< Êxodo 1 >

1 Agora estes são os nomes dos filhos de Israel, que vieram ao Egito (cada homem e sua família vieram com Jacó):
Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli ambao walikwenda Misri na Yakobo, kila mmoja akiwa pamoja na jamaa yake:
2 Reuben, Simeão, Levi e Judá,
Reubeni, Simeoni, Lawi na Yuda;
3 Issachar, Zebulun e Benjamin,
Isakari, Zabuloni na Benyamini;
4 Dan e Naftali, Gad e Asher.
Dani na Naftali, Gadi na Asheri.
5 Todas as almas que saíram do corpo de Jacó eram setenta almas, e José já estava no Egito.
Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu sabini; Yosefu alikuwa tayari yuko Misri.
6 José morreu, assim como todos os seus irmãos, e toda aquela geração.
Basi Yosefu na kaka zake wote na kizazi kile chote walikufa,
7 Os filhos de Israel foram fecundos, e aumentaram abundantemente, e se multiplicaram, e cresceram excessivamente poderosos; e a terra se encheu deles.
lakini Waisraeli walikuwa wamezaana na kuongezeka sana, idadi yao ikawa kubwa mno, kwa hiyo wakaijaza nchi.
8 Agora surgiu um novo rei sobre o Egito, que não conhecia José.
Kisha mfalme mpya ambaye hakufahamu habari za Yosefu akatawala Misri.
9 Ele disse ao seu povo: “Eis que o povo dos filhos de Israel é mais e mais poderoso do que nós”.
Akawaambia watu wake, “Tazameni, Waisraeli wamekuwa wengi mno kwa idadi kutuliko sisi.
10 Venha, vamos lidar sabiamente com eles, para que não se multipliquem, e acontece que quando alguma guerra eclode, eles também se unem a nossos inimigos e lutam contra nós, e escapam da terra”.
Njooni, ni lazima tuwashughulikie kwa uangalifu, la sivyo watazidi kuwa wengi zaidi, na ikiwa patatokea vita, watajiunga na adui zetu kupigana dhidi yetu na kuondoka katika nchi hii.”
11 Por isso, eles colocam os encarregados sobre eles para afligi-los com seus fardos. Eles construíram cidades de armazenamento para o Faraó: Pithom e Raamses.
Basi Wamisri wakaweka wasimamizi wa kuwasimamia na kuwatesa Waisraeli kwa kazi ngumu, nao wakajenga miji ya Pithomu na Ramesesi ya kuweka akiba ya Farao.
12 Mas quanto mais eles os afligiam, mais se multiplicavam e mais se espalhavam. Eles começaram a temer os filhos de Israel.
Lakini walivyozidi kuteswa ndivyo walivyozidi kuongezeka na kuenea katika nchi; Wamisri wakawaogopa Waisraeli,
13 Os egípcios impiedosamente fizeram os filhos de Israel servir,
kwa hiyo wakawatumikisha kwa ukatili.
14 e tornaram suas vidas amargas com serviço duro em argamassa e em tijolos, e em todos os tipos de serviço no campo, todo o seu serviço, no qual impiedosamente os fizeram servir.
Wakafanya maisha ya Waisraeli kuwa machungu kwa kufanya kazi ngumu ya kutengeneza lami na kufyatua matofali, na kazi zote za mashambani; katika kazi zao zote ngumu, Wamisri waliwatumia Waisraeli kwa ukatili.
15 O rei do Egito falou às parteiras hebraicas, das quais o nome de uma era Shiphrah, e o nome da outra Puah,
Mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kimisri waliowazalisha wanawake wa Kiebrania, ambao majina yao ni Shifra na Pua,
16 e ele disse: “Quando você cumprir o dever de uma parteira para com as mulheres hebraicas, e vê-las no banco de nascimento, se for um filho, então você o matará; mas se for uma filha, então ela viverá”.
“Mtakapowazalisha wanawake wa Kiebrania, chunguzeni wanapojifungua. Ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni, lakini ikiwa ni msichana, mwacheni aishi.”
17 Mas as parteiras temiam a Deus, e não fizeram o que o rei do Egito lhes ordenou, mas salvaram os meninos bebês vivos.
Lakini hao wakunga walimcha Mungu na hawakufanya kile mfalme wa Misri alichowaambia kufanya, bali wakawaacha watoto wa kiume waishi.
18 O rei do Egito chamou as parteiras e disse-lhes: “Por que vocês fizeram isso e salvaram os meninos vivos?”.
Ndipo mfalme wa Misri akawaita hao wakunga, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivi? Mbona mmeacha watoto wa kiume waishi?”
19 As parteiras disseram ao faraó: “Porque as mulheres hebraicas não são como as mulheres egípcias; pois elas são vigorosas e dão à luz antes que a parteira chegue até elas”.
Wakunga wakamjibu Farao, “Wanawake wa Kiebrania ni tofauti na wanawake wa Kimisri; wao wana nguvu, nao hujifungua watoto kabla wakunga hawajafika.”
20 Deus lidou bem com as parteiras, e o povo se multiplicou, e cresceu muito poderoso.
Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wakunga hao. Waisraeli wakaongezeka na kuendelea kuwa wengi zaidi.
21 Como as parteiras temiam a Deus, Ele lhes deu famílias.
Kwa vile hao wakunga walimcha Mungu, Mungu akawajalia kuwa na jamaa zao wenyewe.
22 O Faraó ordenou a todo seu povo, dizendo: “Lançareis no rio todo filho que nascer, e toda filha salvareis com vida”.
Kisha Farao akatoa agizo hili kwa watu wake wote: “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania lazima atupwe katika Mto Naili, bali kila mtoto wa kike aachwe aishi.”

< Êxodo 1 >