< 2 Samuel 22 >

1 David falou a Javé a letra desta canção no dia em que Javé o libertou da mão de todos os seus inimigos, e da mão de Saul,
Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
2 e ele disse: “Yahweh é minha rocha”, minha fortaleza, e meu entregador, até mesmo meu;
Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
3 Deus é meu rochedo em quem me refugio; meu escudo, e o corno de minha salvação, minha torre alta, e meu refúgio. Meu salvador, você me salva da violência.
Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
4 Eu chamo Javé, que é digno de ser elogiado; Assim serei salvo de meus inimigos.
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5 Pois as ondas de morte me cercaram. As enchentes de impiedade me fizeram temer.
“Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6 As cordas do Sheol estavam ao meu redor. As armadilhas da morte me pegaram. (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
7 Na minha angústia, invoquei Yahweh. Sim, eu chamei ao meu Deus. Ele ouviu minha voz fora de seu templo. Meu grito chegou aos seus ouvidos.
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
8 Então a terra tremeu e tremeu. As fundações do céu tremeram e foram abaladas, porque ele estava com raiva.
“Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
9 A fumaça subiu de suas narinas. O fogo consumidor saiu de sua boca. Os carvões foram acendidos por ela.
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
10 Ele também curvou os céus, e desceu. A escuridão espessa estava debaixo de seus pés.
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
11 Ele montou em um querubim e voou. Sim, ele foi visto nas asas do vento.
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
12 Ele fez da escuridão um abrigo ao seu redor, coleta de águas, e nuvens espessas dos céus.
Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
13 At a luminosidade diante dele, brasas de fogo foram acendidas.
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
14 Yahweh trovejou do céu. O Altíssimo proferiu sua voz.
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
15 Ele enviou flechas e as espalhou, relâmpagos e os confundiu.
Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
16 Então apareceram os canais do mar. Os alicerces do mundo foram lançados com a reprimenda de Yahweh, ao sopro do sopro de suas narinas.
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
17 Ele mandou do alto e me levou. Ele me tirou de muitas águas.
“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
18 Ele me libertou do meu forte inimigo, daqueles que me odiavam, pois eles eram poderosos demais para mim.
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
19 Eles vieram sobre mim no dia da minha calamidade, mas Yahweh foi meu apoio.
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
20 Ele também me trouxe para um lugar grande. Ele me entregou, porque se deleitou em mim.
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
21 Yahweh me recompensou de acordo com minha retidão. Ele me recompensou de acordo com a limpeza de minhas mãos.
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
22 Pois eu tenho mantido os caminhos de Javé, e não se afastaram maliciosamente do meu Deus.
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
23 Pois todas as suas portarias foram antes de mim. Quanto aos seus estatutos, eu não me afastei deles.
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
24 Eu também era perfeito em relação a ele. Eu me mantive longe de minha iniqüidade.
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
25 Portanto Yahweh me recompensou de acordo com minha retidão, De acordo com minha limpeza na visão dele.
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
26 Com a misericórdia, você se mostrará misericordioso. Com o homem perfeito, você se mostrará perfeito.
“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
27 Com o puro, você se mostrará puro. Com o torto, você se mostrará astuto.
kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
28 Você salvará as pessoas aflitas, mas seus olhos estão voltados para os arrogantes, para que você possa derrubá-los.
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
29 Pois você é minha lâmpada, Yahweh. Yahweh vai iluminar minha escuridão.
Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
30 Pois por você, eu corro contra uma tropa. Por meu Deus, eu pulo um muro.
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
31 Quanto a Deus, seu caminho é perfeito. A palavra de Yahweh é testada. Ele é um escudo para todos aqueles que se refugiam nele.
“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
32 Para quem é Deus, além de Yahweh? Quem é uma rocha, além de nosso Deus?
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
33 Deus é minha fortaleza forte. Ele faz meu caminho perfeito.
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
34 Ele faz seus pés como os pés de corça, e me coloca em meus lugares altos.
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
35 Ele ensina minhas mãos à guerra, para que meus braços dobrem um arco de bronze.
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
36 Você também me deu o escudo de sua salvação. Sua gentileza me fez grande.
Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
37 Você ampliou meus passos sob mim. Meus pés não escorregaram.
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
38 Eu persegui meus inimigos e os destruí. Eu não voltei atrás até que fossem consumidos.
“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
39 Eu os consumi, e os atingiu através deles, para que eles não possam surgir. Sim, eles caíram debaixo dos meus pés.
Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
40 Pois você me armou com força para a batalha. Vocês subjugaram debaixo de mim aqueles que se levantaram contra mim.
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
41 Você também fez meus inimigos virarem as costas para mim, que eu poderia cortar aqueles que me odeiam.
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
42 Eles procuraram, mas não havia ninguém para salvar; mesmo para Yahweh, mas ele não respondeu.
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
43 Then Eu os venci tão pequenos quanto o pó da terra. Eu os esmaguei como lama das ruas, e os espalhei para o exterior.
Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
44 Você também me libertou das lutas do meu povo. Vocês me mantiveram como o chefe das nações. Um povo que eu não conheço me servirá.
“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
45 Os estrangeiros se submeterão a mim. Assim que souberem de mim, eles me obedecerão.
nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
46 Os estrangeiros desaparecerão, e virão tremendo de seus lugares próximos.
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
47 Yahweh vive! Bendito seja o meu rochedo! Exaltado seja Deus, a rocha da minha salvação,
“Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
48 even o Deus que executa a vingança para mim, que faz as pessoas caírem sob mim,
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
49 que me afasta de meus inimigos. Sim, vocês me elevam acima daqueles que se levantam contra mim. Você me livra do homem violento.
aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
50 Portanto, eu lhe darei graças, Javé, entre as nações, e cantará louvores ao seu nome.
Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
51 Ele dá uma grande libertação a seu rei, e mostra bondade amorosa para com seu ungido, a David e à sua descendência, para sempre mais”.
Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”

< 2 Samuel 22 >