< Jó 13 >
1 “Eis que meus olhos viram tudo isso. Meu ouvido ouviu e entendeu.
“Macho yangu yameona hili lote, masikio yangu yamesikia na kulielewa.
2 O que você sabe, eu sei também. Eu não sou inferior a você.
Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; mimi si mtu duni kuliko ninyi.
3 “Certamente eu falaria com o Todo-Poderoso. Desejo raciocinar com Deus.
Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi na kuhojiana shauri langu na Mungu.
4 Mas vocês são falsificadores de mentiras. Vocês são todos médicos sem valor.
Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote!
5 Oh, que você estaria completamente em silêncio! Então você seria sábio.
Laiti wote mngenyamaza kimya! Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima.
6 Ouça agora meu raciocínio. Ouça as súplicas de meus lábios.
Sikieni sasa hoja yangu; sikilizeni kusihi kwangu.
7 Você falará sem retidão por Deus, e falar enganosamente por ele?
Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake?
8 Você vai demonstrar parcialidade com ele? Você vai lutar por Deus?
Mtamwonyesha upendeleo? Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake?
9 É bom que ele o procure? Ou como se engana um homem, você o enganará?
Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu?
10 Ele certamente irá reprová-lo se você mostrar, secretamente, parcialidade.
Hakika angewakemea kama mkiwapendelea watu kwa siri.
11 Sua majestade não vai fazer você ter medo e seu pavor cai sobre você?
Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? Je, hofu yake isingewaangukia ninyi?
12 Your provérbios memoráveis são provérbios de cinzas. Suas defesas são defesas de barro.
Maneno yenu ni mithali za majivu; utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi.
13 “Fique em silêncio! Deixe-me em paz, para que eu possa falar. Venha sobre mim o que quiser.
“Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
14 Por que eu deveria levar minha carne nos dentes? e colocar minha vida na minha mão?
Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
15 Eis que ele vai me matar. Eu não tenho esperança. No entanto, vou manter meus caminhos diante dele.
Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
16 Esta também será minha salvação, que um homem sem Deus não virá antes dele.
Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
17 Ouça atentamente o meu discurso. Que minha declaração esteja em seus ouvidos.
Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
18 Veja agora, eu pus a minha causa em ordem. Eu sei que sou justo.
Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
19 Quem é aquele que vai contender comigo? Pois então eu me calaria e desistiria do espírito.
Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
20 “Só não faça duas coisas para mim, então não me esconderei de seu rosto:
“Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, nami sitajificha uso wako:
21 withdraw sua mão longe de mim, e não deixe que seu terror me faça ter medo.
Ondoa mkono wako uwe mbali nami, nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu.
22 Em seguida, ligue e eu responderei, ou deixe-me falar, e você me responde.
Niite kwenye shauri nami nitajibu, au niache niseme, nawe upate kujibu.
23 Quantas são minhas iniqüidades e meus pecados? Faça-me conhecer minha desobediência e meu pecado.
Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu.
24 Por que você esconde seu rosto? e me considera seu inimigo?
Kwa nini kuuficha uso wako na kunihesabu mimi kuwa adui yako?
25 Você vai assediar uma folha movida? Você vai perseguir o restolho seco?
Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? Je, utayasaka makapi makavu?
26 Para você escrever coisas amargas contra mim, e fazer-me herdar as iniquidades da minha juventude.
Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu.
27 Você também colocou meus pés no estoque, e marcar todos os meus caminhos. Você se prende às solas dos meus pés,
Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. Unazichunga kwa makini njia zangu zote kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu.
28 embora eu esteja decadente como uma coisa podre, como uma peça de vestuário que é comida por traças.
“Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, kama vazi lililoliwa na nondo.