< lUkaH 6 >

1 acaranjca parvvaNO dvitIyadinAt paraM prathamavizrAmavArE zasyakSEtrENa yIzOrgamanakAlE tasya ziSyAH kaNizaM chittvA karESu marddayitvA khAditumArEbhirE|
Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2 tasmAt kiyantaH phirUzinastAnavadan vizrAmavArE yat karmma na karttavyaM tat kutaH kurutha?
Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
3 yIzuH pratyuvAca dAyUd tasya sagginazca kSudhArttAH kiM cakruH sa katham Izvarasya mandiraM pravizya
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4 yE darzanIyAH pUpA yAjakAn vinAnyasya kasyApyabhOjanIyAstAnAnIya svayaM bubhajE saggibhyOpi dadau tat kiM yuSmAbhiH kadApi nApAThi?
Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
5 pazcAt sa tAnavadat manujasutO vizrAmavArasyApi prabhu rbhavati|
Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
6 anantaram anyavizrAmavArE sa bhajanagEhaM pravizya samupadizati| tadA tatsthAnE zuSkadakSiNakara EkaH pumAn upatasthivAn|
Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7 tasmAd adhyApakAH phirUzinazca tasmin dOSamArOpayituM sa vizrAmavArE tasya svAsthyaM karOti navEti pratIkSitumArEbhirE|
Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8 tadA yIzustESAM cintAM viditvA taM zuSkakaraM pumAMsaM prOvAca, tvamutthAya madhyasthAnE tiSTha|
Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9 tasmAt tasmin utthitavati yIzustAn vyAjahAra, yuSmAn imAM kathAM pRcchAmi, vizrAmavArE hitam ahitaM vA, prANarakSaNaM prANanAzanaM vA, EtESAM kiM karmmakaraNIyam?
Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
10 pazcAt caturdikSu sarvvAn vilOkya taM mAnavaM babhASE, nijakaraM prasAraya; tatastEna tathA kRta itarakaravat tasya hastaH svasthObhavat|
Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11 tasmAt tE pracaNPakOpAnvitA yIzuM kiM kariSyantIti parasparaM pramantritAH|
Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12 tataH paraM sa parvvatamAruhyEzvaramuddizya prArthayamAnaH kRtsnAM rAtriM yApitavAn|
Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13 atha dinE sati sa sarvvAn ziSyAn AhUtavAn tESAM madhyE
Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14 pitaranAmnA khyAtaH zimOn tasya bhrAtA Andriyazca yAkUb yOhan ca philip barthalamayazca
Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15 mathiH thOmA AlphIyasya putrO yAkUb jvalantanAmnA khyAtaH zimOn
Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16 ca yAkUbO bhrAtA yihUdAzca taM yaH parakarESu samarpayiSyati sa ISkarIyOtIyayihUdAzcaitAn dvAdaza janAn manOnItAn kRtvA sa jagrAha tathA prErita iti tESAM nAma cakAra|
Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17 tataH paraM sa taiH saha parvvatAdavaruhya upatyakAyAM tasthau tatastasya ziSyasagghO yihUdAdEzAd yirUzAlamazca sOraH sIdOnazca jaladhE rOdhasO jananihAzca Etya tasya kathAzravaNArthaM rOgamuktyarthanjca tasya samIpE tasthuH|
Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18 amEdhyabhUtagrastAzca tannikaTamAgatya svAsthyaM prApuH|
Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19 sarvvESAM svAsthyakaraNaprabhAvasya prakAzitatvAt sarvvE lOkA Etya taM spraSTuM yEtirE|
Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20 pazcAt sa ziSyAn prati dRSTiM kutvA jagAda, hE daridrA yUyaM dhanyA yata IzvarIyE rAjyE vO'dhikArOsti|
Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 hE adhunA kSudhitalOkA yUyaM dhanyA yatO yUyaM tarpsyatha; hE iha rOdinO janA yUyaM dhanyA yatO yUyaM hasiSyatha|
Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22 yadA lOkA manuSyasUnO rnAmahEtO ryuSmAn RtIyiSyantE pRthak kRtvA nindiSyanti, adhamAniva yuSmAn svasamIpAd dUrIkariSyanti ca tadA yUyaM dhanyAH|
“Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23 svargE yuSmAkaM yathESTaM phalaM bhaviSyati, EtadarthaM tasmin dinE prOllasata AnandEna nRtyata ca, tESAM pUrvvapuruSAzca bhaviSyadvAdinaH prati tathaiva vyavAharan|
Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24 kintu hA hA dhanavantO yUyaM sukhaM prApnuta| hanta paritRptA yUyaM kSudhitA bhaviSyatha;
Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25 iha hasantO yUyaM vata yuSmAbhiH zOcitavyaM rOditavyanjca|
Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26 sarvvailAkai ryuSmAkaM sukhyAtau kRtAyAM yuSmAkaM durgati rbhaviSyati yuSmAkaM pUrvvapuruSA mRSAbhaviSyadvAdinaH prati tadvat kRtavantaH|
Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27 hE zrOtArO yuSmabhyamahaM kathayAmi, yUyaM zatruSu prIyadhvaM yE ca yuSmAn dviSanti tESAmapi hitaM kuruta|
“Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28 yE ca yuSmAn zapanti tEbhya AziSaM datta yE ca yuSmAn avamanyantE tESAM maggalaM prArthayadhvaM|
Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29 yadi kazcit tava kapOlE capETAghAtaM karOti tarhi taM prati kapOlam anyaM parAvarttya sammukhIkuru punazca yadi kazcit tava gAtrIyavastraM harati tarhi taM paridhEyavastram api grahItuM mA vAraya|
Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30 yastvAM yAcatE tasmai dEhi, yazca tava sampattiM harati taM mA yAcasva|
Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31 parEbhyaH svAn prati yathAcaraNam apEkSadhvE parAn prati yUyamapi tathAcarata|
Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32 yE janA yuSmAsu prIyantE kEvalaM tESu prIyamANESu yuSmAkaM kiM phalaM? pApilOkA api svESu prIyamANESu prIyantE|
“Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33 yadi hitakAriNa Eva hitaM kurutha tarhi yuSmAkaM kiM phalaM? pApilOkA api tathA kurvvanti|
Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34 yEbhya RNaparizOdhasya prAptipratyAzAstE kEvalaM tESu RNE samarpitE yuSmAkaM kiM phalaM? punaH prAptyAzayA pApIlOkA api pApijanESu RNam arpayanti|
Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35 atO yUyaM ripuSvapi prIyadhvaM, parahitaM kuruta ca; punaH prAptyAzAM tyaktvA RNamarpayata, tathA kRtE yuSmAkaM mahAphalaM bhaviSyati, yUyanjca sarvvapradhAnasya santAnA iti khyAtiM prApsyatha, yatO yuSmAkaM pitA kRtaghnAnAM durvTattAnAnjca hitamAcarati|
Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36 ata Eva sa yathA dayAlu ryUyamapi tAdRzA dayAlavO bhavata|
Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37 aparanjca parAn dOSiNO mA kuruta tasmAd yUyaM dOSIkRtA na bhaviSyatha; adaNPyAn mA daNPayata tasmAd yUyamapi daNPaM na prApsyatha; parESAM dOSAn kSamadhvaM tasmAd yuSmAkamapi dOSAH kSamiSyantE|
“Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38 dAnAnidatta tasmAd yUyaM dAnAni prApsyatha, varanjca lOkAH parimANapAtraM pradalayya sanjcAlya prOnjcAlya paripUryya yuSmAkaM krOPESu samarpayiSyanti; yUyaM yEna parimANEna parimAtha tEnaiva parimANEna yuSmatkRtE parimAsyatE|
Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
39 atha sa tEbhyO dRSTAntakathAmakathayat, andhO janaH kimandhaM panthAnaM darzayituM zaknOti? tasmAd ubhAvapi kiM garttE na patiSyataH?
Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40 gurOH ziSyO na zrESThaH kintu ziSyE siddhE sati sa gurutulyO bhavituM zaknOti|
Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41 aparanjca tvaM svacakSuSi nAsAm adRSTvA tava bhrAtuzcakSuSi yattRNamasti tadEva kutaH pazyami?
Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42 svacakSuSi yA nAsA vidyatE tAm ajnjAtvA, bhrAtastava nEtrAt tRNaM bahiH karOmIti vAkyaM bhrAtaraM kathaM vaktuM zaknOSi? hE kapaTin pUrvvaM svanayanAt nAsAM bahiH kuru tatO bhrAtuzcakSuSastRNaM bahiH karttuM sudRSTiM prApsyasi|
Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43 anyanjca uttamastaruH kadApi phalamanuttamaM na phalati, anuttamataruzca phalamuttamaM na phalati kAraNAdataH phalaistaravO jnjAyantE|
“Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44 kaNTakipAdapAt kOpi uPumbaraphalAni na pAtayati tathA zRgAlakOlivRkSAdapi kOpi drAkSAphalaM na pAtayati|
Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45 tadvat sAdhulOkO'ntaHkaraNarUpAt subhANPAgArAd uttamAni dravyANi bahiH karOti, duSTO lOkazcAntaHkaraNarUpAt kubhANPAgArAt kutsitAni dravyANi nirgamayati yatO'ntaHkaraNAnAM pUrNabhAvAnurUpANi vacAMsi mukhAnnirgacchanti|
Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46 aparanjca mamAjnjAnurUpaM nAcaritvA kutO mAM prabhO prabhO iti vadatha?
“Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47 yaH kazcin mama nikaTam Agatya mama kathA nizamya tadanurUpaM karmma karOti sa kasya sadRzO bhavati tadahaM yuSmAn jnjApayAmi|
Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48 yO janO gabhIraM khanitvA pASANasthalE bhittiM nirmmAya svagRhaM racayati tEna saha tasyOpamA bhavati; yata AplAvijalamEtya tasya mUlE vEgEna vahadapi tadgEhaM lAPayituM na zaknOti yatastasya bhittiH pASANOpari tiSThati|
Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49 kintu yaH kazcin mama kathAH zrutvA tadanurUpaM nAcarati sa bhittiM vinA mRdupari gRhanirmmAtrA samAnO bhavati; yata AplAvijalamAgatya vEgEna yadA vahati tadA tadgRhaM patati tasya mahat patanaM jAyatE|
Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”

< lUkaH 6 >