḥ? bhavataḥ kecchā?
Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimjia Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
18 tadā sa gaditavān, madhyenagaramamukapuṁsaḥ samīpaṁ vrajitvā vadata, guru rgaditavān, matkālaḥ savidhaḥ, saha śiṣyaistvadālaye nistāramahabhojyaṁ bhokṣye|
Akajibu, “Nendeni kwa mtu fulani huko mjini, mkamwambie, ‘Mwalimu asema hivi: Saa yangu imekaribia. Nitaiadhimisha Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.’”
19 tadā śiṣyā yīśostādṛśanideśānurūpakarmma vidhāya tatra nistāramahabhojyamāsādayāmāsuḥ|
Hivyo wanafunzi wakafanya kama vile Yesu alivyokuwa amewaelekeza, nao wakaandaa Pasaka.
20 tataḥ sandhyāyāṁ satyāṁ dvādaśabhiḥ śiṣyaiḥ sākaṁ sa nyaviśat|
Ilipofika jioni, Yesu alikuwa ameketi mezani pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
21 aparaṁ bhuñjāna uktavān yuṣmān tathyaṁ vadāmi, yuṣmākameko māṁ parakareṣu samarpayiṣyati|
Nao walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
22 tadā te'tīva duḥkhitā ekaikaśo vaktumārebhire, he prabho, sa kimahaṁ?
Wakahuzunika sana, wakaanza kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
23 tataḥ sa jagāda, mayā sākaṁ yo jano bhojanapātre karaṁ saṁkṣipati, sa eva māṁ parakareṣu samarpayiṣyati|
Yesu akawaambia, “Yule aliyechovya mkono wake katika bakuli pamoja nami ndiye atakayenisaliti.
24 manujasutamadhi yādṛśaṁ likhitamāste, tadanurūpā tadgati rbhaviṣyati; kintu yena puṁsā sa parakareṣu samarpayiṣyate, hā hā cet sa nājaniṣyata, tadā tasya kṣemamabhaviṣyat|
Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu. Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa!”
25 tadā yihūdānāmā yo janastaṁ parakareṣu samarpayiṣyati, sa uktavān, he guro, sa kimahaṁ? tataḥ sa pratyuktavān, tvayā satyaṁ gaditam|
Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, akasema, “Je, ni mimi Rabi?” Yesu akajibu, “Naam, wewe mwenyewe umesema.”
26 anantaraṁ teṣāmaśanakāle yīśuḥ pūpamādāyeśvarīyaguṇānanūdya bhaṁktvā śiṣyebhyaḥ pradāya jagāda, madvapuḥsvarūpamimaṁ gṛhītvā khādata|
Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu.”
27 paścāt sa kaṁsaṁ gṛhlan īśvarīyaguṇānanūdya tebhyaḥ pradāya kathitavān, sarvvai ryuṣmābhiranena pātavyaṁ,
Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, “Nyweni nyote katika kikombe hiki.
28 yasmādanekeṣāṁ pāpamarṣaṇāya pātitaṁ yanmannūtnaniyamarūpaśoṇitaṁ tadetat|
Hii ndiyo damu yangu ya Agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.
29 aparamahaṁ nūtnagostanīrasaṁ na pāsyāmi, tāvat gostanīphalarasaṁ punaḥ kadāpi na pāsyāmi|
Lakini ninawaambia, tangu sasa sitakunywa tena katika uzao huu wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
30 paścāt te gītamekaṁ saṁgīya jaitunākhyagiriṁ gatavantaḥ|
Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
31 tadānīṁ yīśustānavocat, asyāṁ rajanyāmahaṁ yuṣmākaṁ sarvveṣāṁ vighnarūpo bhaviṣyāmi, yato likhitamāste, "meṣāṇāṁ rakṣako yastaṁ prahariṣyāmyahaṁ tataḥ| meṣāṇāṁ nivaho nūnaṁ pravikīrṇo bhaviṣyati"||
Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu, ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo wa hilo kundi watatawanyika.’
32 kintu śmaśānāt samutthāya yuṣmākamagre'haṁ gālīlaṁ gamiṣyāmi|
Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
33 pitarastaṁ provāca, bhavāṁścet sarvveṣāṁ vighnarūpo bhavati, tathāpi mama na bhaviṣyati|
Petro akajibu, “Hata kama wote watakuacha, kamwe mimi sitakuacha.”
34 tato yīśunā sa uktaḥ, tubhyamahaṁ tathyaṁ kathayāmi, yāminyāmasyāṁ caraṇāyudhasya ravāt pūrvvaṁ tvaṁ māṁ tri rnāṅgīkariṣyasi|
Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
35 tataḥ pitara uditavān, yadyapi tvayā samaṁ marttavyaṁ, tathāpi kadāpi tvāṁ na nāṅgīkariṣyāmi; tathaiva sarvve śiṣyāścocuḥ|
Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wanafunzi wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
36 anantaraṁ yīśuḥ śiṣyaiḥ sākaṁ getśimānīnāmakaṁ sthānaṁ prasthāya tebhyaḥ kathitavān, adaḥ sthānaṁ gatvā yāvadahaṁ prārthayiṣye tāvad yūyamatropaviśata|
Kisha Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake mpaka kwenye bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia, “Kaeni hapa, nami niende kule nikaombe.”
37 paścāt sa pitaraṁ sivadiyasutau ca saṅginaḥ kṛtvā gatavān, śokākulo'tīva vyathitaśca babhūva|
Akamchukua Petro pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kufadhaika.
38 tānavādīcca mṛtiyātaneva matprāṇānāṁ yātanā jāyate, yūyamatra mayā sārddhaṁ jāgṛta|
Kisha Yesu akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe pamoja nami.”
39 tataḥ sa kiñciddūraṁ gatvādhomukhaḥ patan prārthayāñcakre, he matpitaryadi bhavituṁ śaknoti, tarhi kaṁso'yaṁ matto dūraṁ yātu; kintu madicchāvat na bhavatu, tvadicchāvad bhavatu|
Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba akisema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki na kiniondokee. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali kama upendavyo wewe.”
40 tataḥ sa śiṣyānupetya tān nidrato nirīkṣya pitarāya kathayāmāsa, yūyaṁ mayā sākaṁ daṇḍamekamapi jāgarituṁ nāśankuta?
Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamuuliza Petro, “Je, ninyi hamkuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja?
41 parīkṣāyāṁ na patituṁ jāgṛta prārthayadhvañca; ātmā samudyatosti, kintu vapu rdurbbalaṁ|
Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
42 sa dvitīyavāraṁ prārthayāñcakre, he mattāta, na pīte yadi kaṁsamidaṁ matto dūraṁ yātuṁ na śaknoti, tarhi tvadicchāvad bhavatu|
Akaenda tena mara ya pili na kuomba, “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisikinywe, basi mapenzi yako yafanyike.”
43 sa punaretya tān nidrato dadarśa, yatasteṣāṁ netrāṇi nidrayā pūrṇānyāsan|
Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito.
44 paścāt sa tān vihāya vrajitvā tṛtīyavāraṁ pūrvvavat kathayan prārthitavān|
Hivyo akawaacha akaenda zake tena mara ya tatu na kuomba akisema maneno yale yale.
45 tataḥ śiṣyānupāgatya gaditavān, sāmprataṁ śayānāḥ kiṁ viśrāmyatha? paśyata, samaya upāsthāt, manujasutaḥ pāpināṁ kareṣu samarpyate|
Kisha akarudi kwa wanafunzi wake, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Tazameni, saa imefika ambapo Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
46 uttiṣṭhata, vayaṁ yāmaḥ, yo māṁ parakareṣu masarpayiṣyati, paśyata, sa samīpamāyāti|
Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
47 etatkathākathanakāle dvādaśaśiṣyāṇāmeko yihūdānāmako mukhyayājakalokaprācīnaiḥ prahitān asidhāriyaṣṭidhāriṇo manujān gṛhītvā tatsamīpamupatasthau|
Alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale Kumi na Wawili, akafika. Alikuwa amefuatana na umati mkubwa wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.
48 asau parakareṣvarpayitā pūrvvaṁ tān itthaṁ saṅketayāmāsa, yamahaṁ cumbiṣye, so'sau manujaḥ, saeva yuṣmābhi rdhāryyatāṁ|
Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni.”
49 tadā sa sapadi yīśumupāgatya he guro, praṇamāmītyuktvā taṁ cucumbe|
Mara Yuda akamjia Yesu na kumsalimu, “Salamu, Rabi!” Akambusu.
50 tadā yīśustamuvāca, he mitraṁ kimarthamāgatosi? tadā tairāgatya yīśurākramya daghre|
Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.” Kisha wale watu wakasogea mbele, wakamkamata Yesu.
51 tato yīśoḥ saṅgināmekaḥ karaṁ prasāryya koṣādasiṁ bahiṣkṛtya mahāyājakasya dāsamekamāhatya tasya karṇaṁ ciccheda|
Ghafula mmoja wa wale waliokuwa na Yesu alipoona hivyo, akaushika upanga wake, akauchomoa na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
52 tato yīśustaṁ jagāda, khaḍgaṁ svasthāne nidhehi yato ye ye janā asiṁ dhārayanti, taevāsinā vinaśyanti|
Ndipo Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wote watumiao upanga watakufa kwa upanga.
53 aparaṁ pitā yathā madantikaṁ svargīyadūtānāṁ dvādaśavāhinīto'dhikaṁ prahiṇuyāt mayā tamuddiśyedānīmeva tathā prārthayituṁ na śakyate, tvayā kimitthaṁ jñāyate?
Je, unadhani siwezi kumwomba Baba yangu naye mara moja akaniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
54 tathā satītthaṁ ghaṭiṣyate dharmmapustakasya yadidaṁ vākyaṁ tat kathaṁ sidhyet?
Lakini je, yale Maandiko yanayotabiri kwamba ni lazima itendeke hivi yatatimiaje?”
55 tadānīṁ yīśu rjananivahaṁ jagāda, yūyaṁ khaḍgayaṣṭīn ādāya māṁ kiṁ cauraṁ dharttumāyātāḥ? ahaṁ pratyahaṁ yuṣmābhiḥ sākamupaviśya samupādiśaṁ, tadā māṁ nādharata;
Wakati huo, Yesu akawaambia ule umati wa watu, “Je, mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi? Siku kwa siku niliketi Hekaluni nikifundisha, mbona hamkunikamata?
56 kintu bhaviṣyadvādināṁ vākyānāṁ saṁsiddhaye sarvvametadabhūt|tadā sarvve śiṣyāstaṁ vihāya palāyanta|
Lakini haya yote yametukia ili maandiko ya manabii yapate kutimia.” Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.
57 anantaraṁ te manujā yīśuṁ dhṛtvā yatrādhyāpakaprāñcaḥ pariṣadaṁ kurvvanta upāviśan tatra kiyaphānāmakamahāyājakasyāntikaṁ ninyuḥ|
Wale waliokuwa wamemkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, kuhani mkuu, mahali ambapo walimu wa sheria pamoja na wazee walikuwa wamekusanyika.
58 kintu śeṣe kiṁ bhaviṣyatīti vettuṁ pitaro dūre tatpaścād vrajitvā mahāyājakasyāṭṭālikāṁ praviśya dāsaiḥ sahita upāviśat|
Lakini Petro akamfuata kwa mbali hadi uani kwa kuhani mkuu. Akaingia ndani, akaketi pamoja na walinzi ili aone litakalotukia.
59 tadānīṁ pradhānayājakaprācīnamantriṇaḥ sarvve yīśuṁ hantuṁ mṛṣāsākṣyam alipsanta,
Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu ili wapate kumuua.
60 kintu na lebhire| anekeṣu mṛṣāsākṣiṣvāgateṣvapi tanna prāpuḥ|
Lakini hawakupata jambo lolote, ingawa mashahidi wengi wa uongo walijitokeza. Hatimaye wakajitokeza mashahidi wawili wa uongo
61 śeṣe dvau mṛṣāsākṣiṇāvāgatya jagadatuḥ, pumānayamakathayat, ahamīśvaramandiraṁ bhaṁktvā dinatrayamadhye tannirmmātuṁ śaknomi|
na kusema, “Huyu mtu alisema, ‘Ninaweza kulivunja Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.’”
62 tadā mahāyājaka utthāya yīśum avādīt| tvaṁ kimapi na prativadasi? tvāmadhi kimete sākṣyaṁ vadanti?
Kisha kuhani mkuu akasimama na kumwambia Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
63 kintu yīśu rmaunībhūya tasyau| tato mahāyājaka uktavān, tvām amareśvaranāmnā śapayāmi, tvamīśvarasya putro'bhiṣikto bhavasi naveti vada|
Lakini Yesu akakaa kimya. Ndipo kuhani mkuu akamwambia, “Nakuapisha mbele za Mungu aliye hai. Tuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”
64 yīśuḥ pratyavadat, tvaṁ satyamuktavān; ahaṁ yuṣmān tathyaṁ vadāmi, itaḥparaṁ manujasutaṁ sarvvaśaktimato dakṣiṇapārśve sthātuṁ gagaṇasthaṁ jaladharānāruhyāyāntaṁ vīkṣadhve|
Yesu akajibu, “Wewe umenena. Lakini ninawaambia nyote: Siku za baadaye, mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
65 tadā mahāyājako nijavasanaṁ chittvā jagāda, eṣa īśvaraṁ ninditavān, asmākamaparasākṣyeṇa kiṁ prayojanaṁ? paśyata, yūyamevāsyāsyād īśvaranindāṁ śrutavantaḥ,
Ndipo kuhani mkuu akararua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi? Tazama, sasa ninyi mmesikia hayo makufuru.
66 yuṣmābhiḥ kiṁ vivicyate? te pratyūcuḥ, vadhārho'yaṁ|
Uamuzi wenu ni gani?” Wakajibu, “Anastahili kufa.”
67 tato lokaistadāsye niṣṭhīvitaṁ kecit pratalamāhatya kecicca capeṭamāhatya babhāṣire,
Kisha wakamtemea mate usoni na wengine wakampiga ngumi. Wengine wakampiga makofi
68 he khrīṣṭa tvāṁ kaścapeṭamāhatavān? iti gaṇayitvā vadāsmān|
na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo! Ni nani aliyekupiga?”
69 pitaro bahiraṅgana upaviśati, tadānīmekā dāsī tamupāgatya babhāṣe, tvaṁ gālīlīyayīśoḥ sahacaraekaḥ|
Wakati huu Petro alikuwa amekaa nje uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia na kumwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
70 kintu sa sarvveṣāṁ samakṣam anaṅgīkṛtyāvādīt, tvayā yaducyate, tadarthamahaṁ na vedmi|
Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”
71 tadā tasmin bahirdvāraṁ gate 'nyā dāsī taṁ nirīkṣya tatratyajanānavadat, ayamapi nāsaratīyayīśunā sārddham āsīt|
Alipotoka nje kufika kwenye lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona, akawaambia watu waliokuwepo, “Huyu mtu alikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
72 tataḥ sa śapathena punaranaṅgīkṛtya kathitavān, taṁ naraṁ na paricinomi|
Akakana tena kwa kiapo akisema, “Mimi simjui huyo!”
73 kṣaṇāt paraṁ tiṣṭhanto janā etya pitaram avadan, tvamavaśyaṁ teṣāmeka iti tvaduccāraṇameva dyotayati|
Baada ya muda mfupi, wale waliokuwa wamesimama pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana usemi wako ni kama wao.”
74 kintu so'bhiśapya kathitavān, taṁ janaṁ nāhaṁ paricinomi, tadā sapadi kukkuṭo rurāva|
Ndipo Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui mtu huyo!” Papo hapo jogoo akawika.
75 kukkuṭaravāt prāk tvaṁ māṁ trirapāhnoṣyase, yaiṣā vāg yīśunāvādi tāṁ pitaraḥ saṁsmṛtya bahiritvā khedād bhṛśaṁ cakranda|
Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alilokuwa amesema: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.