< Atos 17 >

1 Agora, quando passaram por Amphipolis e Apollonia, chegaram a Tessalônica, onde havia uma sinagoga judaica.
Kwa kupitia Amfipoli na Apolonia, walisafiri mpaka Thesalonika ambako kulikuwa na sunagogi la Wayahudi.
2 Paulo, como era seu costume, foi até eles; e durante três dias de sábado raciocinou com eles a partir das Escrituras,
Paulo alijiunga nao kama ilivyokuwa desturi yake akajadiliana nao Sabato tatu mfululizo, akatumia Maandiko Matakatifu.
3 explicando e demonstrando que o Cristo tinha que sofrer e ressuscitar dos mortos, e dizendo: “Este Jesus, que eu vos proclamo, é o Cristo”.
Aliyaeleza na kuonyesha kwamba ilimbidi Kristo kuteswa na kufufuka kutoka wafu. Akawaambia, “Yesu ambaye mimi namhubiri kwenu ndiye Kristo.”
4 Alguns deles foram persuadidos e se juntaram a Paul e Silas: dos gregos devotos, uma grande multidão, e não poucas das principais mulheres.
Baadhi yao walikubali wakajiunga na Paulo na Sila. Kadhalika, idadi kubwa ya Wagiriki waliomcha Mungu pamoja na wanawake wengi wa tabaka la juu, walijiunga nao.
5 Mas os judeus sem escrúpulos levaram alguns homens perversos do mercado e reunindo uma multidão, colocaram a cidade em alvoroço. Assaltando a casa de Jason, eles procuraram levá-los até o povo.
Lakini Wayahudi wakaona wivu; wakawakodi wafidhuli sokoni, wakafanya kikundi na kuzusha fujo mjini kote. Wakaivamia nyumba ya Yasoni wakitumaini kuwapata humo Paulo na Sila ili wawalete hadharani.
6 Quando não os encontraram, arrastaram Jasão e alguns irmãos diante dos governantes da cidade, gritando: “Estes que viraram o mundo de cabeça para baixo também vieram aqui,
Lakini hawakuwapata na hivyo walimburuta Yasoni pamoja na ndugu wengine mpaka kwa wakuu wa mji, wakapiga kelele: “Watu hawa wamekuwa wakivuruga dunia yote na sasa wako hapa mjini.
7 a quem Jasão recebeu”. Todos eles agem contrariamente aos decretos de César, dizendo que há outro rei, Jesus”!
Yasoni amewakaribisha nyumbani kwake. Wote wanafanya kinyume cha amri ya Kaisari wakisema eti Kuna mfalme mwingine aitwaye Yesu.”
8 A multidão e os governantes da cidade ficaram atormentados quando ouviram estas coisas.
Kwa maneno hayo waliwatia wasiwasi wakuu wa mji na kundi la watu.
9 Quando tomaram a segurança de Jasão e dos demais, eles os deixaram ir.
Wakawafanya Yasoni na wenzake watoe dhamana, kisha wakawaacha waende zao.
10 Os irmãos enviaram imediatamente Paul e Silas à noite para Beroea. Quando chegaram, eles entraram na sinagoga judaica.
Usiku, wale ndugu waliwahimiza Paulo na Sila waende Berea. Mara tu walipofika huko, walikwenda katika sunagogi la Wayahudi.
11 Agora estes eram mais nobres do que os de Tessalônica, na medida em que receberam a palavra com toda a prontidão de espírito, examinando diariamente as Escrituras para ver se estas coisas eram assim.
Watu wa huko walikuwa wasikivu zaidi kuliko wale wa Thesalonika. Waliupokea ule ujumbe kwa hamu kubwa, wakawa wanayachunguza Maandiko Matakatifu kila siku, ili kuona kama yale waliyosema Paulo na Sila yalikuwa kweli.
12 Muitos deles, portanto, acreditavam; também das proeminentes mulheres gregas, e não poucos homens.
Wengi wao waliamini na pia wanawake wa Kigiriki wa tabaka la juu na wanaume pia.
13 Mas quando os judeus de Tessalônica tiveram conhecimento de que a palavra de Deus também foi proclamada por Paulo em Beroea, eles vieram para lá da mesma forma, agitando as multidões.
Lakini, Wayahudi wa Thesalonika walipogundua kwamba Paulo alikuwa anahubiri neno la Mungu huko Berea, walikwenda huko, wakaanza kufanya fujo na kuchochea makundi ya watu.
14 Então os irmãos enviaram imediatamente Paulo para ir até o mar, e Silas e Timóteo ainda lá ficaram.
Wale ndugu wakamsindikiza haraka aende pwani lakini Sila na Timotheo walibaki Berea.
15 Mas aqueles que escoltavam Paulo o levaram até Atenas. Recebendo um mandamento para Silas e Timóteo de que viessem até ele muito rapidamente, eles partiram.
Wale ndugu waliomsindikiza Paulo walikwenda pamoja naye mpaka Athene. Kisha, wakarudi pamoja na maagizo kutoka kwa Paulo kwamba Sila na Timotheo wamfuate upesi iwezekanavyo.
16 Agora, enquanto Paulo esperava por eles em Atenas, seu espírito foi provocado dentro dele ao ver a cidade cheia de ídolos.
Paulo alipokuwa anawasubiri Sila na Timotheo huko Athene, moyo wake ulighadhibika sana alipoona jinsi mji huo ulivyokuwa umejaa sanamu za miungu.
17 Assim, ele raciocinava na sinagoga com os judeus e as pessoas devotas, e no mercado todos os dias com aqueles que o encontravam.
Alijadiliana na Wayahudi na watu wengine waliomcha Mungu katika sunagogi; na kila siku alikuwa na majadiliano sokoni pamoja na wowote wale waliojitokeza.
18 Alguns dos filósofos epicureus e estóicos também estavam conversando com ele. Alguns diziam: “O que este tagarela quer dizer?”. Outros disseram: “Ele parece estar defendendo divindades estrangeiras”, porque ele pregou Jesus e a ressurreição.
Wengine waliofuata falsafa ya Epikuro na Stoiki walibishana naye. Wengine walisema, “Anataka kusema nini huyu bwanamaneno?” Kwa kuwa Paulo alikuwa anahubiri juu ya Yesu na juu ya ufufuo, wengine walisema, “Inaonekana kama anahubiri juu ya miungu ya kigeni.”
19 Eles se apoderaram dele e o levaram para o Areópago, dizendo: “Podemos saber qual é este novo ensinamento, do qual você está falando?
Hivyo walimchukua Paulo, wakampeleka Areopago, wakasema, “Tunataka kujua jambo hili jipya ulilokuwa unazungumzia.
20 Para você trazer certas coisas estranhas aos nossos ouvidos. Queremos saber, portanto, o que significam estas coisas”.
Vitu vingine tulivyosikia kwa masikio yetu vinaonekana kuwa viroja kwetu. Tungependa kujua mambo haya yana maana gani.”
21 Agora todos os atenienses e os estranhos que lá vivem não gastam seu tempo em mais nada, a não ser para contar ou ouvir alguma coisa nova.
Wananchi wa Athene na wakazi wengine wa huko walikuwa wanatumia wakati wao wote kuhadithiana na kusikiliza habari mpyampya.
22 Paulo estava no meio do Areópago e disse: “Vocês, homens de Atenas, eu percebo que são muito religiosos em todas as coisas.
Basi, Paulo alisimama mbele ya baraza la Areopago, akasema, “Wananchi wa Athene! Ninaona kwamba ninyi, kwa vyovyote, ni watu wa dini sana.
23 Pois ao passar e observar os objetos de vosso culto, encontrei também um altar com esta inscrição: “A UM DEUS DESCONHECIDO”. O que, portanto, vós adorais na ignorância, eu vos anuncio.
Sababu yenyewe ni kwamba katika pitapita yangu niliangalia sanamu zenu za ibada nikakuta madhabahu moja ambayo imeandikwa: Kwa ajili ya Mungu yule Asiyejulikana. Basi, huyo mnayemwabudu bila kujua, ndiye ninayemhubiri kwenu.
24 O Deus que fez o mundo e todas as coisas nele, ele, sendo Senhor do céu e da terra, não habita em templos feitos com as mãos.
Mungu, aliyeumba ulimwengu na vyote vilivyomo, ni Bwana wa mbingu na nchi; yeye hakai katika hekalu zilizojengwa na watu.
25 Ele não é servido pelas mãos dos homens, como se precisasse de nada, vendo que ele mesmo dá a toda vida e fôlego e a todas as coisas.
Wala hatumikiwi kwa mikono ya watu kana kwamba anahitaji chochote kile, kwa maana yeye mwenyewe ndiye anayewapa watu uhai, anawawezesha kupumua na anawapa kila kitu.
26 Ele fez de um só sangue cada nação de homens para habitar em toda a superfície da terra, tendo determinado as estações e os limites de suas habitações,
Kutokana na mtu mmoja aliumba mataifa yote na kuyawezesha kuishi duniani kote. Aliamua na kupanga kabla kabisa lini na wapi mataifa hayo yangeishi.
27 para que buscassem o Senhor, se talvez pudessem alcançá-lo e encontrá-lo, embora ele não esteja longe de cada um de nós.
Alifanya hivyo, ili mataifa hayo yapate kumfuata, na kama vile kwa kupapasapapasa, yapate kumfikia. Hata hivyo lakini, Mungu hayuko mbali na kila mmoja wetu.
28 'Pois nele vivemos, nos movemos e temos nosso ser'. Como alguns de seus próprios poetas disseram: 'Pois somos também sua descendência'.
Kama alivyosema mtu mmoja: Ndani yake yeye sisi tunaishi, tunajimudu, na tuko! Ni kama washairi wenu wengine walivyosema: Sisi ni watoto wake.
29 Sendo então a progênie de Deus, não devemos pensar que a natureza divina é como o ouro, ou a prata, ou a pedra, gravada pela arte e pelo design do homem.
Ikiwa basi, sisi ni watoto wa Mungu, haifai kumfikiria Mungu kuwa kama dhahabu, fedha au hata jiwe lililochongwa na kutiwa nakshi na binadamu.
30 Os tempos da ignorância, portanto, Deus não se deu conta. Mas agora Ele ordena que todas as pessoas, em todos os lugares, se arrependam,
Mungu alifanya kama kwamba haoni nyakati zile watu walipokuwa wajinga. Lakini sasa, anaamuru watu wote kila mahali watubu.
31 porque Ele designou um dia em que julgará o mundo com justiça pelo homem que ordenou; do qual Ele deu garantias a todos os homens, na medida em que o ressuscitou dos mortos”.
Kwa maana amekwisha weka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki kwa njia ya mtu mmoja aliyemteua. Mungu amewathibitishia wote jambo hili kwa kumfufua mtu huyo kutoka wafu!”
32 Agora quando ouviram falar da ressurreição dos mortos, alguns escarneceram; mas outros disseram: “Queremos ouvi-los novamente a respeito disso”.
Walipomsikia Paulo anasema juu ya jambo la kufufuka kwa wafu, wengine wao waliangua kicheko; lakini wengine walisema, “Tunataka kukusikia tena juu ya jambo hili!”
33 Assim, Paul saiu de entre eles.
Hivyo, Paulo aliwaacha, akatoka barazani.
34 Mas alguns homens se uniram a ele e acreditaram, incluindo Dionísio, o Areopagita, e uma mulher chamada Damaris, e outros com eles.
Lakini watu kadhaa waliandamana naye, wakawa waumini. Miongoni mwao walikuwa Dionisio wa Areopago, mwanamke mmoja aitwaye Damari na wengineo.

< Atos 17 >