< 1 tImathiyaH 6 >

1 yAvantO lOkA yugadhAriNO dAsAH santi tE svasvasvAminaM pUrNasamAdarayOgyaM manyantAM nO cEd Izvarasya nAmna upadEzasya ca nindA sambhaviSyati|
Wale wote walio chini ya kongwa la utumwa inawapasa kuwahesabu mabwana zao kuwa wanastahili heshima yote, ili jina la Mungu lisitukanwe wala mafundisho yetu.
2 yESAnjca svAminO vizvAsinaH bhavanti taistE bhrAtRtvAt nAvajnjEyAH kintu tE karmmaphalabhOginO vizvAsinaH priyAzca bhavantIti hEtOH sEvanIyA Eva, tvam EtAni zikSaya samupadiza ca|
Wale watumwa ambao wana mabwana waaminio, haiwapasi kupunguza heshima yao kwa sababu wao ni ndugu. Badala yake, wawatumikie hata vizuri zaidi, kwa sababu wale wanaonufaika na huduma yao ni waaminio, ambao ni wapenzi wao. Fundisha mambo haya na uwahimize kuyafuata.
3 yaH kazcid itarazikSAM karOti, asmAkaM prabhO ryIzukhrISTasya hitavAkyAnIzvarabhaktE ryOgyAM zikSAnjca na svIkarOti
Ikiwa mtu yeyote atafundisha mafundisho mapotovu wala hakubaliani na mafundisho manyofu ya Bwana wetu Yesu Kristo na yale ya utauwa,
4 sa darpadhmAtaH sarvvathA jnjAnahInazca vivAdai rvAgyuddhaizca rOgayuktazca bhavati|
huyo amejivuna wala hajui kitu chochote. Yeye amejaa tamaa ya mabishano na ugomvi kuhusu maneno ambavyo matokeo yake ni wivu na mapigano, maneno ya ukorofi, shuku mbaya,
5 tAdRzAd bhAvAd IrSyAvirOdhApavAdaduSTAsUyA bhraSTamanasAM satyajnjAnahInAnAm IzvarabhaktiM lAbhOpAyam iva manyamAnAnAM lOkAnAM vivAdAzca jAyantE tAdRzEbhyO lOkEbhyastvaM pRthak tiSTha|
na kuzozana kusikokoma kati ya watu walioharibika akili zao, walioikosa kweli, na ambao hudhani kwamba utauwa ni njia ya kupata faida.
6 saMyatEcchayA yuktA yEzvarabhaktiH sA mahAlAbhOpAyO bhavatIti satyaM|
Lakini utauwa na kuridhika ni faida kubwa.
7 EtajjagatpravEzanakAlE'smAbhiH kimapi nAnAyi tattayajanakAlE'pi kimapi nEtuM na zakSyata iti nizcitaM|
Kwa kuwa hatukuja humu duniani na kitu chochote, wala hatuwezi kutoka humu na kitu.
8 ataEva khAdyAnyAcchAdanAni ca prApyAsmAbhiH santuSTai rbhavitavyaM|
Lakini kama tuna chakula na mavazi, tutaridhika navyo.
9 yE tu dhaninO bhavituM cESTantE tE parIkSAyAm unmAthE patanti yE cAbhilASA mAnavAn vinAzE narakE ca majjayanti tAdRzESvajnjAnAhitAbhilASESvapi patanti|
Lakini wale watu wanaotamani kuwa na mali kwa haraka huanguka kwenye majaribu, na wamenaswa na tamaa nyingi za kipumbavu zenye kudhuru, zinazowazamisha watu katika uharibifu na maangamizi.
10 yatO'rthaspRhA sarvvESAM duritAnAM mUlaM bhavati tAmavalambya kEcid vizvAsAd abhraMzanta nAnAklEzaizca svAn avidhyan|
Kwa maana kupenda fedha ndiyo shina moja la maovu ya kila namna. Baadhi ya watu wakitamani fedha, wameiacha imani na kujichoma wenyewe kwa maumivu mengi.
11 hE Izvarasya lOka tvam EtEbhyaH palAyya dharmma Izvarabhakti rvizvAsaH prEma sahiSNutA kSAntizcaitAnyAcara|
Lakini wewe, mtu wa Mungu, yakimbie mambo haya yote. Fuata haki, utauwa, imani, upendo, saburi na upole.
12 vizvAsarUpam uttamayuddhaM kuru, anantajIvanam Alambasva yatastadarthaM tvam AhUtO 'bhavaH, bahusAkSiNAM samakSanjcOttamAM pratijnjAM svIkRtavAn| (aiōnios g166)
Pigana vile vita vizuri vya imani. Shika uzima wa milele ambao ndio ulioitiwa ulipokiri ule ukiri mzuri mbele ya mashahidi wengi. (aiōnios g166)
13 aparaM sarvvESAM jIvayiturIzvarasya sAkSAd yazca khrISTO yIzuH pantIyapIlAtasya samakSam uttamAM pratijnjAM svIkRtavAn tasya sAkSAd ahaM tvAm idam AjnjApayAmi|
Nakuagiza mbele za Mungu avipaye vitu vyote uhai, na mbele za Kristo Yesu ambaye alipokuwa anashuhudia mbele ya Pontio Pilato alikiri ukiri mzuri,
14 IzvarENa svasamayE prakAzitavyam asmAkaM prabhO ryIzukhrISTasyAgamanaM yAvat tvayA niSkalagkatvEna nirddOSatvEna ca vidhI rakSyatAM|
uishike amri hii bila dosari wala lawama mpaka kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo,
15 sa IzvaraH saccidAnandaH, advitIyasamrAT, rAjnjAM rAjA, prabhUnAM prabhuH,
ambaye Mungu atamleta kwa wakati wake mwenyewe: yeye ahimidiwaye, aliye peke yake Mtawala, Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana,
16 amaratAyA advitIya AkaraH, agamyatEjOnivAsI, marttyAnAM kEnApi na dRSTaH kEnApi na dRzyazca| tasya gauravaparAkramau sadAtanau bhUyAstAM| AmEn| (aiōnios g166)
yeye peke yake ambaye hapatikani na mauti, na anakaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa, ambaye hakuna mwanadamu aliyemwona wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye milele. Amen. (aiōnios g166)
17 ihalOkE yE dhaninastE cittasamunnatiM capalE dhanE vizvAsanjca na kurvvatAM kintu bhOgArtham asmabhyaM pracuratvEna sarvvadAtA (aiōn g165)
Waagize wale ambao ni matajiri wa ulimwengu huu waache kujivuna, wala wasiweke tumaini lao katika mali ambayo si ya hakika, bali waweke tumaini lao katika Mungu ambaye hutupatia vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie. (aiōn g165)
18 yO'mara Izvarastasmin vizvasantu sadAcAraM kurvvantu satkarmmadhanEna dhaninO sukalA dAtArazca bhavantu,
Waagize watende mema, wawe matajiri katika matendo mema, pia wawe wakarimu na walio tayari kushiriki mali zao na wengine.
19 yathA ca satyaM jIvanaM pApnuyustathA pAratrikAm uttamasampadaM sanjcinvantvEti tvayAdizyantAM|
Kwa njia hii watajiwekea hazina kama msingi kwa ajili ya wakati ujao na hivyo watajipatia uzima, yaani, ule uzima ambao ni wa kweli.
20 hE tImathiya, tvam upanidhiM gOpaya kAlpanikavidyAyA apavitraM pralApaM virOdhOktinjca tyaja ca,
Timotheo, linda kile kilichowekwa amana kwako. Epuka majadiliano yasiyo ya utauwa na mabishano ambayo kwa uongo huitwa elimu,
21 yataH katipayA lOkAstAM vidyAmavalambya vizvAsAd bhraSTA abhavana| prasAdastava sahAyO bhUyAt| AmEn|
ambayo wengine kwa kujidai kuwa nayo wameiacha imani. Neema iwe nanyi. Amen.

< 1 tImathiyaH 6 >