< mathiH 27 >

1 prabhAte jAte pradhAnayAjakalokaprAcInA yIzuM hantuM tatpratikUlaM mantrayitvA
Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri pamoja dhidi ya Yesu ili kumuua.
2 taM badvvA nItvA pantIyapIlAtAkhyAdhipe samarpayAmAsuH|
Wakamfunga, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato, ambaye alikuwa mtawala wa Kirumi.
3 tato yIzoH parakarevvarpayitA yihUdAstatprANAdaNDAjJAM viditvA santaptamanAH pradhAnayAjakalokaprAcInAnAM samakSaM tAstrIMzanmudrAH pratidAyAvAdIt,
Yuda, ambaye alikuwa amemsaliti Yesu, alipoona kuwa Yesu amehukumiwa, akajuta na akarudisha vile vipande thelathini vya fedha alivyopewa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.
4 etannirAgonaraprANaparakarArpaNAt kaluSaM kRtavAnahaM| tadA ta uditavantaH, tenAsmAkaM kiM? tvayA tad budhyatAm|
Akasema, “Nimetenda dhambi, kwa maana nimeisaliti damu isiyo na hatia.” Wakamjibu, “Hilo latuhusu nini sisi? Ni shauri yako.”
5 tato yihUdA mandiramadhye tA mudrA nikSipya prasthitavAn itvA ca svayamAtmAnamudbabandha|
Basi Yuda akavitupa vile vipande vya fedha ndani ya Hekalu akaondoka akaenda kujinyonga.
6 pazcAt pradhAnayAjakAstA mudrA AdAya kathitavantaH, etA mudrAH zoNitamUlyaM tasmAd bhANDAgAre na nidhAtavyAH|
Wale viongozi wa makuhani wakazichukua zile fedha wakasema, “Si halali kuchanganya fedha hizi na sadaka kwa sababu hizi ni fedha zenye damu.”
7 anantaraM te mantrayitvA videzinAM zmazAnasthAnAya tAbhiH kulAlasya kSetramakrINan|
Kwa hiyo baada ya kushauriana, waliamua kuzitumia kununulia shamba la mfinyanzi, liwe mahali pa kuzikia wageni.
8 ato'dyApi tatsthAnaM raktakSetraM vadanti|
Hii ndiyo sababu lile shamba likaitwa Shamba la Damu hadi leo.
9 itthaM sati isrAyelIyasantAnai ryasya mUlyaM nirupitaM, tasya triMzanmudrAmAnaM mUlyaM
Ndipo likatimia lile lililonenwa na nabii Yeremia, kwamba, “Walichukua vile vipande thelathini vya fedha, thamani aliyopangiwa na watu wa Israeli,
10 mAM prati paramezvarasyAdezAt tebhya AdIyata, tena ca kulAlasya kSetraM krItamiti yadvacanaM yirimiyabhaviSyadvAdinA proktaM tat tadAsidhyat|
wakanunulia shamba la mfinyanzi, kama vile Bwana alivyoniagiza.”
11 anantaraM yIzau tadadhipateH sammukha upatiSThati sa taM papraccha, tvaM kiM yihUdIyAnAM rAjA? tadA yIzustamavadat, tvaM satyamuktavAn|
Wakati huo Yesu akiwa amesimama mbele ya mtawala, mtawala akamuuliza, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akasema, “Wewe wasema hivyo.”
12 kintu pradhAnayAjakaprAcInairabhiyuktena tena kimapi na pratyavAdi|
Lakini viongozi wa makuhani na wazee walipomshtaki, hakujibu neno.
13 tataH pIlAtena sa uditaH, ime tvatpratikUlataH kati kati sAkSyaM dadati, tat tvaM na zRNoSi?
Ndipo Pilato akamuuliza, “Je, husikii ni mambo mangapi wanayokushtaki nayo?”
14 tathApi sa teSAmekasyApi vacasa uttaraM noditavAn; tena so'dhipati rmahAcitraM vidAmAsa|
Lakini Yesu hakumjibu hata kwa shtaka moja, kiasi kwamba mtawala alishangaa sana.
15 anyacca tanmahakAle'dhipateretAdRzI rAtirAsIt, prajA yaM kaJcana bandhinaM yAcante, tameva sa mocayatIti|
Basi ilikuwa ni desturi ya mtawala kumfungua mfungwa mmoja aliyechaguliwa na umati wa watu wakati wa sikukuu.
16 tadAnIM barabbAnAmA kazcit khyAtabandhyAsIt|
Wakati huo alikuwepo mfungwa mmoja mwenye sifa mbaya, aliyeitwa Baraba.
17 tataH pIlAtastatra militAn lokAn apRcchat, eSa barabbA bandhI khrISTavikhyAto yIzuzcaitayoH kaM mocayiSyAmi? yuSmAkaM kimIpsitaM?
Hivyo umati wa watu walipokusanyika, Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie nani, Baraba au Yesu yeye aitwaye Kristo?”
18 tairIrSyayA sa samarpita iti sa jJAtavAn|
Kwa kuwa alitambua Yesu alikuwa amekabidhiwa kwake kwa ajili ya wivu.
19 aparaM vicArAsanopavezanakAle pIlAtasya patnI bhRtyaM prahitya tasmai kathayAmAsa, taM dhArmmikamanujaM prati tvayA kimapi na karttavyaM; yasmAt tatkRte'dyAhaM svapne prabhUtakaSTamalabhe|
Pilato akiwa ameketi kwenye kiti cha hukumu, mkewe akampelekea ujumbe huu: “Usiwe na jambo lolote juu ya mtu huyu asiye na hatia, kwa kuwa leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake.”
20 anantaraM pradhAnayAjakaprAcInA barabbAM yAcitvAdAtuM yIzuJca hantuM sakalalokAn prAvarttayan|
Lakini viongozi wa makuhani na wazee wakaushawishi ule umati wa watu kwamba waombe Baraba afunguliwe, naye Yesu auawe.
21 tato'dhipatistAn pRSTavAn, etayoH kamahaM mocayiSyAmi? yuSmAkaM kecchA? te procu rbarabbAM|
Mtawala akawauliza tena, “Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka niwafungulie?” Wakajibu, “Baraba.”
22 tadA pIlAtaH papraccha, tarhi yaM khrISTaM vadanti, taM yIzuM kiM kariSyAmi? sarvve kathayAmAsuH, sa kruzena vidhyatAM|
Pilato akawaambia, “Basi nifanye nini na huyu Yesu aitwaye Kristo?” Wakajibu wote, “Msulubishe!”
23 tato'dhipatiravAdIt, kutaH? kiM tenAparAddhaM? kintu te punarucai rjagaduH, sa kruzena vidhyatAM|
Pilato akauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakazidi kupiga kelele, wakisema, “Msulubishe!”
24 tadA nijavAkyamagrAhyamabhUt, kalahazcApyabhUt, pIlAta iti vilokya lokAnAM samakSaM toyamAdAya karau prakSAlyAvocat, etasya dhArmmikamanuSyasya zoNitapAte nirdoSo'haM, yuSmAbhireva tad budhyatAM|
Pilato alipoona kwamba hawezi kufanya lolote, lakini badala yake ghasia zilikuwa zinaanza, akachukua maji, akanawa mikono yake mbele ya ule umati wa watu, akasema, “Sina hatia juu ya damu ya mtu huyu, hili ni jukumu lenu!”
25 tadA sarvvAH prajAH pratyavocan, tasya zoNitapAtAparAdho'smAkam asmatsantAnAnAJcopari bhavatu|
Watu wote wakajibu, “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!”
26 tataH sa teSAM samIpe barabbAM mocayAmAsa yIzuntu kaSAbhirAhatya kruzena vedhituM samarpayAmAsa|
Basi akawafungulia Baraba. Lakini baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
27 anantaram adhipateH senA adhipate rgRhaM yIzumAnIya tasya samIpe senAsamUhaM saMjagRhuH|
Kisha askari wa mtawala wakampeleka Yesu kwenye Praitorio na wakakusanya kikosi kizima cha askari kumzunguka.
28 tataste tasya vasanaM mocayitvA kRSNalohitavarNavasanaM paridhApayAmAsuH
Wakamvua nguo zake na kumvika vazi la rangi nyekundu, kisha
29 kaNTakAnAM mukuTaM nirmmAya tacchirasi daduH, tasya dakSiNakare vetramekaM dattvA tasya sammukhe jAnUni pAtayitvA, he yihUdIyAnAM rAjan, tubhyaM nama ityuktvA taM tirazcakruH,
wakasokota taji ya miiba, wakaiweka kichwani pake. Wakamwekea fimbo katika mkono wake wa kuume, na wakapiga magoti mbele zake na kumdhihaki, wakisema, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
30 tatastasya gAtre niSThIvaM datvA tena vetreNa zira AjaghnuH|
Wakamtemea mate, wakachukua ile fimbo wakampiga kichwani tena na tena.
31 itthaM taM tiraskRtya tad vasanaM mocayitvA punarnijavasanaM paridhApayAJcakruH, taM kruzena vedhituM nItavantaH|
Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakampeleka ili wakamsulubishe.
32 pazcAtte bahirbhUya kurINIyaM zimonnAmakamekaM vilokya kruzaM voDhuM tamAdadire|
Walipokuwa wakienda, wakakutana na mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
33 anantaraM gulgaltAm arthAt ziraskapAlanAmakasthAnamu pasthAya te yIzave pittamizritAmlarasaM pAtuM daduH,
Wakafika mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
34 kintu sa tamAsvAdya na papau|
Hapo wakampa Yesu divai iliyochanganywa na nyongo ili anywe; lakini alipoionja, akakataa kuinywa.
35 tadAnIM te taM kruzena saMvidhya tasya vasanAni guTikApAtena vibhajya jagRhuH, tasmAt, vibhajante'dharIyaM me te manuSyAH parasparaM| maduttarIyavastrArthaM guTikAM pAtayanti ca||yadetadvacanaM bhaviSyadvAdibhiruktamAsIt, tadA tad asidhyat,
Walipokwisha kumsulubisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura. [Hili lilifanyika ili litimie lile neno lililonenwa na nabii, “Waligawa nguo zangu miongoni mwao na vazi langu wakalipigia kura.”]
36 pazcAt te tatropavizya tadrakSaNakarvvaNi niyuktAstasthuH|
Kisha wakaketi, wakamchunga.
37 aparam eSa yihUdIyAnAM rAjA yIzurityapavAdalipipatraM tacchirasa Urdvve yojayAmAsuH|
Juu ya kichwa chake, kwenye msalaba, wakaandika shtaka lake hivi: Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi.
38 tatastasya vAme dakSiNe ca dvau cairau tena sAkaM kruzena vividhuH|
Wanyangʼanyi wawili walisulubiwa pamoja naye, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto.
39 tadA pAnthA nijaziro lADayitvA taM nindanto jagaduH,
Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao
40 he IzvaramandirabhaJjaka dinatraye tannirmmAtaH svaM rakSa, cettvamIzvarasutastarhi kruzAdavaroha|
na kusema, “Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu, jiokoe mwenyewe basi! Kama wewe ni Mwana wa Mungu, shuka kutoka msalabani.”
41 pradhAnayAjakAdhyApakaprAcInAzca tathA tiraskRtya jagaduH,
Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria pamoja na wazee wakamdhihaki wakisema,
42 so'nyajanAnAvat, kintu svamavituM na zaknoti| yadIsrAyelo rAjA bhavet, tarhIdAnImeva kruzAdavarohatu, tena taM vayaM pratyeSyAmaH|
“Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe! Yeye ni Mfalme wa Israeli! Ashuke sasa kutoka msalabani, nasi tutamwamini.
43 sa Izvare pratyAzAmakarot, yadIzvarastasmin santuSTastarhIdAnImeva tamavet, yataH sa uktavAn ahamIzvarasutaH|
Anamwamini Mungu, basi Mungu na amwokoe sasa kama anamtaka, kwa maana alisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu.’”
44 yau stenau sAkaM tena kruzena viddhau tau tadvadeva taM ninindatuH|
Hata wale wanyangʼanyi waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana vivyo hivyo.
45 tadA dvitIyayAmAt tRtIyayAmaM yAvat sarvvadeze tamiraM babhUva,
Tangu saa sita hadi saa tisa giza liliifunika nchi yote.
46 tRtIyayAme "elI elI lAmA zivaktanI", arthAt madIzvara madIzvara kuto mAmatyAkSIH? yIzuruccairiti jagAda|
Ilipofika saa tisa, Yesu akapaza sauti akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
47 tadA tatra sthitAH kecit tat zrutvA babhASire, ayam eliyamAhUyati|
Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama pale waliposikia hayo, wakasema, “Anamwita Eliya.”
48 teSAM madhyAd ekaH zIghraM gatvA spaJjaM gRhItvA tatrAmlarasaM dattvA nalena pAtuM tasmai dadau|
Ghafula mmoja wao akaenda mbio na kuleta sifongo, akaichovya kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe.
49 itare'kathayan tiSThata, taM rakSitum eliya AyAti naveti pazyAmaH|
Wengine wakasema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”
50 yIzuH punarucairAhUya prANAn jahau|
Yesu alipolia tena kwa sauti kuu, akaitoa roho yake.
51 tato mandirasya vicchedavasanam UrdvvAdadho yAvat chidyamAnaM dvidhAbhavat,
Wakati huo huo pazia la Hekalu likachanika vipande viwili, kuanzia juu hadi chini. Dunia ikatetemeka na miamba ikapasuka.
52 bhUmizcakampe bhUdharovyadIryyata ca| zmazAne mukte bhUripuNyavatAM suptadehA udatiSThan,
Makaburi yakafunguka na miili ya watakatifu waliokuwa wamekufa ikafufuliwa.
53 zmazAnAd vahirbhUya tadutthAnAt paraM puNyapuraM gatvA bahujanAn darzayAmAsuH|
Wakatoka makaburini, na baada ya Yesu kufufuka, waliingia kwenye Mji Mtakatifu na kuwatokea watu wengi.
54 yIzurakSaNAya niyuktaH zatasenApatistatsaGginazca tAdRzIM bhUkampAdighaTanAM dRSTvA bhItA avadan, eSa Izvaraputro bhavati|
Basi yule jemadari na wale waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu walipoona lile tetemeko na yale yote yaliyokuwa yametukia, waliogopa, wakasema, “Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
55 yA bahuyoSito yIzuM sevamAnA gAlIlastatpazcAdAgatAstAsAM madhye
Walikuwako wanawake huko wakiangalia kwa mbali. Hawa walikuwa wamemfuata Yesu tangu Galilaya ili kushughulikia mahitaji yake.
56 magdalInI mariyam yAkUbyozyo rmAtA yA mariyam sibadiyaputrayo rmAtA ca yoSita etA dUre tiSThantyo dadRzuH|
Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo na Yosefu, na mama yao wana wa Zebedayo.
57 sandhyAyAM satyam arimathiyAnagarasya yUSaphnAmA dhanI manujo yIzoH ziSyatvAt
Ilipofika jioni, alifika mtu mmoja tajiri kutoka Arimathaya aitwaye Yosefu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
58 pIlAtasya samIpaM gatvA yIzoH kAyaM yayAce, tena pIlAtaH kAyaM dAtum Adideza|
Akamwendea Pilato ili kumwomba mwili wa Yesu. Pilato akaamuru apewe.
59 yUSaph tatkAyaM nItvA zucivastreNAcchAdya
Yosefu akauchukua mwili wa Yesu, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi,
60 svArthaM zaile yat zmazAnaM cakhAna, tanmadhye tatkAyaM nidhAya tasya dvAri vRhatpASANaM dadau|
na kuuweka katika kaburi lake mwenyewe jipya, alilokuwa amelichonga kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa katika ingilio la kaburi, akaenda zake.
61 kintu magdalInI mariyam anyamariyam ete striyau tatra zmazAnasammukha upavivizatuH|
Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwepo mahali pale, wakiwa wameketi mkabala na kaburi.
62 tadanantaraM nistArotsavasyAyojanadinAt pare'hani pradhAnayAjakAH phirUzinazca militvA pIlAtamupAgatyAkathayan,
Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalizi ya Sabato, viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakamwendea Pilato
63 he maheccha sa pratArako jIvana akathayat, dinatrayAt paraM zmazAnAdutthAsyAmi tadvAkyaM smarAmo vayaM;
na kusema, “Bwana, tumekumbuka kwamba yule mdanganyifu wakati alikuwa bado hai alisema, ‘Baada ya siku tatu nitafufuka.’
64 tasmAt tRtIyadinaM yAvat tat zmazAnaM rakSitumAdizatu, nocet tacchiSyA yAminyAmAgatya taM hRtvA lokAn vadiSyanti, sa zmazAnAdudatiSThat, tathA sati prathamabhrAnteH zeSIyabhrAnti rmahatI bhaviSyati|
Kwa hiyo uamuru kaburi lilindwe kwa uthabiti mpaka baada ya siku tatu. La sivyo, wanafunzi wake wanaweza kuja kuuiba mwili wake na kuwaambia watu kwamba amefufuliwa kutoka kwa wafu. Udanganyifu huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa kwanza.”
65 tadA pIlAta avAdIt, yuSmAkaM samIpe rakSigaNa Aste, yUyaM gatvA yathA sAdhyaM rakSayata|
Pilato akawaambia, “Ninyi mnao askari walinzi. Nendeni, liwekeeni ulinzi kadri mwezavyo.”
66 tataste gatvA taddUrapASANaM mudrAGkitaM kRtvA rakSigaNaM niyojya zmazAnaM rakSayAmAsuH|
Kwa hiyo wakaenda na walinzi ili kulilinda kaburi kwa uthabiti, wakatia muhuri kwenye lile jiwe na kuweka ulinzi.

< mathiH 27 >