< philipinaH 3 >

1 hE bhrAtaraH, zESE vadAmi yUyaM prabhAvAnandata| punaH punarEkasya vacO lEkhanaM mama klEzadaM nahi yuSmadarthanjca bhramanAzakaM bhavati|
Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana! Mimi kuwaandikia mambo yale yale hakuniudhi, kwa maana ni kinga kwa ajili yenu.
2 yUyaM kukkurEbhyaH sAvadhAnA bhavata duSkarmmakAribhyaH sAvadhAnA bhavata chinnamUlEbhyO lOkEbhyazca sAvadhAnA bhavata|
Jihadharini na mbwa, wale watenda maovu, jihadharini na wale wajikatao miili yao, wasemao ili kuokoka ni lazima kutahiriwa.
3 vayamEva chinnatvacO lOkA yatO vayam AtmanEzvaraM sEvAmahE khrISTEna yIzunA zlAghAmahE zarIrENa ca pragalbhatAM na kurvvAmahE|
Kwa maana sisi ndio tulio tohara, sisi tumwabuduo Mungu katika Roho, tunaona fahari katika Kristo Yesu, ambao hatuweki tumaini letu katika mwili,
4 kintu zarIrE mama pragalbhatAyAH kAraNaM vidyatE, kazcid yadi zarIrENa pragalbhatAM cikIrSati tarhi tasmAd api mama pragalbhatAyA gurutaraM kAraNaM vidyatE|
ingawa mimi mwenyewe ninazo sababu za kuutumainia mwili. Kama mtu yeyote akidhani anazo sababu za kuutumainia mwili, mimi zaidi.
5 yatO'ham aSTamadivasE tvakchEdaprApta isrAyElvaMzIyO binyAmInagOSThIya ibrikulajAta ibriyO vyavasthAcaraNE phirUzI
Nilitahiriwa siku ya nane, mimi ni Mwisraeli wa kabila la Benyamini, Mwebrania wa Waebrania. Kwa habari ya sheria, ni Farisayo,
6 dharmmOtsAhakAraNAt samitErupadravakArI vyavasthAtO labhyE puNyE cAnindanIyaH|
kwa habari ya juhudi, nilikuwa nalitesa kanisa, kuhusu haki ipatikanayo kwa sheria, mimi nilikuwa sina hatia.
7 kintu mama yadyat labhyam AsIt tat sarvvam ahaM khrISTasyAnurOdhAt kSatim amanyE|
Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, sasa nayahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.
8 kinjcAdhunApyahaM matprabhOH khrISTasya yIzO rjnjAnasyOtkRSTatAM buddhvA tat sarvvaM kSatiM manyE|
Zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara tupu nikiyalinganisha na faida kubwa ipitayo kiasi cha kumjua Kristo Yesu Bwana wangu, ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote, nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nimpate Kristo.
9 yatO hEtOrahaM yat khrISTaM labhEya vyavasthAtO jAtaM svakIyapuNyanjca na dhArayan kintu khrISTE vizvasanAt labhyaM yat puNyam IzvarENa vizvAsaM dRSTvA dIyatE tadEva dhArayan yat khrISTE vidyEya tadarthaM tasyAnurOdhAt sarvvESAM kSatiM svIkRtya tAni sarvvANyavakarAniva manyE|
Nami nionekane mbele zake bila kuwa na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu kwa njia ya imani.
10 yatO hEtOrahaM khrISTaM tasya punarutthitE rguNaM tasya duHkhAnAM bhAgitvanjca jnjAtvA tasya mRtyOrAkRtinjca gRhItvA
Nataka nimjue Kristo na uweza wa kufufuka kwake na ushirika wa mateso yake, ili nifanane naye katika mauti yake,
11 yEna kEnacit prakArENa mRtAnAM punarutthitiM prAptuM yatE|
ili kwa njia yoyote niweze kufikia ufufuo wa wafu.
12 mayA tat sarvvam adhunA prApi siddhatA vAlambhi tannahi kintu yadartham ahaM khrISTEna dhAritastad dhArayituM dhAvAmi|
Si kwamba nimekwisha kufikia, au kwamba nimekwisha kuwa mkamilifu, la hasha! Bali nakaza mwendo ili nipate kile ambacho kwa ajili yake, nimeshikwa na Kristo Yesu.
13 hE bhrAtaraH, mayA tad dhAritam iti na manyatE kintvEtadaikamAtraM vadAmi yAni pazcAt sthitAni tAni vismRtyAham agrasthitAnyuddizya
Ndugu zangu, sijihesabu kuwa nimekwisha kushika. Lakini ninafanya jambo moja: Ninasahau mambo yale yaliyopita, nakaza mwendo kufikia yale yaliyo mbele.
14 pUrNayatnEna lakSyaM prati dhAvan khrISTayIzunOrddhvAt mAm Ahvayata IzvarAt jEtRpaNaM prAptuM cESTE|
Nakaza mwendo nifikie ile alama ya ushindi iliyowekwa ili nipate tuzo ya mwito mkuu wa Mungu ambao nimeitiwa huko juu mbinguni katika Kristo Yesu.
15 asmAkaM madhyE yE siddhAstaiH sarvvaistadEva bhAvyatAM, yadi ca kanjcana viSayam adhi yuSmAkam aparO bhAvO bhavati tarhIzvarastamapi yuSmAkaM prati prakAzayiSyati|
Hivyo sisi sote tuliokuwa kiroho tuwaze jambo hili, hata mkiwaza mengine katika jambo lolote, Mungu ataliweka wazi hilo nalo.
16 kintu vayaM yadyad avagatA AsmastatrAsmAbhirEkO vidhirAcaritavya EkabhAvai rbhavitavyanjca|
Lakini na tushike sana lile ambalo tumekwisha kulifikia.
17 hE bhrAtaraH, yUyaM mamAnugAminO bhavata vayanjca yAdRgAcaraNasya nidarzanasvarUpA bhavAmastAdRgAcAriNO lOkAn AlOkayadhvaM|
Ndugu zangu, kwa pamoja fuateni mfano wangu na kuwatazama wale wanaofuata kielelezo tulichowawekea.
18 yatO'nEkE vipathE caranti tE ca khrISTasya kruzasya zatrava iti purA mayA punaH punaH kathitam adhunApi rudatA mayA kathyatE|
Kwa maana, kama nilivyokwisha kuwaambia mara nyingi kabla, nami sasa nasema tena hata kwa machozi, watu wengi wanaishi kama adui wa msalaba wa Kristo.
19 tESAM zESadazA sarvvanAza udarazcEzvarO lajjA ca zlAghA pRthivyAnjca lagnaM manaH|
Mwisho wa watu hao ni maangamizi, Mungu wao ni tumbo, na utukufu wao ni aibu, na mawazo yao yamo katika mambo ya dunia.
20 kintvasmAkaM janapadaH svargE vidyatE tasmAccAgamiSyantaM trAtAraM prabhuM yIzukhrISTaM vayaM pratIkSAmahE|
Lakini uenyeji wetu uko mbinguni. Nasi tunamngoja kwa shauku Mwokozi kutoka huko, yaani, Bwana Yesu Kristo,
21 sa ca yayA zaktyA sarvvANyEva svasya vazIkarttuM pArayati tayAsmAkam adhamaM zarIraM rUpAntarIkRtya svakIyatEjOmayazarIrasya samAkAraM kariSyati|
atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, ili upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote chini yake.

< philipinaH 3 >