< prEritAH 5 >
1 tadA anAniyanAmaka EkO janO yasya bhAryyAyA nAma saphIrA sa svAdhikAraM vikrIya
Mtu mmoja aitwaye Anania na mkewe Safira waliuza shamba lao vilevile.
2 svabhAryyAM jnjApayitvA tanmUlyasyaikAMzaM saggOpya sthApayitvA tadanyAMzamAtramAnIya prEritAnAM caraNESu samarpitavAn|
Lakini, mkewe akiwa anajua, Anania akajiwekea sehemu ya fedha alizopata na ile sehemu nyingine akawakabidhi mitume.
3 tasmAt pitarOkathayat hE anAniya bhUmE rmUlyaM kinjcit saggOpya sthApayituM pavitrasyAtmanaH sannidhau mRSAvAkyaM kathayitunjca zaitAn kutastavAntaHkaraNE pravRttimajanayat?
Basi, Petro akamwuliza, “Anania, mbona Shetani ameuingia moyo wako na kukufanya umdanganye Roho Mtakatifu kwa kujiwekea sehemu ya fedha ulizopata kutokana na lile shamba?
4 sA bhUmi ryadA tava hastagatA tadA kiM tava svIyA nAsIt? tarhi svAntaHkaraNE kuta EtAdRzI kukalpanA tvayA kRtA? tvaM kEvalamanuSyasya nikaTE mRSAvAkyaM nAvAdIH kintvIzvarasya nikaTE'pi|
Kabla ya kuliuza lilikuwa mali yako, na baada ya kuliuza, bado hizo fedha zilikuwa zako uzitumie utakavyo. Kwa nini basi, uliamua moyoni mwako kufanya jambo la namna hii? Hukumdanganya mtu; umemdanganya Mungu!”
5 EtAM kathAM zrutvaiva sO'nAniyO bhUmau patan prANAn atyajat, tadvRttAntaM yAvantO lOkA azRNvan tESAM sarvvESAM mahAbhayam ajAyat|
Anania aliposikia hayo, akaanguka chini, akafa. Watu wote waliosikia habari ya tukio hilo waliogopa sana.
6 tadA yuvalOkAstaM vastrENAcchAdya bahi rnItvA zmazAnE'sthApayan|
Vijana wakafika wakaufunika mwili wake, wakamtoa nje, wakamzika.
7 tataH praharaikAnantaraM kiM vRttaM tannAvagatya tasya bhAryyApi tatra samupasthitA|
Baada ya muda wa saa tatu hivi, mke wake, bila kufahamu mambo yaliyotukia, akaingia mle ndani.
8 tataH pitarastAm apRcchat, yuvAbhyAm EtAvanmudrAbhyO bhUmi rvikrItA na vA? EtatvaM vada; tadA sA pratyavAdIt satyam EtAvadbhyO mudrAbhya Eva|
Petro akamwambia, “Niambie! Je, kiasi hiki cha fedha ndicho mlichopata kwa kuuza lile shamba?” Yeye akamjibu, “Naam, ni kiasi hicho.”
9 tataH pitarOkathayat yuvAM kathaM paramEzvarasyAtmAnaM parIkSitum EkamantraNAvabhavatAM? pazya yE tava patiM zmazAnE sthApitavantastE dvArasya samIpE samupatiSThanti tvAmapi bahirnESyanti|
Naye Petro akamwambia, “Mbona mmekula njama kumjaribu Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale watu waliokwenda kumzika mume wako, sasa wako mlangoni na watakuchukua wewe pia.”
10 tataH sApi tasya caraNasannidhau patitvA prANAn atyAkSIt| pazcAt tE yuvAnO'bhyantaram Agatya tAmapi mRtAM dRSTvA bahi rnItvA tasyAH patyuH pArzvE zmazAnE sthApitavantaH|
Mara Safira akaanguka mbele ya miguu ya Petro, akafa. Wale vijana walipoingia, walimkuta amekwisha kufa; hivyo wakamtoa nje, wakamzika karibu na mume wake.
11 tasmAt maNPalyAH sarvvE lOkA anyalOkAzca tAM vArttAM zrutvA sAdhvasaM gatAH|
Kanisa lote pamoja na wote waliosikia habari ya tukio hilo, waliogopa sana.
12 tataH paraM prEritAnAM hastai rlOkAnAM madhyE bahvAzcaryyANyadbhutAni karmmANyakriyanta; tadA ziSyAH sarvva EkacittIbhUya sulEmAnO 'lindE sambhUyAsan|
Mitume walifanya miujiza na maajabu mengi kati ya watu. Waumini walikuwa wakikutana pamoja katika ukumbi wa Solomoni.
13 tESAM sagghAntargO bhavituM kOpi pragalbhatAM nAgamat kintu lOkAstAn samAdriyanta|
Mtu yeyote mwingine ambaye hakuwa mwamini hakuthubutu kujiunga nao. Hata hivyo, watu wengine wasiokuwa wa imani hiyo waliwasifu.
14 striyaH puruSAzca bahavO lOkA vizvAsya prabhuM zaraNamApannAH|
Idadi ya watu waliomwamini Bwana, wanaume kwa wanawake, iliongezeka zaidi na zaidi.
15 pitarasya gamanAgamanAbhyAM kEnApi prakArENa tasya chAyA kasmiMzcijjanE lagiSyatItyAzayA lOkA rOgiNaH zivikayA khaTvayA cAnIya pathi pathi sthApitavantaH|
Kwa sababu hiyo, watu walikuwa wakipeleka wagonjwa barabarani na kuwalaza juu ya vitanda na mikeka ili Petro akipita, walau kivuli chake kiwaguse baadhi yao.
16 caturdiksthanagarEbhyO bahavO lOkAH sambhUya rOgiNO'pavitrabhutagrastAMzca yirUzAlamam Anayan tataH sarvvE svasthA akriyanta|
Watu wengi walifika kutoka katika miji ya kando kando ya Yerusalemu, wakiwaleta wagonjwa wao na wale waliokuwa na pepo wachafu, nao wote wakaponywa.
17 anantaraM mahAyAjakaH sidUkinAM matagrAhiNastESAM sahacarAzca
Kisha, Kuhani Mkuu na wenzake waliokuwa wa kikundi cha Masadukayo wa mahali hapo, wakawaonea mitume wivu.
18 mahAkrOdhAntvitAH santaH prEritAn dhRtvA nIcalOkAnAM kArAyAM baddhvA sthApitavantaH|
Basi, wakawatia nguvuni, wakawafunga ndani ya gereza kuu.
19 kintu rAtrau paramEzvarasya dUtaH kArAyA dvAraM mOcayitvA tAn bahirAnIyAkathayat,
Lakini usiku malaika wa Bwana aliifungua milango ya gereza, akawatoa nje, akawaambia,
20 yUyaM gatvA mandirE daNPAyamAnAH santO lOkAn pratImAM jIvanadAyikAM sarvvAM kathAM pracArayata|
“Nendeni mkasimame Hekaluni na kuwaambia watu kila kitu kuhusu maisha haya mapya.”
21 iti zrutvA tE pratyUSE mandira upasthAya upadiSTavantaH| tadA sahacaragaNEna sahitO mahAyAjaka Agatya mantrigaNam isrAyElvaMzasya sarvvAn rAjasabhAsadaH sabhAsthAn kRtvA kArAyAstAn ApayituM padAtigaNaM prEritavAn|
Mitume walitii, wakaingia Hekaluni asubuhi na mapema, wakaanza kufundisha. Kuhani Mkuu na wenzake walipofika, waliita mkutano wa Baraza kuu, yaani halmashauri yote ya wazee wa Wayahudi halafu wakawatuma watu gerezani wawalete wale mitume.
22 tatastE gatvA kArAyAM tAn aprApya pratyAgatya iti vArttAm avAdiSuH,
Lakini hao watumishi walipofika huko hawakuwakuta mle gerezani. Hivyo walirudi, wakatoa taarifa mkutanoni,
23 vayaM tatra gatvA nirvvighnaM kArAyA dvAraM ruddhaM rakSakAMzca dvArasya bahirdaNPAyamAnAn adarzAma Eva kintu dvAraM mOcayitvA tanmadhyE kamapi draSTuM na prAptAH|
wakisema, “Tulikuta gereza limefungwa kila upande na walinzi wakilinda milango. Lakini tulipofungua hatukumkuta mtu yeyote ndani.”
24 EtAM kathAM zrutvA mahAyAjakO mandirasya sEnApatiH pradhAnayAjakAzca, ita paraM kimaparaM bhaviSyatIti cintayitvA sandigdhacittA abhavan|
Mkuu wa walinzi wa Hekalu na makuhani wakuu waliposikia habari hiyo wakawa na wasiwasi, wasijue yaliyowapata.
25 EtasminnEva samayE kazcit jana Agatya vArttAmEtAm avadat pazyata yUyaM yAn mAnavAn kArAyAm asthApayata tE mandirE tiSThantO lOkAn upadizanti|
Akafika mtu mmoja, akawaambia, “Wale watu mliowafunga gerezani, hivi sasa wamo Hekaluni, wanawafundisha watu.”
26 tadA mandirasya sEnApatiH padAtayazca tatra gatvA cEllOkAH pASANAn nikSipyAsmAn mArayantIti bhiyA vinatyAcAraM tAn Anayan|
Hapo mkuu wa walinzi wa Hekalu pamoja na watu wake walikwenda Hekaluni, akawaleta. Lakini hawakuwakamata kwa kutumia nguvu, maana waliogopa kwamba watu wangewapiga mawe.
27 tE mahAsabhAyA madhyE tAn asthApayan tataH paraM mahAyAjakastAn apRcchat,
Basi, wakawapeleka, wakawasimamisha mbele ya Baraza. Kuhani Mkuu akawaambia,
28 anEna nAmnA samupadESTuM vayaM kiM dRPhaM na nyaSEdhAma? tathApi pazyata yUyaM svESAM tEnOpadEzEnE yirUzAlamaM paripUrNaM kRtvA tasya janasya raktapAtajanitAparAdham asmAn pratyAnEtuM cESTadhvE|
“Tuliwakatazeni waziwazi kufundisha kwa jina la mtu huyu; sasa mmeyaeneza mafundisho yenu pote katika Yerusalemu na mnakusudia kutuwekea lawama ya kifo cha mtu huyo.”
29 tataH pitarOnyaprEritAzca pratyavadan mAnuSasyAjnjAgrahaNAd IzvarasyAjnjAgrahaNam asmAkamucitam|
Hapo Petro, akiwa pamoja na wale mitume wengine, akajibu, “Lazima tumtii Mungu, na siyo binadamu.
30 yaM yIzuM yUyaM kruzE vEdhitvAhata tam asmAkaM paitRka Izvara utthApya
Mungu wa babu zetu alimfufua Yesu baada ya ninyi kumwua kwa kumtundika msalabani.
31 isrAyElvaMzAnAM manaHparivarttanaM pApakSamAnjca karttuM rAjAnaM paritrAtAranjca kRtvA svadakSiNapArzvE tasyAnnatim akarOt|
Huyu ndiye yule aliyekwezwa na Mungu mpaka upande wake wa kulia, akawa kiongozi na Mwokozi, ili awawezeshe watu wa Israeli watubu, wapate kusamehewa dhambi zao.
32 Etasmin vayamapi sAkSiNa AsmahE, tat kEvalaM nahi, Izvara AjnjAgrAhibhyO yaM pavitram AtmanaM dattavAn sOpi sAkSyasti|
Sisi ni mashahidi wa tukio hilo, naye Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wale wanaomtii, anashuhudia pia tukio hilo.”
33 EtadvAkyE zrutE tESAM hRdayAni viddhAnyabhavan tatastE tAn hantuM mantritavantaH|
Wajumbe wote wa lile Baraza waliposikia hayo, wakawaka hasira, hata wakaamua kuwaua.
34 EtasminnEva samayE tatsabhAsthAnAM sarvvalOkAnAM madhyE sukhyAtO gamilIyElnAmaka EkO janO vyavasthApakaH phirUzilOka utthAya prEritAn kSaNArthaM sthAnAntaraM gantum Adizya kathitavAn,
Lakini Mfarisayo mmoja aitwaye Gamalieli ambaye alikuwa mwalimu wa Sheria na aliyeheshimika sana mbele ya watu wote, alisimama mbele ya lile Baraza, akataka wale mitume watolewe nje kwa muda mfupi.
35 hE isrAyElvaMzIyAH sarvvE yUyam EtAn mAnuSAn prati yat karttum udyatAstasmin sAvadhAnA bhavata|
Kisha akawaambia wale wajumbe wa Baraza, “Wananchi wa Israeli, tahadhari kabla ya kutekeleza hicho mnachotaka kuwatenda watu hawa!
36 itaH pUrvvaM thUdAnAmaikO jana upasthAya svaM kamapi mahApuruSam avadat, tataH prAyENa catuHzatalOkAstasya matagrAhiNObhavan pazcAt sa hatObhavat tasyAjnjAgrAhiNO yAvantO lOkAstE sarvvE virkIrNAH santO 'kRtakAryyA abhavan|
Zamani kidogo, kulitokea mtu mmoja jina lake Theuda, akajisema kuwa mtu wa maana na watu karibu mia nne wakajiunga naye. Lakini aliuawa, kisha wafuasi wake wote wakatawanyika na kikundi chake kikafa.
37 tasmAjjanAt paraM nAmalEkhanasamayE gAlIlIyayihUdAnAmaikO jana upasthAya bahUllOkAn svamataM grAhItavAn tataH sOpi vyanazyat tasyAjnjAgrAhiNO yAvantO lOkA Asan tE sarvvE vikIrNA abhavan|
Tena, baadaye, wakati ule wa kuhesabiwa watu, alitokea Yuda wa Galilaya. Huyu naye, aliwavuta watu wakamfuata; lakini naye pia aliuawa, na wafuasi wake wakatawanyika.
38 adhunA vadAmi, yUyam EtAn manuSyAn prati kimapi na kRtvA kSAntA bhavata, yata ESa sagkalpa Etat karmma ca yadi manuSyAdabhavat tarhi viphalaM bhaviSyati|
Na sasa pia mimi nawaambieni, msiwachukulie watu hawa hatua yoyote; waacheni! Kwa maana, ikiwa mpango huu au shughuli hii yao imeanzishwa na binadamu, itatoweka yenyewe.
39 yadIzvarAdabhavat tarhi yUyaM tasyAnyathA karttuM na zakSyatha, varam IzvararOdhakA bhaviSyatha|
Lakini kama imeanzishwa na Mungu, siyo tu kwamba hamtaweza kuwashinda, bali mtajikuta mnapigana na Mungu.” Basi, wakakubaliana naye.
40 tadA tasya mantraNAM svIkRtya tE prEritAn AhUya prahRtya yIzO rnAmnA kAmapi kathAM kathayituM niSidhya vyasarjan|
Hivyo wakawaita wale mitume, wakaamuru wachapwe viboko na kuwaonya wasifundishe tena kwa jina la Yesu; kisha wakawaacha waende zao.
41 kintu tasya nAmArthaM vayaM lajjAbhOgasya yOgyatvEna gaNitA ityatra tE sAnandAH santaH sabhAsthAnAM sAkSAd agacchan|
Basi, mitume wakatoka nje ya ule mkutano wa halmashauri wakiwa wamejaa furaha, kwani walistahili kuaibishwa kwa ajili ya jina la Yesu.
42 tataH paraM pratidinaM mandirE gRhE gRhE cAvizrAmam upadizya yIzukhrISTasya susaMvAdaM pracAritavantaH|
Wakaendelea kila siku kufundisha na kuhubiri Habari Njema ya Kristo, Hekaluni na nyumbani mwa watu.