< 2 Reis 25 >

1 No nono ano de seu reinado, no décimo mês, no décimo dia do mês, veio Nabucodonosor, rei da Babilônia, ele e todo seu exército, contra Jerusalém, e se acamparam contra ela; e construíram fortes contra ela em torno dela.
Ilitokea kwamba katika mwaka wa tisa wa utawala wa mfalme Sedekia, katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya huo mwezi, Nebukadreza mfalme wa Babeli alikuja pamoja na jeshi lake lote kwa ajili ya kupigana dhidi ya Yerusalemu. Akaweka kambi kuelekeana nayo, na wakajenga ukuta kuizunguka.
2 Assim a cidade foi sitiada até o décimo primeiro ano do rei Zedequias.
Hivyo mji huo ulizungukwa mpaka miaka kumi na moja ya utawala wa Sedekia.
3 No nono dia do quarto mês, a fome era severa na cidade, de modo que não havia pão para o povo da terra.
Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa huo mwaka, njaa ilikuwa kali sana kwenye huo mji kwamba hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu wa nchi.
4 Então foi feita uma brecha na cidade, e todos os homens de guerra fugiram à noite pelo caminho do portão entre os dois muros, que ficava junto ao jardim do rei (agora os caldeus estavam contra a cidade ao redor); e o rei foi pelo caminho do Arabah.
Wakati huo ule mji ulikuwa umebomoka ndani, na wapiganaji wote wakakimbia usiku kwa njia ya lango kati ya kuta mbili, karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wote wameuzunguka mji. Mfalme akaenda kuelekea upande wa Araba.
5 Mas o exército caldeu perseguiu o rei e o alcançou nas planícies de Jericó; e todo o seu exército se dispersou dele.
Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuata mfalme Sedekia na kumchukua katika tambarare ya bonde la Mto Yoradani karibu na Yeriko. Jeshi lake lote lilitawanyika wakamwacha.
6 Então capturaram o rei e o levaram até o rei da Babilônia para Ribla; e o julgaram.
Wakamkamata mfalme na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, ambapo walipitisha hukumu juu yake.
7 Eles mataram os filhos de Zedequias diante de seus olhos, depois arrancaram os olhos de Zedequias, amarraram-no em grilhões e o levaram para Babilônia.
Kama kwa watoto wa Sedekia, wakawachinja mbele ya macho yake. Kisha akamtoa macho Sedekia, wakamfunga pingu, na kumpeleka hadi Babeli.
8 Agora no quinto mês, no sétimo dia do mês, que era o décimo nono ano do rei Nabucodonosor, rei da Babilônia, Nebuzaradan, o capitão da guarda, servo do rei da Babilônia, veio a Jerusalém.
Basi katika mwezi wa tano, katika siku ya saba ya mwezi, ambapo ulikuwa mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadreza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani, mtumishi wa mfalme wa Babeli na amrijeshi wa walinzi wake, wakaja hadi Yerusalemu.
9 Ele queimou a casa de Javé, a casa do rei, e todas as casas de Jerusalém. Ele queimou todas as grandes casas com fogo.
Akaichoma moto nyumba ya Yahwe, nyumba ya mfalme, na nyumba zote za Yeruselemu; pia kila jengo la muhimu katika mji akayachoma.
10 Todo o exército dos caldeus, que estava com o capitão da guarda, derrubou os muros ao redor de Jerusalém.
Kama kwa kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu, jeshi lote la Wababeli ambao walikuwa chini ya amrishi wa walinzi wakaziharibu.
11 Nebuzaradan o capitão da guarda levou cativo o resto do povo que ficou na cidade e aqueles que tinham desertado para o rei da Babilônia - todo o resto da multidão.
Basi watu waliokuwa wamebaki ambao walikuwa wameondoka katika mji, wale waliokuwa wameasi kwa mfalme wa Babeli, na mabaki ya watu-Nebuzadani, amiri jeshi wa mlinzi, wakachukuliwa kwenda utumwani.
12 Mas o capitão da guarda deixou alguns dos mais pobres da terra para trabalhar os vinhedos e os campos.
Lakini amiri jeshi wa mlinzi aliwaacha baadhi ya maskini wa nchi ili wafanye kazi kwenye shamba la mizabibu na kulima.
13 Os caldeus quebraram os pilares de bronze que estavam na casa de Yahweh e as bases e o mar de bronze que estavam na casa de Yahweh, e levaram as peças de bronze para a Babilônia.
Na zile nguzo za shaba ambazo zilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, na misimamio na bahari ya chuma ambayo ilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, Wakaldayo wakazivunja vipande vipande na kubeba shaba kuirudisha Babeli.
14 Eles tiraram as panelas, as pás, os rapé, as colheres e todos os vasos de bronze com os quais ministraram.
Masufuria, mabeleshi, makasi, vijiko, na vyombo vyote vya shaba ambavyo kuhani alivyokuwa amevitunza kwenye hekalu-Wakaldayo wakavichukua vyote.
15 O capitão da guarda tirou as panelas de fogo, as bacias, o que era de ouro, para o ouro, e o que era de prata, para a prata.
Masufuria ya kuhamisha majivu na mabakuli ambayo yalikuwa yametengenezwa kwa dhahabu, na yale yaliyotengenezwa kwa fedha-yule nahodha wa mlinzi wa mfalme akavichukua pia.
16 Os dois pilares, o único mar, e as bases, que Salomão havia feito para a casa de Yahweh, o bronze de todas estas embarcações não foi pesado.
Zile nguzo mbili, ile bahari, na vile vitako ambavyo Suleimani alivitengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yahwe shaba ya vyombo hivyo vyote haikuwa na uzani.
17 A altura de um pilar era de dezoito côvados, e sobre ele havia um capital de bronze. A altura do capital era de três côvados, com rede e romãs na capital ao redor, tudo de bronze; e o segundo pilar com sua rede era como estes.
Urefu wa ile nguzo ya kwanza ulikuwa ridhaa kumi na nane, na kichwa cha shaba kilikuwa juu yake. Na urefu wa kichwa ulikuwa ridhaa tatu, pamoja na mapambo ya wavu na makomamanga yote yakizunguka kwenye hicho kichwa, vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa shaba. Na ile nguzo nyingine ilikuwa vivyo hivyo kama ile ya kwanza pamoja na wavu wake.
18 O capitão da guarda levou Seraías, o sacerdote chefe, Sofonias, o segundo sacerdote, e os três guardas do umbral;
Yule amiri jeshi wa mlinzi akamchukua Seraya kuhani mkuu, pamoja za Sefania, yule kuhani wa pili, na walinzi watatu wa kwenye lango.
19 e da cidade ele levou um oficial que foi colocado sobre os homens de guerra; e cinco homens daqueles que viram o rosto do rei, que foram encontrados na cidade; e o escriba, o capitão do exército, que reuniu o povo da terra, e sessenta homens do povo da terra, que foram encontrados na cidade.
Kutoka mjini akamchukua mlinzi, afisa mmoja ambaye aliyekuwa msimamizi wa maaskari, na watu watano ambao walikuwa wakimshauri mfalme, ambao walikuwa bado katika mji. Pia alimchukua mfungwa wa afisa jeshi la mfalme, kwa ajili ya kuandika watu kwenye jeshi, pamoja na watu sitini muhimu kutoka hiyo nchi ambao walikuwa katika mji.
20 Nebuzaradan o capitão da guarda os levou e os trouxe ao rei da Babilônia para Riblah.
Kisha Nebuzaradani, amiri wa mlinzi, akawachukua na kuwapeleka kwa mfalme Babeli huko Ribla.
21 O rei da Babilônia os atacou e os matou em Riblah, na terra de Hamath. Então Judá foi levado cativo para fora de sua terra.
Mfalme wa Babeli akawaua huko Ribla katika nchi ya Hamathi. Kwa njia hii, Yuda akaiacha nchi yake kwenda utumwani.
22 Quanto ao povo que ficou na terra de Judá, que Nabucodonosor, rei da Babilônia, havia deixado, até mesmo sobre eles fez de Gedalias o filho de Ahikam, o filho de Shaphan, governador.
Na wale watu waliokuwa wamebakia katika nchi ya Yuda, wale ambao Nebukadreza mfalme wa Babeli aliwaacha, akamuweka Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, msimamizi wao.
23 Agora quando todos os capitães das forças, eles e seus homens, ouviram que o rei da Babilônia havia feito Gedalias governador, vieram a Gedalias para Mizpá, até mesmo Ismael, filho de Netanias, Johananan, filho de Kareah, Seraías, filho de Tanhumeth, o netofatita, e Jaazanias, filho do maacatita, eles e seus homens.
Kisha wakati maamiri wote wa majeshi, wao na watu wao, waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemfanya Gedalia kuwa liwali, wakaenda kwa Gedalia huko Mispa. Hawa watu walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofa, na Yezania mwana wa Mmaaka-wao na watu wao.
24 Gedaliah jurou a eles e a seus homens, e lhes disse: “Não tenham medo por causa dos servos dos caldeus. Habitem na terra e sirvam o rei da Babilônia, e estará bem com vocês”.
Gedalia akafanya kiapo kwa watu wake na kuwaambia, “Msiwaogope Wakaldayo. Muishi katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vema kwenu.”
25 Mas no sétimo mês, veio Ismael, filho de Nethaniah, filho de Elishama, da descendência real, e dez homens com ele, e atingiu Gedaliah para que ele morresse, com os judeus e os caldeus que estavam com ele em Mizpah.
Lakini ilitokea kwamba katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, kutoka familia ya kifalme, wakaja na watu kumi na kumshambulia Gedalia. Gedalia akafa, pamoja na watu wa Yuda na Wababeli ambao walikuwa pamoja nae huko Mizpa.
26 Todo o povo, tanto pequeno quanto grande, e os capitães das forças se levantaram e vieram ao Egito; pois tinham medo dos caldeus.
Kisha wale watu wote, kutoka chini kwenda juu, na maamiri wa jeshi, wakainuka na kwenda Misri, kwasababu walikuwa wanawaogopa Wababeli.
27 No trigésimo sétimo ano do cativeiro de Joaquim, rei de Judá, no décimo segundo mês, no vigésimo sétimo dia do mês, Evilmerodach, rei da Babilônia, no ano em que começou a reinar, libertou Joaquim, rei de Judá, da prisão,
Ilitokea baadaye katika mwaka wa thelathini na saba wa utumwa wa Yekonia mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya ishirini na saba ya mwezi, Evil-merodaki mfalme wa Babeli akamtoa Yekonia mfalme wa Yuda kutoka gerezani. Hii ilitokea katika mwaka ambao Evil-Merodaki alipoanza kutawala.
28 e falou gentilmente com ele e colocou seu trono acima do trono dos reis que estavam com ele na Babilônia,
Akaongea naye kwa ukarimu na kumpatia kiti kizuri zaidi kuliko kile cha wafalme wengine ambao walikuwa pamoja naye Babeli.
29 e mudou suas vestes de prisão. Jehoiachin comeu pão diante dele continuamente todos os dias de sua vida;
Evil-Merodaki akamvua Yekonia nguo za gerezani,
30 e para sua mesada, houve uma mesada contínua dada pelo rei, todos os dias uma porção, todos os dias de sua vida.
na Yekinia akala siku zote kwenye meza ya mfalme katika maisha yake yote yaliyokuwa yamebakia.

< 2 Reis 25 >