< Псалтирь 107 >

1 Аллилуия. Славьте Господа, ибо Он благ, ибо вовек милость Его!
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 Так да скажут избавленные Господом, которых избавил Он от руки врага,
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 и собрал от стран, от востока и запада, от севера и моря.
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Они блуждали в пустыне по безлюдному пути и не находили населенного города;
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 терпели голод и жажду, душа их истаевала в них.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 Но воззвали к Господу в скорби своей, и Он избавил их от бедствий их,
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 и повел их прямым путем, чтобы они шли к населенному городу.
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 Да славят Господа за милость Его и за чудные дела Его для сынов человеческих:
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 ибо Он насытил душу жаждущую и душу алчущую исполнил благами.
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 Они сидели во тьме и тени смертной, окованные скорбью и железом;
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 ибо не покорялись словам Божиим и небрегли о воле Всевышнего.
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 Он смирил сердце их работами; они преткнулись, и не было помогающего.
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 Но воззвали к Господу в скорби своей, и Он спас их от бедствий их;
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 вывел их из тьмы и тени смертной, и расторгнул узы их.
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 Да славят Господа за милость Его и за чудные дела Его для сынов человеческих:
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 ибо Он сокрушил врата медные и вереи железные сломил.
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Безрассудные страдали за беззаконные пути свои и за неправды свои;
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 от всякой пищи отвращалась душа их, и они приближались ко вратам смерти.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 Но воззвали к Господу в скорби своей, и Он спас их от бедствий их;
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 послал слово Свое и исцелил их, и избавил их от могил их.
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 Да славят Господа за милость Его и за чудные дела Его для сынов человеческих!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 Да приносят Ему жертву хвалы и да возвещают о делах Его с пением!
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Отправляющиеся на кораблях в море, производящие дела на больших водах,
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 видят дела Господа и чудеса Его в пучине:
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 Он речет, - и восстанет бурный ветер и высоко поднимает волны его:
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 восходят до небес, нисходят до бездны; душа их истаевает в бедствии;
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 они кружатся и шатаются, как пьяные, и вся мудрость их исчезает.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 Но воззвали к Господу в скорби своей, и Он вывел их из бедствия их.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 Он превращает бурю в тишину, и волны умолкают.
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 И веселятся, что они утихли, и Он приводит их к желаемой пристани.
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 Да славят Господа за милость Его и за чудные дела Его для сынов человеческих!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 Да превозносят Его в собрании народном и да славят Его в сонме старейшин!
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 Он превращает реки в пустыню и источники вод - в сушу,
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 землю плодородную - в солончатую, за нечестие живущих на ней.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 Он превращает пустыню в озеро, и землю иссохшую - в источники вод;
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 и поселяет там алчущих, и они строят город для обитания;
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 засевают поля, насаждают виноградники, которые приносят им обильные плоды.
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 Он благословляет их, и они весьма размножаются, и скота их не умаляет.
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 Уменьшились они и упали от угнетения, бедствия и скорби,
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 Он изливает бесчестие на князей и оставляет их блуждать в пустыне, где нет путей.
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 Бедного же извлекает из бедствия и умножает род его, как стада овец.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 Праведники видят сие и радуются, а всякое нечестие заграждает уста свои.
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 Кто мудр, тот заметит сие и уразумеет милость Господа.
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

< Псалтирь 107 >