< Joel 3 >

1 “Pois, eis que naqueles dias, e nesse tempo, quando restauro a fortuna de Judá e Jerusalém,
“Katika siku hizo na wakati huo, nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,
2 Vou reunir todas as nações, e os levará para o vale de Jehoshaphat; e eu executarei o julgamento sobre eles lá para meu povo, e por minha herança, Israel, a quem eles dispersaram entre as nações. Eles dividiram minhas terras,
nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta katika Bonde la Yehoshafati Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli, kwa kuwa waliwatawanya watu wangu miongoni mwa mataifa na kuigawa nchi yangu.
3 e lançaram sorteio para o meu povo, e deram um menino para uma prostituta, e venderam uma garota por vinho, para que eles pudessem beber.
Wanawapigia kura watu wangu na kuwauza wavulana ili kupata makahaba; waliwauza wasichana ili wapate kunywa mvinyo.
4 “Sim, e o que você é para mim, Tyre e Sidon, e todas as regiões da Filístia? Você vai me pagar? E se você me pagar, Devolverei rápida e rapidamente seu reembolso sobre sua própria cabeça.
“Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.
5 Porque você levou minha prata e meu ouro, e levaram meus melhores tesouros para seus templos,
Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.
6 and venderam os filhos de Judá e os filhos de Jerusalém para os filhos dos gregos, que você pode removê-los longe de suas fronteiras.
Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.
7 Behold, eu os agitarei para fora do lugar onde os vendeu, e devolverá seu reembolso com sua própria cabeça;
“Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.
8 and Eu venderei seus filhos e suas filhas nas mãos dos filhos de Judá, e eles os venderão aos homens de Sabá, a uma nação distante, pois Yahweh o disse”.
Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.
9 Proclaim isto entre as nações: “Prepare-se para a guerra! Agitar os homens poderosos. Que todos os guerreiros se aproximem. Deixe-os subir.
Tangazeni hili miongoni mwa mataifa: Jiandaeni kwa vita! Amsha askari! Wanaume wote wapiganaji wasogee karibu na kushambulia.
10 Beat suas partes de arado em espadas, e seus ganchos de poda em lanças. Que os fracos digam: “Eu sou forte”.
Majembe yenu yafueni yawe panga na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki. Aliye dhaifu na aseme, “Mimi nina nguvu!”
11 Hurry e venham, todos vocês das nações vizinhas, e se reúnam”. Porque os seus poderosos devem ir até lá, Yahweh.
Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote, kusanyikeni huko. Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!
12 “Que as nações se despertem, e subir até o vale de Jehoshaphat; pois ali eu me sentarei para julgar todas as nações vizinhas.
“Mataifa na yaamshwe; na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati, kwa kuwa nitaketi mahali pale kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.
13 Put na foice; para a colheita está madura. Venha, pisa, pois o lagar está cheio, as cubas transbordam, pois sua maldade é grande”.
Tia mundu, kwa kuwa mavuno yamekomaa. Njooni, mkanyage zabibu, kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa na mapipa yanafurika: kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”
14 Multitudes, multidões no vale da decisão! Pois o dia de Yahweh está próximo no vale da decisão.
Umati mkubwa, umati mkubwa katika bonde la uamuzi! Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu katika bonde la uamuzi.
15 The o sol e a lua estão escurecidos, e as estrelas retiram seu brilho.
Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota hazitatoa mwanga wake tena.
16 Yahweh rugirá de Zion, e trovões de Jerusalém; e os céus e a terra tremerão; mas Yahweh será um refúgio para seu povo, e um refúgio para as crianças de Israel.
Bwana atanguruma kutoka Sayuni na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu; dunia na mbingu vitatikisika. Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.
17 “Portanto, você saberá que eu sou Yahweh, seu Deus, morando em Zion, minha montanha sagrada. Então Jerusalém será santa, e nenhum desconhecido passará mais por ela.
“Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu, nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Yerusalemu utakuwa mtakatifu; kamwe wageni hawatavamia tena.
18 It acontecerá nesse dia, que as montanhas vão derrubar o vinho doce, as colinas fluirão com leite, todos os riachos de Judá fluirão com as águas; e uma fonte sairá da casa de Yahweh, e regará o vale de Shittim.
“Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya, na vilima vitatiririka maziwa; mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji. Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana na kunywesha Bonde la Shitimu.
19 Egypt será uma desolação e Edom será uma região desolada e selvagem, pela violência cometida contra as crianças de Judá, porque eles derramaram sangue inocente em suas terras.
Lakini Misri itakuwa ukiwa, Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda, ambao katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.
20 But Judah será habitada para sempre, e Jerusalém de geração em geração.
Yuda itakaliwa na watu milele na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.
21 I limparão seu sangue que eu não limpei, para Yahweh mora em Zion”.
Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe, nitasamehe.”

< Joel 3 >