< 1 karinthinaH 4 >
1 lOkA asmAn khrISTasya paricArakAn Izvarasya nigUThavAkyadhanasyAdhyakSAMzca manyantAM|
Basi, watu na watuhesabu sisi kuwa tu watumishi wa Kristo na mawakili wa siri za Mungu.
2 kinjca dhanAdhyakSENa vizvasanIyEna bhavitavyamEtadEva lOkai ryAcyatE|
Tena, litakiwalo ni mawakili waonekane kuwa waaminifu.
3 atO vicArayadbhi ryuSmAbhiranyaiH kaizcin manujai rvA mama parIkSaNaM mayAtIva laghu manyatE 'hamapyAtmAnaM na vicArayAmi|
Lakini kwangu mimi ni jambo dogo sana kwamba nihukumiwe na ninyi au na mahakama yoyote ya kibinadamu. Naam, hata mimi mwenyewe sijihukumu.
4 mayA kimapyaparAddhamityahaM na vEdmi kintvEtEna mama niraparAdhatvaM na nizcIyatE prabhurEva mama vicArayitAsti|
Dhamiri yangu ni safi, lakini hilo halinihesabii kuwa asiye na hatia. Bwana ndiye anihukumuye.
5 ata upayuktasamayAt pUrvvam arthataH prabhOrAgamanAt pUrvvaM yuSmAbhi rvicArO na kriyatAM| prabhurAgatya timirENa pracchannAni sarvvANi dIpayiSyati manasAM mantraNAzca prakAzayiSyati tasmin samaya IzvarAd Ekaikasya prazaMsA bhaviSyati|
Kwa hiyo msihukumu jambo lolote kabla ya wakati wake. Ngojeni mpaka Bwana atakapokuja. Yeye atayaleta nuruni mambo yale yaliyofichwa gizani, na kuweka wazi nia za mioyo ya wanadamu. Wakati huo kila mmoja atapokea sifa anayostahili kutoka kwa Mungu.
6 hE bhrAtaraH sarvvANyEtAni mayAtmAnam ApallavanjcOddizya kathitAni tasyaitat kAraNaM yuyaM yathA zAstrIyavidhimatikramya mAnavam atIva nAdariSyadhba ItthanjcaikEna vaiparItyAd aparENa na zlAghiSyadhba EtAdRzIM zikSAmAvayOrdRSTAntAt lapsyadhvE|
Basi ndugu zangu, mambo haya nimeyafanya kwangu binafsi na Apolo kwa faida yenu, ili mweze kujifunza kutoka kwetu maana ya ule usemi usemao, “Msivuke zaidi ya yale yaliyoandikwa.” Hivyo hamtajivunia mtu fulani na kumdharau mwingine.
7 aparAt kastvAM vizESayati? tubhyaM yanna datta tAdRzaM kiM dhArayasi? adattEnEva dattEna vastunA kutaH zlAghasE?
Kwa maana ni nani aliyewafanya kuwa tofauti na wengine? Ni nini mlicho nacho ambacho hamkupokea? Nanyi kama mlipokea, kwa nini mnajivuna kama vile hamkupokea?
8 idAnImEva yUyaM kiM tRptA labdhadhanA vA? asmAsvavidyamAnESu yUyaM kiM rAjatvapadaM prAptAH? yuSmAkaM rAjatvaM mayAbhilaSitaM yatastEna yuSmAbhiH saha vayamapi rAjyAMzinO bhaviSyAmaH|
Sasa tayari mnayo yale yote mnayohitaji! Tayari mmekwisha kuwa matajiri! Mmekuwa wafalme, tena bila sisi! Laiti mngekuwa wafalme kweli ili na sisi tupate kuwa wafalme pamoja nanyi!
9 prEritA vayaM zESA hantavyAzcEvEzvarENa nidarzitAH| yatO vayaM sarvvalOkAnAm arthataH svargIyadUtAnAM mAnavAnAnjca kautukAspadAni jAtAH|
Kwa maana ninaona kwamba Mungu ametuweka sisi mitume katika nafasi ya mwisho kabisa, kama watu waliohukumiwa kufa kwenye uwanja wa tamasha, kwa sababu tumefanywa kuwa maonyesho kwa ulimwengu wote, kwa malaika na kwa wanadamu pia.
10 khrISTasya kRtE vayaM mUPhAH kintu yUyaM khrISTEna jnjAninaH, vayaM durbbalA yUyanjca sabalAH, yUyaM sammAnitA vayanjcApamAnitAH|
Kwa ajili ya Kristo sisi ni wajinga, lakini ninyi mna hekima sana ndani ya Kristo. Sisi tu dhaifu, lakini ninyi mna nguvu. Tunadharauliwa, lakini ninyi mnaheshimiwa.
11 vayamadyApi kSudhArttAstRSNArttA vastrahInAstAPitA AzramarahitAzca santaH
Mpaka saa hii tuna njaa na kiu, tu uchi, tumepigwa na hatuna makao.
12 karmmaNi svakarAn vyApArayantazca duHkhaiH kAlaM yApayAmaH| garhitairasmAbhirAzIH kathyatE dUrIkRtaiH sahyatE ninditaiH prasAdyatE|
Tunafanya kazi kwa bidii kwa mikono yetu wenyewe. Tunapolaaniwa, tunabariki, tunapoteswa, tunastahimili,
13 vayamadyApi jagataH sammArjanIyOgyA avakarA iva sarvvai rmanyAmahE|
tunaposingiziwa, tunajibu kwa upole. Mpaka sasa tumekuwa kama takataka ya dunia na uchafu wa ulimwengu.
14 yuSmAn trapayitumahamEtAni likhAmIti nahi kintu priyAtmajAniva yuSmAn prabOdhayAmi|
Siwaandikii mambo haya ili kuwaaibisha, bali ili kuwaonya, kama wanangu wapendwa.
15 yataH khrISTadharmmE yadyapi yuSmAkaM dazasahasrANi vinEtArO bhavanti tathApi bahavO janakA na bhavanti yatO'hamEva susaMvAdEna yIzukhrISTE yuSmAn ajanayaM|
Hata kama mnao walimu 10,000 katika Kristo, lakini hamna baba wengi. Mimi nilikuwa baba yenu katika Kristo Yesu kwa kuwaletea Injili.
16 atO yuSmAn vinayE'haM yUyaM madanugAminO bhavata|
Basi nawasihi igeni mfano wangu.
17 ityarthaM sarvvESu dharmmasamAjESu sarvvatra khrISTadharmmayOgyA yE vidhayO mayOpadizyantE tAn yO yuSmAn smArayiSyatyEvambhUtaM prabhOH kRtE priyaM vizvAsinanjca madIyatanayaM tImathiyaM yuSmAkaM samIpaM prESitavAnahaM|
Kwa sababu hii ninamtuma Timotheo, mwanangu mpendwa na mwaminifu katika Bwana. Yeye atawakumbusha kuhusu njia za maisha yangu katika Kristo Yesu, ambayo yanakubaliana na mafundisho yangu ninayofundisha katika kila kanisa.
18 aparamahaM yuSmAkaM samIpaM na gamiSyAmIti buddhvA yuSmAkaM kiyantO lOkA garvvanti|
Baadhi yenu mmekuwa na jeuri mkidhani kuwa sitafika kwenu.
19 kintu yadi prabhEricchA bhavati tarhyahamavilambaM yuSmatsamIpamupasthAya tESAM darpadhmAtAnAM lOkAnAM vAcaM jnjAsyAmIti nahi sAmarthyamEva jnjAsyAmi|
Lakini kama Bwana akipenda, nitafika kwenu mapema, nami nitapenda kujua, si tu kile wanachosema hawa watu jeuri, bali pia kujua nguvu yao.
20 yasmAdIzvarasya rAjatvaM vAgyuktaM nahi kintu sAmarthyayuktaM|
Kwa kuwa Ufalme wa Mungu si maneno matupu tu bali ni nguvu.
21 yuSmAkaM kA vAnjchA? yuSmatsamIpE mayA kiM daNPapANinA gantavyamuta prEmanamratAtmayuktEna vA?
Ninyi amueni. Je, nije kwenu na fimbo, au nije kwa upendo na kwa roho ya upole?