< လူကး 23 >

1 တတး သဘာသ္ထား သရွွလောကာ ဥတ္ထာယ တံ ပီလာတသမ္မုခံ နီတွာပြောဒျ ဝက္တုမာရေဘိရေ,
Kisha umati wote wa watu ukainuka na kumpeleka Yesu kwa Pilato.
2 သွမဘိၐိက္တံ ရာဇာနံ ဝဒန္တံ ကဲမရရာဇာယ ကရဒါနံ နိၐေဓန္တံ ရာဇျဝိပရျျယံ ကုရ္တ္တုံ ပြဝရ္တ္တမာနမ် ဧန ပြာပ္တာ ဝယံ၊
Nao wakaanza kumshtaki wakisema: “Tumemwona huyu mtu akipotosha taifa letu, akiwazuia watu wasilipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Kristo, mfalme.”
3 တဒါ ပီလာတသ္တံ ပၖၐ္ဋဝါန် တွံ ကိံ ယိဟူဒီယာနာံ ရာဇာ? သ ပြတျုဝါစ တွံ သတျမုက္တဝါန်၊
Basi Pilato akamuuliza Yesu, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe wasema.”
4 တဒါ ပီလာတး ပြဓာနယာဇကာဒိလောကာန် ဇဂါဒ်, အဟမေတသျ ကမပျပရာဓံ နာပ္တဝါန်၊
Pilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”
5 တတသ္တေ ပုနး သာဟမိနော ဘူတွာဝဒန်, ဧၐ ဂါလီလ ဧတတ္သ္ထာနပရျျန္တေ သရွွသ္မိန် ယိဟူဒါဒေၑေ သရွွာလ္လောကာနုပဒိၑျ ကုပြဝၖတ္တိံ ဂြာဟီတဝါန်၊
Lakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”
6 တဒါ ပီလာတော ဂါလီလပြဒေၑသျ နာမ ၑြုတွာ ပပြစ္ဆ, ကိမယံ ဂါလီလီယော လောကး?
Pilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?”
7 တတး သ ဂါလီလ္ပြဒေၑီယဟေရောဒြာဇသျ တဒါ သ္ထိတေသ္တသျ သမီပေ ယီၑုံ ပြေၐယာမာသ၊
Alipofahamu kwamba Yesu alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu.
8 တဒါ ဟေရောဒ် ယီၑုံ ဝိလောကျ သန္တုတောၐ, ယတး သ တသျ ဗဟုဝၖတ္တာန္တၑြဝဏာတ် တသျ ကိဉိစဒါၑ္စရျျကရ္မ္မ ပၑျတိ ဣတျာၑာံ ကၖတွာ ဗဟုကာလမာရဘျ တံ ဒြၐ္ဋုံ ပြယာသံ ကၖတဝါန်၊
Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha.
9 တသ္မာတ် တံ ဗဟုကထား ပပြစ္ဆ ကိန္တု သ တသျ ကသျာပိ ဝါကျသျ ပြတျုတ္တရံ နောဝါစ၊
Herode akamuuliza maswali mengi, lakini Yesu hakumjibu lolote.
10 အထ ပြဓာနယာဇကာ အဓျာပကာၑ္စ ပြောတ္တိၐ္ဌန္တး သာဟသေန တမပဝဒိတုံ ပြာရေဘိရေ၊
Wakati huo viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwepo wakitoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
11 ဟေရောဒ် တသျ သေနာဂဏၑ္စ တမဝဇ္ဉာယ ဥပဟာသတွေန ရာဇဝသ္တြံ ပရိဓာပျ ပုနး ပီလာတံ ပြတိ တံ ပြာဟိဏောတ်၊
Herode na askari wake wakamdhihaki Yesu na kumfanyia mzaha. Wakamvika vazi zuri sana, wakamrudisha kwa Pilato.
12 ပူရွွံ ဟေရောဒ္ပီလာတယေား ပရသ္ပရံ ဝဲရဘာဝ အာသီတ် ကိန္တု တဒ္ဒိနေ ဒွယော ရ္မေလနံ ဇာတမ်၊
Siku hiyo, Herode na Pilato wakawa marafiki; kabla ya jambo hili walikuwa na uadui kati yao.
13 ပၑ္စာတ် ပီလာတး ပြဓာနယာဇကာန် ၑာသကာန် လောကာံၑ္စ ယုဂပဒါဟူယ ဗဘာၐေ,
Basi Pilato akawaita pamoja viongozi wa makuhani, viongozi wengine na watu,
14 ရာဇျဝိပရျျယကာရကောယမ် ဣတျုက္တွာ မနုၐျမေနံ မမ နိကဋမာနဲၐ္ဋ ကိန္တု ပၑျတ ယုၐ္မာကံ သမက္ၐမ် အသျ ဝိစာရံ ကၖတွာပိ ပြောက္တာပဝါဒါနုရူပေဏာသျ ကောပျပရာဓး သပြမာဏော န ဇာတး,
akawaambia, “Ninyi mlimleta huyu mtu kwangu kana kwamba ni mtu anayewachochea watu ili waasi. Nimemhoji mbele yenu nami nimeona hakuna msingi wowote wa mashtaka yenu dhidi yake.
15 ယူယဉ္စ ဟေရောဒး သန္နိဓော် ပြေၐိတာ မယာ တတြာသျ ကောပျပရာဓသ္တေနာပိ န ပြာပ္တး၊ ပၑျတာနေန ဝဓဟေတုကံ ကိမပိ နာပရာဒ္ဓံ၊
Wala Herode hakumwona na kosa lolote, ndiyo sababu amemrudisha kwetu. Kama mnavyoona, mtu huyu hakufanya jambo lolote linalostahili kifo.
16 တသ္မာဒေနံ တာဍယိတွာ ဝိဟာသျာမိ၊
Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi na kumwachia.” [
17 တတြောတ္သဝေ တေၐာမေကော မောစယိတဝျး၊
Kwa kuwa ilikuwa lazima kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa Sikukuu.]
18 ဣတိ ဟေတောသ္တေ ပြောစ္စဲရေကဒါ ပြောစုး, ဧနံ ဒူရီကၖတျ ဗရဗ္ဗာနာမာနံ မောစယ၊
Ndipo watu wote wakapiga kelele kwa pamoja, “Mwondoe mtu huyo! Tufungulie Baraba!”
19 သ ဗရဗ္ဗာ နဂရ ဥပပ္လဝဝဓာပရာဓာဘျာံ ကာရာယာံ ဗဒ္ဓ အာသီတ်၊
(Baraba alikuwa amefungwa gerezani kwa sababu ya maasi yaliyokuwa yametokea mjini, na kwa ajili ya uuaji.)
20 ကိန္တု ပီလာတော ယီၑုံ မောစယိတုံ ဝါဉ္ဆန် ပုနသ္တာနုဝါစ၊
Pilato, akitaka kumwachia Yesu, akasema nao tena.
21 တထာပျေနံ ကြုၑေ ဝျဓ ကြုၑေ ဝျဓေတိ ဝဒန္တသ္တေ ရုရုဝုး၊
Lakini wao wakaendelea kupiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!”
22 တတး သ တၖတီယဝါရံ ဇဂါဒ ကုတး? သ ကိံ ကရ္မ္မ ကၖတဝါန်? နာဟမသျ ကမပိ ဝဓာပရာဓံ ပြာပ္တး ကေဝလံ တာဍယိတွာမုံ တျဇာမိ၊
Kwa mara ya tatu, Pilato akawauliza, “Kwani amefanya kosa gani huyu mtu? Sikuona kwake sababu yoyote inayostahili adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi, na kisha nitamwachia.”
23 တထာပိ တေ ပုနရေနံ ကြုၑေ ဝျဓ ဣတျုက္တွာ ပြောစ္စဲရ္ဒၖဎံ ပြာရ္ထယာဉ္စကြိရေ;
Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu zaidi, wakidai kwamba Yesu asulubiwe. Hivyo, kelele zao zikashinda.
24 တတး ပြဓာနယာဇကာဒီနာံ ကလရဝေ ပြဗလေ သတိ တေၐာံ ပြာရ္ထနာရူပံ ကရ္တ္တုံ ပီလာတ အာဒိဒေၑ၊
Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu kwamba madai yao yatimizwe.
25 ရာဇဒြောဟဝဓယောရပရာဓေန ကာရာသ္ထံ ယံ ဇနံ တေ ယယာစိရေ တံ မောစယိတွာ ယီၑုံ တေၐာမိစ္ဆာယာံ သမာရ္ပယတ်၊
Akamfungua yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika uasi dhidi ya serikali na mauaji. Akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfanyie watakavyo.
26 အထ တေ ယီၑုံ ဂၖဟီတွာ ယာန္တိ, ဧတရှိ ဂြာမာဒါဂတံ ၑိမောနနာမာနံ ကုရီဏီယံ ဇနံ ဓၖတွာ ယီၑေား ပၑ္စာန္နေတုံ တသျ သ္ကန္ဓေ ကြုၑမရ္ပယာမာသုး၊
Walipokuwa wakienda naye, wakamkamata mtu mmoja aitwaye Simoni mwenyeji wa Kirene, aliyekuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shambani. Wakambebesha msalaba, wakamlazimisha auchukue nyuma ya Yesu.
27 တတော လောကာရဏျမဓျေ ဗဟုသ္တြိယော ရုဒတျော ဝိလပန္တျၑ္စ ယီၑေား ပၑ္စာဒ် ယယုး၊
Idadi kubwa ya watu wakamfuata Yesu, wakiwamo wanawake waliokuwa wakimlilia na kumwombolezea.
28 ကိန္တု သ ဝျာဃုဋျ တာ ဥဝါစ, ဟေ ယိရူၑာလမော နာရျျော ယုယံ မဒရ္ထံ န ရုဒိတွာ သွာရ္ထံ သွာပတျာရ္ထဉ္စ ရုဒိတိ;
Yesu akawageukia, akawaambia, “Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi bali jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu.
29 ပၑျတ ယး ကဒါပိ ဂရ္ဘဝတျော နာဘဝန် သ္တနျဉ္စ နာပါယယန် တာဒၖၑီ ရွန္ဓျာ ယဒါ ဓနျာ ဝက္ၐျန္တိ သ ကာလ အာယာတိ၊
Kwa maana wakati utafika mtakaposema, ‘Wamebarikiwa wanawake tasa, ambao matumbo yao hayakuzaa, wala matiti yao hayakunyonyesha!’
30 တဒါ ဟေ ၑဲလာ အသ္မာကမုပရိ ပတတ, ဟေ ဥပၑဲလာ အသ္မာနာစ္ဆာဒယတ ကထာမီဒၖၑီံ လောကာ ဝက္ၐျန္တိ၊
Ndipo “‘wataiambia milima, “Tuangukieni!” na vilima, “Tufunikeni!”’
31 ယတး သတေဇသိ ၑာခိနိ စေဒေတဒ် ဃဋတေ တရှိ ၑုၐ္ကၑာခိနိ ကိံ န ဃဋိၐျတေ?
Kwa maana kama wamefanya hivi kwa mti mbichi, kwa mti mkavu itakuwaje?”
32 တဒါ တေ ဟန္တုံ ဒွါဝပရာဓိနော် တေန သာရ္ဒ္ဓံ နိနျုး၊
Watu wengine wawili wahalifu, walipelekwa pamoja na Yesu ili wakasulubiwe.
33 အပရံ ၑိရးကပါလနာမကသ္ထာနံ ပြာပျ တံ ကြုၑေ ဝိဝိဓုး; တဒ္ဒွယောရပရာဓိနောရေကံ တသျ ဒက္ၐိဏော တဒနျံ ဝါမေ ကြုၑေ ဝိဝိဓုး၊
Walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, hapo ndipo walipomsulubisha Yesu pamoja na hao wahalifu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto.
34 တဒါ ယီၑုရကထယတ်, ဟေ ပိတရေတာန် က္ၐမသွ ယတ ဧတေ ယတ် ကရ္မ္မ ကုရွွန္တိ တန် န ဝိဒုး; ပၑ္စာတ္တေ ဂုဋိကာပါတံ ကၖတွာ တသျ ဝသ္တြာဏိ ဝိဘဇျ ဇဂၖဟုး၊
Yesu akasema, “Baba, wasamehe, kwa maana hawajui walitendalo!” Wakagawana nguo zake kwa kupiga kura.
35 တတြ လောကသံဃသ္တိၐ္ဌန် ဒဒရ္ၑ; တေ တေၐာံ ၑာသကာၑ္စ တမုပဟသျ ဇဂဒုး, ဧၐ ဣတရာန် ရက္ၐိတဝါန် ယဒီၑွရေဏာဘိရုစိတော 'ဘိၐိက္တသ္တြာတာ ဘဝတိ တရှိ သွမဓုနာ ရက္ၐတု၊
Watu wakasimama hapo wakimwangalia, nao viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.”
36 တဒနျး သေနာဂဏာ ဧတျ တသ္မဲ အမ္လရသံ ဒတွာ ပရိဟသျ ပြောဝါစ,
Askari nao wakaja, wakamdhihaki. Wakamletea siki ili anywe,
37 စေတ္တွံ ယိဟူဒီယာနာံ ရာဇာသိ တရှိ သွံ ရက္ၐ၊
na wakamwambia, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
38 ယိဟူဒီယာနာံ ရာဇေတိ ဝါကျံ ယူနာနီယရောမီယေဗြီယာက္ၐရဲ ရ္လိခိတံ တစ္ဆိရသ ဦရ္ဒ္ဓွေ'သ္ထာပျတ၊
Kwenye msalaba juu ya kichwa chake, kulikuwa na maandishi haya: Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi. Maandishi haya yalikuwa yameandikwa kwa lugha za Kiyunani, Kilatini na Kiebrania.
39 တဒေါဘယပါရ္ၑွယော ရွိဒ္ဓေါ် ယာဝပရာဓိနော် တယောရေကသ္တံ ဝိနိန္ဒျ ဗဘာၐေ, စေတ္တွမ် အဘိၐိက္တောသိ တရှိ သွမာဝါဉ္စ ရက္ၐ၊
Mmoja wa wale wahalifu waliosulubiwa pamoja naye akamtukana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe mwenyewe na utuokoe na sisi.”
40 ကိန္တွနျသ္တံ တရ္ဇယိတွာဝဒတ်, ဤၑွရာတ္တဝ ကိဉ္စိဒပိ ဘယံ နာသ္တိ ကိံ? တွမပိ သမာနဒဏ္ဍောသိ,
Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akasema, “Je, wewe humwogopi Mungu, wakati uko kwenye adhabu iyo hiyo?
41 ယောဂျပါတြေ အာဝါံ သွသွကရ္မ္မဏာံ သမုစိတဖလံ ပြာပ္နုဝး ကိန္တွနေန ကိမပိ နာပရာဒ္ဓံ၊
Sisi tumehukumiwa kwa haki kwa kuwa tunapata tunayostahili kwa ajili ya matendo yetu. Lakini huyu mtu hajafanya kosa lolote.”
42 အထ သ ယီၑုံ ဇဂါဒ ဟေ ပြဘေ ဘဝါန် သွရာဇျပြဝေၑကာလေ မာံ သ္မရတု၊
Kisha akasema, “Yesu, unikumbuke utakapokuja katika Ufalme wako.”
43 တဒါ ယီၑုး ကထိတဝါန် တွာံ ယထာရ္ထံ ဝဒါမိ တွမဒျဲဝ မယာ သာရ္ဒ္ဓံ ပရလောကသျ သုခသ္ထာနံ ပြာပ္သျသိ၊
Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
44 အပရဉ္စ ဒွိတီယယာမာတ် တၖတီယယာမပရျျန္တံ ရဝေသ္တေဇသောန္တရှိတတွာတ် သရွွဒေၑော'န္ဓကာရေဏာဝၖတော
Ilikuwa kama saa sita mchana, nalo giza likafunika nchi yote hadi saa tisa,
45 မန္ဒိရသျ ယဝနိကာ စ ဆိဒျမာနာ ဒွိဓာ ဗဘူဝ၊
kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili.
46 တတော ယီၑုရုစ္စဲရုဝါစ, ဟေ ပိတ ရ္မမာတ္မာနံ တဝ ကရေ သမရ္ပယေ, ဣတျုက္တွာ သ ပြာဏာန် ဇဟော်၊
Yesu akapaza sauti yake akasema, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.
47 တဒဲတာ ဃဋနာ ဒၖၐ္ဋွာ ၑတသေနာပတိရီၑွရံ ဓနျမုက္တွာ ကထိတဝါန် အယံ နိတာန္တံ သာဓုမနုၐျ အာသီတ်၊
Yule jemadari alipoona yaliyotukia, akamsifu Mungu, akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.”
48 အထ ယာဝန္တော လောကာ ဒြၐ္ဋုမ် အာဂတာသ္တေ တာ ဃဋနာ ဒၖၐ္ဋွာ ဝက္ၐးသု ကရာဃာတံ ကၖတွာ ဝျာစုဋျ ဂတား၊
Watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hili walipoyaona hayo, wakapigapiga vifua vyao kwa huzuni na kwenda zao.
49 ယီၑော ရ္ဇ္ဉာတယော ယာ ယာ ယောၐိတၑ္စ ဂါလီလသ္တေန သာရ္ဒ္ဓမာယာတာသ္တာ အပိ ဒူရေ သ္ထိတွာ တတ် သရွွံ ဒဒၖၑုး၊
Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wale wanawake waliokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyatazama mambo haya.
50 တဒါ ယိဟူဒီယာနာံ မန္တြဏာံ ကြိယာဉ္စာသမ္မနျမာန ဤၑွရသျ ရာဇတွမ် အပေက္ၐမာဏော
Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,
51 ယိဟူဒိဒေၑီယော 'ရိမထီယနဂရီယော ယူၐဖ္နာမာ မန္တြီ ဘဒြော ဓာရ္မ္မိကၑ္စ ပုမာန္
lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa.
52 ပီလာတာန္တိကံ ဂတွာ ယီၑော ရ္ဒေဟံ ယယာစေ၊
Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
53 ပၑ္စာဒ် ဝပုရဝရောဟျ ဝါသသာ သံဝေၐ္ဋျ ယတြ ကောပိ မာနုၐော နာသ္ထာပျတ တသ္မိန် ၑဲလေ သွာတေ ၑ္မၑာနေ တဒသ္ထာပယတ်၊
Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado.
54 တဒ္ဒိနမာယောဇနီယံ ဒိနံ ဝိၑြာမဝါရၑ္စ သမီပး၊
Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.
55 အပရံ ယီၑုနာ သာရ္ဒ္ဓံ ဂါလီလ အာဂတာ ယောၐိတး ပၑ္စာဒိတွာ ၑ္မၑာနေ တတြ ယထာ ဝပုး သ္ထာပိတံ တစ္စ ဒၖၐ္ဋွာ
Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yosefu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa.
56 ဝျာဃုဋျ သုဂန္ဓိဒြဝျတဲလာနိ ကၖတွာ ဝိဓိဝဒ် ဝိၑြာမဝါရေ ဝိၑြာမံ စကြုး၊
Kisha wakarudi nyumbani, wakaandaa manukato na marhamu ya kuupaka huo mwili. Lakini wakapumzika siku ya Sabato kama ilivyoamriwa.

< လူကး 23 >