< Псалтирь 68 >

1 Начальнику хора. Псалом Давида. Песнь. Да восстанет Бог, и расточатся враги Его, и да бегут от лица Его ненавидящие Его.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
2 Как рассеивается дым, Ты рассей их; как тает воск от огня, так нечестивые да погибнут от лица Божия.
Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
3 А праведники да возвеселятся, да возрадуются пред Богом и восторжествуют в радости.
Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
4 Пойте Богу нашему, пойте имени Его, превозносите Шествующего на небесах; имя Ему: Господь, и радуйтесь пред лицем Его.
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
5 Отец сирот и судья вдов Бог во святом Своем жилище.
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
6 Бог одиноких вводит в дом, освобождает узников от оков, а непокорные остаются в знойной пустыне.
Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
7 Боже! когда Ты выходил пред народом Твоим, когда Ты шествовал пустынею,
Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
8 земля тряслась, даже небеса таяли от лица Божия, и этот Синай - от лица Бога, Бога Израилева.
dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
9 Обильный дождь проливал Ты, Боже, на наследие Твое, и когда оно изнемогало от труда, Ты подкреплял его.
Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
10 Народ Твой обитал там; по благости Твоей, Боже, Ты готовил необходимое для бедного.
Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
11 Господь даст слово: провозвестниц великое множество.
Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
12 Цари воинств бегут, бегут, а сидящая дома делит добычу.
“Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
13 Расположившись в уделах своих, вы стали, как голубица, которой крылья покрыты серебром, а перья чистым золотом:
Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
14 когда Всемогущий рассеял царей на сей земле, она забелела, как снег на Селмоне.
Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
15 Гора Божия - гора Васанская! гора высокая - гора Васанская!
Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
16 что вы завистливо смотрите, горы высокие, на гору, на которой Бог благоволит обитать и будет Господь обитать вечно?
Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
17 Колесниц Божиих тьмы, тысячи тысяч; среди их Господь на Синае, во святилище.
Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
18 Ты восшел на высоту, пленил плен, принял дары для человеков, так чтоб и из противящихся могли обитать у Господа Бога.
Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
19 Благословен Господь всякий день. Бог возлагает на нас бремя, но Он же и спасает нас.
Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
20 Бог для нас - Бог во спасение; во власти Господа Вседержителя врата смерти.
Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
21 Но Бог сокрушит голову врагов Своих, волосатое темя закоснелого в своих беззакониях.
Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
22 Господь сказал: “от Васана возвращу, выведу из глубины морской,
Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
23 чтобы ты погрузил ногу твою, как и псы твои язык свой, в крови врагов”.
ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
24 Видели шествие Твое, Боже, шествие Бога моего, Царя моего во святыне:
Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
25 впереди шли поющие, позади играющие на орудиях, в средине девы с тимпанами:
Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
26 “в собраниях благословите Бога Господа, вы - от семени Израилева!”
Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
27 Там Вениамин младший - князь их; князья Иудины - владыки их, князья Завулоновы, князья Неффалимовы.
Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
28 Бог твой предназначил тебе силу. Утверди, Боже, то, что Ты соделал для нас!
Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
29 Ради храма Твоего в Иерусалиме цари принесут Тебе дары.
Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
30 Укроти зверя в тростнике, стадо волов среди тельцов народов, хвалящихся слитками серебра; рассыпь народы, желающие браней.
Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
31 Придут вельможи из Египта; Ефиопия прострет руки свои к Богу.
Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
32 Царства земные! пойте Богу, воспевайте Господа,
Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
33 шествующего на небесах небес от века. Вот, Он дает гласу Своему глас силы.
mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
34 Воздайте славу Богу! величие Его - над Израилем, и могущество Его - на облаках.
Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
35 Страшен Ты, Боже, во святилище Твоем. Бог Израилев - Он дает силу и крепость народу Своему. Благословен Бог!
Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!

< Псалтирь 68 >