< 1 karinthinaH 8 >

1 dEvaprasAdE sarvvESAm asmAkaM jnjAnamAstE tadvayaM vidmaH| tathApi jnjAnaM garvvaM janayati kintu prEmatO niSThA jAyatE|
Sasa kuhusu chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu, tunajua kwamba “sisi sote tuna ujuzi.” Lakini ujuzi hujivuna, bali upendo hujenga.
2 ataH kazcana yadi manyatE mama jnjAnamAsta iti tarhi tEna yAdRzaM jnjAnaM cESTitavyaM tAdRzaM kimapi jnjAnamadyApi na labdhaM|
Mtu yeyote anayedhani kwamba anajua kitu, bado hajui kama impasavyo kujua.
3 kintu ya IzvarE prIyatE sa IzvarENApi jnjAyatE|
Lakini mtu ampendaye Mungu, hujulikana naye Mungu.
4 dEvatAbaliprasAdabhakSaNE vayamidaM vidmO yat jaganmadhyE kO'pi dEvO na vidyatE, EkazcEzvarO dvitIyO nAstIti|
Hivyo basi, kuhusu kula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu: Tunajua kwamba “Sanamu si kitu chochote kabisa duniani,” na kwamba “Kuna Mungu mmoja tu.”
5 svargE pRthivyAM vA yadyapi kESucid Izvara iti nAmArOpyatE tAdRzAzca bahava IzvarA bahavazca prabhavO vidyantE
Kwa kuwa hata kama wapo hao wanaoitwa miungu, kama wakiwa mbinguni au duniani (kama ilivyo kweli wapo “miungu” wengi na “mabwana” wengi),
6 tathApyasmAkamadvitIya IzvaraH sa pitA yasmAt sarvvESAM yadarthanjcAsmAkaM sRSTi rjAtA, asmAkanjcAdvitIyaH prabhuH sa yIzuH khrISTO yEna sarvvavastUnAM yEnAsmAkamapi sRSTiH kRtA|
kwetu sisi yuko Mungu mmoja, aliye Baba, ambaye vitu vyote vyatoka kwake na kwa ajili yake sisi twaishi; na kuna Bwana mmoja tu, Yesu Kristo, ambaye kwa yeye vitu vyote vimekuwepo na kwa yeye tunaishi.
7 adhikantu jnjAnaM sarvvESAM nAsti yataH kEcidadyApi dEvatAM sammanya dEvaprasAdamiva tad bhakSyaM bhunjjatE tEna durbbalatayA tESAM svAntAni malImasAni bhavanti|
Lakini si wote wanaojua jambo hili. Baadhi ya watu bado wamezoea sanamu kuwa halisi hivi kwamba wanapokula chakula kama hicho wanadhani kimetolewa sadaka kwa sanamu na kwa kuwa dhamiri zao ni dhaifu, dhamiri yao inanajisika.
8 kintu bhakSyadravyAd vayam IzvarENa grAhyA bhavAmastannahi yatO bhugktvA vayamutkRSTA na bhavAmastadvadabhugktvApyapakRSTA na bhavAmaH|
Lakini chakula hakituleti karibu na Mungu, wala hatupotezi chochote tusipokula, wala hatuongezi chochote kama tukila.
9 atO yuSmAkaM yA kSamatA sA durbbalAnAm unmAthasvarUpA yanna bhavEt tadarthaM sAvadhAnA bhavata|
Lakini angalieni jinsi mnavyotumia uhuru wenu usije ukawa kikwazo kwao walio dhaifu.
10 yatO jnjAnaviziSTastvaM yadi dEvAlayE upaviSTaH kEnApi dRzyasE tarhi tasya durbbalasya manasi kiM prasAdabhakSaNa utsAhO na janiSyatE?
Kwa maana kama mtu yeyote mwenye dhamiri dhaifu akiwaona ninyi wenye ujuzi huu mkila katika hekalu la sanamu, je, si atatiwa moyo kula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu?
11 tathA sati yasya kRtE khrISTO mamAra tava sa durbbalO bhrAtA tava jnjAnAt kiM na vinaMkSyati?
Kwa njia hiyo, huyo ndugu mwenye dhamiri dhaifu, ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake, ataangamia kwa sababu ya ujuzi wenu.
12 ityanEna prakArENa bhrAtRNAM viruddham aparAdhyadbhistESAM durbbalAni manAMsi vyAghAtayadbhizca yuSmAbhiH khrISTasya vaiparItyEnAparAdhyatE|
Mnapotenda dhambi dhidi ya ndugu zenu kwa njia hii na kujeruhi dhamiri zao zilizo dhaifu, mnamkosea Kristo.
13 atO hEtOH pizitAzanaM yadi mama bhrAtu rvighnasvarUpaM bhavEt tarhyahaM yat svabhrAtu rvighnajanakO na bhavEyaM tadarthaM yAvajjIvanaM pizitaM na bhOkSyE| (aiōn g165)
Kwa hiyo, kama kile ninachokula kitamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke. (aiōn g165)

< 1 karinthinaH 8 >