< Gênesis 2 >

1 Os céus, a terra e toda a sua vasta gama foram terminados.
Kwa hiyo mbingu na dunia zikakamilika, pamoja na vyote vilivyomo.
2 No sétimo dia, Deus terminou seu trabalho que havia feito; e descansou no sétimo dia de todo o seu trabalho que havia feito.
Katika siku ya saba Mungu alikuwa amekamilisha kazi aliyokuwa akiifanya, hivyo siku ya saba akapumzika kutoka kazi zake zote.
3 Deus abençoou o sétimo dia e o tornou santo, porque descansou nele de todo o seu trabalho de criação que havia feito.
Mungu akaibariki siku ya saba akaifanya takatifu, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kazi zote za kuumba alizokuwa amefanya.
4 Esta é a história das gerações dos céus e da terra quando foram criados, no dia em que Javé Deus fez a terra e os céus.
Haya ndiyo maelezo ya mbingu na dunia wakati zilipoumbwa. Bwana Mungu alipoziumba mbingu na dunia,
5 Nenhuma planta do campo ainda estava na terra, e nenhuma erva do campo ainda havia brotado; pois Javé Deus não havia causado a chuva na terra. Não havia um homem para cultivar o solo,
hapakuwepo na mche wa shambani uliokuwa umejitokeza ardhini, wala hapakuwepo na mmea wa shamba uliokuwa umeota, kwa kuwa Bwana Mungu alikuwa hajanyeshea mvua juu ya nchi, na hapakuwepo mtu wa kuilima ardhi,
6 mas uma névoa subiu da terra, e regou toda a superfície do solo.
lakini umande ulitokeza kutoka ardhini na kunyesha uso wote wa nchi:
7 Yahweh Deus formou o homem do pó da terra, e soprou em suas narinas o sopro da vida; e o homem se tornou uma alma viva.
Bwana Mungu alimuumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi, akampulizia pumzi ya uhai puani mwake, naye mtu akawa kiumbe hai.
8 Yahweh Deus plantou um jardim ao leste, no Éden, e ali colocou o homem que havia formado.
Basi Bwana Mungu alikuwa ameotesha bustani upande wa mashariki, katika Edeni, huko akamweka huyo mtu aliyemuumba.
9 Do solo Javé Deus fez crescer toda árvore agradável à vista e boa para o alimento, incluindo a árvore da vida no meio do jardim e a árvore do conhecimento do bem e do mal.
Bwana Mungu akafanya aina zote za miti ziote kutoka ardhini, miti yenye kupendeza macho na mizuri kwa chakula. Katikati ya bustani ulikuwepo mti wa uzima na mti wa kujua mema na mabaya.
10 Um rio saiu do Éden para regar o jardim; e dali se separou, e se tornou a nascente de quatro rios.
Mto wa kunyeshea bustani ulitiririka toka Edeni, kuanzia hapa ukagawanyika kuwa mito minne.
11 O nome do primeiro é Pishon: corre por toda a terra de Havilah, onde há ouro;
Mto wa kwanza uliitwa Pishoni, nao huzunguka nchi yote ya Havila ambako kuna dhahabu.
12 e o ouro daquela terra é bom. O Bdellium e a pedra ônix também estão lá.
(Dhahabu ya nchi hiyo ni nzuri, bedola na vito shohamu pia hupatikana huko.)
13 O nome do segundo rio é Gihon. É o mesmo rio que corre por toda a terra de Cush.
Jina la mto wa pili ni Gihoni, ambao huzunguka nchi yote ya Kushi.
14 O nome do terceiro rio é Hiddekel. Este é o que corre na frente da Assíria. O quarto rio é o Eufrates.
Jina la mto wa tatu ni Tigrisi, unaopita mashariki ya Ashuru. Mto wa nne ni Frati.
15 Yahweh Deus tomou o homem e o colocou no jardim do Éden para cultivá-lo e guardá-lo.
Bwana Mungu akamchukua huyo mtu, akamweka kwenye Bustani ya Edeni ailime na kuitunza.
16 Javé Deus ordenou ao homem, dizendo: “Podeis comer livremente de toda árvore do jardim;
Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akamwambia, “Uko huru kula matunda ya mti wowote katika bustani,
17 mas não comereis da árvore do conhecimento do bem e do mal; porque no dia em que dela comerdes, certamente morrereis”.
lakini kamwe usile matunda ya mti wa kujua mema na mabaya, kwa maana siku utakapokula matunda yake, hakika utakufa.”
18 Yahweh Deus disse: “Não é bom para o homem estar sozinho”. Vou fazer dele um ajudante comparável a ele”.
Bwana Mungu akasema, “Si vyema huyu mtu awe peke yake. Nitamfanyia msaidizi wa kumfaa.”
19 Do chão Yahweh Deus formou cada animal do campo, e cada ave do céu, e os trouxe ao homem para ver o que ele os chamaria. O que quer que o homem chamasse cada ser vivo, tornou-se seu nome.
Basi Bwana Mungu alikuwa amefanyiza kutoka ardhi wanyama wote wa porini na ndege wote wa angani. Akawaleta kwa huyu mtu aone atawaitaje, nalo jina lolote alilokiita kila kiumbe hai, likawa ndilo jina lake.
20 O homem deu nomes a todo o gado, e às aves do céu, e a todos os animais do campo; mas para o homem não foi encontrado um ajudante comparável a ele.
Hivyo Adamu akawapa majina wanyama wote wa kufugwa, ndege wa angani, na wanyama wote wa porini. Lakini kwa Adamu hakupatikana msaidizi wa kumfaa.
21 Yahweh Deus fez com que o homem caísse num sono profundo. Enquanto o homem dormia, ele pegou uma de suas costelas e fechou a carne em seu lugar.
Hivyo Bwana Mungu akamfanya Adamu kulala usingizi mzito, naye alipokuwa amelala akachukua moja ya mbavu zake, akapafunika mahali pale kwa nyama.
22 Yahweh Deus fez uma mulher da costela que ele havia tirado do homem, e a trouxe ao homem.
Kisha Bwana Mungu akamfanya mwanamke kutoka kwenye ule ubavu aliouchukua kutoka kwa huyo mwanaume, akamleta huyo mwanamke kwa huyo mwanaume.
23 O homem disse: “Isto agora é osso dos meus ossos, e carne da minha carne”. Ela será chamada 'mulher,' porque foi tirada do homem”.
Huyo mwanaume akasema, “Huyu sasa ni mfupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu, ataitwa ‘mwanamke,’ kwa kuwa alitolewa katika mwanaume.”
24 Portanto, um homem deixará seu pai e sua mãe, e se unirá à sua esposa, e eles serão uma só carne.
Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
25 O homem e sua esposa estavam ambos nus, e não tinham vergonha.
Adamu na mkewe wote wawili walikuwa uchi, wala hawakuona aibu.

< Gênesis 2 >