< mArkaH 3 >
1 anantaraM yIzuH puna rbhajanagRhaM praviSTastasmin sthAnE zuSkahasta EkO mAnava AsIt|
Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na huko palikuwa na mtu aliyepooza mkono.
2 sa vizrAmavArE tamarOgiNaM kariSyati navEtyatra bahavastam apavadituM chidramapEkSitavantaH|
Wakawa wanamwangalia waone kama atamponya siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki.
3 tadA sa taM zuSkahastaM manuSyaM jagAda madhyasthAnE tvamuttiSTha|
Yesu akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Njoo hapa mbele ya watu wote.”
4 tataH paraM sa tAn papraccha vizrAmavArE hitamahitaM tathA hi prANarakSA vA prANanAza ESAM madhyE kiM karaNIyaM? kintu tE niHzabdAstasthuH|
Kisha Yesu akawauliza, “Je, ni lipi lililo halali siku ya Sabato: Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao wakanyamaza kimya.
5 tadA sa tESAmantaHkaraNAnAM kAThinyAddhEtO rduHkhitaH krOdhAt cartudazO dRSTavAn taM mAnuSaM gaditavAn taM hastaM vistAraya, tatastEna hastE vistRtE taddhastO'nyahastavad arOgO jAtaH|
Yesu akawatazama pande zote kwa hasira, akahuzunika sana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa kabisa!
6 atha phirUzinaH prasthAya taM nAzayituM hErOdIyaiH saha mantrayitumArEbhirE|
Kisha Mafarisayo wakatoka nje, nao wakaanza kufanya shauri la kumuua Yesu wakiwa na Maherode.
7 ataEva yIzustatsthAnaM parityajya ziSyaiH saha punaH sAgarasamIpaM gataH;
Yesu pamoja na wanafunzi wake wakaondoka huko wakaenda baharini, nao umati mkubwa wa watu kutoka Galilaya ukamfuata.
8 tatO gAlIlyihUdA-yirUzAlam-idOm-yardannadIpArasthAnEbhyO lOkasamUhastasya pazcAd gataH; tadanyaH sOrasIdanOH samIpavAsilOkasamUhazca tasya mahAkarmmaNAM vArttaM zrutvA tasya sannidhimAgataH|
Waliposikia mambo yote aliyokuwa akiyafanya, umati mkubwa wa watu ukamjia kutoka Uyahudi, Yerusalemu, Idumaya, na ngʼambo ya Yordani, pamoja na wale wa sehemu za karibu na Tiro na Sidoni.
9 tadA lOkasamUhazcEt tasyOpari patati ityAzagkya sa nAvamEkAM nikaTE sthApayituM ziSyAnAdiSTavAn|
Kwa sababu ya umati mkubwa wa watu, aliwaambia wanafunzi wake waweke tayari mashua ndogo kwa ajili yake, ili kuwazuia watu kumsonga.
10 yatO'nEkamanuSyANAmArOgyakaraNAd vyAdhigrastAH sarvvE taM spraSTuM parasparaM balEna yatnavantaH|
Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa.
11 aparanjca apavitrabhUtAstaM dRSTvA taccaraNayOH patitvA prOcaiH prOcuH, tvamIzvarasya putraH|
Kila mara pepo wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kupiga kelele wakisema, “Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
12 kintu sa tAn dRPham AjnjApya svaM paricAyituM niSiddhavAn|
Lakini aliwaonya wasimseme yeye ni nani.
13 anantaraM sa parvvatamAruhya yaM yaM praticchA taM tamAhUtavAn tatastE tatsamIpamAgatAH|
Yesu akapanda mlimani na kuwaita wale aliowataka, nao wakamjia.
14 tadA sa dvAdazajanAn svEna saha sthAtuM susaMvAdapracArAya prEritA bhavituM
Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri
15 sarvvaprakAravyAdhInAM zamanakaraNAya prabhAvaM prAptuM bhUtAn tyAjayitunjca niyuktavAn|
na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu.
16 tESAM nAmAnImAni, zimOn sivadiputrO
Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro);
17 yAkUb tasya bhrAtA yOhan ca AndriyaH philipO barthalamayaH,
Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo);
18 mathI thOmA ca AlphIyaputrO yAkUb thaddIyaH kinAnIyaH zimOn yastaM parahastESvarpayiSyati sa ISkariyOtIyayihUdAzca|
Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
19 sa zimOnE pitara ityupanAma dadau yAkUbyOhanbhyAM ca binErigiz arthatO mEghanAdaputrAvityupanAma dadau|
na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.
20 anantaraM tE nivEzanaM gatAH, kintu tatrApi punarmahAn janasamAgamO 'bhavat tasmAttE bhOktumapyavakAzaM na prAptAH|
Kisha Yesu aliporudi nyumbani, umati wa watu ukakusanyika tena, kiasi kwamba yeye na wanafunzi wake hawakuweza kula chakula.
21 tatastasya suhRllOkA imAM vArttAM prApya sa hatajnjAnObhUd iti kathAM kathayitvA taM dhRtvAnEtuM gatAH|
Ndugu zake walipopata habari wakaja ili kumchukua kwa maana watu walikuwa wakisema, “Amerukwa na akili.”
22 aparanjca yirUzAlama AgatA yE yE'dhyApakAstE jagadurayaM puruSO bhUtapatyAbiSTastEna bhUtapatinA bhUtAn tyAjayati|
Walimu wa sheria walioteremka kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli! Anatoa pepo wachafu kwa kutumia mkuu wa pepo wachafu!”
23 tatastAnAhUya yIzu rdRSTAntaiH kathAM kathitavAn zaitAn kathaM zaitAnaM tyAjayituM zaknOti?
Basi Yesu akawaita na kuzungumza nao kwa mifano akasema: “Shetani awezaje kumtoa Shetani?
24 kinjcana rAjyaM yadi svavirOdhEna pRthag bhavati tarhi tad rAjyaM sthiraM sthAtuM na zaknOti|
Kama ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
25 tathA kasyApi parivArO yadi parasparaM virOdhI bhavati tarhi sOpi parivAraH sthiraM sthAtuM na zaknOti|
Nayo nyumba kama ikigawanyika dhidi yake yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
26 tadvat zaitAn yadi svavipakSatayA uttiSThan bhinnO bhavati tarhi sOpi sthiraM sthAtuM na zaknOti kintUcchinnO bhavati|
Naye Shetani kama akijipinga mwenyewe na awe amegawanyika, hawezi kusimama bali mwisho wake umewadia.
27 aparanjca prabalaM janaM prathamaM na baddhA kOpi tasya gRhaM pravizya dravyANi luNThayituM na zaknOti, taM badvvaiva tasya gRhasya dravyANi luNThayituM zaknOti|
Hakuna mtu yeyote awezaye kuingia kwenye nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu. Ndipo ataweza kuteka nyara mali zake.
28 atOhEtO ryuSmabhyamahaM satyaM kathayAmi manuSyANAM santAnA yAni yAni pApAnIzvaranindAnjca kurvvanti tESAM tatsarvvESAmaparAdhAnAM kSamA bhavituM zaknOti,
Amin, nawaambia, dhambi zote na makufuru yote ya wanadamu watasamehewa.
29 kintu yaH kazcit pavitramAtmAnaM nindati tasyAparAdhasya kSamA kadApi na bhaviSyati sOnantadaNPasyArhO bhaviSyati| (aiōn , aiōnios )
Lakini yeyote anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn , aiōnios )
30 tasyApavitrabhUtO'sti tESAmEtatkathAhEtOH sa itthaM kathitavAn|
Yesu alisema hivi kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”
31 atha tasya mAtA bhrAtRgaNazcAgatya bahistiSThanatO lOkAn prESya tamAhUtavantaH|
Kisha wakaja ndugu zake Yesu pamoja na mama yake. Wakasimama nje, wakamtuma mtu kumwita.
32 tatastatsannidhau samupaviSTA lOkAstaM babhASirE pazya bahistava mAtA bhrAtarazca tvAm anvicchanti|
Umati wa watu ulikuwa umeketi kumzunguka, nao wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”
33 tadA sa tAn pratyuvAca mama mAtA kA bhrAtarO vA kE? tataH paraM sa svamIpOpaviSTAn ziSyAn prati avalOkanaM kRtvA kathayAmAsa
Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”
34 pazyataitE mama mAtA bhrAtarazca|
Kisha akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka pande zote, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
35 yaH kazcid IzvarasyESTAM kriyAM karOti sa Eva mama bhrAtA bhaginI mAtA ca|
Mtu yeyote anayetenda mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”