< lūkaḥ 23 >
1 tataḥ sabhāsthāḥ sarvvalokā utthāya taṁ pīlātasammukhaṁ nītvāprodya vaktumārebhire,
Kisha umati wote wa watu ukainuka na kumpeleka Yesu kwa Pilato.
2 svamabhiṣiktaṁ rājānaṁ vadantaṁ kaimararājāya karadānaṁ niṣedhantaṁ rājyaviparyyayaṁ kurttuṁ pravarttamānam ena prāptā vayaṁ|
Nao wakaanza kumshtaki wakisema: “Tumemwona huyu mtu akipotosha taifa letu, akiwazuia watu wasilipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Kristo, mfalme.”
3 tadā pīlātastaṁ pṛṣṭavān tvaṁ kiṁ yihūdīyānāṁ rājā? sa pratyuvāca tvaṁ satyamuktavān|
Basi Pilato akamuuliza Yesu, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe wasema.”
4 tadā pīlātaḥ pradhānayājakādilokān jagād, ahametasya kamapyaparādhaṁ nāptavān|
Pilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”
5 tataste punaḥ sāhamino bhūtvāvadan, eṣa gālīla etatsthānaparyyante sarvvasmin yihūdādeśe sarvvāllokānupadiśya kupravṛttiṁ grāhītavān|
Lakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”
6 tadā pīlāto gālīlapradeśasya nāma śrutvā papraccha, kimayaṁ gālīlīyo lokaḥ?
Pilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?”
7 tataḥ sa gālīlpradeśīyaherodrājasya tadā sthitestasya samīpe yīśuṁ preṣayāmāsa|
Alipofahamu kwamba Yesu alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu.
8 tadā herod yīśuṁ vilokya santutoṣa, yataḥ sa tasya bahuvṛttāntaśravaṇāt tasya kiñicadāścaryyakarmma paśyati ityāśāṁ kṛtvā bahukālamārabhya taṁ draṣṭuṁ prayāsaṁ kṛtavān|
Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha.
9 tasmāt taṁ bahukathāḥ papraccha kintu sa tasya kasyāpi vākyasya pratyuttaraṁ novāca|
Herode akamuuliza maswali mengi, lakini Yesu hakumjibu lolote.
10 atha pradhānayājakā adhyāpakāśca prottiṣṭhantaḥ sāhasena tamapavadituṁ prārebhire|
Wakati huo viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwepo wakitoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
11 herod tasya senāgaṇaśca tamavajñāya upahāsatvena rājavastraṁ paridhāpya punaḥ pīlātaṁ prati taṁ prāhiṇot|
Herode na askari wake wakamdhihaki Yesu na kumfanyia mzaha. Wakamvika vazi zuri sana, wakamrudisha kwa Pilato.
12 pūrvvaṁ herodpīlātayoḥ parasparaṁ vairabhāva āsīt kintu taddine dvayo rmelanaṁ jātam|
Siku hiyo, Herode na Pilato wakawa marafiki; kabla ya jambo hili walikuwa na uadui kati yao.
13 paścāt pīlātaḥ pradhānayājakān śāsakān lokāṁśca yugapadāhūya babhāṣe,
Basi Pilato akawaita pamoja viongozi wa makuhani, viongozi wengine na watu,
14 rājyaviparyyayakārakoyam ityuktvā manuṣyamenaṁ mama nikaṭamānaiṣṭa kintu paśyata yuṣmākaṁ samakṣam asya vicāraṁ kṛtvāpi proktāpavādānurūpeṇāsya kopyaparādhaḥ sapramāṇo na jātaḥ,
akawaambia, “Ninyi mlimleta huyu mtu kwangu kana kwamba ni mtu anayewachochea watu ili waasi. Nimemhoji mbele yenu nami nimeona hakuna msingi wowote wa mashtaka yenu dhidi yake.
15 yūyañca herodaḥ sannidhau preṣitā mayā tatrāsya kopyaparādhastenāpi na prāptaḥ|paśyatānena vadhahetukaṁ kimapi nāparāddhaṁ|
Wala Herode hakumwona na kosa lolote, ndiyo sababu amemrudisha kwetu. Kama mnavyoona, mtu huyu hakufanya jambo lolote linalostahili kifo.
16 tasmādenaṁ tāḍayitvā vihāsyāmi|
Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi na kumwachia.” [
17 tatrotsave teṣāmeko mocayitavyaḥ|
Kwa kuwa ilikuwa lazima kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa Sikukuu.]
18 iti hetoste proccairekadā procuḥ, enaṁ dūrīkṛtya barabbānāmānaṁ mocaya|
Ndipo watu wote wakapiga kelele kwa pamoja, “Mwondoe mtu huyo! Tufungulie Baraba!”
19 sa barabbā nagara upaplavavadhāparādhābhyāṁ kārāyāṁ baddha āsīt|
(Baraba alikuwa amefungwa gerezani kwa sababu ya maasi yaliyokuwa yametokea mjini, na kwa ajili ya uuaji.)
20 kintu pīlāto yīśuṁ mocayituṁ vāñchan punastānuvāca|
Pilato, akitaka kumwachia Yesu, akasema nao tena.
21 tathāpyenaṁ kruśe vyadha kruśe vyadheti vadantaste ruruvuḥ|
Lakini wao wakaendelea kupiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!”
22 tataḥ sa tṛtīyavāraṁ jagāda kutaḥ? sa kiṁ karmma kṛtavān? nāhamasya kamapi vadhāparādhaṁ prāptaḥ kevalaṁ tāḍayitvāmuṁ tyajāmi|
Kwa mara ya tatu, Pilato akawauliza, “Kwani amefanya kosa gani huyu mtu? Sikuona kwake sababu yoyote inayostahili adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi, na kisha nitamwachia.”
23 tathāpi te punarenaṁ kruśe vyadha ityuktvā proccairdṛḍhaṁ prārthayāñcakrire;
Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu zaidi, wakidai kwamba Yesu asulubiwe. Hivyo, kelele zao zikashinda.
24 tataḥ pradhānayājakādīnāṁ kalarave prabale sati teṣāṁ prārthanārūpaṁ karttuṁ pīlāta ādideśa|
Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu kwamba madai yao yatimizwe.
25 rājadrohavadhayoraparādhena kārāsthaṁ yaṁ janaṁ te yayācire taṁ mocayitvā yīśuṁ teṣāmicchāyāṁ samārpayat|
Akamfungua yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika uasi dhidi ya serikali na mauaji. Akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfanyie watakavyo.
26 atha te yīśuṁ gṛhītvā yānti, etarhi grāmādāgataṁ śimonanāmānaṁ kurīṇīyaṁ janaṁ dhṛtvā yīśoḥ paścānnetuṁ tasya skandhe kruśamarpayāmāsuḥ|
Walipokuwa wakienda naye, wakamkamata mtu mmoja aitwaye Simoni mwenyeji wa Kirene, aliyekuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shambani. Wakambebesha msalaba, wakamlazimisha auchukue nyuma ya Yesu.
27 tato lokāraṇyamadhye bahustriyo rudatyo vilapantyaśca yīśoḥ paścād yayuḥ|
Idadi kubwa ya watu wakamfuata Yesu, wakiwamo wanawake waliokuwa wakimlilia na kumwombolezea.
28 kintu sa vyāghuṭya tā uvāca, he yirūśālamo nāryyo yuyaṁ madarthaṁ na ruditvā svārthaṁ svāpatyārthañca ruditi;
Yesu akawageukia, akawaambia, “Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi bali jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu.
29 paśyata yaḥ kadāpi garbhavatyo nābhavan stanyañca nāpāyayan tādṛśī rvandhyā yadā dhanyā vakṣyanti sa kāla āyāti|
Kwa maana wakati utafika mtakaposema, ‘Wamebarikiwa wanawake tasa, ambao matumbo yao hayakuzaa, wala matiti yao hayakunyonyesha!’
30 tadā he śailā asmākamupari patata, he upaśailā asmānācchādayata kathāmīdṛśīṁ lokā vakṣyanti|
Ndipo “‘wataiambia milima, “Tuangukieni!” na vilima, “Tufunikeni!”’
31 yataḥ satejasi śākhini cedetad ghaṭate tarhi śuṣkaśākhini kiṁ na ghaṭiṣyate?
Kwa maana kama wamefanya hivi kwa mti mbichi, kwa mti mkavu itakuwaje?”
32 tadā te hantuṁ dvāvaparādhinau tena sārddhaṁ ninyuḥ|
Watu wengine wawili wahalifu, walipelekwa pamoja na Yesu ili wakasulubiwe.
33 aparaṁ śiraḥkapālanāmakasthānaṁ prāpya taṁ kruśe vividhuḥ; taddvayoraparādhinorekaṁ tasya dakṣiṇo tadanyaṁ vāme kruśe vividhuḥ|
Walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, hapo ndipo walipomsulubisha Yesu pamoja na hao wahalifu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.
34 tadā yīśurakathayat, he pitaretān kṣamasva yata ete yat karmma kurvvanti tan na viduḥ; paścātte guṭikāpātaṁ kṛtvā tasya vastrāṇi vibhajya jagṛhuḥ|
Yesu akasema, “Baba, wasamehe, kwa maana hawajui walitendalo!” Wakagawana nguo zake kwa kupiga kura.
35 tatra lokasaṁghastiṣṭhan dadarśa; te teṣāṁ śāsakāśca tamupahasya jagaduḥ, eṣa itarān rakṣitavān yadīśvareṇābhirucito 'bhiṣiktastrātā bhavati tarhi svamadhunā rakṣatu|
Watu wakasimama hapo wakimwangalia, nao viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.”
36 tadanyaḥ senāgaṇā etya tasmai amlarasaṁ datvā parihasya provāca,
Askari nao wakaja, wakamdhihaki. Wakamletea siki ili anywe,
37 cettvaṁ yihūdīyānāṁ rājāsi tarhi svaṁ rakṣa|
na wakamwambia, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
38 yihūdīyānāṁ rājeti vākyaṁ yūnānīyaromīyebrīyākṣarai rlikhitaṁ tacchirasa ūrddhve'sthāpyata|
Kwenye msalaba juu ya kichwa chake, kulikuwa na maandishi haya: Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi. Maandishi haya yalikuwa yameandikwa kwa lugha za Kiyunani, Kilatini na Kiebrania.
39 tadobhayapārśvayo rviddhau yāvaparādhinau tayorekastaṁ vinindya babhāṣe, cettvam abhiṣiktosi tarhi svamāvāñca rakṣa|
Mmoja wa wale wahalifu waliosulubiwa pamoja naye akamtukana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe mwenyewe na utuokoe na sisi.”
40 kintvanyastaṁ tarjayitvāvadat, īśvarāttava kiñcidapi bhayaṁ nāsti kiṁ? tvamapi samānadaṇḍosi,
Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akasema, “Je, wewe humwogopi Mungu, wakati uko kwenye adhabu iyo hiyo?
41 yogyapātre āvāṁ svasvakarmmaṇāṁ samucitaphalaṁ prāpnuvaḥ kintvanena kimapi nāparāddhaṁ|
Sisi tumehukumiwa kwa haki kwa kuwa tunapata tunayostahili kwa ajili ya matendo yetu. Lakini huyu mtu hajafanya kosa lolote.”
42 atha sa yīśuṁ jagāda he prabhe bhavān svarājyapraveśakāle māṁ smaratu|
Kisha akasema, “Yesu, unikumbuke utakapokuja katika Ufalme wako.”
43 tadā yīśuḥ kathitavān tvāṁ yathārthaṁ vadāmi tvamadyaiva mayā sārddhaṁ paralokasya sukhasthānaṁ prāpsyasi|
Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
44 aparañca dvitīyayāmāt tṛtīyayāmaparyyantaṁ ravestejasontarhitatvāt sarvvadeśo'ndhakāreṇāvṛto
Ilikuwa kama saa sita mchana, nalo giza likafunika nchi yote hadi saa tisa,
45 mandirasya yavanikā ca chidyamānā dvidhā babhūva|
kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili.
46 tato yīśuruccairuvāca, he pita rmamātmānaṁ tava kare samarpaye, ityuktvā sa prāṇān jahau|
Yesu akapaza sauti yake akasema, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.
47 tadaitā ghaṭanā dṛṣṭvā śatasenāpatirīśvaraṁ dhanyamuktvā kathitavān ayaṁ nitāntaṁ sādhumanuṣya āsīt|
Yule jemadari alipoona yaliyotukia, akamsifu Mungu, akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.”
48 atha yāvanto lokā draṣṭum āgatāste tā ghaṭanā dṛṣṭvā vakṣaḥsu karāghātaṁ kṛtvā vyācuṭya gatāḥ|
Watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hili walipoyaona hayo, wakapigapiga vifua vyao kwa huzuni na kwenda zao.
49 yīśo rjñātayo yā yā yoṣitaśca gālīlastena sārddhamāyātāstā api dūre sthitvā tat sarvvaṁ dadṛśuḥ|
Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wale wanawake waliokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyatazama mambo haya.
50 tadā yihūdīyānāṁ mantraṇāṁ kriyāñcāsammanyamāna īśvarasya rājatvam apekṣamāṇo
Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,
51 yihūdideśīyo 'rimathīyanagarīyo yūṣaphnāmā mantrī bhadro dhārmmikaśca pumān
lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa.
52 pīlātāntikaṁ gatvā yīśo rdehaṁ yayāce|
Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
53 paścād vapuravarohya vāsasā saṁveṣṭya yatra kopi mānuṣo nāsthāpyata tasmin śaile svāte śmaśāne tadasthāpayat|
Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado.
54 taddinamāyojanīyaṁ dinaṁ viśrāmavāraśca samīpaḥ|
Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.
55 aparaṁ yīśunā sārddhaṁ gālīla āgatā yoṣitaḥ paścāditvā śmaśāne tatra yathā vapuḥ sthāpitaṁ tacca dṛṣṭvā
Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yosefu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa.
56 vyāghuṭya sugandhidravyatailāni kṛtvā vidhivad viśrāmavāre viśrāmaṁ cakruḥ|
Kisha wakarudi nyumbani, wakaandaa manukato na marhamu ya kuupaka huo mwili. Lakini wakapumzika siku ya Sabato kama ilivyoamriwa.