< 1 Pedro 2 >
1 Afastando, portanto, toda maldade, todo engano, hipocrisia, inveja e todo mal falado,
Basi, acheni uovu wote; uongo, unafiki, wivu na maneno ya kashfa visiweko tena.
2 como bebês recém-nascidos, ansiosos pelo puro leite espiritual, para que com ele vocês possam crescer,
Kama vile watoto wachanga wanavyotamani maziwa, nanyi pia mnapaswa kuwa na hamu ya maziwa halisi ya kiroho, ili kwa nguvu yake mpate kukua na kukombolewa.
3 se de fato provaram que o Senhor é gracioso.
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mmegundua kwamba Bwana ni mwema.”
4 venha a ele, uma pedra viva, rejeitada de fato pelos homens, mas escolhida por Deus, preciosa.
Basi, mwendeeni Bwana! Yeye ndiye jiwe hai lililokataliwa na watu; lakini mbele ya Mungu ni jiwe teule, na la thamani kubwa.
5 Você também como pedra viva é construída como uma casa espiritual, para ser um sacerdócio santo, para oferecer sacrifícios espirituais, aceitáveis a Deus através de Jesus Cristo.
Mwendeeni yeye kama mawe hai mkajengeke na kuwa nyumba ya kiroho, ambamo mtatumikia kama makuhani watakatifu, kutolea dhabihu za kiroho zenye kumpendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.
6 Porque está contida na Escritura, “Eis que deposito em Sião uma pedra angular principal, escolhida e preciosa”. Aquele que acredita nele não ficará desapontado”.
Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Tazama! Naweka huko sioni jiwe kuu la msingi, jiwe la thamani kubwa nililoliteua. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa.”
7 Para você que acredita, portanto, ser a honra, mas para aqueles que são desobedientes, “A pedra que os construtores rejeitaram tornou-se a principal pedra angular”.
Kwenu ninyi mnaoamini, jiwe hilo ni la thamani kubwa; lakini kwa wale wasioamini, “Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi.”
8 e, “uma pedra de tropeço e uma rocha de ofensa”. Pois eles tropeçam na palavra, sendo desobedientes, para o que também foram nomeados.
Tena Maandiko yasema: “Jiwe hilo ni jiwe la kujikwaa, mwamba wa kuwaangusha watu.” Watu hujikwaa kwa sababu hawauamini ule ujumbe; na ndivyo walivyopangiwa tangu mwanzo.
9 Mas vocês são uma raça escolhida, um sacerdócio real, uma nação santa, um povo de posse de Deus, para que proclamem a excelência d'Aquele que os chamou das trevas para sua maravilhosa luz.
Lakini ninyi ni ukoo mteule, makuhani wa Mfalme, taifa takatifu; watu wake Mungu mwenyewe, mlioteuliwa kutangaza matendo makuu ya Mungu aliyewaiteni kutoka gizani akawaingizeni katika mwanga wake mkuu.
10 No passado, você não era um povo, mas agora é o povo de Deus, que não tinha obtido misericórdia, mas agora obteve misericórdia.
Wakati mmoja ninyi hamkuwa watu wa Mungu, lakini sasa ninyi ni watu wake; wakati mmoja hamkupewa huruma ya Mungu, lakini sasa mmeipokea.
11 Amados, suplico-vos, como estrangeiros e peregrinos, que vos abstenhais das luxúrias carnais que guerreiam contra a alma,
Wapenzi wangu, nawasihi ninyi kama wageni na wakimbizi hapa duniani! Achaneni na tamaa za mwili ambazo hupingana na roho.
12 tendo bom comportamento entre as nações, para que, naquilo de que falam contra vós como malfeitores, possam ver vossas boas obras e glorificar a Deus no dia da visitação.
Mwenendo wenu kati ya watu wasiomjua Mungu unapaswa kuwa mwema kabisa, ili hata watakapowasingizieni kwamba mnatenda mabaya, waweze kutambua matendo yenu mema na hivyo wamtukuze Mungu Siku ya kuja kwake.
13 Portanto, sujeitai-vos a toda ordenança do homem por amor do Senhor: seja ao rei, como supremo,
Basi, jiwekeni chini ya mamlaka yote ya kibinadamu, kwa ajili ya Bwana: utii kwa mfalme aliye mtawala mkuu,
14 ou aos governadores, como por ele enviados para vingança dos malfeitores e para louvor aos que fazem o bem.
utii kwa wakuu wa mikoa ambao wameteuliwa naye kuwaadhibu wahalifu na kuwasifu watendao mema.
15 Pois esta é a vontade de Deus, que, fazendo o bem, se cale a ignorância dos homens tolos.
Maana Mungu anataka mweze kuyakomesha maneno ya kijinga ya watu wasio na akili kwa matendo mema mnayofanya.
16 Vivam como pessoas livres, mas não usando sua liberdade para um manto de maldade, mas como servos de Deus.
Ishini kama watu huru; lakini msiutumie uhuru wenu kuuficha ubaya, bali ishini kama watumishi wa Mungu.
17 Honrar a todos os homens. Amar a irmandade. Temam a Deus. Honrar o rei.
Waheshimuni watu wote, wapendeni ndugu zenu waumini, mcheni Mungu, mheshimuni mfalme.
18 Servants, esteja sujeito a seus senhores com todo respeito, não só aos bons e gentis, mas também aos ímpios.
Enyi watumishi wa nyumbani, watiini wakuu wenu kwa heshima yote, wawe wema na wapole au wenye kuchukiza.
19 Pois é louvável se alguém suporta a dor, sofrendo injustamente, por causa da consciência para com Deus.
Maana kama mnavumilia maumivu ya mateso msiyostahili kwa sababu mwajua kwamba Mungu anataka hivyo, basi Mungu atawafadhili.
20 Pois que glória é essa se, quando se peca, pacientemente se suporta a surra? Mas se, quando você se sai bem, você pacientemente suporta o sofrimento, isto é louvável para Deus.
Maana, mtapata tuzo gani mkivumilia mapigo mnayostahili kwa sababu ya makosa yenu? Lakini kama mnavumilia mateso hata ingawa mmetenda mema, Mungu atawapeni baraka kwa ajili hiyo.
21 Pois você foi chamado a isto, porque Cristo também sofreu por nós, deixando-lhe um exemplo, para que você siga seus passos,
Hayo ndiyo mliyoitiwa; maana Kristo mwenyewe aliteseka kwa ajili yenu, akawaachieni mfano, ili muufuate mwenendo wake.
22 que não pecou, “nem se encontrou engano em sua boca”.
Yeye hakutenda dhambi, wala neno la udanganyifu halikusikika mdomoni mwake.
23 Quando ele foi amaldiçoado, ele não amaldiçoou de volta. Quando sofreu, ele não ameaçou, mas se comprometeu com aquele que julga com justiça.
Alipotukanwa yeye hakujibu kwa tukano; alipoteseka yeye hakutoa vitisho, bali aliyaweka matumaini yake kwa Mungu, hakimu mwenye haki.
24 Ele mesmo carregou nossos pecados em seu corpo sobre a árvore, para que nós, tendo morrido para os pecados, pudéssemos viver para a justiça. Foi curado por suas feridas.
Yeye mwenyewe alizibeba dhambi zetu katika mwili wake juu ya msalaba, tupate kufa kuhusu dhambi, na kuishi kwa ajili ya uadilifu. Kwa majeraha yake, ninyi mmeponywa.
25 Pois vocês se extraviaram como ovelhas; mas agora voltaram para o Pastor e Supervisor de suas almas.
Ninyi mlikuwa kama kondoo waliokuwa wamepotea; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mlinzi wa roho zenu.