< Oufunuo 6 >

1 Nenywa omwanangole nahigula emihuri saba, nonvwa omo daahwehwomi wane ayanga hwizu lyalyalengene nashi olapuho ogwemvula “Enzaa!”
Kisha nikaangalia wakati Mwana-Kondoo akivunja ile lakiri ya kwanza miongoni mwa zile saba. Ndipo nikasikia mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akisema kwa sauti kama ya radi: “Njoo!”
2 Nenya paline fwalasi enzelu! Yapandile alinembakuli, wapata itaji. Afumile aje amenile yamena aje aamene.
Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mweupe! Yeye aliyempanda alikuwa na upinde, naye akapewa taji, akampanda akatoka akiwa kama mshindi aelekeaye katika kushinda.
3 Owakati owo omwanangole nahigula omuhuri owa bhele, nonvwa owewomi owabhele ayanga, “Enzaa!”
Alipoivunja ile lakiri ya pili, nikamsikia yule kiumbe wa pili mwenye uhai akisema, “Njoo!”
4 Nantele efalasi iyamwabho wafumila - oshamwamu nansiomwote. Yapende apete oruhusa yahwefwe owinza mnsi, aje abhantu bhabholanaje. Ono yapandile apete ipanga igosi.
Ndipo akatokea farasi mwingine mwekundu sana. Yeye aliyempanda akapewa uwezo wa kuondoa amani duniani na kuwafanya watu wauane. Yeye akapewa upanga mkubwa.
5 Omwanangole nahigula gula omuhuri owa tatu, nonvwa owomi owatatu ayanga, “Enzaa!” Nalola efalasi enjilu, yapandile ali nemizani mkhono gwakwe.
Mwana-kondoo alipoivunja ile lakiri ya tatu, nikamsikia yule kiumbe wa tatu mwenye uhai akisema, “Njoo!” Nikatazama, na mbele yangu alikuwepo farasi mweusi! Yeye aliyempanda alikuwa na mizani mkononi mwake.
6 Nonvwa esauti yehabhoneshe aje omo wabhala ebhe womi ayanga, “empimilo eyengano huhela emoo na humpinulo zitatu evye hela emoo. Lelo osanankanye amafutane vya mwele.”
Ndipo nikasikia kile kilichokuwa kama sauti katikati ya wale viumbe wanne wenye uhai ikisema, “Kipimo kimoja cha ngano kwa mshahara wa kibarua wa siku moja, na vipimo vitatu vya shayiri kwa mshahara wa kibarua cha siku moja. Lakini usiharibu mafuta wala divai!”
7 Omwanangole nahiguye omuhuri ogwa uune, ehwonvwa esauti owe womi owaune ayanga, “Enzaa!”
Alipovunja ile lakiri ya nne, nikasikia sauti ya yule kiumbe wa nne mwenye uhai ikisema, “Njoo!”
8 Nantele nalola efalasi envuvya yapende yakwiziwe itawa lyakwe yafwiye, na hwilongo walihulondozya. Bhapete amadalaka pamwanya apadodo epensi, abude nipanga, nenzala ne mpongo, na huhanu ezya mwisengo mnsi. (Hadēs g86)
Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mwenye rangi ya kijivujivu! Yeye aliyempanda aliitwa Mauti, naye Kuzimu alikuwa akimfuata nyuma yake kwa karibu. Wakapewa mamlaka juu ya robo ya dunia, kuua kwa upanga, njaa, tauni na kwa wanyama wakali wa dunia. (Hadēs g86)
9 Wakati omwanangole nahiguye omhuri ogwa sanu, ehaloli pansi pa madhabahu huroho zyabhala bhabahli bhabudilwe huvizu elyizu lya Ngolobhe nafumilane noshuhuda bhabhaukhete athibitizye.
Mwana-kondoo alipoivunja ile lakiri ya tano, nikaona chini ya madhabahu, roho za wale waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu na kwa ajili ya ushuhuda walioutunza.
10 Bhalila hu sautu engosi, “paka ndii, Yatabhala ponti, ozelu owemwoyo nelyoli, obholonje bhabhakhala pamwanya ya pansi, awuzye ipanto elye danda lyetu?”
Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, “Hata lini, Ee Bwana Mwenyezi, uliye mtakatifu na mwaminifu, hutawahukumu na kulipiza kisasi juu ya watu waishio duniani kwa ajili ya damu yetu?”
11 Nantele shila omo apete inkanzu izelu bhabhozyewa aje bhawanziwa agole hashe hata pebhaye embazyo yonti eyatumishi amwabho na aholo bhabho abheshishe na abheshilume pabhabhaye bhashele bhabhagogwe, nashibhala bhabhagojilwe.
Kisha kila mmoja wao akapewa joho jeupe na wakaambiwa wangoje kwa muda kidogo zaidi, mpaka idadi ya ndugu zao na watumishi wenzao watakaouawa kama wao walivyouawa, itakapotimia.
12 Wakati omwanangole nahiguye omuhuri ogwa sita, nahenyizye palinitensya igosi. Isanya lyabha lilu nashi igunilaelyemenda amilu, omwezi gwabhanashi idanda.
Nikatazama akiivunja ile lakiri ya sita. Pakatokea tetemeko kuu la nchi, na jua likawa jeusi kama nguo ya gunia iliyotengenezwa kwa singa za mbuzi, na mwezi wote ukawa mwekundu kama damu.
13 Entondwe ezya mwanya zyagwa paka pansi, nashi ikwi nalilagazya amadondo gakwe owakati wisasa nauyinzanyiwa ne nvulungwe.
Nyota zilizo angani zikaanguka ardhini kama vile matunda ya mtini yasiyokomaa yaangukavyo wakati mti wake unapotikiswa na upepo mkali.
14 Emwanya ehipeli nashi ibangili lyalizyongozyewe. Kila ligamba ensinyomosu yamenze zya samiziwe pazyakheye.
Anga ikatoweka kama vile karatasi isokotwavyo, na kila mlima na kila kisiwa kikaondolewa mahali pake.
15 Nantele amwene abhensi na bhantu akhaya nabhala asimamizi ebhibho, atajili, ebhe nguvu, na kila omo yali watumwe na mmwalaogwe magamba.
Ndipo wafalme wa dunia, wakuu wote, majemadari, matajiri, wenye nguvu na kila mtu, mtumwa na mtu huru, wakajificha katika mapango na kwenye miamba ya milima.
16 Bhaga bhozya amagamba namiala, “Tigweleli! Tufisii humaso gakwe yakheye pitengo elyeshimwene afume hwilyoyo elyamwanangole.
Wakaiita milima na miamba wakisema, “Tuangukieni, mkatufiche na uso wake yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na mkatuepushe na ghadhabu ya Mwana-Kondoo!
17 Afwatane isiku igosi elyelyoyo lyabho lipalamiye, hwenu yawezizye ahwemelelee?”
Kwa maana siku ile kuu ya ghadhabu yao imewadia. Je, ni nani awezaye kustahimili?”

< Oufunuo 6 >