< 2 Samuel 15 >
1 Depois disso, Absalom preparou uma carruagem e cavalos para si mesmo, e cinqüenta homens para correr diante dele.
Baada ya muda, Absalomu akajipatia magari ya vita na farasi pamoja na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.
2 Absalom levantou-se cedo, e ficou ao lado do caminho do portão. Quando qualquer homem tinha um processo que deveria vir ao rei para julgamento, então Absalão chamou-o e disse: “De que cidade você é?”. Ele disse: “Seu servo é de uma das tribos de Israel”.
Akawa anaamka asubuhi na mapema na kusimama kando ya barabara inayoelekea kwenye lango la mji. Wakati wowote alipokuja mtu yeyote mwenye mashtaka yanayohitaji kuletwa mbele ya mfalme kwa maamuzi, Absalomu naye angemwita na kumuuliza, “Wewe unatoka mji upi?” Naye angejibu, “Mtumishi wako anatoka katika mojawapo ya makabila ya Israeli.”
3 Absalom disse a ele: “Eis que seus assuntos são bons e corretos; mas não há nenhum homem deputizado pelo rei para ouvi-lo”.
Kisha Absalomu angemwambia, “Tazama, malalamiko yako ni ya haki na sawasawa, lakini hakuna mwakilishi wa mfalme wa kukusikiliza.”
4 Absalom disse ainda: “Oh, que eu fui feito juiz na terra, que todo homem que tem algum processo ou causa pudesse vir a mim, e eu lhe faria justiça!”
Absalomu aliongeza, “Laiti tu ningeteuliwa kuwa mwamuzi katika nchi. Ndipo kila mmoja mwenye mashtaka au shauri angekuja kwangu nami ningeona kwamba anapata haki.”
5 Foi assim, que quando qualquer homem se aproximou para se curvar diante dele, ele estendeu sua mão, pegou-o e o beijou.
Pia, wakati mtu yeyote alipomkaribia ili kusujudu mbele yake, Absalomu alinyoosha mkono wake na kumshika pia kumbusu.
6 Absalão fez este tipo de coisa a todo Israel que veio ao rei para ser julgado. Então Absalão roubou os corações dos homens de Israel.
Absalomu akaendelea na tabia hii mbele ya Waisraeli wote waliomjia mfalme kumwomba awape haki; kwa hiyo Absalomu akaiba mioyo ya watu wa Israeli.
7 Ao final de quarenta anos, Absalom disse ao rei: “Por favor, deixe-me ir e pagar meu voto, que eu prometi a Javé, em Hebron.
Mnamo mwisho wa mwaka wa nne, Absalomu akamwambia mfalme, “Naomba unipe ruhusa niende Hebroni nikatimize nadhiri niliyomwekea Bwana.
8 Por seu servo fez um voto enquanto eu ficava em Geshur, na Síria, dizendo: “Se Javé me trouxer de fato a Jerusalém, então eu servirei a Javé”.
Wakati mtumishi wako alipokuwa huko Geshuri katika nchi ya Aramu, niliweka nadhiri hii, ‘Ikiwa Bwana atanirudisha Yerusalemu, nitamwabudu Bwana huko Hebroni.’”
9 O rei lhe disse: “Vá em paz”. Então, ele se levantou e foi para Hebron.
Mfalme akamwambia, “Enenda kwa amani.” Hivyo akaenda Hebroni.
10 Mas Absalom enviou espiões por todas as tribos de Israel, dizendo: “Assim que ouvirdes o som da trombeta, direis: 'Absalom é rei em Hebron!
Kisha Absalomu akatuma wajumbe kwa siri katika makabila yote ya Israeli, kusema, “Mara mtakaposikia sauti ya tarumbeta basi semeni, ‘Absalomu ni mfalme huko Hebroni.’”
11 Duzentos homens foram com Absalom para fora de Jerusalém, que foram convidados, e foram em sua simplicidade; e não sabiam de nada.
Watu mia mbili kutoka Yerusalemu walikuwa wamefuatana na Absalomu. Walikuwa wamealikwa kama wageni nao walikwenda kwa nia njema, pasipo kujua lolote.
12 Absalom mandou chamar Ahithophel, o Gilonita, conselheiro de David, de sua cidade, até mesmo de Giloh, enquanto ele estava oferecendo os sacrifícios. A conspiração era forte, pois o povo aumentava continuamente com Absalom.
Wakati Absalomu alipokuwa anatoa dhabihu, pia akatuma aitwe Ahithofeli, Mgiloni, mshauri wa Daudi, aje kutoka Gilo, ambao ndio mji wake wa nyumbani. Kwa hiyo mpango wa hila ukapata nguvu, na idadi ya waliofuatana na Absalomu ikaongezeka.
13 Um mensageiro veio a Davi, dizendo: “Os corações dos homens de Israel estão atrás de Absalom”.
Mjumbe akaja na kumwambia Daudi, “Mioyo ya watu wa Israeli inaambatana na Absalomu.”
14 David disse a todos os seus servos que estavam com ele em Jerusalém: “Levantai-vos! Vamos fugir, ou então nenhum de nós escapará de Absalão. Apresse-se para partir, para que ele não nos ultrapasse rapidamente e derrube o mal sobre nós, e atinja a cidade com o fio da espada”.
Ndipo Daudi akawaambia maafisa wake wote waliokuwa pamoja naye huko Yerusalemu, “Njooni! Ni lazima tukimbie, la sivyo hakuna hata mmoja wetu atakayeokoka kutoka mkononi mwa Absalomu. Ni lazima tuondoke kwa haraka, la sivyo atakuja mbio na kutupata, atatuangamiza na kuupiga mji kwa upanga.”
15 Os servos do rei disseram ao rei: “Eis que seus servos estão prontos para fazer o que meu senhor, o rei, escolher”.
Maafisa wa mfalme wakamjibu, “Watumishi wako tu tayari kufanya lolote mfalme bwana wetu analochagua.”
16 O rei saiu, e toda sua casa atrás dele. O rei deixou dez mulheres, que eram concubinas, para manter a casa.
Mfalme akatoka, pamoja na watu wa nyumbani mwake wakimfuata; lakini akawaacha masuria kumi ili kuangalia jumba la kifalme.
17 O rei saiu, e todas as pessoas atrás dele; e elas ficaram em Beth Merhak.
Hivyo mfalme akaondoka, pamoja na watu wote wakimfuata, wakatua mahali mbali kiasi.
18 Todos os seus servos passaram ao seu lado; e todos os queretitas, e todos os peletitas, e todos os gittitas, seiscentos homens que vieram depois dele de Gate, passaram diante do rei.
Watu wake wote wakatembea, wakampita wakiwa wamefuatana na Wakerethi na Wapelethi wote; pia Wagiti wote mia sita waliokuwa wamefuatana naye kutoka Gathi wakapita mbele ya mfalme.
19 Então o rei disse a Ittai, o Gittita: “Por que você também vai conosco? Volte e fique com o rei, pois você é um estrangeiro e também um exilado. Volte para o seu próprio lugar.
Mfalme akamwambia Itai, Mgiti, “Kwa nini ufuatane na sisi? Rudi ukakae pamoja na Mfalme Absalomu. Wewe ni mgeni, mkimbizi kutoka nchini mwako.
20 Whereas você veio mas ontem, devo hoje fazer você subir e descer conosco, já que vou onde posso? Volte, e leve seus irmãos de volta. Misericórdia e verdade estejam com você”.
Ulikuja jana tu. Nami leo nikufanye utangetange pamoja nasi, wakati sijui niendako? Rudi, nawe ukawachukue watu wa kwenu. Wema na uaminifu na viwe pamoja nawe.”
21 Ittai respondeu ao rei e disse: “Como Yahweh vive, e como meu senhor o rei vive, certamente em que lugar meu senhor o rei está, seja para a morte ou para a vida, seu servo também estará lá”.
Lakini Itai akamjibu mfalme, “Hakika kama Bwana aishivyo na kama mfalme bwana wangu aishivyo, popote mfalme bwana wangu atakapokuwa, ikiwa ni kuishi au kufa, hapo ndipo mtumishi wako atakapokuwa.”
22 David disse ao Ittai: “Vá e passe por cima”. Ittai o Gittita passou por cima, e todos os seus homens, e todos os pequenos que estavam com ele.
Daudi akamwambia Itai, “Songa mbele, endelea.” Kwa hiyo Itai, Mgiti, akaendelea pamoja na watu wake wote, pia jamaa zote waliokuwa pamoja naye.
23 Todo o país chorou com voz alta e todas as pessoas passaram para o outro lado. O próprio rei também passou sobre o riacho Kidron, e todo o povo passou em direção ao caminho do deserto.
Watu wote wa nje ya mji wakalia kwa sauti wakati watu wote walipokuwa wakipita. Mfalme naye akavuka Bonde la Kidroni, nao watu wote wakaelekea jangwani.
24 Eis que Zadoque também veio, e todos os levitas com ele, levando a arca da aliança de Deus; e puseram a arca de Deus; e Abiatar subiu até que todo o povo terminou de passar para fora da cidade.
Sadoki pia alikuwako, kadhalika Walawi wote waliokuwa pamoja naye walikuwa wamechukua Sanduku la Agano la Mungu. Wakaweka chini Sanduku la Mungu, naye Abiathari akatoa dhabihu mpaka watu wote walipokuwa wameondoka mjini.
25 O rei disse a Zadok: “Carreguem a arca de Deus de volta para a cidade. Se eu encontrar favor aos olhos de Iavé, Ele me trará novamente, e me mostrará tanto ela quanto sua habitação;
Kisha mfalme akamwambia Sadoki, “Rudisha Sanduku la Mungu mjini. Ikiwa nitapata kibali mbele za Bwana, atanirudisha, nami nitaliona Sanduku hili tena pamoja na Maskani yake.
26 mas se Ele disser, 'não tenho prazer em você', eis que aqui estou eu. Deixe-o fazer comigo o que lhe parece bom”.
Lakini kama yeye atasema, ‘Mimi sipendezwi nawe,’ basi mimi niko tayari; yeye na anifanye chochote aonacho chema kwake.”
27 O rei disse também ao sacerdote Zadok: “Você não é um vidente? Volte para a cidade em paz, e seus dois filhos com você, Ahimaaz seu filho e Jonathan o filho de Abiathar”.
Pia mfalme alimwambia kuhani Sadoki, “Je, wewe si mwonaji? Rudi mjini kwa amani pamoja na mwanao Ahimaasi na Yonathani mwana wa Abiathari. Wewe na Abiathari wachukueni wana wenu wawili.
28 Eis que eu ficarei nos vaus do deserto até que venha a notícia de você para me informar”.
Nitasubiri kwenye vivuko katika jangwa mpaka neno litakapotoka kwenu kuniarifu.”
29 Zadok, portanto, e Abiatar levaram a arca de Deus a Jerusalém novamente; e lá permaneceram.
Kwa hiyo Sadoki na Abiathari wakarudisha Sanduku la Mungu mpaka Yerusalemu na kukaa huko.
30 Davi subiu pela subida do Monte das Oliveiras, e chorou ao subir; e tinha a cabeça coberta e andava descalço. Todas as pessoas que estavam com ele cobriram sua cabeça, e subiram, chorando enquanto subiam.
Bali Daudi akaendelea, akapanda Mlima wa Mizeituni, akaenda huku analia, akiwa amefunika kichwa chake na bila viatu miguuni. Watu wote waliokuwa pamoja naye nao wakafunika vichwa vyao, wakawa wanapanda mlima huku wanalia.
31 Someone disse a David, dizendo: “Ahithophel está entre os conspiradores com Absalom”. David disse: “Yahweh, por favor, transforme o conselho de Ahithophel em tolice”.
Basi Daudi alikuwa ameambiwa, “Ahithofeli alikuwa miongoni mwa washiriki wa shauri baya la Absalomu.” Ndipo Daudi akaomba, akisema, “Ee Bwana, geuza shauri la Ahithofeli kuwa ujinga.”
32 Quando Davi chegou ao topo, onde Deus era adorado, eis que Hushai, o Arquiteto, veio ao seu encontro com sua túnica rasgada e terra sobre sua cabeça.
Daudi alipofika kwenye kilele cha mlima, mahali ambapo watu walikuwa wamezoea kumwabudu Mungu, Hushai, Mwariki, alikuwako huko kumlaki, joho lake likiwa limeraruka na mavumbi kichwani mwake.
33 David lhe disse: “Se você passar comigo, então será um fardo para mim;
Daudi akamwambia, “Kama ukienda pamoja nami, utakuwa mzigo kwangu.
34 mas se você voltar à cidade, e disser a Absalão: 'Eu serei seu servo, ó rei'. Como fui servo de seu pai no passado, então serei agora seu servo; então você derrotará para mim o conselho de Ahithophel”.
Lakini ikiwa utarudi mjini na kumwambia Absalomu, ‘Nitakuwa mtumishi wako, ee mfalme; nilikuwa mtumishi wa baba yako wakati uliopita, lakini sasa nitakuwa mtumishi wako,’ basi utaweza kunisaidia kwa kupinga shauri la Ahithofeli.
35 Você não tem Zadok e Abiathar, os sacerdotes, lá com você? Portanto, o que quer que você ouça fora da casa do rei, diga isso a Zadok e Abiathar, os sacerdotes.
Je, makuhani Sadoki na Abiathari hawatakuwa pamoja nawe? Waambie lolote utakalosikia katika jumba la mfalme.
36 Eis que eles têm lá com eles seus dois filhos, Ahimaaz, filho de Zadok, e Jonathan, filho de Abiathar. Enviai-me tudo o que ouvirdes por eles”.
Wana wao wawili, Ahimaasi mwana wa Sadoki na Yonathani mwana wa Abiathari, wako pamoja nao huko. Watume kwangu na lolote utakalosikia.”
37 Então Hushai, amigo de David, veio à cidade; e Absalom veio a Jerusalém.
Kwa hiyo Hushai, rafiki wa Daudi, akafika Yerusalemu wakati Absalomu alipokuwa anaingia mjini.