< Luke 6 >

1 Jisua'n Sabath nîn loilâi a pala, a ruoisingeiin buvûi an china, an kutin an muoi minsâia, an sâka.
Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2 Pharisee senkhat ngeiin, “Ithomo, ei Balamin Sabathnia tho loi ranga ai ti hah, nin thoa?” tiin an rekela.
Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
3 Jisua'n an kôma, “David le a mingeiin an vonchâm lâia an itho hah nin pore ngâi loi mini?
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4 Pathien Ina a sea, Pathien ranga ipêk, Ochaingei tiloiin chu tûte sâk rang Balam niloi vâipôl a laka, a sâka, a mingei a minsâk hah?” tiin a thuona.
Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
5 Hanchu Jisua'n, “Miriem Nâipasal hih Sabathni Pumapa ani” a tipe ngeia.
Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
6 Hanchu, Sabathni danga chu Jisua Synagog taka a sea, a minchu ngeia, mahan mi inkhat kut changtienga phalkhatthi a oma.
Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7 Balam minchupungei senkhat le Pharisee senkhat ngeiin Jisua an nôn theina rang abi rokin Sabathnin a mindam le a mindam loi an enrichika.
Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8 Jisua'n an mindonna a rieta, damloi kôma, “Inding inla moton tieng hin hong roh,” a tia, hanchu ânthoia ânding zoia.
Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9 Hanchu Jisua'n an kôma, “Ei Balamin Sabathnia, asa rangin mo, dûk mintong rangin mo? mi phal. Mi ringna min jôk rangin mo, minmang rangin mo?” a tia.
Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
10 An rêngin a en titira, hanchu, a kôma, “Nu kut phar roh” a tia. A phara, a kut a dam pe zoia.
Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11 Hanchu, an taksi oka, Jisua chunga an tho thei rang lam an inkereng zoia.
Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12 Ma zora han Jisua chubai tho rangin muol chunga a sea, mahan, Pathien kôm jânkhovârin chubai a thoa.
Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13 Hanchu khuo a hong vârin chu a ruoisingei a koibûma, an lâia mi sômleinik a thanga, Tîrton, ai be ngei chu,
Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14 Simon (Peter, ai phuo) le a nâipa Andrew; Jacob le John, Philip le Bartholomew,
Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15 Mathew le Thomas, Alpheaus nâipasal Jacob le Simon (zelot an ti)
Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16 Jacob nâipasal Judas le a minsûrpu, Judas Iscariot ngei anni.
Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17 Hanchu, Jisua le tîrtonngei hah muol chung renga an juong chuma, a ruoisi tamtak ngei leh mun inchamna an indinga, ha muna han mipui tamtak Judea ram murdi renga, Jerusalem renga, tuikhanglien pang khopuilienngei, Tyre le Sidon renga mingei an oma.
Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18 A chongril rangâi rang le an natna ngei mindam ranga hong anni. Ratha saloi ngeiin dûk an mintong ngei khom an honga an dama.
Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19 A sinthotheina a jôk sikin, mipui murdi'n ama tôn rangin an bôka, an rêngin an dam pak zoi.
Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20 Jisua'n, a ruoisingei a ena, a tia, “Nangni ânriengngei chu satvur nin ni, Pathien Rêngram nin ta ani sikin.
Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 Nangni atûna vonchâmngei, chu satvur nin ni, Nin la khop rang sikin. Nangni atûna a chapngei, chu satvur nin ni, Nan lân nui rang sikin!”
Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22 “Miriem Nâipasal sika, mingeiin nangni an mumâka, nangni an henga, nangni an êroa, puoloingei nangni an ti tena, chu satvur nin ni.
“Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23 Ma anghan a hong tungin chu râisânin lâm roi. Invâna, râisânman luttak nin rangin dara a om sikin. Asikchu an richibulngei khomin dêipungei chunga ma angdên han an lei tho ngâi ani.”
Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24 “Ania, nangni atûna ânchongngei, nin chung ântak, nunkhohoi nin mang zoi sikin!
Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25 Nangni atûna akhopngei, nin chung ântak, Nan la châm rang sikin! Nangni atûna ânnui ngei nin chung ântak, Inngûia nan la chap rang sikin!”
Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26 “Mi tinin nangni an minpâk tenan chu nin chung ântak, ha ang dêna han an richibulngei khomin dêipu dikloingei an lei manpâk ngâi ani.”
Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27 “Ke he ariet murdi'n, nan râlngei lungkham ungla, nangni mumâk ngei satna rang tho pe ngei roi.
“Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28 khomâk nangni sâm ngei satvur ungla, dûk nangni tho ngei chubai tho pe roi.
Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29 Mîn na mâi a bêna anîn chu, kângkhat tieng khom do pe sa roh, mîn na kâncholi chung a lâka anîn chu asûnga khom pêk sa roh.
Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30 Mîn neinun nang an zonga anîn chu pêk roh, na ta an lâk khomin zong khâi no roh.
Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31 Nu chunga na nuomlam an tho angin mi chunga tho roh.
Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32 Mi lungkham nangni mu ngei vai lungkham nin mun te, inmo satvurna nan man ranga? mi nunsiengeii luo anni lungkham amu ngei chu anni khomin an lungkham ngâi.
“Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33 Nin chunga sin sa tho ngei vai chunga sin sa nin thoa aninte inmo satvurna nin man ranga? Mi nunsiengeiin luo ha anga han chu an tho ngâi.
Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34 Man nôk ranga na sabei ngei kôma vai ne pêka aninte, inmo satvurna na man ranga? Mi nunsiengeiin luo, abipui man nôkna rangin chu, mi nunsiengei kôma an pêk ngâi!
Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35 Ni thei no nih! Na râlngei lungkham inla, an satna rang sin pe ngei roh, ite man nôk rangin sabei loiin mintâng ngei roh. Hanchu, râisânman alien man nan ta, Ânchungtak Pathien nâingei nîng nin tih. Ama chu râisânna chang riet loi ngei le mi nunsiengei a lungkham ngâi.
Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36 Nin pa'n mi a lungkham angin nangni khomin lungkham roi.”
Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37 “Midang jêk no ungla, Pathien'n nangni jêk no nih. Midang dem no ungla, Pathien'n nangni dem no nih. Mi ngâidam ungla, Pathien'n nangni ngâidam a tih.
“Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38 Pêk ungla, hanchu, Pathien'n nangni pêng a tih, mintena sa, namdên êt, le inîkin, min liemin, nin kuta akeng theidôrin nangni pêng a tih. Mi nin minte pena nanâka han Pathien'n nangni minte pênah a tih,” a tia.
Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
39 Jisua'n hi chongmintêk hih a rila, “Mitcho inkhatin mitcho adang ruoi thei mak; a ruoia anîn chu an ruonin khursodopa tâk an tih.
Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40 Minchupu nêkin ânchûpu lien uol maka, han, ânchupu khom a zoi tikin chu minchupu ang a tih.
Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41 Ithomo, ni mita thingbong a om mindon bak loia, na lâibungpa mita ronok a om hah ne en?
Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42 Inmo ni mita thingbong mu loiin, na lâibungpa kôma, ni mita ronok nang lei kêl pe rong ni ti thei ranga? Asarotholngei, Ni mita thingbong kêl bak inla, hanchu, na lâibungpa mita ronok mu minthâr thei ni tih.”
Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43 “Thingkung adamin mara saloi inra maka, thingkung damloiin mara sa inra ngâi mak.
“Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44 Thingkung tin an mara chita ei riet; riling rânga theichang pot ngâi mak chea, riling ranga grape pot ngâi mak che.
Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45 Mi sân chu a mulung sûnga neinun sa a kelsuoa, mi nunsien chu a mulung sûnga neinun saloi a kelsuo ngâi, mulung sûnga asip hah kêng bâiin a misîrsuok ngâi.”
Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46 “Ithomo ko chongbe jôm loia, Pumapa, Pumapa, mi nan ti?
“Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47 Tukhom ko kôma honga, ko chong rangâia ko chongjôm chu imo ai ang nangni ril ki tih.
Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48 Ha mi hah chu a in sin lungpui chunga a lungphûm inthûk taka phun ang hah ani. Tuilienin a suka, innîk maka, adet ngita sin ani sikin.
Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49 Ania, tutukhom ke he rieta, ko chong jôm loi chu, lungphûm loia in sina, tuilienin asuka, achim kelena, ânphôi chit ang hah ani,” a tia.
Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”

< Luke 6 >