< prEritAH 19 >
1 karinthanagara ApallasaH sthitikAlE paula uttarapradEzairAgacchan iphiSanagaram upasthitavAn| tatra katipayaziSyAn sAkSat prApya tAn apRcchat,
Wakati Apolo alipokuwa Korintho, Paulo alisafiri sehemu za bara, akafika Efeso ambako aliwakuta wanafunzi kadhaa.
2 yUyaM vizvasya pavitramAtmAnaM prAptA na vA? tatastE pratyavadan pavitra AtmA dIyatE ityasmAbhiH zrutamapi nahi|
Akauliza, “Je, mlipopata kuwa waumini mlipokea Roho Mtakatifu?” Nao wakamjibu, “La! Hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatujasikia.”
3 tadA sA'vadat tarhi yUyaM kEna majjitA abhavata? tE'kathayan yOhanO majjanEna|
Naye akasema, “Sasa mlipata ubatizo wa namna gani?” Wakamjibu, “Ubatizo wa Yohane.”
4 tadA paula uktavAn itaH paraM ya upasthAsyati tasmin arthata yIzukhrISTE vizvasitavyamityuktvA yOhan manaHparivarttanasUcakEna majjanEna jalE lOkAn amajjayat|
Naye Paulo akasema, “Ubatizo wa Yohane ulikuwa wa kuonyesha kwamba watu wametubu. Yohane aliwaambia watu wamwamini yule ambaye alikuwa anakuja baada yake, yaani Yesu.”
5 tAdRzIM kathAM zrutvA tE prabhO ryIzukhrISTasya nAmnA majjitA abhavan|
Baada ya kusikia hayo, walibatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
6 tataH paulEna tESAM gAtrESu karE'rpitE tESAmupari pavitra AtmAvarUPhavAn, tasmAt tE nAnAdEzIyA bhASA bhaviSyatkathAzca kathitavantaH|
Basi, Paulo akawawekea mikono, na Roho Mtakatifu akawashukia, wakaanza kusema lugha mbalimbali na kutangaza ujumbe wa Mungu.
7 tE prAyENa dvAdazajanA Asan|
Wote jumla, walikuwa watu wapatao kumi na wawili.
8 paulO bhajanabhavanaM gatvA prAyENa mAsatrayam Izvarasya rAjyasya vicAraM kRtvA lOkAn pravartya sAhasEna kathAmakathayat|
Kwa muda wa miezi mitatu Paulo alikuwa akienda katika sunagogi, akawa na majadiliano ya kuvutia sana juu ya Ufalme wa Mungu.
9 kintu kaThinAntaHkaraNatvAt kiyantO janA na vizvasya sarvvESAM samakSam Etatpathasya nindAM karttuM pravRttAH, ataH paulastESAM samIpAt prasthAya ziSyagaNaM pRthakkRtvA pratyahaM turAnnanAmnaH kasyacit janasya pAThazAlAyAM vicAraM kRtavAn|
Lakini wengine walikuwa wakaidi, wakakataa kuamini, wakaanza kuongea vibaya hadharani juu ya Njia ya Bwana. Hapo Paulo alivunja uhusiano nao, akawachukua pembeni wale wanafunzi wake, akawa anazungumza nao kila siku katika jumba la masomo la Turano.
10 itthaM vatsaradvayaM gataM tasmAd AziyAdEzanivAsinaH sarvvE yihUdIyA anyadEzIyalOkAzca prabhO ryIzOH kathAm azrauSan|
Aliendelea kufanya hivyo kwa muda wa miaka miwili hata wakazi wote wa Asia, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, wakaweza kusikia neno la Bwana.
11 paulEna ca Izvara EtAdRzAnyadbhutAni karmmANi kRtavAn
Mungu alifanya miujiza ya ajabu kwa mikono ya Paulo.
12 yat paridhEyE gAtramArjanavastrE vA tasya dEhAt pIPitalOkAnAm samIpam AnItE tE nirAmayA jAtA apavitrA bhUtAzca tEbhyO bahirgatavantaH|
Watu walikuwa wakichukua leso na nguo nyingine za kazi ambazo Paulo alikuwa amezitumia, wakazipeleka kwa wagonjwa, nao wakaponywa magonjwa yao; na wale waliokuwa na pepo wabaya wakatokwa na pepo hao.
13 tadA dEzATanakAriNaH kiyantO yihUdIyA bhUtApasAriNO bhUtagrastanOkAnAM sannidhau prabhE ryIzO rnAma japtvA vAkyamidam avadan, yasya kathAM paulaH pracArayati tasya yIzO rnAmnA yuSmAn AjnjApayAmaH|
Wayahudi kadhaa wenye kupunga pepo wabaya, walisafiri huko na huko, wakijaribu kulitumia jina la Bwana Yesu kwa wale waliokuwa wamepagawa na pepo wabaya. Walikuwa wakisema: “Ninawaamuru kwa jina la Yesu ambaye Paulo anamhubiri.”
14 skivanAmnO yihUdIyAnAM pradhAnayAjakasya saptabhiH puttaistathA kRtE sati
Watoto saba wa Skewa, Kuhani Mkuu wa Kiyahudi, walikuwa miongoni mwa hao waliokuwa wanafanya hivyo.
15 kazcid apavitrO bhUtaH pratyuditavAn, yIzuM jAnAmi paulanjca paricinOmi kintu kE yUyaM?
Lakini pepo mbaya aliwajibu, “Ninamfahamu Yesu, ninamjua pia Paulo, lakini ninyi ni nani?”
16 ityuktvA sOpavitrabhUtagrastO manuSyO lamphaM kRtvA tESAmupari patitvA balEna tAn jitavAn, tasmAttE nagnAH kSatAggAzca santastasmAd gEhAt palAyanta|
Kisha yule mtu aliyepagawa aliwarukia wote kwa kishindo, akawashinda nguvu. Na hao watoto wa Skewa wakakimbia kutoka ile nyumba wakiwa uchi na wamejaa majeraha.
17 sA vAg iphiSanagaranivAsinasaM sarvvESAM yihUdIyAnAM bhinnadEzIyAnAM lOkAnAnjca zravOgOcarIbhUtA; tataH sarvvE bhayaM gatAH prabhO ryIzO rnAmnO yazO 'varddhata|
Kila mtu huko Efeso, Myahudi na asiye Myahudi, alisikia juu ya tukio hilo. Wote waliingiwa na hofu, wakalitukuza jina la Bwana Yesu.
18 yESAmanEkESAM lOkAnAM pratItirajAyata ta Agatya svaiH kRtAH kriyAH prakAzarUpENAggIkRtavantaH|
Waumini wengi walijitokeza wakakiri hadharani mambo waliyokuwa wametenda.
19 bahavO mAyAkarmmakAriNaH svasvagranthAn AnIya rAzIkRtya sarvvESAM samakSam adAhayan, tatO gaNanAM kRtvAbudhyanta panjcAyutarUpyamudrAmUlyapustakAni dagdhAni|
Wengine waliokuwa wameshughulikia mambo ya uchawi hapo awali, walikusanya vitabu vyao, wakavichoma mbele ya wote. Walikisia gharama ya vitabu hivyo, wakaona yafikia vipande vya fedha elfu hamsini.
20 itthaM prabhOH kathA sarvvadEzaM vyApya prabalA jAtA|
Kwa namna hiyo, neno la Bwana lilizidi kuenea na kuwa na nguvu zaidi.
21 sarvvESvEtESu karmmasu sampannESu satsu paulO mAkidaniyAkhAyAdEzAbhyAM yirUzAlamaM gantuM matiM kRtvA kathitavAn tatsthAnaM yAtrAyAM kRtAyAM satyAM mayA rOmAnagaraM draSTavyaM|
Baada ya mambo hayo, Paulo aliamua kwenda Yerusalemu kwa kupitia Makedonia na Akaya. Alisema, “Baada ya kufika huko, itanilazimu kuona Roma pia.”
22 svAnugatalOkAnAM tImathiyErAstau dvau janau mAkidaniyAdEzaM prati prahitya svayam AziyAdEzE katipayadinAni sthitavAn|
Hivyo, aliwatuma wawili wa wasaidizi wake, Timotheo na Erasto, wamtangulie kwenda Makedonia, naye akabaki kwa muda huko Asia.
23 kintu tasmin samayE matE'smin kalahO jAtaH|
Wakati huo ndipo kulipotokea ghasia kubwa huko Efeso kwa sababu ya hiyo Njia ya Bwana.
24 tatkAraNamidaM, arttimIdEvyA rUpyamandiranirmmANEna sarvvESAM zilpinAM yathESTalAbham ajanayat yO dImItriyanAmA nAPIndhamaH
Kulikuwa na mfua fedha mmoja aitwaye Demetrio, ambaye alikuwa na kazi ya kutengeneza sanamu za nyumba ya mungu wa kike aitwaye Artemi. Shughuli hiyo iliwapatia mafundi faida kubwa.
25 sa tAn tatkarmmajIvinaH sarvvalOkAMzca samAhUya bhASitavAn hE mahEcchA EtEna mandiranirmmANEnAsmAkaM jIvikA bhavati, Etad yUyaM vittha;
Demetrio aliwakusanya hao wafanyakazi pamoja na wengine waliokuwa na kazi kama hiyo, akawaambia, “Wananchi, mnafahamu kwamba kipato chetu kinatokana na biashara hii.
26 kintu hastanirmmitEzvarA IzvarA nahi paulanAmnA kEnacijjanEna kathAmimAM vyAhRtya kEvalEphiSanagarE nahi prAyENa sarvvasmin AziyAdEzE pravRttiM grAhayitvA bahulOkAnAM zEmuSI parAvarttitA, Etad yuSmAbhi rdRzyatE zrUyatE ca|
Sasa, mnaweza kusikia na kujionea wenyewe mambo Paulo anayofanya, si tu hapa Efeso, ila pia kote katika Asia. Yeye amewashawishi na kuwageuza watu wakakubali kwamba miungu ile iliyotengenezwa na watu si miungu hata kidogo.
27 tEnAsmAkaM vANijyasya sarvvathA hAnEH sambhavanaM kEvalamiti nahi, AziyAdEzasthai rvA sarvvajagatsthai rlOkaiH pUjyA yArtimI mahAdEvI tasyA mandirasyAvajnjAnasya tasyA aizvaryyasya nAzasya ca sambhAvanA vidyatE|
Hivyo iko hatari kwamba biashara yetu itakuwa na jina baya. Si hivyo tu, bali pia jambo hilo linaweza kuifanya nyumba ya mungu Artemi kuwa si kitu cha maana. Hatimaye sifa zake huyo ambaye Asia na dunia yote inamwabudu, zitakwisha.”
28 EtAdRzIM kathAM zrutvA tE mahAkrOdhAnvitAH santa uccaiHkAraM kathitavanta iphiSIyAnAm arttimI dEvI mahatI bhavati|
Waliposikia hayo, waliwaka hasira, wakaanza kupiga kelele: “Mkuu ni Artemi, wa Efeso!”
29 tataH sarvvanagaraM kalahEna paripUrNamabhavat, tataH paraM tE mAkidanIyagAyAristArkhanAmAnau paulasya dvau sahacarau dhRtvaikacittA raggabhUmiM javEna dhAvitavantaH|
Mji wote ukajaa ghasia. Wakawavamia Gayo na Aristarko, wenyeji wa Makedonia, ambao walikuwa wasafiri wenzake Paulo, wakakimbia nao mpaka kwenye ukumbi wa michezo.
30 tataH paulO lOkAnAM sannidhiM yAtum udyatavAn kintu ziSyagaNastaM vAritavAn|
Paulo mwenyewe alitaka kuukabili huo umati wa watu, lakini wale waumini walimzuia.
31 paulasyatmIyA AziyAdEzasthAH katipayAH pradhAnalOkAstasya samIpaM naramEkaM prESya tvaM raggabhUmiM mAgA iti nyavEdayan|
Maofisa wengine wa huo mkoa wa Asia, waliokuwa rafiki zake, walimtumia Paulo ujumbe wakimsihi asijihatarishe kwa kwenda kwenye ukumbi wa michezo.
32 tatO nAnAlOkAnAM nAnAkathAkathanAt sabhA vyAkulA jAtA kiM kAraNAd EtAvatI janatAbhavat Etad adhikai rlOkai rnAjnjAyi|
Wakati huo, kila mtu alikuwa anapayuka; wengine hili na wengine lile, mpaka hata ule mkutano ukavurugika. Wengi hawakujua hata sababu ya kukutana kwao.
33 tataH paraM janatAmadhyAd yihUdIyairbahiSkRtaH sikandarO hastEna sagkEtaM kRtvA lOkEbhya uttaraM dAtumudyatavAn,
Kwa vile Wayahudi walimfanya Aleksanda ajitokeze mbele, baadhi ya watu katika ule umati walidhani kuwa ndiye. Basi, Aleksanda aliwaashiria watu kwa mkono akitaka kujitetea mbele ya ule umati wa watu.
34 kintu sa yihUdIyalOka iti nizcitE sati iphiSIyAnAm arttimI dEvI mahatIti vAkyaM prAyENa panjca daNPAn yAvad EkasvarENa lOkanivahaiH prOktaM|
Lakini walipotambua kuwa yeye ni Myahudi, wote kwa sauti moja walipiga kelele: “Mkuu ni Artemi wa Efeso!” Wakaendelea kupayukapayuka hivyo kwa muda wa saa mbili.
35 tatO nagarAdhipatistAn sthirAn kRtvA kathitavAn hE iphiSAyAH sarvvE lOkA AkarNayata, artimImahAdEvyA mahAdEvAt patitAyAstatpratimAyAzca pUjanama iphiSanagarasthAH sarvvE lOkAH kurvvanti, Etat kE na jAnanti?
Hatimaye karani wa mji alifaulu kuwanyamazisha, akawaambia, “Wananchi wa Efeso, kila mtu anajua kwamba mji huu wa Efeso ni mlinzi wa nyumba ya mungu Artemi na mlinzi wa ile sanamu iliyoanguka kutoka mbinguni.
36 tasmAd EtatpratikUlaM kEpi kathayituM na zaknuvanti, iti jnjAtvA yuSmAbhiH susthiratvEna sthAtavyam avivicya kimapi karmma na karttavyanjca|
Hakuna anayeweza kukana mambo haya. Hivyo basi, tulieni; msifanye chochote bila hadhari.
37 yAn EtAn manuSyAn yUyamatra samAnayata tE mandiradravyApahArakA yuSmAkaM dEvyA nindakAzca na bhavanti|
Mmewaita watu hawa hapa ingawaje hawakuikufuru nyumba ya mungu wala kumtukana mungu wetu wa kike.
38 yadi kanjcana prati dImItriyasya tasya sahAyAnAnjca kAcid Apatti rvidyatE tarhi pratinidhilOkA vicArasthAnanjca santi, tE tat sthAnaM gatvA uttarapratyuttarE kurvvantu|
Kama, basi Demetrio na wafanyakazi wake wana mashtaka yao kuhusu watu hawa, yapo mahakama na wakuu wa mikoa; wanaweza kushtakiana huko.
39 kintu yuSmAkaM kAcidaparA kathA yadi tiSThati tarhi niyamitAyAM sabhAyAM tasyA niSpatti rbhaviSyati|
Kama mna matatizo mengine, yapelekeni katika kikao halali.
40 kintvEtasya virOdhasyOttaraM yEna dAtuM zaknum EtAdRzasya kasyacit kAraNasyAbhAvAd adyatanaghaTanAhEtO rAjadrOhiNAmivAsmAkam abhiyOgO bhaviSyatIti zagkA vidyatE|
Kwa maana tungaliweza kushtakiwa kwa kusababisha ghasia kutokana na vituko vya leo. Ghasia hii haina msingi halali na hatungeweza kutoa sababu za kuridhisha za ghasia hiyo.”
41 iti kathayitvA sa sabhAsthalOkAn visRSTavAn|
Baada ya kusema hayo aliuvunja mkutano.