< Provérbios 10 >

1 Os provérbios de Salomão. Um filho sábio faz um pai feliz; mas um filho tolo traz tristeza para sua mãe.
Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
2 Os tesouros da maldade não lucram nada, mas a retidão se livra da morte.
Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
3 Yahweh não vai permitir que a alma dos justos passe fome, mas ele afasta o desejo dos ímpios.
Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
4 Ele se torna pobre que trabalha com a mão preguiçosa, mas a mão do diligente traz riqueza.
Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
5 Aquele que se reúne no verão é um filho sábio, mas aquele que dorme durante a colheita é um filho que causa vergonha.
Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
6 As bênçãos estão na cabeça dos justos, mas a violência cobre a boca dos malvados.
Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
7 A memória dos justos é abençoada, mas o nome dos ímpios apodrecerá.
Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
8 Os sábios de coração aceitam os mandamentos, mas um tolo falador vai cair.
Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
9 Aquele que caminha sem culpa, certamente caminha, mas aquele que perverte seus caminhos será descoberto.
Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
10 One que pisca com o olho causa tristeza, mas um tolo falador vai cair.
Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
11 A boca dos justos é uma fonte de vida, mas a violência cobre a boca dos malvados.
Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
12 O ódio agita a luta, mas o amor cobre todos os males.
Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
13 A sabedoria é encontrada nos lábios daquele que tem discernimento, mas uma vara é para a parte de trás daquele que não tem entendimento.
Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
14 Os sábios colocam o conhecimento, mas a boca do tolo está perto da ruína.
Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
15 A riqueza do homem rico é sua cidade forte. A destruição dos pobres é sua pobreza.
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
16 O trabalho dos justos leva à vida. O aumento dos ímpios leva ao pecado.
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
17 He está no caminho da vida quem presta atenção à correção, mas aquele que abandona a repreensão, desvia os outros.
Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
18 Aquele que esconde o ódio tem lábios mentirosos. Aquele que profere uma calúnia é um tolo.
Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
19 Na multidão de palavras não falta desobediência, mas aquele que refreia seus lábios faz sabiamente.
Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
20 A língua dos justos é como a prata escolhida. O coração dos ímpios tem pouco valor.
Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
21 Os lábios dos justos alimentam muitos, mas os tolos morrem por falta de compreensão.
Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
22 A bênção de Yahweh traz riqueza, e ele não lhe acrescenta nenhum problema.
Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
23 É um prazer tolo fazer a maldade, mas a sabedoria é o prazer de um homem de entendimento.
Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
24 O que o medo maligno os ultrapassará, mas o desejo dos justos será concedido.
Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
25 Quando o redemoinho passa, o mal já não é mais; mas os justos permanecem firmes para sempre.
Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
26 Como vinagre até os dentes e como fumaça até os olhos, Assim é o preguiçoso para aqueles que o enviam.
Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 O medo de Yahweh prolonga os dias, mas os anos dos ímpios devem ser encurtados.
Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
28 A perspectiva dos justos é a alegria, mas a esperança dos ímpios perecerá.
Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
29 O caminho de Yahweh é um refúgio para os verticais, mas é uma destruição para os trabalhadores da iniqüidade.
Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
30 Os justos nunca serão removidos, mas os ímpios não vão habitar na terra.
Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
31 A boca dos justos produz sabedoria, mas a língua perversa será cortada.
Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
32 Os lábios dos justos sabem o que é aceitável, mas a boca dos malvados é perversa.
Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.

< Provérbios 10 >