< 2 OPetro 1 >
1 Simoni Peturo, Utumwi na tumwa owa Yesu Kilisti hwabhala bhambilile ololezyo lulola olwemonde nashi satahambilile ate, ololesyo lwali mhati mlyoli eya Ngolobhi ofwozi wetu OYesu Kilisti.
Simoni Petro, mtumishi na mtume wa Yesu Kristo: Kwa wale ambao kwa njia ya haki ya Mungu na Mwokozi wetu Yesu Kristo mmepokea imani iliyo na thamani kama yetu:
2 Owene ubhe hulimwe owinza wojelole ashelelee enjele enzya Ngolobhi no Gosi wetu oYesu Kilisti.
Neema na amani iwe kwenu kwa wingi katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
3 Ashelelee enjele ezya Ngolobhi zyajile enongwa zyekwe zyoti aeje oputi owesiku, Atume hwa Ngolobhi yatikwizi zye hu winza tutumle hwakwe.
Uweza wake wa uungu umetupatia mambo yote tunayohitaji kwa ajili ya uzima na uchaji wa Mungu, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.
4 Hwidala eli asobhezyezye nantele nakazye evintu abhambile eli nantele atibheshe bhagali hulisi zya Ngolobhe. Shatihwendelela azileshe embibhi ezyamusi ene.
Kwa sababu hiyo, ametukirimia ahadi zake kuu na za thamani kupitia mambo haya, ili kupitia hayo mpate kuwa washiriki wa asili ya uungu, na kuokoka kutoka upotovu ulioko duniani unaosababishwa na tamaa mbaya.
5 Nantele humbombo ene digani alongozye owinza widala elinza lyenyu, nantele, owinza, njele.
Kwa sababu hii hasa, jitahidini sana katika imani yenu kuongeza wema; na katika wema, maarifa;
6 Ashilile enjele hashe ashele hashe sabuli ashilile sabuli outauwa.
katika maarifa, kiasi; katika kiasi, saburi; katika saburi, utauwa;
7 Ashilile outauwa lugano olwa holo na shililo olugano olwaholo, nolugano.
katika utauwa, upendano wa ndugu; na katika upendano wa ndugu, upendo.
8 Nkashile enongwa ezi zi hweli muhati mwenyu, nkamuhwedelela akulemuhali mwenyu eshi amwe saga mbhe sembhe bhantu bhasepapa amadondolo nantele enjile ezye gosi wetu oYesu Kristi.
Kwa maana haya yakiwa ndani yenu kwa wingi na kuzidi kuongezeka, yanawasaidia msikose bidii wala kutozaa matunda katika kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
9 Nantele wawoli yasagali nenongwaezi, azilola eviluvili pepe wene, omwene sagalola ayewelwe alyozyo lwembibhi zya kwa hale.
Lakini mtu yeyote asipokuwa na mambo haya haoni mbali, na ni kipofu, naye amesahau kule kutakaswa kutoka dhambi zake za zamani.
10 Eshi mwaholobhane mbombo ahwiyomezwe nantele ohwiyenye oteule no kwizwo hwajili yetu nkashele mubhombe ego sagamubhabomele.
Kwa hiyo, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuuthibitisha wito wenu na uteule wenu. Kwa maana mkifanya hivyo, hamtajikwaa kamwe,
11 Esho mbhahwipele evinji hundwango ogwahwijilelile mwa mwene owilawila hwa gosi wetu nofyozi oYesu Kilisti. (aiōnios )
na mtajaliwa kwa ukarimu mwingi kuingia katika ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. (aiōnios )
12 Eshi ane embabhehani abhakombosye engwa ezyo wila hata nkashele mgamenye, neshi mlishinza ashilile hulyoli.
Hivyo nitawakumbusha mambo haya siku zote, hata ingawa mnayajua na mmethibitishwa katika kweli mliyo nayo.
13 Esebhaje endishinza abha damzye na bhakombosya juu yenogwa ene, sudi sehwi nantele mwihenje eli.
Naona ni vyema kuwakumbusha mambo haya wakati wote niwapo katika hema hili ambalo ni mwili wangu,
14 Nantele emenye aje esikundodo ebusongole ihenje lyane nashi ogosi oYesu Kilisti sandanjile.
kwa sababu najua ya kwamba hivi karibuni nitaliweka kando, kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyoliweka wazi kwangu.
15 Embajenzye nanali hwajili mkomboshe enongwa ezyo nkashile ane nasogola.
Nami nitafanya kila juhudi kuona kwamba baada ya kuondoka kwangu mtaweza kuyakumbuka mambo haya siku zote.
16 Nkashi atesagatafwatile embagulwe zyazya hinjie nu sitadi pala patabhabholele juu ya nguvu na hwibhonesya hwa Gosi wetu oYesu Kilisti nantele atali bhashahidi owa hwitutamle hwakwe.
Tulipowafahamisha juu ya uweza na kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo, hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, bali tulishuhudia kwa macho yetu ukuu wake.
17 Omwene ahambilile otutumsane heshima afume hwa Ngolobhe baba pala izu hovwelwe afume hwa tutamu gosi uyanyile. Ono mwana wane yegene nantele ganewane yesangwelwe tee.”
Alipewa heshima na utukufu kutoka kwa Mungu Baba, sauti ilipomjia katika Utukufu Mkuu, ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa naye sana.”
18 Tahovwe zyeizu eli palifuma humwanya pala patahali nawo hula hwigamba elinza.
Sisi wenyewe tuliisikia sauti hii ambayo ilitoka mbinguni, wakati tulipokuwa pamoja naye kwenye ule mlima mtakatifu.
19 Abalyo hwelyo mubhomba shinza alenganye, nashi okhozyo palukhozya enkisi paka pahusha huntondwe zyazibhonehana mazasha zwazibhaneha humoyo genyu.
Nasi tunalo pia neno la hakika zaidi la unabii, ambalo mtafanya vyema mkiliangalia kwa bidii, kama vile nuru inavyongʼaa gizani, hadi kupambazuka na nyota ya asubuhi izuke mioyoni mwenu.
20 Mmanye ega aje naumo okuwa wasimbwa hunsebho senbho hukuwa yoyo.
Zaidi ya yote, yawapasa mjue kwamba hakuna unabii katika Maandiko uliofasiriwa kama alivyopenda nabii mwenyewe.
21 Nantenamo okwa yahezeleda lya bhatu pewilwe Ompepo Fijiliya yajile fume hwa Ngolobhe.
Kwa maana unabii haukuja kamwe kwa mapenzi ya mwanadamu, bali watu walinena yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.