< Atos 7 >

1 O sumo sacerdote disse: “São estas coisas assim?”
Basi, Kuhani Mkuu akamwuliza, “Je, mambo haya ni kweli?”
2 Ele disse: “Irmãos e pais, escutem. O Deus da glória apareceu a nosso pai Abraão quando ele estava na Mesopotâmia, antes de viver em Haran,
Naye Stefano akasema, “Ndugu zangu na akina baba, nisikilizeni! Mungu alimtokea baba yetu Abrahamu alipokuwa kule Mesopotamia kabla hajaenda kukaa kule Harani.
3 e lhe disse: “Saia de sua terra e afaste-se de seus parentes, e venha para uma terra que eu lhe mostrarei”.
Mungu alimwambia: Ondoka katika nchi yako; waache watu wa ukoo wako; nenda katika nchi nitakayokuonyesha!
4 Então ele saiu da terra dos caldeus e viveu em Haran. De lá, quando seu pai faleceu, Deus o levou para esta terra onde você está vivendo agora.
Kwa hivyo, Abrahamu alihama nchi ya Kaldayo, akaenda kukaa Harani. Baada ya kifo cha baba yake, Mungu alimtoa tena Harani akaja kukaa katika nchi hii mnayokaa sasa.
5 Ele não lhe deu nenhuma herança nela, não, nem mesmo para colocar o pé. Ele prometeu que a daria a ele por uma posse, e à sua descendência depois dele, quando ainda não tivesse nenhum filho.
Mungu hakumpa hata sehemu moja ya nchi hii iwe mali yake; hata hivyo, alimwahidia kumpa nchi hii iwe yake na ya wazawa wake, ingawaje wakati huu hakuwa na mtoto.
6 Deus falou assim: que sua prole viveria como alienígena em uma terra estranha, e que seria escravizada e maltratada por quatrocentos anos.
Mungu alimwambia hivi: Wazao wako watapelekwa katika nchi inayotawaliwa na watu wengine, na huko watafanywa watumwa na kutendewa vibaya kwa muda wa miaka mia nne.
7 'Eu julgarei a nação à qual eles estarão em cativeiro', disse Deus, 'e depois disso eles sairão e me servirão neste lugar'.
Lakini mimi nitalihukumu taifa hilo litakalowafanya watumwa. Kisha nitawatoa katika nchi hiyo ili waje kuniabudu mahali hapa.
8 Ele lhe deu o pacto da circuncisão. Assim Abraão tornou-se o pai de Isaac, e o circuncidou no oitavo dia. Isaque se tornou o pai de Jacó, e Jacó se tornou o pai dos doze patriarcas.
Halafu Mungu aliifanya tohara iwe ishara ya agano. Hivyo, Abrahamu alimtahiri mtoto wake Isaka, siku ya nane baada ya kuzaliwa. Na Isaka, vivyo hivyo, alimtahiri Yakobo. Naye Yakobo aliwatendea wale mababu kumi na wawili vivyo hivyo.
9 “Os patriarcas, movidos de ciúmes contra José, venderam-no para o Egito. Deus estava com ele
“Wale mababu walimwonea wivu Yosefu, wakamuuza utumwani Misri. Lakini Mungu alikuwa pamoja naye,
10 e o libertou de todas as suas aflições, dando-lhe favor e sabedoria diante do Faraó, rei do Egito. Ele o fez governador do Egito e de toda a sua casa.
akamwokoa katika taabu zake zote. Mungu alimjalia fadhili na hekima mbele ya Farao, mfalme wa Misri, hata Farao akamweka awe mkuu wa ile nchi na nyumba ya kifalme.
11 Agora veio uma fome sobre toda a terra do Egito e de Canaã, e uma grande aflição. Nossos pais não encontraram comida.
Kisha, kulizuka njaa kubwa katika nchi yote ya Misri na Kanaani, ikasababisha dhiki kubwa. Babu zetu hawakuweza kupata chakula chochote.
12 Mas quando Jacó soube que havia grãos no Egito, enviou nossos pais pela primeira vez.
Basi, Yakobo alipopata habari kwamba huko Misri kulikuwa na nafaka, aliwatuma watoto wake, yaani babu zetu, waende huko Misri mara ya kwanza.
13 Na segunda vez José foi dado a conhecer a seus irmãos, e a família de José foi revelada ao Faraó.
Katika safari yao ya pili, Yosefu alijitambulisha kwa ndugu zake, na Farao akaifahamu jamaa ya Yosefu.
14 José enviou e convocou Jacó, seu pai e todos os seus parentes, setenta e cinco almas.
Yosefu alituma ujumbe kwa baba yake na jamaa yote, jumla watu sabini na tano, waje Misri.
15 Jacó desceu ao Egito e morreu, ele mesmo e nossos pais;
Hivyo, Yakobo alikwenda Misri ambako yeye na babu zetu wengine walikufa.
16 e eles foram trazidos de volta a Siquém e colocados no túmulo que Abraão comprou por um preço em prata dos filhos de Hamor de Siquém.
Miili yao ililetwa mpaka Shekemu, ikazikwa katika kaburi Abrahamu alilonunua kutoka kwa kabila la Hamori kwa kiasi fulani cha fedha.
17 “Mas quando se aproximava o tempo da promessa que Deus havia jurado a Abraão, o povo cresceu e se multiplicou no Egito,
“Wakati ulipotimia Mungu aitimize ahadi aliyompa Abrahamu, idadi ya wale watu kule Misri ilikwisha ongezeka na kuwa kubwa zaidi.
18 até que surgiu um rei diferente que não conhecia José.
Mwishowe, mfalme mmoja ambaye hakumtambua Yosefu alianza kutawala huko Misri.
19 O mesmo aproveitou-se de nossa raça e maltratou nossos pais, forçando-os a abandonar seus bebês, para que não continuassem vivos.
Alilifanyia taifa letu ukatili, akawatendea vibaya babu zetu kwa kuwalazimisha waweke nje watoto wao wachanga ili wafe.
20 Naquela época nasceu Moisés, e era muito bonito para Deus. Ele foi alimentado por três meses na casa de seu pai.
Mose alizaliwa wakati huo. Alikuwa mtoto mzuri sana. Alilelewa nyumbani kwa muda wa miezi mitatu,
21 Quando ele foi abandonado, a filha do Faraó o acolheu e o criou como seu próprio filho.
na alipotolewa nje, binti wa Farao alimchukua, akamlea kama mtoto wake.
22 Moisés foi instruído em toda a sabedoria dos egípcios. Ele era poderoso em suas palavras e obras.
Mose alifundishwa mambo yote ya hekima ya Wamisri akawa mashuhuri kwa maneno na matendo.
23 Mas quando ele tinha quarenta anos de idade, veio ao seu coração visitar seus irmãos, os filhos de Israel.
“Alipokuwa na umri wa miaka arobaini aliamua kwenda kuwaona ndugu zake Waisraeli.
24 Ao ver um deles sofrendo mal, ele o defendeu e vingou aquele que era oprimido, atingindo o egípcio.
Huko alimwona mmoja wao akitendewa vibaya, akaenda kumwokoa, na kulipiza kisasi, akamuua yule Mmisri.
25 Ele supunha que seus irmãos entendiam que Deus, por sua mão, estava lhes dando libertação; mas eles não entendiam.
(Alidhani kwamba Waisraeli wenzake wangeelewa kwamba Mungu angemtumia yeye kuwakomboa, lakini hawakuelewa hivyo.)
26 “No dia seguinte, ele lhes apareceu enquanto lutavam, e os exortou a ficarem em paz novamente, dizendo: 'Senhores, vocês são irmãos'. Por que vocês se enganam uns aos outros?
Kesho yake, aliwaona Waisraeli wawili wakipigana, akajaribu kuwapatanisha, akisema: Ninyi ni ndugu; kwa nini basi, kutendeana vibaya ninyi kwa ninyi?
27 Mas aquele que fez mal ao próximo o afastou, dizendo: 'Quem fez de vocês um soberano e um juiz sobre nós?
Yule aliyekuwa anampiga mwenzake alimsukuma Mose kando akisema: Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi wa watu?
28 Você quer me matar como matou o egípcio ontem?
Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri jana?
29 Moisés fugiu deste ditado, e se tornou um estranho na terra de Midian, onde se tornou o pai de dois filhos.
Baada ya kusikia hayo Mose alikimbia, akaenda kukaa katika nchi ya Midiani na huko akapata watoto wawili.
30 “Quando quarenta anos foram cumpridos, um anjo do Senhor apareceu-lhe no deserto do Monte Sinai, em uma chama de fogo em um arbusto.
“Miaka arobaini ilipotimia, malaika wa Bwana alimtokea Mose katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto kule jangwani karibu na mlima Sinai.
31 Quando Moisés o viu, ele se perguntou à vista. Ao aproximar-se para ver, a voz do Senhor veio até ele,
Mose alistaajabu sana kuona jambo hilo hata akasogea karibu ili achungulie; lakini alisikia sauti ya Bwana:
32 'Eu sou o Deus de seus pais: o Deus de Abraão, o Deus de Isaac, e o Deus de Jacó'. Moisés tremeu e não ousou olhar.
Mimi ni Mungu wa baba zako, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo! Mose akatetemeka kwa hofu na wala hakuthubutu kutazama zaidi.
33 O Senhor disse-lhe: 'Tirai as sandálias, pois o lugar em que estais é terra santa'.
Bwana akamwambia: Vua viatu vyako maana hapa unaposimama ni mahali patakatifu.
34 Certamente vi a aflição do meu povo que está no Egito, e ouvi seus gemidos. Desci para entregá-los. Agora venha, eu o enviarei ao Egito”.
Nimeyaona mabaya wanayotendewa watu wangu kule Misri. Nimesikia kilio chao, nami nimekuja kuwaokoa. Basi sasa, nitakutuma Misri.
35 “Este Moisés a quem recusaram, dizendo: 'Quem te fez governante e juiz?'-Deus o enviou como governante e libertador pela mão do anjo que lhe apareceu no mato.
“Huyu Mose ndiye yule watu wa Israeli waliyemkataa waliposema: Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi wetu? Kwa njia ya yule malaika aliyemtokea katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto, Mungu alimtuma Mose huyo awe kiongozi na mkombozi.
36 Este homem os conduziu para fora, tendo feito maravilhas e sinais no Egito, no Mar Vermelho e no deserto por quarenta anos.
Ndiye aliyewaongoza wale watu watoke Misri kwa kufanya miujiza na maajabu katika nchi ya Misri, katika bahari ya Shamu na jangwani kwa muda wa miaka arobaini.
37 Este é aquele Moisés que disse aos filhos de Israel: 'O Senhor nosso Deus levantará um profeta para vós do meio de vossos irmãos, como eu'.
Mose ndiye aliyewaambia watu wa Israeli: Mungu atawateulieni nabii kama mimi kutoka katika ndugu zenu ninyi wenyewe.
38 Este é aquele que estava na assembléia no deserto com o anjo que lhe falou no Monte Sinai, e com nossos pais, que receberam revelações vivas para nos dar,
Wakati watu wa Israeli walipokutana pamoja kule jangwani, Mose ndiye aliyekuwako huko pamoja nao. Alikuwa huko pamoja na babu zetu na yule malaika aliyeongea naye mlimani Sinai; ndiye aliyekabidhiwa yale maneno yaletayo uzima atupe sisi.
39 a quem nossos pais não seriam obedientes, mas o rejeitaram e voltaram em seus corações para o Egito,
“Lakini yeye ndiye babu zetu waliyemkataa kumsikiliza; walimsukuma kando, wakatamani kurudi Misri.
40 dizendo a Aarão: 'Fazei-nos deuses que irão adiante de nós, pois quanto a este Moisés que nos conduziu para fora da terra do Egito, não sabemos o que aconteceu com ele'.
Walimwambia Aroni: Tutengenezee miungu itakayotuongoza njiani, maana hatujui yaliyompata Mose huyu aliyetuongoza kutoka Misri!
41 Eles fizeram um bezerro naqueles dias, e trouxeram um sacrifício ao ídolo, e se alegraram com as obras de suas mãos.
Hapo ndipo walipojitengenezea sanamu ya ndama, wakaitambikia na kukifanyia sherehe kitu ambacho ni kazi ya mikono yao wenyewe.
42 Mas Deus se afastou e os entregou para servir ao exército do céu, como está escrito no livro dos profetas, “Você me ofereceu animais mortos e sacrifícios? quarenta anos no deserto, ó casa de Israel?
Lakini Mungu aliondoka kati yao, akawaacha waabudu nyota za anga, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha manabii: Enyi watu wa Israeli! Si mimi mliyenitolea dhabihu na sadaka kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani!
43 Você assumiu o tabernáculo de Moloch, a estrela de seu deus Rephan, os números que você fez para adorar, por isso vos levarei para além da Babilônia”.
Ninyi mlikibeba kibanda cha mungu Moloki, na sanamu ya nyota ya mungu wenu Refani. Sanamu mlizozifanya ndizo mlizoabudu. Kwa sababu hiyo nitakupeleka mateka mbali kupita Babuloni!
44 “Nossos pais tinham o tabernáculo do testemunho no deserto, como aquele que falou com Moisés lhe ordenou que o fizesse de acordo com o padrão que ele tinha visto;
Kule jangwani babu zetu walikuwa na lile hema lililoshuhudia kuweko kwa Mungu. Lilitengenezwa kama Mungu alivyomwambia Mose alifanye; nakala kamili ya kile alichoonyeshwa.
45 que também nossos pais, por sua vez, trouxeram com Josué quando entraram na posse das nações que Deus expulsou diante da face de nossos pais para os dias de Davi,
Kisha babu zetu walilipokezana wao kwa wao mpaka wakati wa Yoshua, walipoinyakua ile nchi kutoka kwa mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele yao. Hapo lilikaa mpaka nyakati za Daudi.
46 que encontrou favor aos olhos de Deus, e pediu para encontrar uma morada para o Deus de Jacó.
Daudi alipata upendeleo kwa Mungu, akamwomba Mungu ruhusa ya kumjengea makao yeye aliye Mungu wa Yakobo.
47 Mas Salomão construiu-lhe uma casa.
Lakini Solomoni ndiye aliyemjengea Mungu nyumba.
48 Entretanto, o Altíssimo não habita em templos feitos com as mãos, como diz o profeta,
“Hata hivyo, Mungu Mkuu haishi katika nyumba zilizojengwa na binadamu; kama nabii asemavyo:
49 'o céu é meu trono, e a terra um escabelo para os meus pés. Que tipo de casa você vai me construir?” diz o Senhor. Ou qual é o lugar do meu descanso?
Bwana asema: Mbingu ni kiti changu cha enzi na dunia ni kiti changu cha kuwekea miguu.
50 Minha mão não fez todas essas coisas”?
Ni nyumba ya namna gani basi mnayoweza kunijengea, na ni mahali gani nitakapopumzika? Vitu hivi vyote ni mimi nimevifanya, au sivyo?
51 “Você de pescoço duro e incircunciso no coração e nos ouvidos, você sempre resiste ao Espírito Santo! Como fizeram seus pais, assim fazem vocês.
“Enyi wakaidi wakuu! Mioyo na masikio yenu ni kama ya watu wa mataifa. Ninyi ni kama baba zenu. Siku zote mnampinga Roho Mtakatifu.
52 Qual dos profetas não foi perseguido por seus pais? Eles mataram aqueles que predisseram a vinda do Justo, dos quais vocês se tornaram agora traidores e assassinos.
Je, yuko nabii yeyote ambaye baba zenu hawakumtesa? Waliwaua hao Mungu aliowatuma watangaze kuja kwake yule Mwenye Haki. Na sasa, ninyi mmemsaliti, mkamuua.
53 Vocês receberam a lei como ela foi ordenada pelos anjos, e não a cumpriram”!
Ninyi mliipokea ile Sheria iliyoletwa kwenu na Malaika, lakini hamkuitii.”
54 Agora, quando ouviram estas coisas, foram cortados até o coração, e lhe rangeram os dentes.
Wale wazee wa Baraza waliposikia hayo, walighadhibika sana, wakamsagia meno kwa hasira.
55 Mas ele, estando cheio do Espírito Santo, olhou firmemente para o céu e viu a glória de Deus, e Jesus em pé à direita de Deus,
Lakini Stefano akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akatazama juu mbinguni, akauona utukufu wa Mungu na Yesu amekaa upande wa kulia wa Mungu.
56 e disse: “Eis que vejo os céus abertos e o Filho do Homem em pé à direita de Deus”!
Akasema, “Tazameni! Ninaona mbingu zimefunuliwa na Mwana wa Mtu amesimama upande wa kulia wa Mungu.”
57 Mas eles gritaram com voz alta e pararam seus ouvidos, depois se apressaram a golpeá-lo com um só acordo.
Hapo, watu wote katika kile kikao cha Baraza, wakapiga kelele na kuziba masikio yao kwa mikono yao. Kisha wakamrukia wote kwa pamoja,
58 Eles o expulsaram da cidade e o apedrejaram. As testemunhas colocaram suas vestes aos pés de um jovem chamado Saul.
wakamtoa nje ya mji, wakampiga mawe. Wale mashahidi wakayaweka makoti yao chini ya ulinzi wa kijana mmoja jina lake Saulo.
59 Apedrejaram Estêvão quando ele gritou, dizendo: “Senhor Jesus, receba meu espírito”!
Waliendelea kumpiga mawe Stefano, huku akiwa anasali: “Bwana Yesu, ipokee roho yangu!”
60 Ele se ajoelhou e gritou com voz alta: “Senhor, não detenha este pecado contra eles”! Quando ele disse isto, ele adormeceu.
Akapiga magoti, akalia kwa sauti kubwa: “Bwana, usiwalaumu kwa sababu ya dhambi hii.” Baada ya kusema hivyo, akafa.

< Atos 7 >