< Ezequiel 38 >

1 A palavra de Javé veio a mim, dizendo:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 “Filho do homem, dirige teu rosto para Gog, da terra de Magog, o príncipe de Rosh, Meseque e Tubal, e profetiza contra ele,
“Mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya Gogu, katika nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali, tabiri dhidi yake
3 e diz: 'O Senhor Javé diz: “Eis que estou contra ti, Gog, príncipe de Rosh, Meseque e Tubal.
na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu, mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
4 Eu te darei a volta, e colocarei ganchos em suas mandíbulas, e te trarei para fora, com todo seu exército, cavalos e cavaleiros, todos eles vestidos com armadura completa, uma grande companhia com escudo e bucha, todos eles manejando espadas;
Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukutia ndoana kwenye mataya yako na kukutoa nje wewe pamoja na jeshi lako lote, yaani, farasi wako, wapanda farasi wako waliojiandaa tayari kwa vita, pamoja na kundi kubwa la wajeuri wakiwa na ngao na vigao, wote wakipunga panga zao.
5 Pérsia, Cush, e Put com eles, todos eles com escudo e capacete;
Uajemi, Kushi na Putu watakuwa pamoja nao, wote wakiwa na ngao na kofia za chuma,
6 Gomer, e todas as suas hordas; a casa de Togarmah nas partes mais altas do norte, e todas as suas hordas - até mesmo muitos povos contigo.
pia Gomeri pamoja na vikosi vyake vyote, na Beth-Togarma kutoka kaskazini ya mbali pamoja na vikosi vyake vyote, mataifa mengi wakiwa pamoja nawe.
7 “““Esteja preparado, sim, prepare-se, você e todas as suas empresas que são montadas para você, e seja um guarda para eles.
“‘Jiandae, uwe tayari, wewe na makundi yako yote ya wajeuri yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe waamrishe.
8 Depois de muitos dias, você será visitado. Nos últimos anos vocês entrarão na terra que é trazida da espada, que é recolhida de muitos povos, nas montanhas de Israel, que têm sido um desperdício contínuo; mas ela é trazida dos povos e eles viverão em segurança, todos eles.
Baada ya siku nyingi utaitwa vitani. Katika miaka ijayo, utaivamia nchi ile ambayo imepona kutoka vita, ambayo watu wake walikusanywa kutoka mataifa mengi kuja katika milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeachwa ukiwa. Wameletwa kutoka mataifa na sasa wote wanaishi katika hali ya salama.
9 Você subirá. Vocês virão como uma tempestade. Serás como uma nuvem para cobrir a terra, tu e todas as tuas hordas, e muitos povos contigo”.
Wewe na vikosi vyako vyote na mataifa mengi yaliyo pamoja nawe mtapanda juu, mtawazoa kama tufani na kuifunika nchi kama wingu.
10 “'O Senhor Javé diz: “Acontecerá naquele dia que as coisas entrarão em sua mente, e você elaborará um plano maligno.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mawazo yataingia moyoni mwako nawe utapanga mipango mibaya.
11 Você dirá: 'Eu irei para a terra das aldeias não muradas'. Irei até aqueles que estão em repouso, que habitam com segurança, todos eles habitando sem muros, e não tendo barras nem portões,
Utasema, “Nitapigana vita na nchi ambayo vijiji vyake havina maboma. Nitawashambulia watu wanaoishi kwa amani na wasiotarajia vita: wote wanaishi bila maboma na bila malango na makomeo.
12 para tomar o saque e para tomar presas; para virar a mão contra os lugares devastados que são habitados, e contra as pessoas que estão reunidas fora das nações, que adquiriram gado e bens, que habitam no meio da terra”.
Nitateka mateka na kuchukua nyara mali za wale waliorudi kuishi katika mahame na wale watu waliokusanywa kutoka kwa mataifa, ambao sasa wana mifugo na mali nyingi, wanaoishi katikati ya nchi.”
13 Sheba, Dedan e os comerciantes de Tarshish, com todos os seus jovens leões, lhe perguntarão: “Você veio para tomar o saque? Você reuniu sua empresa para levar a presa, para levar prata e ouro, para levar gado e mercadorias, para levar grandes pilhagens?”
Sheba na Dedani pamoja na wafanyabiashara wa Tarshishi na vijiji vyake vyote watakuambia, “Je, umekuja kuteka mateka? Je, umekusanya makundi yako ya wajeuri ili kuchukua nyara mali, kutwaa fedha na dhahabu, kutunyangʼanya mifugo na mali na kuteka nyara nyingi zaidi?”’
14 “Portanto, filho do homem, profetiza e diz a Gog: 'O Senhor Javé diz: “Naquele dia, quando meu povo Israel habitar em segurança, você não o saberá?
“Kwa hiyo, mwanadamu, tabiri na umwambie Gogu: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile, watu wangu Israeli watakapokuwa wanaishi salama, Je, wewe mwenyewe hutalijua hilo?
15 Você virá de seu lugar, dos confins do norte, você, e muitos povos com você, todos montados a cavalo, uma grande companhia e um poderoso exército.
Utakuja kutoka kwako huko kaskazini ya mbali, ukiwa pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kundi kubwa, jeshi kuu.
16 Você enfrentará meu povo Israel como uma nuvem para cobrir a terra. Acontecerá nos últimos dias que eu te trarei contra minha terra, para que as nações me conheçam quando eu for santificado em ti, Gog, diante de seus olhos”.
Utakuja dhidi ya watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Siku zijazo, ee Gogu, nitakuleta wewe dhidi ya nchi yangu, ili kwamba mataifa wapate kunijua Mimi nitakapojionyesha mtakatifu kwa kukupitia wewe mbele ya macho yao.
17 “'O Senhor Javé diz: “Você é aquele de quem eu falei no passado por meus servos, os profetas de Israel, que profetizaram naqueles dias durante anos que eu o traria contra eles?
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, wewe si yule niliyenena juu yako katika siku za zamani kwa kupitia kwa watumishi wangu manabii wa Israeli? Wakati ule walitabiri kwa miaka mingi kwamba ningekuleta upigane nao.
18 Acontecerá naquele dia, quando Gog vier contra a terra de Israel”, diz o Senhor Yahweh, “que minha ira subirá em minhas narinas”.
Hili ndilo litakalotokea katika siku ile: Gogu atakaposhambulia nchi ya Israeli, hasira yangu kali itaamka, asema Bwana Mwenyezi.
19 Pois no meu ciúme e no fogo da minha ira eu falei”. Certamente naquele dia haverá um grande tremor na terra de Israel,
Katika wivu wangu na ghadhabu yangu kali ninasema kuwa wakati ule patakuwepo tetemeko kuu katika nchi ya Israeli.
20 para que os peixes do mar, as aves do céu, os animais do campo, todas as coisas rastejantes que rastejam sobre a terra, e todos os homens que estão na superfície da terra tremam na minha presença. Então as montanhas serão derrubadas, os lugares íngremes cairão, e todos os muros cairão no chão.
Samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kondeni, kila kiumbe kitambaacho ardhini, na watu wote walio juu ya uso wa nchi watatetemeka mbele zangu. Milima itapinduka, majabali yatapasuka na kila ukuta utaanguka chini.
21 Vou pedir uma espada contra ele para todas as minhas montanhas”, diz o Senhor Yahweh. “A espada de cada homem será contra seu irmão”.
Nitaita upanga vita dhidi ya Gogu juu ya milima yangu yote, asema Bwana Mwenyezi. Upanga wa kila mtu utakuwa dhidi ya ndugu yake.
22 Entrarei em juízo com ele com pestilência e com sangue”. Choverei sobre ele, sobre suas hordas, e sobre os muitos povos que estão com ele, chuvas torrenciais com grandes pedras de granizo, fogo e enxofre.
Nitatekeleza hukumu juu yake kwa tauni na kwa umwagaji wa damu. Nitaifanya mvua ya mafuriko kunyesha, mvua ya mawe na moto wa kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya mataifa mengi walio pamoja naye.
23 Eu me engrandecerei e me santificarei, e me darei a conhecer aos olhos de muitas nações. Então eles saberão que eu sou Yahweh”.
Nami hivyo ndivyo nitakavyoonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu, nami nitajijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’

< Ezequiel 38 >