< Ezequiel 1 >

1 Agora no trigésimo ano, no quarto mês, no quinto dia do mês, como eu estava entre os cativos junto ao rio Chebar, os céus foram abertos, e eu vi visões de Deus.
Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.
2 No dia 5 do mês, que foi o quinto ano do cativeiro do rei Joaquim,
Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,
3 a palavra de Javé chegou a Ezequiel, o sacerdote, filho de Buzi, na terra dos caldeus junto ao rio Chebar; e a mão de Javé estava sobre ele.
neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.
4 Eu olhei, e eis que um vento tempestuoso saiu do norte: uma grande nuvem, com relâmpagos cintilantes, e um brilho ao redor dela, e do meio dela como se fosse metal incandescente, do meio do fogo.
Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.
5 Out de seu centro veio a semelhança de quatro seres vivos. Esta era a aparência deles: Eles tinham a semelhança de um homem.
Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,
6 Todos tinham quatro rostos, e cada um deles tinha quatro asas.
lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.
7 Seus pés eram retos. A sola de seus pés era como a sola de um pé de bezerro; e eles brilhavam como bronze polido.
Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.
8 Eles tinham as mãos de um homem sob suas asas em seus quatro lados. Os quatro tinham seus rostos e suas asas assim:
Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,
9 Suas asas estavam unidas umas às outras. Eles não se viraram quando foram. Cada um foi direto para a frente.
nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.
10 Quanto à semelhança de seus rostos, eles tinham o rosto de um homem. Os quatro tinham o rosto de um leão no lado direito. Os quatro tinham o rosto de um boi do lado esquerdo. Os quatro também tinham o rosto de uma águia.
Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.
11 Such eram seus rostos. Suas asas estavam estendidas acima. Duas asas de cada uma tocavam a outra, e duas cobriam seus corpos.
Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.
12 Cada uma delas foi em frente. Para onde o espírito deveria ir, eles foram. Eles não se viraram quando foram.
Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.
13 Quanto à semelhança dos seres vivos, sua aparência era como brasas de fogo ardentes, como a aparência de tochas. O fogo subia e descia entre as criaturas vivas. O fogo era brilhante e os relâmpagos se apagavam do fogo.
Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.
14 Os seres vivos correram e voltaram como a aparência de um relâmpago.
Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.
15 Agora que vi os seres vivos, eis que havia uma roda sobre a terra ao lado dos seres vivos, para cada uma das quatro faces da mesma.
Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.
16 A aparência das rodas e seu trabalho era como um berilo. As quatro tinham uma semelhança. Sua aparência e seu trabalho era como se fosse uma roda dentro de uma roda.
Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.
17 Quando eles foram, eles foram em suas quatro direções. Eles não giram quando vão.
Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.
18 Quanto às jantes, elas eram altas e horríveis; e as quatro tinham as jantes cheias de olhos por toda parte.
Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.
19 Quando os seres vivos foram embora, as rodas foram ao lado deles. Quando os seres vivos foram erguidos da terra, as rodas foram erguidas.
Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.
20 Para onde quer que o espírito fosse, elas iam. O espírito estava para ir para lá. As rodas foram levantadas ao lado delas; pois o espírito do ser vivente estava nas rodas.
Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
21 Quando estas foram, estas foram. Quando estas ficaram de pé, estas ficaram de pé. Quando estas foram erguidas da terra, as rodas foram erguidas ao lado delas; pois o espírito do ser vivente estava nas rodas.
Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
22 Sobre a cabeça do ser vivo havia a semelhança de uma extensão, como um cristal fantástico para se olhar, estendida sobre suas cabeças acima.
Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.
23 Debaixo da extensão, suas asas estavam retas, uma em direção à outra. Cada uma tinha duas que cobriam este lado, e cada uma tinha duas que cobriam seus corpos deste lado.
Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.
24 Quando eles foram, ouvi o ruído de suas asas como o ruído de grandes águas, como a voz do Todo-Poderoso, um ruído de tumulto como o ruído de um exército. Quando ficaram de pé, baixaram as asas.
Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi, kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.
25 Havia uma voz acima da extensão que estava sobre suas cabeças. Quando ficaram de pé, baixaram as asas.
Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.
26 Acima da extensão que estava sobre suas cabeças estava a semelhança de um trono, como a aparência de uma pedra de safira. Sobre a semelhança do trono havia uma semelhança como a aparência de um homem sobre ele acima.
Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.
27 Eu vi como se fosse metal brilhante, como a aparência de fogo dentro dele ao redor, a partir da aparência de sua cintura e para cima; e a partir da aparência de sua cintura e para baixo eu vi como se fosse a aparência de fogo, e havia brilho ao redor dele.
Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.
28 Como a aparência do arco-íris que está na nuvem no dia da chuva, assim era a aparência do brilho ao seu redor. Esta foi a aparência da semelhança da glória de Yahweh. Quando a vi, caí de cara, e ouvi uma voz de um que falava.
Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka. Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.

< Ezequiel 1 >