< 1 tImathiyaH 2 >

1 mama prathama AdEzO'yaM, prArthanAvinayanivEdanadhanyavAdAH karttavyAH,
Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,
2 sarvvESAM mAnavAnAM kRtE vizESatO vayaM yat zAntatvEna nirvvirOdhatvEna cEzcarabhaktiM vinItatvanjcAcarantaH kAlaM yApayAmastadarthaM nRpatInAm uccapadasthAnAnjca kRtE tE karttavyAH|
kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.
3 yatO'smAkaM tArakasyEzvarasya sAkSAt tadEvOttamaM grAhyanjca bhavati,
Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,
4 sa sarvvESAM mAnavAnAM paritrANaM satyajnjAnaprAptinjcEcchati|
ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
5 yata EkO'dvitIya IzvarO vidyatE kinjcEzvarE mAnavESu caikO 'dvitIyO madhyasthaH
Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,
6 sa narAvatAraH khrISTO yIzu rvidyatE yaH sarvvESAM muktE rmUlyam AtmadAnaM kRtavAn| EtEna yEna pramANEnOpayuktE samayE prakAzitavyaM,
ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.
7 tadghOSayitA dUtO vizvAsE satyadharmmE ca bhinnajAtIyAnAm upadEzakazcAhaM nyayUjyE, EtadahaM khrISTasya nAmnA yathAtathyaM vadAmi nAnRtaM kathayAmi|
Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
8 atO mamAbhimatamidaM puruSaiH krOdhasandEhau vinA pavitrakarAn uttOlya sarvvasmin sthAnE prArthanA kriyatAM|
Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.
9 tadvat nAryyO'pi salajjAH saMyatamanasazca satyO yOgyamAcchAdanaM paridadhatu kinjca kEzasaMskAraiH kaNakamuktAbhi rmahArghyaparicchadaizcAtmabhUSaNaM na kurvvatyaH
Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10 svIkRtEzvarabhaktInAM yOSitAM yOgyaiH satyarmmabhiH svabhUSaNaM kurvvatAM|
bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.
11 nArI sampUrNavinItatvEna nirvirOdhaM zikSatAM|
Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
12 nAryyAH zikSAdAnaM puruSAyAjnjAdAnaM vAhaM nAnujAnAmi tayA nirvvirOdhatvam AcaritavyaM|
Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
13 yataH prathamam AdamastataH paraM havAyAH sRSTi rbabhUva|
Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
14 kinjcAdam bhrAntiyuktO nAbhavat yOSidEva bhrAntiyuktA bhUtvAtyAcAriNI babhUva|
Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
15 tathApi nArIgaNO yadi vizvAsE prEmni pavitratAyAM saMyatamanasi ca tiSThati tarhyapatyaprasavavartmanA paritrANaM prApsyati|
Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.

< 1 tImathiyaH 2 >