< Yohana 5 >

1 Baada yepo hwali neshikulukulusha Yahudi no Yesu alizubhile abhale hu Yelusalemu.
Baada ya hapo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, na Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
2 Hula hu Yelusalemu hwali ni birika pandyango gwe ngole, lyalyalihwetwa hu lugha yeShiabrania hu Bethzatha, lyape lili na matao gasanu.
Na kule Yerusalemu palikuwa na birika kwenye mlango wa kondoo, lililokuwa likiitwa kwa lugha ya Kiebrania Bethzatha, nalo lina matao matano.
3 Abhantu bhinji abhinu bhahali, ampofu, avewete, bhabhahomele bhali bhagonile mumatao ego. (Khatililaga: Amazu ge sitali 3 segabhoneha mu nakala enyinza zi mwaha. “Bhagolezezye amenze avwalanganye.”') Hwa hali owakati umo ohalozelu muhati ya Gosi na vwalanganye menze.
Idadi kubwa ya wagonjwa ilikuwemo, vipofu, viwete, au waliopooza walikuwa wamelala katika matao hayo. (Zingatia: Maneno ya mstari wa 3 hayaonekani katika nakala nzuri za kale. “Wakisubiri maji kutibuliwa.”) Kwa hakikia wakati fulani malaika alishuka ndani ya Bwana na kuyatibua maji.
4 Ola wa hali wa kwanza ahwinjile muhati amenze nagavwalanganywa oyo abhanga mwomi afumilane na hahonti hahali ha khetwe omuda ogwo.
Kwahiyo, yule ambaye alikuwa wa kwanza kuingia ndani ya baada ya maji kutibuliwa alifanywa mzima kutokana na chochote kilichokuwa kimemshika kwa wakati huo.
5 No muntu wali abhinile humaha thelathini na nane wli mhati ye matao.
Na mtu mmoja aliyekuwa ameugua kwa muda wa miaka thelathini na minane alikuwa ndani ya matao.
6 O Yesu nalolile agonile mhati ye matao nawamanya aje agonile pala omuda gwinji oYesu abhozya, “Ajile ohwanza abhe mwomi?”
Yesu alipomwona amelala ndani ya matao na baada ya kutambua kuwa amelala pale kwa muda mrefu Yesu alimwambia, “Je unataka kuwa mzima?”
7 Ola abhinu ajile, “Gosi sendi no muntu wambeshe mwi birika omuda amenze nagavwalanganywa. Lwelenga ahwinjile omuntu owenje antangulila.”
Yule mgonjwa akamjibu, “Bwana sina mtu, wa kuniweka katika birika wakati maji yanapotibuliwa. Wakati ninapojaribu kuingia mtu mwingine hunitangulia.”
8 O Yesu wabhozya, “Bhoha ayeje igodolo lya ho obhalaje.”
Yesu akamwambia, “Inuka na uchukue godoro lako na uende.”
9 Omuntu ola wapona, wega eshitala shakwe na wabhala. Isiku elyo lyali lisiku lye Sabato.
Mara yule mtu akaponywa, akachukua kintanda chake na akaenda. Na siku hiyo ilikuwa siku ya Sabato.
10 Ayahudi bhabhozya omuntu ola waponyiziwe, “Sanyono lisiku lya Sabato, solohusiwa abebe igodoro lyaho.”
Hivyo Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, “Leo ni siku ya Sabato, na hauruhusiwi kubeba godoro lako.”
11 Omwene ajile waponiziwe yayoyo wambozezye, “Ege igodoro lyaho bhalaga.”
Akajibu, yeye aliyeniponya ndiye aliyeniambia, “Chukua godoro lako na uende.”
12 Bhabhozezye, “Wenu wabhozyezye 'Ege igodoro lyaho bhalaga?'”
Wakauliza, “Ni nani aliyekuambia 'Chukua godoro lako na uende?'''
13 Haha nkashe ola waponile sagamenye, afwatanaje oYesu ali asogoye shi siri. Afuatanaje hwali awantu winji esehemu eyo.
Ingawa, yule aliyeponywa hakumjua, kwa sababu Yesu alikuwa ameondoka kwa siri. Kwa kuwa kulikuwa na watu wengi katika sehemu hiyo.
14 Pamande yakwe oYesu amweje ola umuntu mshibhanza na hubhozye, “Enya, aponole! “Uganje abhombe mbibhi nantele ogakhomana ni jambo ibhibhi sana.”
Baada ya hapo Yesu alimkuta yule mtu hekaluni na akamwambia, “Tazama, umepona! “Usitende dhambi tena usije ukapatwa na jambo baya zaidi.”
15 Omuntu ola abhalile abhabhozye Ayahudi aje oYesu wamponezye.
Yule mtu akaenda na kuwataarifu Wayahudi kuwa Yesu ndiye aliyemponya.
16 Eshi, afuatanaje amambo ego Ayahudi bhayemvezye oYesu, afuatanaje abhombile amambo ega isiku lye Sabato.
Hivyo, kwa sababu ya mambo hayo Wayahudi walimtesa Yesu, kwa sababu alifanya mambo haya siku ya Sabato.
17 O Yesu wabhabhozya, “Odaada wane abhomba embombo paka esalezi nane ebhomba embombo.”
Yesu akawambia, “Baba yangu anafanya kazi hata sasa nami nafanya kazi.”
18 Hunamuna eye Ayahudi bhahendeleye azidi bhahanzaga aje sababu yanankanye eSabato, ila hukwizye Ongolobhe oDaada wakwe, alihweshele sawa no Ngolobhe.
Kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kumtafuta ili wamuue sio tu kwa sababu ya kuivunja Sabato, bali kwa kumwita Mungu Baba yake, akijifanya kuwa sawa na Mungu.
19 O Yesu ajile, “Etesheli, etesheli, Omwana sagabhomba ahantu hahonti ila hala halolile Oise wakwe abhomba, afuatanaje hahonti habhomba Oise haheho hanzabhombe Omwana.
Yesu akawajibu, “Amini, amini, Mwana hawezi kufanya kitu chochote isipokuwa kile ambacho amemwona Baba yake anakifanya, kwa kuwa chochote Baba akifanyacho ndicho na Mwana atakachofanya.
20 Afuatanaje oDaada agene Omwana, na ahulanga kila hantu habhomba na ahaulanga amambo amagosi ashile ega ili nkamuswigage.”
Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, na amwonyesha kila kitu anachokifanya na atamwonyesha mambo makubwa kuliko haya ili kwamba mzidi kushangaa.”
21 Afuatanaje nanshi shila oDaada nafufula awafwe na abhapele owomi, sheshesho Omwana wope ahupele wowonti wagene.
Kwa kuwa kama vile ambavyo Baba awafufuavyo wafu na kuwapa uzima, halikadhalika Mwana pia humpa yeyote ampendaye.
22 Afuatane naje oDaada sahulonga wowonti, ila apiye Omwana alonje hwonti
Kwa kuwa Baba hamhukumu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote
23 ili bhonti bhamwogope Omwana sebhahu mwogopa oDaada. Umwene wasihumwogopa Omwana sahamwogope no Daada wantumile.
ili kwamba wote wamuheshimu Mwana kama vile Mwana anavyomuheshimu Baba. Yeye asiyemuheshimu Mwana hamuheshimu Baba aliyemtuma.
24 Eteshela, eteshela, omwene wahonvwa izu lyane na humweteshele wantumile ali no womi we wilawila na sagailongwa. Yaani ashilile afume hunfwa ahwinjile huwomi. (aiōnios g166)
Amini, amini, yeye asikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenituma anao uzima wa milele na hatahukumiwa. Badala yake, amepita kutoka mautini na kuingia uzimani. (aiōnios g166)
25 Eteshela, eteshela, embabhozya ensiku zihwenza na zihweli lula abhafwe nabhayovnwa izu lyakwe Omwana wa Ngolobhe, na bhonti bhabhayonvwa waikhala.
Amini, amini, nawambia wakati unakuja na sasa upo ambao wafu watasikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wote watakao sikia wataishi.
26 Nanshi shila oDaada shali nowomi mhati yakwe yoyo,
Kwa kuwa kama vile Baba alivyo na uzima ndani yake mwenyewe,
27 shesho apiye Omwana abhe no womi wope oDaada apiye Omwana amamlaka ili aje alongaje afuatanaje Mwana wa Adamu.
kadhalika amempa Mwana kuwa na uzima ndani yake, na Baba amempa Mwana mamlaka ili kwamba ahukumu kwa kuwa ni Mwana wa Adamu.
28 Munganje shangale hweli afuatanaje zihwenza ensiku abhafwe hbonti bhabhali mumakaburi bhayonvwa izu lyakwe
Msishangazwe na hili, kwa kuwa wakati unakuja ambao wafu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake
29 na bhope bhaifuma hunze: hwabhabhombaga enyinza ulyovyosyolwe womi, bhabhabhombaga embibhi oluvyosnsyo lwa longwe.
nao watatoka nje: kwa waliotenda mema kwa ufufuo wa uzima, na walio tenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.
30 Sengabhomba ahantu hahonti afume huline nene. Nanshi shehovwa, shesho shelola alonje na alonje hwane hwe lyoli afuatanaje sehwanza she songwa ane, ila shasongwa omwane wantumile.
Siwezi kufanya kitu chochote kutoka kwangu mwenyewe. Kama nisikiavyo, ndivyo ninavyo hukumu na hukumu yangu ni ya haki kwa kuwa sitafuti mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.
31 Nkashe ehwihakikisya nene, luhakikisyo lwane selwabhanga lwe lyoli.
Kama nikijishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu usingelikuwa wa kweli.
32 Ahweli wamwabho wahakikisya ahusuane emanya aje lyoli uluhakikisho lwa hakikisizya ane we lyoli.
Kuna mwingine anayeshuhudia kuhusu mimi na ninajua kwa hakika ushuhuda anaonishuhudia ni wa kweli.
33 Mutumile hwa Yohana wope ahakikisizye lyoli.
Mmetuma kwa Yohana naye ameishuhudia kweli.
34 Hata sheshi ulihakikisyo lwenduposhela selufuma hwa bhantu. Ninayasema haya ili kwamba mweze kuokolewa.
Hatahivyo, ushuhuda ninaoupokea hautoki kwa mwanadamu. Ninayasema haya ili kwamba mweze kuokolewa.
35 O Yohana ali lukhozyo lwalwa hahaga, na khozye mwahali tayari aisongwe huu muda ododo olukhozyo lwakwe.
Yohana alikuwa ni taa iliyokuwa ikiwaka na kung'ara, na mlikuwa tayari kuifurahia kwa muda kitambo nuru yake.
36 Ulwetesho lwendi nalwo gosi ashile lula lwa Yohana, humbombo zila Odaada yza mpiye azikamilisye, anzyo embombo zyezibhomba zibhonesya aje Odaada antumile.
Ushuhuda nilionao ni mkuu kuliko ule wa Yohana, kwa kazi ambazo Baba amenipa kuzikamilisha, hizo kazi nizifanyazo zashuhudia kuwa Baba amenituma.
37 Odaada wantumile yoyo ahakikisizye ahusu ane. Semuwaile ahomvwe izu lyakwe au alole obele gwakwe omuda gwagwonti.
Baba aliyenituma yeye mwenyewe ameshuhudia kuhusu mimi. Hamjawahi kusikia sauti yake wala kuona umbo lake wakati wowote.
38 Semulinalyo izu lyakwe nkalikhale muhati afuatanaje semwamwetesheye omwene wantumile.
Hamna neno lake likikaa ndani yenu kwa kuwa hamumwamini yeye aliyetumwa.
39 Mugenyelezya amazu msewa aje muhati yakwe muli owomi wewila wila, gego amazu gahakikisya ehabari zyane (aiōnios g166)
Mnayachunguza maandiko mkidhani ndani yake mna uzima wa milele, na hayo maandiko yanashuhudia habari zangu na (aiōnios g166)
40 semuhwanza ahwenez huline nkampate owomi wewilawila.
hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima wa milele.
41 Siposhela huhwhiyonvwe afume hwa wantu,
Sipokei sifa kutoka kwa watu,
42 ehwelewa aje nalumo olugano lwa Ngolobhe muhati yenyu.
lakini ninajua kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu ninyi wenyewe.
43 Enenzele hwitawa lya Daada wane, semwamposheye. Nkashe owenje ayenze hwitawa lyakwe handamwaposheye.
Nimekuja kwa jina la Baba yangu, hamukuweza kunipokea. Kama mwingine akija kwa jina lake mngempokea.
44 Aje mwahenzaga ahweteshele amwe mwamposhela esifa afume hwa kila muntu wenyu ila semuhwanza esifa yefuma hwa Ngolobhe mwene?
Je mnawezaje kuamini ninyi ambao mnapokea sifa kutoka kwa kila mmoja wenu lakini hamtafuti sifa itokayo kwa Mungu wa pekee?
45 Msagaje ane embabhatake hwitazi lya Daada. Wabhataka amwe yo Musa, ambayo mubheshele ategemele hwa mwa hale.
Msidhani mimi nitawashitaki mbele za Baba. Anayewashitaki ninyi ni Musa, ambaye ninyi mmeweka matumaini yenu kwake.
46 Mugali aje mhumweteshele oMusa, handamunetesheye nane afuatanaje ahaandishe ahusu ane.
Kama mngekuwa mnamwamini Musa, mngeniamini mimi kwa sababu aliandika kuhusu habari zangu.
47 Nkase muhwetehsele bhole amazu gane?
Kama hamuamini maandiko yake, mtawezaje kuamini maneno yangu?

< Yohana 5 >