< yOhanaH 9 >
1 tataH paraM yIzurgacchan mArgamadhyE janmAndhaM naram apazyat|
Yesu alipokuwa akipita, akamwona mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa.
2 tataH ziSyAstam apRcchan hE gurO narOyaM svapApEna vA svapitrAH pApEnAndhO'jAyata?
Wanafunzi wake wakamuuliza, “Rabi, ni nani aliyetenda dhambi, ni huyu mtu au wazazi wake hata azaliwe kipofu?”
3 tataH sa pratyuditavAn Etasya vAsya pitrOH pApAd EtAdRzObhUda iti nahi kintvanEna yathEzvarasya karmma prakAzyatE taddhEtOrEva|
Yesu akawajibu, “Huyu mtu wala wazazi wake hawakutenda dhambi. Alizaliwa kipofu ili kazi za Mungu zidhihirishwe katika maisha yake.
4 dinE tiSThati matprErayituH karmma mayA karttavyaM yadA kimapi karmma na kriyatE tAdRzI nizAgacchati|
Yanipasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana, kwa kuwa usiku waja ambapo hakuna mtu awezaye kufanya kazi.
5 ahaM yAvatkAlaM jagati tiSThAmi tAvatkAlaM jagatO jyOtiHsvarUpOsmi|
Wakati niko ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
6 ityukttA bhUmau niSThIvaM nikSipya tEna pagkaM kRtavAn
Baada ya kusema haya, akatema mate ardhini, akatengeneza tope kwa mate na kumpaka yule mtu kipofu machoni.
7 pazcAt tatpagkEna tasyAndhasya nEtrE pralipya tamityAdizat gatvA zilOhE 'rthAt prEritanAmni sarasi snAhi| tatOndhO gatvA tatrAsnAt tataH prannacakSu rbhUtvA vyAghuTyAgAt|
Kisha akamwambia, “Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu.” (Siloamu maana yake ni aliyetumwa.) Ndipo yule kipofu akaenda, akanawa, naye akarudi akiwa anaona.
8 aparanjca samIpavAsinO lOkA yE ca taM pUrvvamandham apazyan tE bakttum Arabhanta yOndhalOkO vartmanyupavizyAbhikSata sa EvAyaM janaH kiM na bhavati?
Majirani zake na wale wote waliokuwa wamemwona hapo awali akiombaomba wakaanza kuuliza, “Je, huyu si yule aliyekuwa akiketi akiombaomba?”
9 kEcidavadan sa Eva kEcidavOcan tAdRzO bhavati kintu sa svayamabravIt sa EvAhaM bhavAmi|
Wengine wakasema, “Ndiye.” Wengine wakasema, “Siye, bali wamefanana.” Lakini yeye akawaambia, “Mimi ndiye.”
10 ataEva tE 'pRcchan tvaM kathaM dRSTiM pAptavAn?
Wakamuuliza, “Basi macho yako yalifumbuliwaje?”
11 tataH sOvadad yIzanAmaka EkO janO mama nayanE pagkEna pralipya ityAjnjApayat zilOhakAsAraM gatvA tatra snAhi| tatastatra gatvA mayi snAtE dRSTimahaM labdhavAn|
Yeye akawajibu, “Yule mtu aitwaye Yesu alitengeneza tope, akanipaka machoni mwangu, naye akaniambia nenda ukanawe katika Bwawa la Siloamu, ndipo nikanawa nami nikapata kuona!”
12 tadA tE 'vadan sa pumAn kutra? tEnOkttaM nAhaM jAnAmi|
Wale wakamuuliza, “Yeye huyo mtu yuko wapi?” Akawajibu, “Sijui.”
13 aparaM tasmin pUrvvAndhE janE phirUzinAM nikaTam AnItE sati phirUzinOpi tamapRcchan kathaM dRSTiM prAptOsi?
Wakamleta kwa Mafarisayo yule mtu aliyekuwa kipofu hapo awali.
14 tataH sa kathitavAn sa pagkEna mama nEtrE 'limpat pazcAd snAtvA dRSTimalabhE|
Basi siku hiyo Yesu alipotengeneza tope na kuyafungua macho ya huyo mtu ilikuwa Sabato.
15 kintu yIzu rvizrAmavArE karddamaM kRtvA tasya nayanE prasannE'karOd itikAraNAt katipayaphirUzinO'vadan
Mafarisayo nao wakaanza kumuuliza alivyopata kuponywa. Naye akawaambia, “Alinipaka tope kwenye macho yangu, nikanawa na sasa ninaona.”
16 sa pumAn IzvarAnna yataH sa vizrAmavAraM na manyatE| tatOnyE kEcit pratyavadan pApI pumAn kim EtAdRzam AzcaryyaM karmma karttuM zaknOti?
Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Huyu mtu hatoki kwa Mungu, kwa sababu hashiki Sabato.” Lakini wengine wakasema, “Awezaje mtu mwenye dhambi kufanya miujiza kama hii?” Wakagawanyika.
17 itthaM tESAM parasparaM bhinnavAkyatvam abhavat| pazcAt tE punarapi taM pUrvvAndhaM mAnuSam aprAkSuH yO janastava cakSuSI prasannE kRtavAn tasmin tvaM kiM vadasi? sa ukttavAn sa bhavizadvAdI|
Hivyo wakamwambia tena yule mtu aliyekuwa kipofu, “Wewe ndiwe uliyefumbuliwa macho, wasemaje kuhusu mtu huyo?” Maana macho yako ndiyo yaliyofumbuliwa. Yeye akawajibu, “Yeye ni nabii.”
18 sa dRSTim AptavAn iti yihUdIyAstasya dRSTiM prAptasya janasya pitrO rmukhAd azrutvA na pratyayan|
Wale Wayahudi hawakuamini ya kuwa mtu huyo alikuwa kipofu, akapata kuona, mpaka walipowaita wazazi wake.
19 ataEva tE tAvapRcchan yuvayO ryaM putraM janmAndhaM vadathaH sa kimayaM? tarhIdAnIM kathaM draSTuM zaknOti?
Wakawauliza, “Je, huyu ni mtoto wenu, ambaye mnasema alizaliwa kipofu? Imekuwaje basi sasa anaona?”
20 tatastasya pitarau pratyavOcatAm ayam AvayOH putra A janErandhazca tadapyAvAM jAnIvaH
Wazazi wake wakajibu, “Tunajua ya kuwa huyu ni mtoto wetu na ya kuwa alizaliwa kipofu.
21 kintvadhunA kathaM dRSTiM prAptavAn tadAvAM n jAnIvaH kOsya cakSuSI prasannE kRtavAn tadapi na jAnIva ESa vayaHprApta EnaM pRcchata svakathAM svayaM vakSyati|
Lakini sisi hatujui ni kwa jinsi gani kwamba sasa anaona, wala hatujui ni nani aliyemfungua macho yake. Muulizeni, yeye ni mtu mzima na anaweza kujieleza mwenyewe.”
22 yihUdIyAnAM bhayAt tasya pitarau vAkyamidam avadatAM yataH kOpi manuSyO yadi yIzum abhiSiktaM vadati tarhi sa bhajanagRhAd dUrIkAriSyatE yihUdIyA iti mantraNAm akurvvan
Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliwaogopa Wayahudi kwani walikuwa wamekubaliana kuwa mtu yeyote atakayemkiri Yesu kuwa ndiye Kristo atafukuzwa kutoka sinagogi.
23 atastasya pitarau vyAharatAm ESa vayaHprApta EnaM pRcchata|
Kwa hiyo wazazi wake wakasema, “Yeye ni mtu mzima. Muulizeni.”
24 tadA tE punazca taM pUrvvAndham AhUya vyAharan Izvarasya guNAn vada ESa manuSyaH pApIti vayaM jAnImaH|
Hivyo kwa mara ya pili wakamwita yule aliyekuwa kipofu, nao wakamwambia, “Mpe Mungu utukufu! Sisi tunafahamu kuwa mtu huyu aliyekuponya ni mwenye dhambi.”
25 tadA sa ukttavAn sa pApI na vEti nAhaM jAnE pUrvAmandha Asamaham adhunA pazyAmIti mAtraM jAnAmi|
Akawajibu, “Mimi sijui kama yeye ni mwenye dhambi. Lakini jambo moja ninalojua, nilikuwa kipofu na sasa ninaona.”
26 tE punarapRcchan sa tvAM prati kimakarOt? kathaM nEtrE prasannE 'karOt?
Wakamuuliza, “Alikufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
27 tataH sOvAdId EkakRtvOkathayaM yUyaM na zRNutha tarhi kutaH punaH zrOtum icchatha? yUyamapi kiM tasya ziSyA bhavitum icchatha?
Akawajibu, “Tayari nimekwisha kuwaambia, nanyi hamtaki kunisikiliza. Mbona mnataka kusikia tena? Je, ninyi nanyi mnataka kuwa wanafunzi wake?”
28 tadA tE taM tiraskRtya vyAharan tvaM tasya ziSyO vayaM mUsAH ziSyAH|
Ndipo wakamtukana na kusema, “Wewe ndiwe mwanafunzi wake, Sisi ni wanafunzi wa Mose.
29 mUsAvaktrENEzvarO jagAda tajjAnImaH kintvESa kutratyalOka iti na jAnImaH|
Tunajua kwamba Mungu alisema na Mose, lakini kwa habari ya mtu huyu hatujui atokako.”
30 sOvadad ESa mama lOcanE prasannE 'karOt tathApi kutratyalOka iti yUyaM na jAnItha Etad AzcaryyaM bhavati|
Yule mtu akawajibu, “Hili ni jambo la ajabu! Hamjui anakotoka, naye amenifungua macho yangu!
31 IzvaraH pApinAM kathAM na zRNOti kintu yO janastasmin bhaktiM kRtvA tadiSTakriyAM karOti tasyaiva kathAM zRNOti Etad vayaM jAnImaH|
Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomcha na kumtii.
32 kOpi manuSyO janmAndhAya cakSuSI adadAt jagadArambhAd EtAdRzIM kathAM kOpi kadApi nAzRNOt| (aiōn )
Tangu zamani hatujasikia kwamba mtu amemponya yeyote aliyezaliwa kipofu. (aiōn )
33 asmAd ESa manuSyO yadIzvarAnnAjAyata tarhi kinjcidapIdRzaM karmma karttuM nAzaknOt|
Kama huyu mtu hakutoka kwa Mungu, asingeweza kufanya lolote.”
34 tE vyAharan tvaM pApAd ajAyathAH kimasmAn tvaM zikSayasi? pazcAttE taM bahirakurvvan|
Wao wakamjibu, “Wewe ulizaliwa katika dhambi kabisa, nawe unajaribu kutufundisha?” Wakamfukuza atoke nje.
35 tadanantaraM yihUdIyaiH sa bahirakriyata yIzuriti vArttAM zrutvA taM sAkSAt prApya pRSTavAn Izvarasya putrE tvaM vizvasiSi?
Yesu aliposikia kuwa wamemfukuzia nje yule mtu aliyemfumbua macho, alimkuta akamuuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?”
36 tadA sa pratyavOcat hE prabhO sa kO yat tasminnahaM vizvasimi?
Yule mtu akamjibu, “Yeye ni nani, Bwana? Niambie ili nipate kumwamini.”
37 tatO yIzuH kathitavAn tvaM taM dRSTavAn tvayA sAkaM yaH kathaM kathayati saEva saH|
Yesu akamjibu, “Umekwisha kumwona, naye anayezungumza nawe, ndiye.”
38 tadA hE prabhO vizvasimItyuktvA sa taM praNAmat|
Yule mtu akasema, “Bwana, naamini.” Naye akamwabudu.
39 pazcAd yIzuH kathitavAn nayanahInA nayanAni prApnuvanti nayanavantazcAndhA bhavantItyabhiprAyENa jagadAham Agaccham|
Yesu akasema, “Nimekuja ulimwenguni humu kwa ajili ya kuhukumu, ili wale walio vipofu wapate kuona, nao wale wanaoona, wawe vipofu.”
40 Etat zrutvA nikaTasthAH katipayAH phirUzinO vyAharan vayamapi kimandhAH?
Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa karibu naye wakamsikia na kumwambia, “Je, kweli sisi ni vipofu?”
41 tadA yIzuravAdId yadyandhA abhavata tarhi pApAni nAtiSThan kintu pazyAmIti vAkyavadanAd yuSmAkaM pApAni tiSThanti|
Yesu akawajibu, “Kama mngekuwa vipofu kweli, msingekuwa na hatia ya dhambi, lakini kwa kuwa mnasema, ‘Tunaona,’ basi mna hatia.