< 1 karinthinaH 14 >
1 yUyaM prEmAcaraNE prayatadhvam AtmikAn dAyAnapi vizESata IzvarIyAdEzakathanasAmarthyaM prAptuM cESTadhvaM|
Fuateni upendo na kutaka sana karama za roho, hasa karama ya unabii.
2 yO janaH parabhASAM bhASatE sa mAnuSAn na sambhASatE kintvIzvaramEva yataH kEnApi kimapi na budhyatE sa cAtmanA nigUPhavAkyAni kathayati;
Kwa maana mtu yeyote anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu bali anasema na Mungu. Kwa kuwa hakuna mtu yeyote anayemwelewa, kwani anasema mambo ya siri kwa roho.
3 kintu yO jana IzvarIyAdEzaM kathayati sa parESAM niSThAyai hitOpadEzAya sAntvanAyai ca bhASatE|
Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji.
4 parabhASAvAdyAtmana Eva niSThAM janayati kintvIzvarIyAdEzavAdI samitE rniSThAM janayati|
Anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, bali atoaye unabii hulijenga kanisa.
5 yuSmAkaM sarvvESAM parabhASAbhASaNam icchAmyahaM kintvIzvarIyAdEzakathanam adhikamapIcchAmi| yataH samitE rniSThAyai yEna svavAkyAnAm arthO na kriyatE tasmAt parabhASAvAdita IzvarIyAdEzavAdI zrEyAn|
Ningependa kila mmoja wenu anene kwa lugha lakini ningependa zaidi nyote mtoe unabii. Kwa kuwa yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, isipokuwa atafsiri, ili kanisa lipate kujengwa.
6 hE bhrAtaraH, idAnIM mayA yadi yuSmatsamIpaM gamyatE tarhIzvarIyadarzanasya jnjAnasya vEzvarIyAdEzasya vA zikSAyA vA vAkyAni na bhASitvA parabhASAM bhASamANEna mayA yUyaM kimupakAriSyadhvE?
Sasa ndugu zangu, kama nikija kwenu nikasema kwa lugha mpya nitawafaidia nini kama sikuwaletea ufunuo au neno la maarifa au unabii au mafundisho?
7 aparaM vaMzIvallakyAdiSu niSprANiSu vAdyayantrESu vAditESu yadi kkaNA na viziSyantE tarhi kiM vAdyaM kiM vA gAnaM bhavati tat kEna bOddhuM zakyatE?
Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, kama vile filimbi au kinubi, mtu atajuaje ni wimbo gani unaoimbwa kusipokuwa na tofauti ya upigaji?
8 aparaM raNatUryyA nisvaNO yadyavyaktO bhavEt tarhi yuddhAya kaH sajjiSyatE?
Tena kama tarumbeta haitoi sauti inayoeleweka, ni nani atakayejiandaa kwa ajili ya vita?
9 tadvat jihvAbhi ryadi sugamyA vAk yuSmAbhi rna gadyEta tarhi yad gadyatE tat kEna bhOtsyatE? vastutO yUyaM digAlApina iva bhaviSyatha|
Vivyo hivyo na ninyi, kama mkinena maneno yasiyoeleweka katika akili, mtu atajuaje mnalosema? Kwa maana mtakuwa mnasema hewani tu.
10 jagati katiprakArA uktayO vidyantE? tAsAmEkApi nirarthikA nahi;
Bila shaka ziko sauti nyingi ulimwenguni, wala hakuna isiyo na maana.
11 kintUktErarthO yadi mayA na budhyatE tarhyahaM vaktrA mlEccha iva maMsyE vaktApi mayA mlEccha iva maMsyatE|
Basi kama sielewi maana ya hiyo sauti, nitakuwa mgeni kwa yule msemaji, naye atakuwa mgeni kwangu.
12 tasmAd AtmikadAyalipsavO yUyaM samitE rniSThArthaM prAptabahuvarA bhavituM yatadhvaM,
Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani kuwa na karama za rohoni, jitahidini kuzidi sana katika karama kwa ajili ya kulijenga kanisa.
13 ataEva parabhASAvAdI yad arthakarO'pi bhavEt tat prArthayatAM|
Kwa sababu hii, yeye anenaye kwa lugha na aombe kwamba apate kutafsiri kile anachonena.
14 yadyahaM parabhASayA prarthanAM kuryyAM tarhi madIya AtmA prArthayatE, kintu mama buddhi rniSphalA tiSThati|
Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu inaomba, lakini akili yangu haina matunda.
15 ityanEna kiM karaNIyaM? aham AtmanA prArthayiSyE buddhyApi prArthayiSyE; aparaM AtmanA gAsyAmi buddhyApi gAsyAmi|
Nifanyeje basi? Nitaomba kwa roho, na pia nitaomba kwa akili yangu. Nitaimba kwa roho na nitaimba kwa akili yangu pia.
16 tvaM yadAtmanA dhanyavAdaM karOSi tadA yad vadasi tad yadi ziSyEnEvOpasthitEna janEna na buddhyatE tarhi tava dhanyavAdasyAntE tathAstviti tEna vaktaM kathaM zakyatE?
Ikiwa unabariki kwa roho, mtu mwingine atakayejikuta miongoni mwa hao wasiojua, atawezaje kusema “Amen” katika kushukuru kwako, wakati haelewi unachosema?
17 tvaM samyag IzvaraM dhanyaM vadasIti satyaM tathApi tatra parasya niSThA na bhavati|
Mnaweza kuwa mnatoa shukrani kweli, sawa, lakini huyo mtu mwingine hajengeki.
18 yuSmAkaM sarvvEbhyO'haM parabhASAbhASaNE samarthO'smIti kAraNAd IzvaraM dhanyaM vadAmi;
Namshukuru Mungu kwamba mimi nanena kwa lugha kuliko ninyi nyote.
19 tathApi samitau parOpadEzArthaM mayA kathitAni panjca vAkyAni varaM na ca lakSaM parabhASIyAni vAkyAni|
Lakini ndani ya kanisa ni afadhali niseme maneno matano ya kueleweka ili niwafundishe wengine kuliko kusema maneno 10,000 kwa lugha.
20 hE bhrAtaraH, yUyaM buddhyA bAlakAiva mA bhUta parantu duSTatayA zizavaiva bhUtvA buddhyA siddhA bhavata|
Ndugu zangu, msiwe kama watoto katika kufikiri kwenu, afadhali kuhusu uovu mwe kama watoto wachanga, lakini katika kufikiri kwenu, mwe watu wazima.
21 zAstra idaM likhitamAstE, yathA, ityavOcat parEzO'ham AbhASiSya imAn janAn| bhASAbhiH parakIyAbhi rvaktraizca paradEzibhiH| tathA mayA kRtE'pImE na grahISyanti madvacaH||
Katika Sheria imeandikwa kwamba: “Kupitia kwa watu wenye lugha ngʼeni na kupitia midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, lakini hata hivyo hawatanisikiliza,” asema Bwana.
22 ataEva tat parabhASAbhASaNaM avizcAsinaH prati cihnarUpaM bhavati na ca vizvAsinaH prati; kintvIzvarIyAdEzakathanaM nAvizvAsinaH prati tad vizvAsinaH pratyEva|
Basi kunena kwa lugha ni ishara, si kwa watu waaminio, bali kwa wasioamini, wakati unabii si kwa ajili ya wasioamini, bali kwa ajili ya waaminio.
23 samitibhuktESu sarvvESu Ekasmin sthAnE militvA parabhASAM bhASamANESu yadi jnjAnAkAgkSiNO'vizvAsinO vA tatrAgacchEyustarhi yuSmAn unmattAn kiM na vadiSyanti?
Kwa hiyo kama kanisa lote likikutana na kila mmoja akanena kwa lugha, kisha wakaingia wageni wasioelewa wasioamini, je, hawatasema kwamba wote mna wazimu?
24 kintu sarvvESvIzvarIyAdEzaM prakAzayatsu yadyavizvAsI jnjAnAkAgkSI vA kazcit tatrAgacchati tarhi sarvvairEva tasya pApajnjAnaM parIkSA ca jAyatE,
Lakini kama mtu asiyeamini au asiyeelewa akiingia wakati kila mtu anatoa unabii, ataaminishwa na watu wote kuwa yeye ni mwenye dhambi na kuhukumiwa na wote,
25 tatastasyAntaHkaraNasya guptakalpanAsu vyaktIbhUtAsu sO'dhOmukhaH patan IzvaramArAdhya yuSmanmadhya IzvarO vidyatE iti satyaM kathAmEtAM kathayiSyati|
nazo siri za moyo wake zitawekwa wazi. Kwa hiyo ataanguka chini na kumwabudu Mungu akikiri, “Kweli Mungu yuko katikati yenu!”
26 hE bhrAtaraH, sammilitAnAM yuSmAkam EkEna gItam anyEnOpadEzO'nyEna parabhASAnyEna aizvarikadarzanam anyEnArthabOdhakaM vAkyaM labhyatE kimEtat? sarvvamEva paraniSThArthaM yuSmAbhiH kriyatAM|
Basi tuseme nini ndugu zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana wimbo, au neno la mafundisho, au ufunuo, lugha mpya au atatafsiri. Mambo yote yatendeke kwa ajili ya kulijenga kanisa.
27 yadi kazcid bhASAntaraM vivakSati tarhyEkasmin dinE dvijanEna trijanEna vA parabhASA kathyatAM tadadhikairna kathyatAM tairapi paryyAyAnusArAt kathyatAM, EkEna ca tadarthO bOdhyatAM|
Kama mtu yeyote akinena kwa lugha, basi waseme watu wawili au watatu si zaidi, mmoja baada ya mwingine na lazima awepo mtu wa kutafsiri.
28 kintvarthAbhidhAyakaH kO'pi yadi na vidyatE tarhi sa samitau vAcaMyamaH sthitvEzvarAyAtmanE ca kathAM kathayatu|
Lakini kama hakuna mtu wa kutafsiri, hao watu na wanyamaze kimya kanisani na wanene na nafsi zao wenyewe na Mungu.
29 aparaM dvau trayO vEzvarIyAdEzavaktAraH svaM svamAdEzaM kathayantu tadanyE ca taM vicArayantu|
Manabii wawili au watatu wanene na wengine wapime yale yasemwayo.
30 kintu tatrAparENa kEnacit janEnEzvarIyAdEzE labdhE prathamEna kathanAt nivarttitavyaM|
Kama mtu yeyote aliyeketi karibu, akipata ufunuo, basi yule wa kwanza na anyamaze.
31 sarvvE yat zikSAM sAntvanAnjca labhantE tadarthaM yUyaM sarvvE paryyAyENEzvarIyAdEzaM kathayituM zaknutha|
Kwa maana wote mnaweza kutoa unabii, mmoja baada ya mwingine, ili kila mtu apate kufundishwa na kutiwa moyo.
32 IzvarIyAdEzavaktRNAM manAMsi tESAm adhInAni bhavanti|
Roho za manabii huwatii manabii.
33 yata IzvaraH kuzAsanajanakO nahi suzAsanajanaka EvEti pavitralOkAnAM sarvvasamitiSu prakAzatE|
Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni Mungu wa amani. Kama ilivyo katika makusanyiko yote ya watakatifu,
34 aparanjca yuSmAkaM vanitAH samitiSu tUSNImbhUtAstiSThantu yataH zAstralikhitEna vidhinA tAH kathApracAraNAt nivAritAstAbhi rnighrAbhi rbhavitavyaM|
wanawake wanapaswa kuwa kimya kanisani. Hawaruhusiwi kusema, bali wanyenyekee kama sheria isemavyo.
35 atastA yadi kimapi jijnjAsantE tarhi gEhESu patIn pRcchantu yataH samitimadhyE yOSitAM kathAkathanaM nindanIyaM|
Kama wakitaka kuuliza kuhusu jambo lolote, wawaulize waume zao nyumbani. Kwa maana ni aibu kwa mwanamke kuzungumza kanisani.
36 aizvaraM vacaH kiM yuSmattO niragamata? kEvalaM yuSmAn vA tat kim upAgataM?
Je, neno la Mungu lilianzia kwenu? Au ni ninyi tu ambao neno la Mungu limewafikia?
37 yaH kazcid AtmAnam IzvarIyAdEzavaktAram AtmanAviSTaM vA manyatE sa yuSmAn prati mayA yad yat likhyatE tatprabhunAjnjApitam ItyurarI karOtu|
Kama mtu yeyote akidhani kwamba yeye ni nabii, au ana karama za rohoni, basi na akubali kwamba haya ninayoandika ni maagizo kutoka kwa Bwana.
38 kintu yaH kazcit ajnjO bhavati sO'jnja Eva tiSThatu|
Kama mtu akipuuza jambo hili yeye mwenyewe atapuuzwa.
39 ataEva hE bhrAtaraH, yUyam IzvarIyAdEzakathanasAmarthyaM labdhuM yatadhvaM parabhASAbhASaNamapi yuSmAbhi rna nivAryyatAM|
Kwa hiyo ndugu zangu, takeni sana kutoa unabii na msikataze watu kusema kwa lugha.
40 sarvvakarmmANi ca vidhyanusArataH suparipATyA kriyantAM|
Lakini kila kitu kitendeke kwa heshima na kwa utaratibu.