< mArkaH 14 >

1 tadA nistArOtsavakiNvahInapUpOtsavayOrArambhasya dinadvayE 'vaziSTE pradhAnayAjakA adhyApakAzca kEnApi chalEna yIzuM dharttAM hantunjca mRgayAnjcakrirE;
Zilikuwa zimebaki siku mbili tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka, na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumkamata Yesu kwa hila na kumuua.
2 kintu lOkAnAM kalahabhayAdUcirE, nacOtsavakAla ucitamEtaditi|
Lakini walisema, “Tusilifanye jambo hili wakati wa Sikukuu, maana watu wanaweza wakafanya ghasia.”
3 anantaraM baithaniyApurE zimOnakuSThinO gRhE yOzau bhOtkumupaviSTE sati kAcid yOSit pANParapASANasya sampuTakEna mahArghyOttamatailam AnIya sampuTakaM bhaMktvA tasyOttamAggE tailadhArAM pAtayAnjcakrE|
Yesu alikuwa Bethania nyumbani kwa Simoni aliyekuwa na ukoma. Wakati alipokuwa ameketi mezani akila chakula cha jioni, mwanamke mmoja aliingia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa. Akaivunja hiyo chupa, akamiminia hayo manukato kichwani mwa Yesu.
4 tasmAt kEcit svAntE kupyantaH kathitavaMntaH kutOyaM tailApavyayaH?
Baadhi ya watu waliokuwepo pale walikuwa wakisemezana wao kwa wao, “Upotevu huu wote ni wa nini?
5 yadyEtat taila vyakrESyata tarhi mudrApAdazatatrayAdapyadhikaM tasya prAptamUlyaM daridralOkEbhyO dAtumazakSyata, kathAmEtAM kathayitvA tayA yOSitA sAkaM vAcAyuhyan|
Mafuta haya yangeweza kuuzwa kwa zaidi ya dinari 300, na fedha hizo wakapewa maskini.” Wakamkemea vikali huyo mwanamke.
6 kintu yIzuruvAca, kuta Etasyai kRcchraM dadAsi? mahyamiyaM karmmOttamaM kRtavatI|
Lakini Yesu akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Mwacheni! Yeye amenitendea jambo zuri sana.
7 daridrAH sarvvadA yuSmAbhiH saha tiSThanti, tasmAd yUyaM yadEcchatha tadaiva tAnupakarttAM zaknutha, kintvahaM yubhAbhiH saha nirantaraM na tiSThAmi|
Maskini mtakuwa nao siku zote na mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaotaka. Lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
8 asyA yathAsAdhyaM tathaivAkarOdiyaM, zmazAnayApanAt pUrvvaM samEtya madvapuSi tailam amarddayat|
Huyu mwanamke amenitendea lile aliloweza. Ameumiminia mwili wangu manukato ili kuniandaa kwa maziko yangu.
9 ahaM yuSmabhyaM yathArthaM kathayAmi, jagatAM madhyE yatra yatra susaMvAdOyaM pracArayiSyatE tatra tatra yOSita EtasyAH smaraNArthaM tatkRtakarmmaitat pracArayiSyatE|
Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
10 tataH paraM dvAdazAnAM ziSyANAmEka ISkariyOtIyayihUdAkhyO yIzuM parakarESu samarpayituM pradhAnayAjakAnAM samIpamiyAya|
Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi kumi na wawili, akaenda kwa viongozi wa makuhani ili kumsaliti Yesu kwao.
11 tE tasya vAkyaM samAkarNya santuSTAH santastasmai mudrA dAtuM pratyajAnata; tasmAt sa taM tESAM karESu samarpaNAyOpAyaM mRgayAmAsa|
Walifurahi sana kusikia jambo hili na wakaahidi kumpa fedha. Hivyo yeye akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti.
12 anantaraM kiNvazUnyapUpOtsavasya prathamE'hani nistArOtmavArthaM mESamAraNAsamayE ziSyAstaM papracchaH kutra gatvA vayaM nistArOtsavasya bhOjyamAsAdayiSyAmaH? kimicchati bhavAn?
Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo kwa desturi mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wa Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
13 tadAnIM sa tESAM dvayaM prErayan babhASE yuvayOH puramadhyaM gatayOH satO ryO janaH sajalakumbhaM vahan yuvAM sAkSAt kariSyati tasyaiva pazcAd yAtaM;
Basi akawatuma wawili miongoni mwa wanafunzi wake, akawaambia, “Nendeni mjini. Huko mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni.
14 sa yat sadanaM pravEkSyati tadbhavanapatiM vadataM, gururAha yatra saziSyOhaM nistArOtsavIyaM bhOjanaM kariSyAmi, sA bhOjanazAlA kutrAsti?
Mwambieni mwenye nyumba ile atakayoingia, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba changu cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
15 tataH sa pariSkRtAM susajjitAM bRhatIcanjca yAM zAlAM darzayiSyati tasyAmasmadarthaM bhOjyadravyANyAsAdayataM|
Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kilichopambwa tena kilicho tayari. Tuandalieni humo.”
16 tataH ziSyau prasthAya puraM pravizya sa yathOktavAn tathaiva prApya nistArOtsavasya bhOjyadravyANi samAsAdayEtAm|
Wale wanafunzi wakaondoka na kwenda mjini, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
17 anantaraM yIzuH sAyaMkAlE dvAdazabhiH ziSyaiH sArddhaM jagAma;
Ilipofika jioni, Yesu akaja pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
18 sarvvESu bhOjanAya prOpaviSTESu sa tAnuditavAn yuSmAnahaM yathArthaM vyAharAmi, atra yuSmAkamEkO janO yO mayA saha bhuMktE mAM parakErESu samarpayiSyatE|
Walipoketi mezani wakila, Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti, mmoja anayekula pamoja nami.”
19 tadAnIM tE duHkhitAH santa EkaikazastaM praSTumArabdhavantaH sa kimahaM? pazcAd anya EkObhidadhE sa kimahaM?
Wakaanza kuhuzunika na kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
20 tataH sa pratyavadad EtESAM dvAdazAnAM yO janO mayA samaM bhOjanApAtrE pANiM majjayiSyati sa Eva|
Akawajibu, “Ni mmoja miongoni mwenu ninyi kumi na wawili, yule anayechovya mkate kwenye bakuli pamoja nami.
21 manujatanayamadhi yAdRzaM likhitamAstE tadanurUpA gatistasya bhaviSyati, kintu yO janO mAnavasutaM samarpayiSyatE hanta tasya janmAbhAvE sati bhadramabhaviSyat|
Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa.”
22 aparanjca tESAM bhOjanasamayE yIzuH pUpaM gRhItvEzvaraguNAn anukIrtya bhagktvA tEbhyO dattvA babhASE, Etad gRhItvA bhunjjIdhvam Etanmama vigraharUpaM|
Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni mle; huu ndio mwili wangu.”
23 anantaraM sa kaMsaM gRhItvEzvarasya guNAn kIrttayitvA tEbhyO dadau, tatastE sarvvE papuH|
Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, nao wote wakanywa kutoka humo.
24 aparaM sa tAnavAdId bahUnAM nimittaM pAtitaM mama navInaniyamarUpaM zONitamEtat|
Akawaambia, “Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.
25 yuSmAnahaM yathArthaM vadAmi, Izvarasya rAjyE yAvat sadyOjAtaM drAkSArasaM na pAsyAmi, tAvadahaM drAkSAphalarasaM puna rna pAsyAmi|
Amin, nawaambia, sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya katika Ufalme wa Mungu.”
26 tadanantaraM tE gItamEkaM saMgIya bahi rjaitunaM zikhariNaM yayuH
Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
27 atha yIzustAnuvAca nizAyAmasyAM mayi yuSmAkaM sarvvESAM pratyUhO bhaviSyati yatO likhitamAstE yathA, mESANAM rakSakanjcAhaM prahariSyAmi vai tataH| mESANAM nivahO nUnaM pravikIrNO bhaviSyati|
Yesu akawaambia, “Ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo watatawanyika.’
28 kantu madutthAnE jAtE yuSmAkamagrE'haM gAlIlaM vrajiSyAmi|
Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
29 tadA pitaraH pratibabhASE, yadyapi sarvvESAM pratyUhO bhavati tathApi mama naiva bhaviSyati|
Petro akasema, “Hata kama wengine wote watakuacha, mimi sitakuacha.”
30 tatO yIzuruktAvAn ahaM tubhyaM tathyaM kathayAmi, kSaNAdAyAmadya kukkuTasya dvitIyavAraravaNAt pUrvvaM tvaM vAratrayaM mAmapahnOSyasE|
Yesu akamwambia, “Amin, nakuambia; leo, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, wewe mwenyewe utanikana mara tatu.”
31 kintu sa gAPhaM vyAharad yadyapi tvayA sArddhaM mama prANO yAti tathApi kathamapi tvAM nApahnOSyE; sarvvE'pItarE tathaiva babhASirE|
Lakini Petro akasisitiza zaidi, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
32 aparanjca tESu gEtzimAnInAmakaM sthAna gatESu sa ziSyAn jagAda, yAvadahaM prArthayE tAvadatra sthAnE yUyaM samupavizata|
Wakaenda mahali paitwapo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa, nami niende nikaombe.”
33 atha sa pitaraM yAkUbaM yOhananjca gRhItvA vavrAja; atyantaM trAsitO vyAkulitazca tEbhyaH kathayAmAsa,
Kisha akawachukua pamoja naye Petro, Yakobo na Yohana. Akaanza kuhuzunika sana na kutaabika.
34 nidhanakAlavat prANO mE'tIva daHkhamEti, yUyaM jAgratOtra sthAnE tiSThata|
Akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe.”
35 tataH sa kinjciddUraM gatvA bhUmAvadhOmukhaH patitvA prArthitavAnEtat, yadi bhavituM zakyaM tarhi duHkhasamayOyaM mattO dUrIbhavatu|
Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba kwamba kama ingewezekana saa hiyo ya mateso imwondokee.
36 aparamuditavAn hE pita rhE pitaH sarvvEM tvayA sAdhyaM, tatO hEtOrimaM kaMsaM mattO dUrIkuru, kintu tan mamEcchAtO na tavEcchAtO bhavatu|
Akasema, “Abba, Baba, mambo yote yawezekana kwako. Niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali vile upendavyo wewe.”
37 tataH paraM sa Etya tAn nidritAn nirIkSya pitaraM prOvAca, zimOn tvaM kiM nidrAsi? ghaTikAmEkAm api jAgarituM na zaknOSi?
Akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Simoni, umelala? Je, hukuweza kukesha hata kwa saa moja?
38 parIkSAyAM yathA na patatha tadarthaM sacEtanAH santaH prArthayadhvaM; mana udyuktamiti satyaM kintu vapurazaktikaM|
Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
39 atha sa punarvrajitvA pUrvvavat prArthayAnjcakrE|
Akaenda tena kuomba, akisema maneno yale yale.
40 parAvRtyAgatya punarapi tAn nidritAn dadarza tadA tESAM lOcanAni nidrayA pUrNAni, tasmAttasmai kA kathA kathayitavyA ta Etad bOddhuM na zEkuH|
Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito. Nao hawakujua la kumwambia.
41 tataHparaM tRtIyavAraM Agatya tEbhyO 'kathayad idAnImapi zayitvA vizrAmyatha? yathESTaM jAtaM, samayazcOpasthitaH pazyata mAnavatanayaH pApilOkAnAM pANiSu samarpyatE|
Akaja mara ya tatu, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Imetosha! Saa imewadia. Tazameni, Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
42 uttiSThata, vayaM vrajAmO yO janO mAM parapANiSu samarpayiSyatE pazyata sa samIpamAyAtaH|
Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
43 imAM kathAM kathayati sa, EtarhidvAdazAnAmEkO yihUdA nAmA ziSyaH pradhAnayAjakAnAm upAdhyAyAnAM prAcInalOkAnAnjca sannidhEH khaggalaguPadhAriNO bahulOkAn gRhItvA tasya samIpa upasthitavAn|
Yesu alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili, akatokea. Alikuwa amefuatana na umati wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, na wazee.
44 aparanjcAsau parapANiSu samarpayitA pUrvvamiti sagkEtaM kRtavAn yamahaM cumbiSyAmi sa EvAsau tamEva dhRtvA sAvadhAnaM nayata|
Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni, mkamchukue chini ya ulinzi.”
45 atO hEtOH sa Agatyaiva yOzOH savidhaM gatvA hE gurO hE gurO, ityuktvA taM cucumba|
Mara Yuda akamjia Yesu na kusema, “Rabi.” Akambusu.
46 tadA tE tadupari pANInarpayitvA taM dadhnuH|
Wale watu wakamkamata Yesu, wakamweka chini ya ulinzi.
47 tatastasya pArzvasthAnAM lOkAnAmEkaH khaggaM niSkOSayan mahAyAjakasya dAsamEkaM prahRtya tasya karNaM cicchEda|
Ndipo mmoja wa wale waliokuwa wamesimama karibu aliuchomoa upanga wake na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
48 pazcAd yIzustAn vyAjahAra khaggAn laguPAMzca gRhItvA mAM kiM cauraM dharttAM samAyAtAH?
Kisha Yesu akawaambia, “Mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?
49 madhyEmandiraM samupadizan pratyahaM yuSmAbhiH saha sthitavAnatahaM, tasmin kAlE yUyaM mAM nAdIdharata, kintvanEna zAstrIyaM vacanaM sEdhanIyaM|
Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini Maandiko sharti yatimie.”
50 tadA sarvvE ziSyAstaM parityajya palAyAnjcakrirE|
Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha, wakakimbia.
51 athaikO yuvA mAnavO nagnakAyE vastramEkaM nidhAya tasya pazcAd vrajan yuvalOkai rdhRtO
Kijana mmoja, ambaye hakuwa amevaa kitu isipokuwa alijitanda nguo ya kitani, alikuwa akimfuata Yesu. Walipomkamata,
52 vastraM vihAya nagnaH palAyAnjcakrE|
alikimbia uchi, akaliacha vazi lake.
53 aparanjca yasmin sthAnE pradhAnayAjakA upAdhyAyAH prAcInalOkAzca mahAyAjakEna saha sadasi sthitAstasmin sthAnE mahAyAjakasya samIpaM yIzuM ninyuH|
Wakampeleka Yesu kwa kuhani mkuu, nao viongozi wa makuhani wote, na wazee na walimu wa sheria wote wakakusanyika pamoja.
54 pitarO dUrE tatpazcAd itvA mahAyAjakasyATTAlikAM pravizya kigkaraiH sahOpavizya vahnitApaM jagrAha|
Petro akamfuata kwa mbali, hadi uani kwa kuhani mkuu. Huko akaketi pamoja na walinzi, akiota moto.
55 tadAnIM pradhAnayAjakA mantriNazca yIzuM ghAtayituM tatprAtikUlyEna sAkSiNO mRgayAnjcakrirE, kintu na prAptAH|
Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumuua. Lakini hawakupata jambo lolote.
56 anEkaistadviruddhaM mRSAsAkSyE dattEpi tESAM vAkyAni na samagacchanta|
Wengi walitoa ushahidi wa uongo dhidi yake, lakini maelezo yao hayakukubaliana.
57 sarvvazESE kiyanta utthAya tasya prAtikUlyEna mRSAsAkSyaM dattvA kathayAmAsuH,
Ndipo wengine wakasimama wakatoa ushahidi wa uongo dhidi yake, wakisema:
58 idaM karakRtamandiraM vinAzya dinatrayamadhyE punaraparam akarakRtaM mandiraM nirmmAsyAmi, iti vAkyam asya mukhAt zrutamasmAbhiriti|
“Sisi tulimsikia akisema, ‘Mimi nitalibomoa Hekalu hili lililojengwa na wanadamu, na katika siku tatu nitajenga jingine ambalo halikujengwa na wanadamu.’”
59 kintu tatrApi tESAM sAkSyakathA na saggAtAH|
Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukukubaliana.
60 atha mahAyAjakO madhyEsabham utthAya yIzuM vyAjahAra, EtE janAstvayi yat sAkSyamaduH tvamEtasya kimapyuttaraM kiM na dAsyasi?
Basi kuhani mkuu akasimama mbele yao, akamuuliza Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
61 kintu sa kimapyuttaraM na datvA maunIbhUya tasyau; tatO mahAyAjakaH punarapi taM pRSTAvAn tvaM saccidAnandasya tanayO 'bhiSiktastratA?
Lakini Yesu akakaa kimya, hakusema neno lolote. Kuhani mkuu akamuuliza tena, “Je, wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu Aliyebarikiwa?”
62 tadA yIzustaM prOvAca bhavAmyaham yUyanjca sarvvazaktimatO dakSINapArzvE samupavizantaM mEgha mAruhya samAyAntanjca manuSyaputraM sandrakSyatha|
Yesu akajibu, “Mimi ndimi. Nanyi mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
63 tadA mahAyAjakaH svaM vamanaM chitvA vyAvaharat
Kuhani mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi?
64 kimasmAkaM sAkSibhiH prayOjanam? IzvaranindAvAkyaM yuSmAbhirazrAvi kiM vicArayatha? tadAnIM sarvvE jagadurayaM nidhanadaNPamarhati|
Ninyi mmesikia hayo makufuru. Uamuzi wenu ni gani?” Wote wakamhukumu kwamba anastahili kifo.
65 tataH kazcit kazcit tadvapuSi niSThIvaM nicikSEpa tathA tanmukhamAcchAdya capETEna hatvA gaditavAn gaNayitvA vada, anucarAzca capETaistamAjaghnuH
Kisha baadhi ya watu wakaanza kumtemea mate; wakamfunga kitambaa machoni, wakampiga kwa ngumi na kumwambia, “Tabiri!” Walinzi wakamchukua na kumpiga makofi.
66 tataH paraM pitarE'TTAlikAdhaHkOSThE tiSThati mahAyAjakasyaikA dAsI samEtya
Petro alipokuwa bado yuko chini kwenye ua wa jumba la kifalme, tazama akaja mmoja wa watumishi wa kike wa kuhani mkuu.
67 taM vihnitApaM gRhlantaM vilOkya taM sunirIkSya babhASE tvamapi nAsaratIyayIzOH sagginAm EkO jana AsIH|
Alipomwona Petro akiota moto, akamtazama sana, akamwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
68 kintu sOpahnutya jagAda tamahaM na vadmi tvaM yat kathayami tadapyahaM na buddhyE| tadAnIM pitarE catvaraM gatavati kukkuTO rurAva|
Lakini Petro akakana, akasema, “Sijui wala sielewi unalosema.” Naye akaondoka kuelekea kwenye njia ya kuingilia.
69 athAnyA dAsI pitaraM dRSTvA samIpasthAn janAn jagAda ayaM tESAmEkO janaH|
Yule mtumishi wa kike alipomwona mahali pale, akawaambia tena wale waliokuwa wamesimama hapo, “Huyu mtu ni mmoja wao.”
70 tataH sa dvitIyavAram apahnutavAn pazcAt tatrasthA lOkAH pitaraM prOcustvamavazyaM tESAmEkO janaH yatastvaM gAlIlIyO nara iti tavOccAraNaM prakAzayati|
Lakini Petro akakana tena. Baada ya muda kidogo wale waliokuwa wamesimama hapo karibu na Petro wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya!”
71 tadA sa zapathAbhizApau kRtvA prOvAca yUyaM kathAM kathayatha taM naraM na jAnE'haM|
Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui huyu mtu mnayesema habari zake!”
72 tadAnIM dvitIyavAraM kukkuTO 'rAvIt| kukkuTasya dvitIyaravAt pUrvvaM tvaM mAM vAratrayam apahnOSyasi, iti yadvAkyaM yIzunA samuditaM tat tadA saMsmRtya pitarO rOditum Arabhata|
Papo hapo jogoo akawika mara ya pili. Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alikuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Akavunjika moyo, akalia sana.

< mArkaH 14 >