< Иов 13 >
1 Вот, все это видело око мое, слышало ухо мое и заметило для себя.
Tazama, jicho langu limeyaona haya yote; sikio langu limeyasikia na kuyaelewa hayo.
2 Сколько знаете вы, знаю и я: не ниже я вас.
Kile mnachokifahamu, ndicho hicho mimi pia ninachokifahamu; Mimi siyo duni kwenu ninyi.
3 Но я к Вседержителю хотел бы говорить и желал бы состязаться с Богом.
Hata hivyo, Mimi ningeweza kuzungumza na mwenye nguvu; Mimi natamani kusemezana na Mungu.
4 А вы сплетчики лжи; все вы бесполезные врачи.
Lakini ninyi mnauficha ukweli kwa uongo; ninyi nyote ni tabibu msiokuwa na thamani.
5 О, если бы вы только молчали! это было бы вменено вам в мудрость.
Laiti, kwamba kwa pamoja mngeshikilia amani yenu! Hilo lingekuwa hekima yenu ninyi.
6 Выслушайте же рассуждения мои и вникните в возражение уст моих.
Sikia sasa kuhoji kwangu; Sikiliza kusihi kwa midomo yangu mwenyewe.
7 Надлежало ли вам ради Бога говорить неправду и для Него говорить ложь?
Ninyi mtazungumza visivyo haki kwa ajili ya Mungu, na ninyi mtazungumza udanganyifu kwa yeye? Ni kweli ninyi mngeonyesha ukarimu kwa yeye?
8 Надлежало ли вам быть лицеприятными к Нему и за Бога так препираться?
Ni kweli ninyi mngetetea katika mahakama kama mawakili wa Mungu?
9 Хорошо ли будет, когда Он испытает вас? Обманете ли Его, как обманывают человека?
Je, kweli ingekuwa vizuri kwenu wakati yeye akiwatafuta ninyi? Mngeweza ninyi kumdanganya yeye kama mlivyoweza kuwadanganya watu?
10 Строго накажет Он вас, хотя вы и скрытно лицемерите.
Yeye kwa hakika angewathibitisha upya ninyi ikiwa katika siri ninyi mmeonyesha kutokukamilika.
11 Неужели величие Его не устрашает вас, и страх Его не нападает на вас?
Je, ukuu wake usingewafanya ninyi muogope? Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?
12 Напоминания ваши подобны пеплу; оплоты ваши - оплоты глиняные.
Hadithi zenu za misemo ya kukariri, ni mithali zimetengenezwa kwa majivu; utetezi wenu ni utetezi uliotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi.
13 Замолчите предо мною, и я буду говорить, что бы ни постигло меня.
Shikilieni amani yenu, mniache peke yangu, ili ya kwamba nipate kusema, acheni yaje yale yanayoweza kuja kwangu.
14 Для чего мне терзать тело мое зубами моими и душу мою полагать в руку мою?
Nitaichukua nyama yangu mwenywewe katika meno yangu; Nitayachukua maisha yangu katika mikono yangu.
15 Вот, Он убивает меня, но я буду надеяться; я желал бы только отстоять пути мои пред лицом Его!
Tazama, ikiwa ataniua mimi, sitakuwa na tumaini lililobakia; hata hivyo, nitazitetea njia zangu mbele zake yeye.
16 И это уже в оправдание мне, потому что лицемер не пойдет пред лице Его!
Hiki kitakuwa sababu ya kutohesabiwa hatia, kwamba mimi sikuja mbele zake kama mtu asiyemcha Mungu.
17 Выслушайте внимательно слово мое и объяснение мое ушами вашими.
Mungu, sikiliza kwa makini kuzungumza kwangu; ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.
18 Вот, я завел судебное дело: знаю, что буду прав.
Tazama sasa, Nimeuweka utetezi wangu katika mpangilio, Mimi ninafahamu kwamba mimi sina hatia.
19 Кто в состоянии оспорить меня? Ибо я скоро умолкну и испущу дух.
Ni nani anayeweza kushindana na mimi katika mahakama? Ikiwa mlikuja kufanya hivyo, na kama mimi nilithibitishwa kukosea, ndipo ningekuwa kimya na kuyatoa maisha yangu.
20 Двух только вещей не делай со мною, и тогда я не буду укрываться от лица Твоего:
Mungu, fanya mambo mawili kwa ajili yangu, na tena Mimi sitajificha kutoka katika uso wako.
21 удали от меня руку Твою, и ужас Твой да не потрясает меня.
Ondoa kutoka kwangu mkono wako unaotesa, na usiache utisho wako unifanye mimi kuogopa.
22 Тогда зови, и я буду отвечать, или буду говорить я, а Ты отвечай мне.
Ndipo niite mimi, na mimi nitakujibu; au uniache mimi niseme na wewe na wewe unijibu mimi.
23 Сколько у меня пороков и грехов? покажи мне беззаконие мое и грех мой.
Je, maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
24 Для чего скрываешь лице Твое и считаешь меня врагом Тебе?
Kwa nini unaficha uso wako kutoka kwangu mimi na kunitendea mimi kama adui yako?
25 Не сорванный ли листок Ты сокрушаешь и не сухую ли соломинку преследуешь?
Je, wewe utalitesa jani linalopeperushwa? Je, utaendelea kulifuatilia bua kavu?
26 Ибо Ты пишешь на меня горькое и вменяешь мне грехи юности моей,
Kwa maana wew unaandika chini vitu vichungu dhidi yangu mimi; wewe unanifanya mimi kurithi uovu wa ujana wangu.
27 и ставишь в колоду ноги мои и подстерегаешь все стези мои, - гонишься по следам ног моих.
Wewe pia unaiweka miguu yangu katika nguo nyembamba; wewe waangalia njia zangu zote; wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.
28 А он, как гниль, распадается, как одежда, изъеденная молью.
japokuwa mimi ni kama kitu kilichooza ambacho hutupwa mbali, kama vazi lile ambalo nondo wamelila.