< 4-я Царств 12 >

1 В седьмой год Ииуя воцарился Иоас и сорок лет царствовал в Иерусалиме. Имя матери его Цивья, из Вирсавии.
Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba.
2 И делал Иоас угодное в очах Господних во все дни свои, доколе наставлял его священник Иодай;
Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza.
3 только высоты не были отменены; народ еще приносил жертвы и курения на высотах.
Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
4 И сказал Иоас священникам: все серебро посвящаемое, которое приносят в дом Господень, серебро от приходящих, серебро, вносимое за каждую душу по оценке, все серебро, сколько кому приходит на сердце принести в дом Господень,
Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni.
5 пусть берут священники себе, каждый от своего знакомого, и пусть исправляют они поврежденное в храме, везде, где найдется повреждение.
Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”
6 Но как до двадцать третьего года царя Иоаса священники не исправляли повреждений в храме,
Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu.
7 то царь Иоас позвал священника Иодая и священников и сказал им: почему вы не исправляете повреждений в храме? Не берите же отныне серебра у знакомых своих, а на починку повреждений в храме отдайте его.
Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.”
8 И согласились священники не брать серебра у народа на исправление повреждений в храме.
Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.
9 И взял священник Иодай один ящик, и сделал отверстие сверху его, и поставил его подле жертвенника на правой стороне, где входили в дом Господень. И полагали туда священники, стоящие на страже у порога, все серебро, приносимое в дом Господень.
Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana.
10 И когда видели, что много серебра в ящике, приходили писец царский и первосвященник, и завязывали в мешки, и пересчитывали серебро, найденное в доме Господнем;
Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko.
11 и отдавали сосчитанное серебро в руки производителям работ, приставленным к дому Господню, а сии издерживали его на плотников и строителей, работавших в доме Господнем,
Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi,
12 и на делателей стен и на каменотесов, также на покупку дерев и тесаных камней, для починки повреждений в доме Господнем, и на все, что расходовалось для поддержания храма.
waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.
13 Но не сделано было для дома Господня серебряных блюд, ножей, чаш для окропления, труб, всяких сосудов золотых и сосудов серебряных из серебра, приносимого в дом Господень,
Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana;
14 а производителям работ отдавали его, и починивали им дом Господень.
zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu.
15 И не требовали отчета от тех людей, которым поручали серебро для раздачи производителям работ, ибо они действовали честно.
Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote.
16 Серебро за жертву о преступлении и серебро за жертву о грехе не вносилось в дом Господень: священникам оно принадлежало.
Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.
17 Тогда выступил в поход Азаил, царь Сирийский, и пошел войною на Геф, и взял его; и вознамерился Азаил идти на Иерусалим.
Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu.
18 Но Иоас, царь Иудейский, взял все пожертвованное, что пожертвовали храму Иосафат, и Иорам и Охозия, отцы его, цари Иудейские, и что он сам пожертвовал, и все золото, найденное в сокровищницах дома Господня и дома царского, и послал Азаилу, царю Сирийскому; и он отступил от Иерусалима.
Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.
19 Прочее об Иоасе и обо всем, что он сделал, написано в летописи царей Иудейских.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 И восстали слуги его, и составили заговор, и убили Иоаса в доме Милло, на дороге к Силле.
Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila.
21 Его убили слуги его: Иозакар, сын Шимеаты, и Иегозавад, сын Шомеры; и он умер, и похоронили его с отцами его в городе Давидовом. И воцарился Амасия, сын его, вместо него.
Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 4-я Царств 12 >