< Притчи 21 >

1 Сердце царя - в руке Господа, как потоки вод: куда захочет, Он направляет его.
Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
2 Всякий путь человека прям в глазах его; но Господь взвешивает сердца.
Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
3 Соблюдение правды и правосудия более угодно Господу, нежели жертва.
Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
4 Гордость очей и надменность сердца, отличающие нечестивых, - грех.
Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
5 Помышления прилежного стремятся к изобилию, а всякий торопливый терпит лишение.
Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
6 Приобретение сокровища лживым языком - мимолетное дуновение ищущих смерти.
Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
7 Насилие нечестивых обрушится на них, потому что они отреклись соблюдать правду.
Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
8 Превратен путь человека развращенного; а кто чист, того действие прямо.
Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
9 Лучше жить в углу на кровле, нежели со сварливою женою в пространном доме.
Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
10 Душа нечестивого желает зла: не найдет милости в глазах его и друг его.
Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
11 Когда наказывается кощунник, простой делается мудрым; и когда вразумляется мудрый, то он приобретает знание.
Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
12 Праведник наблюдает за домом нечестивого: как повергаются нечестивые в несчастие.
Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
13 Кто затыкает ухо свое от вопля бедного, тот и сам будет вопить, - и не будет услышан.
Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
14 Подарок тайный тушит гнев, и дар в пазуху - сильную ярость.
Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15 Соблюдение правосудия - радость для праведника и страх для делающих зло.
Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16 Человек, сбившийся с пути разума, водворится в собрании мертвецов.
Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17 Кто любит веселье, обеднеет; а кто любит вино и тук, не разбогатеет.
Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18 Выкупом будет за праведного нечестивый и за прямодушного - лукавый.
Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19 Лучше жить в земле пустынной, нежели с женою сварливою и сердитою.
Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20 Вожделенное сокровище и тук - в доме мудрого; а глупый человек расточает их.
Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
21 Соблюдающий правду и милость найдет жизнь, правду и славу.
Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
22 Мудрый входит в город сильных и ниспровергает крепость, на которую они надеялись.
Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
23 Кто хранит уста свои и язык свой, тот хранит от бед душу свою.
Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
24 Надменный злодей - кощунник имя ему - действует в пылу гордости.
Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
25 Алчба ленивца убьет его, потому что руки его отказываются работать;
Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26 всякий день он сильно алчет, а праведник дает и не жалеет.
Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
27 Жертва нечестивых - мерзость, особенно когда с лукавством приносят ее.
Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
28 Лжесвидетель погибнет; а человек, который говорит, что знает, будет говорить всегда.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
29 Человек нечестивый дерзок лицом своим, а праведный держит прямо путь свой.
Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
30 Нет мудрости, и нет разума, и нет совета вопреки Господу.
Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
31 Коня приготовляют на день битвы, но победа - от Господа.
Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.

< Притчи 21 >