+ mathiH 1 >
1 ibrAhImaH santAnO dAyUd tasya santAnO yIzukhrISTastasya pUrvvapuruSavaMzazrENI|
Habari za ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Abrahamu:
2 ibrAhImaH putra ishAk tasya putrO yAkUb tasya putrO yihUdAstasya bhrAtarazca|
Abrahamu akamzaa Isaki, Isaki akamzaa Yakobo, Yakobo akawazaa Yuda na ndugu zake,
3 tasmAd yihUdAtastAmarO garbhE pErassErahau jajnjAtE, tasya pErasaH putrO hiSrON tasya putrO 'rAm|
Yuda akawazaa Peresi na Zera, ambao mama yao alikuwa Tamari, Peresi akamzaa Hesroni, Hesroni akamzaa Aramu,
4 tasya putrO 'mmInAdab tasya putrO nahazOn tasya putraH salmOn|
Aramu akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
5 tasmAd rAhabO garbhE bOyam jajnjE, tasmAd rUtO garbhE ObEd jajnjE, tasya putrO yizayaH|
Salmoni akamzaa Boazi, na mama yake Boazi alikuwa Rahabu, Boazi akamzaa Obedi, ambaye mama yake alikuwa Ruthu, Obedi akamzaa Yese,
6 tasya putrO dAyUd rAjaH tasmAd mRtOriyasya jAyAyAM sulEmAn jajnjE|
Yese akamzaa Daudi ambaye alikuwa mfalme. Daudi akamzaa Solomoni, ambaye mama yake ni yule aliyekuwa mke wa Uria.
7 tasya putrO rihabiyAm, tasya putrO'biyaH, tasya putra AsA: |
Solomoni akamzaa Rehoboamu, Rehoboamu akamzaa Abiya, Abiya akamzaa Asa,
8 tasya sutO yihOzAphaT tasya sutO yihOrAma tasya suta uSiyaH|
Asa akamzaa Yehoshafati, Yehoshafati akamzaa Yoramu, Yoramu akamzaa Uzia,
9 tasya sutO yOtham tasya suta Aham tasya sutO hiSkiyaH|
Uzia akamzaa Yothamu, Yothamu akamzaa Ahazi, Ahazi akamzaa Hezekia,
10 tasya sutO minaziH, tasya suta AmOn tasya sutO yOziyaH|
Hezekia akamzaa Manase, Manase akamzaa Amoni, Amoni akamzaa Yosia,
11 bAbilnagarE pravasanAt pUrvvaM sa yOziyO yikhaniyaM tasya bhrAtRMzca janayAmAsa|
wakati wa uhamisho wa Babeli, Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake.
12 tatO bAbili pravasanakAlE yikhaniyaH zaltIyElaM janayAmAsa, tasya sutaH sirubbAvil|
Baada ya uhamisho wa Babeli: Yekonia alimzaa Shealtieli, Shealtieli akamzaa Zerubabeli,
13 tasya sutO 'bOhud tasya suta ilIyAkIm tasya sutO'sOr|
Zerubabeli akamzaa Abiudi, Abiudi akamzaa Eliakimu, Eliakimu akamzaa Azori,
14 asOraH sutaH sAdOk tasya suta AkhIm tasya suta ilIhUd|
Azori akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Akimu, Akimu akamzaa Eliudi,
15 tasya suta iliyAsar tasya sutO mattan|
Eliudi akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Matani, Matani akamzaa Yakobo,
16 tasya sutO yAkUb tasya sutO yUSaph tasya jAyA mariyam; tasya garbhE yIzurajani, tamEva khrISTam (arthAd abhiSiktaM) vadanti|
naye Yakobo akamzaa Yosefu ambaye alikuwa mumewe Maria, mama yake Yesu, aitwaye Kristo.
17 ittham ibrAhImO dAyUdaM yAvat sAkalyEna caturdazapuruSAH; A dAyUdaH kAlAd bAbili pravasanakAlaM yAvat caturdazapuruSA bhavanti| bAbili pravAsanakAlAt khrISTasya kAlaM yAvat caturdazapuruSA bhavanti|
Hivyo, kulikuwepo na jumla ya vizazi kumi na vinne tangu Abrahamu mpaka Daudi, vizazi kumi na vinne tangu Daudi hadi wakati wa uhamisho kwenda utumwani Babeli, na vizazi kumi na vinne tangu wakati wa uhamisho kwenda utumwani Babeli hadi Kristo.
18 yIzukhrISTasya janma kaththatE| mariyam nAmikA kanyA yUSaphE vAgdattAsIt, tadA tayOH saggamAt prAk sA kanyA pavitrENAtmanA garbhavatI babhUva|
Basi Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi: Maria mama yake alikuwa ameposwa na Yosefu, lakini kabla hawajakutana kimwili, Maria alionekana kuwa na mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
19 tatra tasyAH pati ryUSaph saujanyAt tasyAH kalaggaM prakAzayitum anicchan gOpanEnE tAM pArityaktuM manazcakrE|
Kwa kuwa Yosefu, mwanaume aliyekuwa amemposa alikuwa mtu mwadilifu, hakutaka kumwaibisha Maria hadharani, aliazimu kumwacha kwa siri.
20 sa tathaiva bhAvayati, tadAnIM paramEzvarasya dUtaH svapnE taM darzanaM dattvA vyAjahAra, hE dAyUdaH santAna yUSaph tvaM nijAM jAyAM mariyamam AdAtuM mA bhaiSIH|
Lakini mara alipoazimu kufanya jambo hili, malaika wa Bwana akamtokea katika ndoto na kusema, “Yosefu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria awe mke wako, kwa maana mimba aliyo nayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
21 yatastasyA garbhaH pavitrAdAtmanO'bhavat, sA ca putraM prasaviSyatE, tadA tvaM tasya nAma yIzum (arthAt trAtAraM) karISyasE, yasmAt sa nijamanujAn tESAM kaluSEbhya uddhariSyati|
Naye atamzaa mwana, nawe utamwita Jina lake Yesu, kwa maana yeye ndiye atakayewaokoa watu wake kutoka dhambi zao.”
22 itthaM sati, pazya garbhavatI kanyA tanayaM prasaviSyatE| immAnUyEl tadIyanjca nAmadhEyaM bhaviSyati|| immAnUyEl asmAkaM saggIzvaraityarthaH|
Haya yote yalitukia ili litimie lile Bwana alilokuwa amenena kupitia nabii, akisema:
23 iti yad vacanaM purvvaM bhaviSyadvaktrA IzvaraH kathAyAmAsa, tat tadAnIM siddhamabhavat|
“Tazama, bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, nao watamwita Jina lake Imanueli”: maana yake, “Mungu pamoja nasi.”
24 anantaraM yUSaph nidrAtO jAgarita utthAya paramEzvarIyadUtasya nidEzAnusArENa nijAM jAyAM jagrAha,
Yosefu alipoamka kutoka usingizini, akafanya kama vile alivyoagizwa na malaika wa Bwana, akamchukua Maria kuwa mke wake.
25 kintu yAvat sA nijaM prathamasutaM a suSuvE, tAvat tAM nOpAgacchat, tataH sutasya nAma yIzuM cakrE|
Lakini hawakukutana kimwili mpaka Maria alipojifungua mwanawe kifungua mimba akamwita Jina lake Yesu.