< Êxodo 23 >
1 “Você não deve divulgar um relatório falso. Não junte sua mão aos ímpios para ser uma testemunha maliciosa.
“Usieneze habari za uongo. Usimsaidie mtu mwovu kwa kuwa shahidi mwenye nia ya kudhuru wengine.
2 “Você não deve seguir uma multidão para fazer o mal. Você não testemunhará em tribunal ao lado de uma multidão para perverter a justiça.
“Usifuate umati wa watu katika kutenda mabaya. Unapotoa ushahidi kwenye mashtaka, usipotoshe haki ukijumuika na umati wa watu,
3 “Não favorecerá um homem pobre em sua causa.
nawe usimpendelee mtu maskini katika mashtaka yake.
4 “Se você encontrar o boi de seu inimigo ou o burro dele se desviando, certamente o trará de volta para ele novamente.
“Kama ukikutana na maksai au punda wa adui yako anapotea, hakikisha umemrudisha kwake.
5 “Se você vir o burro dele que o odeia cair sob seu fardo, não o deixe. Você certamente o ajudará com isso.
Ukiona punda wa mtu anayekuchukia ameanguka na mzigo wake, usimwache hapo alipoangukia; hakikisha kuwa umemsaidia.
6 “Você não deve negar justiça a seu pobre povo em seus processos judiciais.
“Usiwanyime haki watu wako walio maskini katika mashtaka yao.
7 “Mantenha-se longe de uma acusação falsa, e não mate os inocentes e justos; pois eu não justificarei os ímpios.
Ujiepushe na mashtaka ya uongo, wala usimuue mtu asiye na hatia au mtu mwaminifu, kwa maana sitamhesabia hana hatia yeye aliye na hatia.
8 “Você não aceitará suborno, pois um suborno cega aqueles que têm visão e perverte as palavras dos justos.
“Usipokee rushwa, kwa kuwa rushwa hupofusha wale waonao, na kupinda maneno ya wenye haki.
9 “Você não oprimirá um estrangeiro, pois você conhece o coração de um estrangeiro, uma vez que foi um estrangeiro na terra do Egito.
“Usimwonee mgeni; ninyi wenyewe mnajua jinsi mgeni anavyojisikia, kwa sababu mlikuwa wageni Misri.
10 “Durante seis anos semearás tua terra, e recolherás em seu aumento,
“Kwa muda wa miaka sita mtapanda mashamba yenu na kuvuna mazao,
11 mas no sétimo ano a deixarás descansar e ficar em pousio, para que os pobres de teu povo possam comer; e o que eles deixarem o animal do campo comerá. Da mesma forma, você lidará com seu vinhedo e com seu olival.
lakini katika mwaka wa saba usiilime ardhi wala kuitumia, ili watu walio maskini miongoni mwenu waweze kupata chakula kutoka kwenye hayo mashamba, nao wanyama pori wapate chakula kwa yale mabaki watakayobakiza. Utafanya hivyo katika shamba lako la mizabibu na la mizeituni.
12 “Seis dias você fará seu trabalho, e no sétimo dia descansará, para que seu boi e seu burro descansem, e o filho de seu servo, e o estrangeiro possa ser refrescado.
“Kwa siku sita fanya kazi zako, lakini siku ya saba usifanye kazi, ili maksai wako na punda wako wapate kupumzika, naye mtumwa aliyezaliwa nyumbani mwako, pamoja na mgeni, wapate kustarehe.
13 “Tenha cuidado para fazer todas as coisas que lhe disse; e não invoque o nome de outros deuses ou mesmo deixe que eles sejam ouvidos de sua boca.
“Uzingatie kutenda kila kitu nilichokuambia. Usiombe kwa majina ya miungu mingine, wala usiyaruhusu kusikika kinywani mwako.
14 “Você deverá observar uma festa para mim três vezes ao ano.
“Mara tatu kwa mwaka utanifanyia sikukuu.
15 Você observará a festa dos pães ázimos. Sete dias comereis pães ázimos, como vos ordenei, na hora marcada no mês de Abibe (pois nele saístes do Egito), e ninguém aparecerá vazio diante de mim.
“Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu; kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu kama nilivyokuagiza. Fanya jambo hili kwa wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa sababu katika mwezi huo ulitoka Misri. “Mtu yeyote asije mbele yangu mikono mitupu.
16 E a festa da colheita, os primeiros frutos de vosso trabalho, que semeais no campo; e a festa da colheita, no final do ano, quando vos reunirdes em vosso trabalho fora do campo.
“Utaadhimisha Sikukuu ya Mavuno kwa malimbuko ya mazao yako uliyopanda katika shamba lako. “Utaadhimisha Sikukuu ya Kukusanya mavuno mwishoni mwa mwaka, unapokusanya mavuno yako toka shambani.
17 Três vezes no ano, todos os seus machos aparecerão perante o Senhor Javé.
“Mara tatu kwa mwaka wanaume wote watakuja mbele za Bwana Mwenyezi.
18 “Você não oferecerá o sangue do meu sacrifício com pão levedado. A gordura do meu banquete não permanecerá a noite toda até a manhã.
“Msitoe damu ya dhabihu kwangu pamoja na kitu chochote kilicho na chachu. “Mafuta ya mnyama wa sadaka ya sikukuu yangu yasibakizwe mpaka asubuhi.
19 Você trará o primeiro dos primeiros frutos de sua terra para a casa de Yahweh, seu Deus. “Você não deve ferver um cabrito no leite de sua mãe.
“Utaleta malimbuko bora ya ardhi yako katika nyumba ya Bwana Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
20 “Eis que envio um anjo diante de vocês, para mantê-los no caminho e para trazê-los ao lugar que preparei.
“Tazama, ninamtuma malaika akutangulie mbele yako akulinde njiani na kukuleta mpaka mahali nilipoandaa.
21 Preste atenção nele, e escute sua voz. Não o provoque, pois ele não perdoará sua desobediência, pois meu nome está nele.
Mtamtii na kusikiliza kile anachokisema. Usiasi dhidi yake; hatakusamehe uasi wako, kwa maana Jina langu limo ndani yake.
22 Mas se você realmente ouvir sua voz, e fizer tudo o que eu falar, então eu serei um inimigo para seus inimigos, e um adversário para seus adversários.
Kama ukitii kweli kweli kile asemacho na kufanya yote nisemayo, nitakuwa adui wa adui zako, na nitawapinga wale wakupingao.
23 Pois meu anjo irá perante vós, e vos levará ao amorreu, ao hitita, ao perizeu, ao cananeu, ao hivita e ao jebuseu; e eu os cortarei.
Malaika wangu atatangulia mbele yako na kukuleta katika nchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanaani, Wahivi na Wayebusi, nami nitawafutilia mbali.
24 Não vos curvareis diante de seus deuses, nem os servireis, nem seguireis suas práticas, mas os derrubareis totalmente e demolireis seus pilares.
Usiisujudie miungu yao, au kuiabudu, wala kufuata desturi yao. Utayabomoa kabisa na kuvunjavunja mawe yao ya ibada vipande vipande.
25 Servirás a Javé teu Deus, e ele abençoará teu pão e tua água, e eu tirarei do meio de ti a doença.
Utamwabudu Bwana Mungu wako, na baraka zake zitakuwa juu ya vyakula vyako na maji yako. Nami nitaondoa maradhi miongoni mwako,
26 Ninguém abortará ou será estéril em sua terra. Cumprirei o número de seus dias.
na hakuna atakayeharibu mimba wala atakayekuwa tasa katika nchi yako. Nami nitakupa maisha makamilifu.
27 Enviarei meu terror diante de vocês, e confundirei todas as pessoas a quem vocês vêm, e farei com que todos os seus inimigos voltem as costas para vocês.
“Nitapeleka utisho wangu mbele yako na kufadhaisha kila taifa utakalolifikia. Nitafanya adui zako wote wakupe kisogo na kukimbia.
28 Enviarei o vespeiro diante de vocês, que expulsará o Hivita, o Canaanita e o Hitita, de diante de vocês.
Nitatanguliza manyigu mbele yako kuwafukuza Wahivi, Wakanaani na Wahiti waondoke njiani mwako.
29 Não os expulsarei de diante de vocês em um ano, para que a terra não se torne desolada e os animais do campo não se multipliquem contra vocês.
Lakini sitawafukuza kwa mara moja, kwa sababu nchi itabaki ukiwa na wanyama pori watakuwa wengi mno kwako.
30 Pouco a pouco os expulsarei de diante de vocês, até que vocês tenham aumentado e herdado a terra.
Nitawafukuza kidogo kidogo mbele yako, mpaka uwe umeongezeka kiasi cha kutosha kuimiliki nchi.
31 Fixarei sua fronteira do Mar Vermelho até o mar dos filisteus, e do deserto até o rio; pois eu entregarei os habitantes da terra em suas mãos, e você os expulsará de sua frente.
“Nitaweka mipaka ya nchi yako kuanzia Bahari ya Shamu hadi Bahari ya Wafilisti, na kuanzia jangwani hadi Mto Frati. Nitawatia watu wanaoishi katika nchi hizo mikononi mwako, nawe utawafukuza watoke mbele yako.
32 Não fareis nenhum pacto com eles, nem com seus deuses.
Usifanye agano lolote nao wala na miungu yao.
33 Eles não habitarão em tua terra, para que não te façam pecar contra mim, pois se servires os deuses deles, isso certamente será um laço para ti”.
Usiwaache waishi katika nchi yako, la sivyo watakusababisha utende dhambi dhidi yangu, kwa sababu ibada ya miungu yao hakika itakuwa mtego kwako.”