< 2 Samuel 2 >
1 Depois disso, David perguntou a Yahweh, dizendo: “Devo subir em alguma das cidades de Judá? Yahweh disse a ele: “Suba”. David disse: “Onde devo subir?”. Ele disse: “Para Hebron”.
Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
2 Então David foi para lá com suas duas esposas, Ahinoam, a Jezreelitess, e Abigail, a esposa de Nabal, a Carmelita.
Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
3 David educou seus homens que estavam com ele, cada homem com sua casa. Eles viviam nas cidades de Hebron.
Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
4 Os homens de Judá vieram, e ali ungiram Davi rei sobre a casa de Judá. Eles disseram a Davi: “Os homens de Jabesh Gilead foram os que enterraram Saul”.
Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
5 David enviou mensageiros aos homens de Jabesh Gilead, e disse-lhes: “Abençoados sois vós por Javé, que mostrastes esta bondade a vosso senhor, até mesmo a Saul, e o sepultastes”.
akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
6 Agora que Yahweh possa mostrar a você bondade e a verdade amorosa. Eu também te recompensarei por esta gentileza, porque fizeste isto.
Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
7 Agora, pois, que vossas mãos sejam fortes e valentes; pois Saul, vosso senhor, está morto, e também a casa de Judá me ungiram rei sobre eles”.
Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
8 Now Abner, filho de Ner, capitão do exército de Saul, havia levado Ishbosheth, o filho de Saul, e o trouxe para Mahanaim.
Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
9 Ele o fez rei sobre Gileade, sobre os ashuritas, sobre Jezreel, sobre Efraim, sobre Benjamim, e sobre todo Israel.
Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
10 Ishbosheth, filho de Saul, tinha quarenta anos de idade quando começou a reinar sobre Israel, e reinou dois anos. Mas a casa de Judá seguiu Davi.
Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
11 O tempo em que Davi foi rei em Hebron sobre a casa de Judá foi de sete anos e seis meses.
Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
12 Abner, filho de Ner, e os criados de Ishbosheth, filho de Saul, saíram de Mahanaim para Gibeon.
Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
13 Joab, filho de Zeruia, e os servos de Davi saíram ao encontro deles na piscina de Gibeon; e eles se sentaram, um de um lado da piscina e o outro do outro lado da piscina.
Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
14 Abner disse a Joab: “Por favor, deixe os jovens se levantarem e competirem diante de nós”. Joab disse: “Que se levantem!”
Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
15 Então eles se levantaram e passaram por cima por número: doze para Benjamim e para Ishbosheth, o filho de Saul, e doze dos servos de Davi.
Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
16 Cada um deles pegou seu adversário pela cabeça e empurrou sua espada para o lado de seu companheiro; assim, caíram juntos. Portanto, aquele lugar em Gibeon foi chamado Helkath Hazzurim.
Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
17 A batalha foi muito severa naquele dia; e Abner foi espancado, e os homens de Israel, diante dos servos de Davi.
Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
18 Os três filhos de Zeruia estavam lá: Joab, Abishai, e Asahel. Asahel era tão leve de pé como uma gazela selvagem.
Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
19 Asahel perseguiu Abner. Ele não virou para a mão direita nem para a esquerda por seguir Abner.
Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
20 Então Abner olhou atrás dele e disse: “É você, Asahel?” Ele respondeu: “E é”.
Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
21 Abner disse-lhe: “Vire-se para sua mão direita ou para sua esquerda e pegue um dos jovens, e pegue sua armadura”. Mas Asahel não se afastaria de segui-lo.
Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
22 Abner disse novamente a Asahel: “Vire-se para longe de me seguir. Por que eu deveria golpeá-lo até o chão? Como então eu poderia olhar Joab seu irmão na cara”?
Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
23 However, ele se recusou a se virar. Por isso Abner com a ponta traseira da lança o atingiu no corpo, de modo que a lança saiu atrás dele; e ele caiu lá embaixo e morreu no mesmo lugar. Todos os que chegaram ao lugar onde Asahel caiu e morreu ficaram parados.
Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
24 Mas Joab e Abishai perseguiram a Abner. O sol se pôs quando chegaram à colina de Ammah, que está diante de Giah pelo caminho do deserto de Gibeon.
Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
25 As crianças de Benjamin se reuniram depois de Abner e se tornaram uma banda, e ficaram no topo de uma colina.
Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
26 Então Abner chamou Joab, e disse: “Devorará a espada para sempre? Você não sabe que será amargura no último final? Quanto tempo vai demorar então, até que você peça ao povo que volte de seguir seus irmãos”?
Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
27 Joab disse: “Como Deus vive, se você não tivesse falado, certamente pela manhã o povo teria ido embora, e não cada um seguia seu irmão”.
Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
28 Então Joab tocou a trombeta; e todo o povo parou e não perseguiu mais Israel, e não lutou mais.
Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
29 Abner e seus homens passaram toda aquela noite pelo Arabah; e eles passaram pelo Jordão, e passaram por todo Bithron, e chegaram a Mahanaim.
Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
30 Joab voltou de seguir Abner; e quando reuniu todo o povo, dezenove homens de David e Asahel estavam desaparecidos.
Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
31 Mas os servos de David haviam atingido os homens de Benjamin Abner, de modo que trezentos e sessenta homens morreram.
Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
32 Eles pegaram Asahel e o enterraram no túmulo de seu pai, que estava em Belém. Joab e seus homens foram a noite toda, e o dia quebrou sobre eles em Hebron.
Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.