< Números 19 >
1 Yahweh falou com Moisés e com Arão, dizendo:
Bwana akamwambia Mose na Aroni:
2 “Este é o estatuto da lei que Yahweh ordenou. Diga aos filhos de Israel que lhe tragam uma novilha vermelha sem mancha, na qual não há defeito, e que nunca foi jungida.
“Hivi ndivyo sheria ambayo Bwana ameagiza itakavyo: Waambie Waisraeli wakuletee mtamba mwekundu asiye na dosari wala waa, na ambaye hajapata kufungwa nira.
3 Você a entregará a Eleazar, o sacerdote, e ele a trará para fora do acampamento, e alguém a matará diante de sua face.
Mpeni kuhani Eleazari huyo mtamba; naye atatolewa nje ya kambi na kuchinjwa mbele yake huyo kuhani.
4 Eleazar, o sacerdote, tomará um pouco do sangue dela com o dedo, e aspergirá o sangue dela em direção à frente da Tenda da Reunião sete vezes.
Kisha kuhani Eleazari atachukua baadhi ya damu yake kwenye kidole chake na kuinyunyiza mara saba kuelekea upande wa mbele ya Hema la Kukutania.
5 A novilha será queimada à sua vista; sua pele, e sua carne, e seu sangue, com seu esterco, será queimado.
Wakati angali akitazama, mtamba huyo atateketezwa: ngozi yake, nyama yake, damu na sehemu zake za ndani.
6 O padre pegará madeira de cedro, hissopo e escarlate e atirá-la-á no meio da queima da novilha.
Kuhani atachukua kuni za mti wa mwerezi, hisopo na sufu nyekundu, na kuvitupa kwenye huyo mtamba anayeungua.
7 Então o sacerdote lavará suas vestes, e banhará sua carne em água, e depois entrará no acampamento, e o sacerdote ficará imundo até a noite.
Baada ya hayo, kuhani lazima afue nguo zake, na aoge mwili wake kwa maji. Kisha anaweza kurudi kambini, lakini atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada mpaka jioni.
8 Aquele que a queimar lavará suas vestes em água, e banhará sua carne em água, e será imundo até a noite.
Mtu amchomaye huyo mtamba lazima naye pia afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye pia atakuwa najisi mpaka jioni.
9 “Um homem limpo recolherá as cinzas da novilha e as depositará fora do acampamento em um lugar limpo; e será guardado para a congregação das crianças de Israel para uso na água para limpeza de impurezas. É uma oferta pelo pecado.
“Mtu ambaye ni safi atakusanya majivu ya mtamba huyo na kuyaweka mahali ambapo ni safi nje ya kambi kwa taratibu za kiibada. Yatahifadhiwa na jumuiya ya Kiisraeli kwa matumizi katika maji ya utakaso; ni kwa ajili ya kutakasa kutoka dhambini.
10 Aquele que recolher as cinzas da novilha lavará suas roupas, e ficará imundo até a noite. Será para os filhos de Israel, e para o estrangeiro que vive como um estrangeiro entre eles, por um estatuto para sempre.
Mtu akusanyaye majivu ya huyo mtamba ni lazima pia afue nguo zake, kadhalika naye pia atakuwa najisi hadi jioni. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa Waisraeli na kwa wageni wanaoishi miongoni mwao.
11 “Aquele que tocar o cadáver de qualquer homem será imundo por sete dias.
“Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote atakuwa najisi kwa siku saba.
12 Ele se purificará com água no terceiro dia, e no sétimo dia estará limpo; mas se não se purificar no terceiro dia, então no sétimo dia não estará limpo.
Ni lazima ajitakase mwenyewe kwa maji katika siku ya tatu na siku ya saba, ndipo atakuwa safi. Lakini kama hatajitakasa mwenyewe katika siku ya tatu na ya saba, hatakuwa safi.
13 Quem tocar um morto, o corpo de um homem que morreu, e não se purificar, profanará o tabernáculo de Javé; e essa alma será cortada de Israel; porque a água para a impureza não foi aspergida sobre ele, ele será imundo. Sua impureza ainda está sobre ele.
Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote na kushindwa kujitakasa mwenyewe hunajisi Maskani ya Bwana. Mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na Israeli. Kwa sababu hajanyunyiziwa maji ya utakaso, yeye ni najisi; unajisi wake unabaki juu yake.
14 “Esta é a lei quando um homem morre em uma tenda: todos que entram na tenda, e todos que estão na tenda, devem estar imundos sete dias.
“Hii ndiyo sheria itumikayo wakati mtu amekufa ndani ya hema: Yeyote aingiaye ndani ya hema hilo na yeyote aliye ndani yake watakuwa najisi kwa muda wa siku saba,
15 Todo recipiente aberto, que não tem cobertura presa, é imundo.
nacho kila chombo kisicho na kifuniko juu yake kitakuwa najisi.
16 “Quem no campo aberto tocar alguém que for morto com uma espada, ou um cadáver, ou um osso de um homem, ou uma sepultura, será imundo sete dias.
“Mtu yeyote aliyeko nje mahali pa wazi agusaye mtu aliyeuawa kwa upanga au mtu aliyekufa kwa kifo cha kawaida, au mtu yeyote agusaye mfupa wa mtu aliyekufa au kaburi, atakuwa najisi kwa siku saba.
17 “Para os impuros, eles devem tomar das cinzas da queima da oferta pelo pecado; e água corrente deve ser derramada sobre eles em um recipiente.
“Kwa mtu aliye najisi, weka majivu ya sadaka ya utakaso wa dhambi ndani ya chombo, umimine maji safi juu yao.
18 Uma pessoa limpa pegará o hissopo, mergulhá-lo-á na água e aspergi-lo-á sobre a tenda, sobre todos os vasos, sobre as pessoas que lá estavam e sobre aquele que tocou o osso, ou o morto, ou o morto, ou a sepultura.
Kisha mtu aliye safi kwa kawaida za kiibada atachukua hisopo, achovye ndani ya maji, na kunyunyizia hema na vifaa vyote pamoja na watu ambao walikuwamo. Pia ni lazima amnyunyizie mtu yeyote ambaye amegusa mfupa wa mtu aliyekufa, au kaburi, au mtu ambaye ameuawa, au mtu ambaye amekufa kifo cha kawaida.
19 A pessoa limpa deve aspergir sobre o impuro no terceiro dia, e no sétimo dia. No sétimo dia, ele o purificará. Ele lavará suas roupas e se banhará em água, e será limpo à noite.
Mtu ambaye ni safi ndiye atakayemnyunyizia yeyote ambaye ni najisi siku ya tatu na siku ya saba, na katika siku ya saba atamtakasa mtu huyo. Mtu ambaye ametakaswa lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, na jioni ile atakuwa safi.
20 Mas o homem que for imundo, e não se purificar, essa alma será extirpada do meio da assembléia, porque contaminou o santuário de Iavé. A água para a impureza não foi aspergida sobre ele. Ele é impuro.
Lakini ikiwa mtu ambaye ni najisi hakujitakasa mwenyewe, ni lazima akatiliwe mbali na jumuiya, kwa sababu ameinajisi Maskani ya Bwana. Maji ya utakaso hayajanyunyizwa juu yake, naye ni najisi.
21 Será um estatuto perpétuo para eles. Aquele que asperge a água para a impureza lavará suas roupas, e aquele que toca a água para a impureza será imundo até a noite.
Hii ni sheria ya kudumu kwao. “Mtu yeyote ambaye ananyunyiza yale maji ya utakaso lazima pia afue nguo zake, na yeyote ambaye hugusa maji ya utakaso atakuwa najisi mpaka jioni.
22 “O que a pessoa imunda tocar será imundo; e a alma que tocar será imunda até a noite”.
Kitu chochote anachogusa mtu aliye najisi kitakuwa najisi, na yeyote akigusaye huwa najisi mpaka jioni.”