< Псалтирь 75 >
1 Начальнику хора. Не погуби. Псалом Асафа. Песнь. Славим Тебя, Боже, славим, ибо близко имя Твое; возвещают чудеса Твои.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 “Когда изберу время, Я произведу суд по правде.
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 Колеблется земля и все живущие на ней: Я утвержу столпы ее”.
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 Говорю безумствующим: “не безумствуйте”, и нечестивым: “не поднимайте рога,
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 не поднимайте высоко рога вашего, не говорите жестоковыйно”,
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
6 ибо не от востока и не от запада и не от пустыни возвышение,
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 но Бог есть судия: одного унижает, а другого возносит;
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 ибо чаша в руке Господа, вино кипит в ней, полное смешения, и Он наливает из нее. Даже дрожжи ее будут выжимать и пить все нечестивые земли.
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
9 А я буду возвещать вечно, буду воспевать Бога Иаковлева,
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 все роги нечестивых сломлю, и вознесутся роги праведника.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.