< 1 Reis 15 >

1 Now no décimo oitavo ano do rei Jeroboão, filho de Nebat, Abijam começou a reinar sobre Judá.
Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
2 Ele reinou três anos em Jerusalém. O nome de sua mãe era Maacah, filha de Abishalom.
naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
3 Ele caminhou em todos os pecados de seu pai, o que havia feito antes dele; e seu coração não era perfeito com Javé, seu Deus, como o coração de Davi, seu pai.
Alitenda dhambi zote baba yake alizotenda kabla yake; moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake ulivyokuwa.
4 Entretanto, por amor a Davi, Javé, seu Deus, deu-lhe uma lâmpada em Jerusalém, para fundar seu filho depois dele e estabelecer Jerusalém;
Pamoja na hayo, kwa ajili ya Daudi, Bwana Mungu wake akampa taa katika Yerusalemu kwa kumwinua mwana atawale badala yake na kwa kuifanya Yerusalemu kuwa imara.
5 porque Davi fez o que era certo aos olhos de Javé, e não se afastou de nada do que lhe ordenou todos os dias de sua vida, exceto somente no caso de Urias, o hitita.
Kwa kuwa Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana na hakushindwa kushika maagizo yote ya Bwana siku zote za uhai wake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
6 Agora havia guerra entre Rehoboam e Jeroboão todos os dias de sua vida.
Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote wa maisha ya Abiya.
7 O resto dos atos de Abijam, e tudo o que ele fez, não estão escritos no livro das crônicas dos reis de Judá? Houve uma guerra entre Abijam e Jeroboão.
Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Abiya na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
8 Abijam dormiu com seus pais, e eles o enterraram na cidade de David; e Asa seu filho reinou em seu lugar.
Naye Abiya akalala na baba zake akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake.
9 No vigésimo ano de Jeroboão, rei de Israel, Asa começou a reinar sobre Judá.
Katika mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akawa mfalme wa Yuda,
10 Ele reinou quarenta e um anos em Jerusalém. O nome de sua mãe era Maaca, filha de Abishalom.
naye akatawala katika Yerusalemu miaka arobaini na mmoja. Bibi yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
11 Asa fez o que era certo aos olhos de Iavé, como fez Davi, seu pai.
Asa akatenda yaliyo mema machoni mwa Bwana, kama alivyokuwa ametenda Daudi baba yake.
12 Ele expulsou os sodomitas da terra e removeu todos os ídolos que seus pais haviam feito.
Akawafukuza mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu kutoka nchi na kuondoa sanamu zote ambazo baba zake walikuwa wametengeneza.
13 Ele também removeu Maacah sua mãe de ser rainha, porque ela tinha feito uma imagem abominável para uma Asherah. Asa cortou sua imagem e a queimou no riacho Kidron.
Hata akamwondoa bibi yake Maaka kwenye wadhifa wake kama mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
14 Mas os lugares altos não foram tirados. No entanto, o coração de Asa foi perfeito com Yahweh durante todos os seus dias.
Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
15 Ele trouxe para a casa de Yahweh as coisas que seu pai havia dedicado, e as coisas que ele mesmo havia dedicado: prata, ouro e utensílios.
Akaleta ndani ya Hekalu la Bwana fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
16 Houve guerra entre Asa e Baasha, rei de Israel, durante todos os seus dias.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zote za utawala wao.
17 Baasa, rei de Israel, subiu contra Judá, e construiu Ramá, para não permitir que ninguém saísse ou entrasse para Asa, rei de Judá.
Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
18 Então Asa pegou toda a prata e o ouro que ficou nos tesouros da casa de Iavé, e os tesouros da casa do rei, e os entregou na mão de seus servos. Então o rei Asa os enviou a Ben Hadad, filho de Tabrimmon, filho de Hezion, rei da Síria, que vivia em Damasco, dizendo:
Kisha Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imeachwa katika hazina za Hekalu la Bwana na za jumba lake mwenyewe la kifalme. Akawakabidhi maafisa wake na kuwatuma kwa Ben-Hadadi mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Aramu, aliyekuwa akitawala Dameski.
19 “Que haja um tratado entre mim e você, assim entre meu pai e seu pai”. Eis que enviei a você um presente de prata e ouro. Ide, rompei vosso tratado com Baasa, rei de Israel, para que ele se afaste de mim”.
“Akasema na pawepo mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi ya fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
20 Ben Hadad ouviu o rei Asa, e enviou os capitães de seus exércitos contra as cidades de Israel, e atingiu Ijon, e Dan, e Abel Beth Maacah, e todo o Chinneroth, com todas as terras de Naftali.
Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Akaishinda miji ya Iyoni, Dani, Abel-Beth-Maaka na Kinerethi yote, pamoja na Naftali.
21 Quando Baasha soube disso, ele parou de construir Ramah, e viveu em Tirzah.
Wakati Baasha aliposikia hili, akaacha kuijenga Rama na akaenda kuishi Tirsa.
22 Então o rei Asa fez uma proclamação a todo Judá. Ninguém estava isento. Eles carregaram as pedras de Ramah, e sua madeira, com a qual Baasha tinha construído; e o rei Asa usou-a para construir Geba de Benjamin, e Mizpah.
Kisha Mfalme Asa akatoa amri kwa Yuda yote, pasipo kumbagua hata mmoja, kubeba mawe na mbao kutoka Rama, ambazo Baasha alikuwa akitumia huko. Mfalme Asa akazitumia kujengea Geba iliyoko Benyamini na Mispa pia.
23 Agora o resto de todos os atos de Asa, e todas as suas forças, e tudo o que ele fez, e as cidades que ele construiu, não estão escritos no livro das crônicas dos reis de Judá? Mas na época de sua velhice ele estava doente em seus pés.
Kwa matukio yote ya utawala wa Asa, mafanikio yake yote, yote aliyofanya na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Katika uzee wake, hata hivyo, alipata ugonjwa wa miguu.
24 Asa dormiu com seus pais, e foi enterrado com seus pais na cidade de seu pai David; e Jehoshaphat seu filho reinou em seu lugar.
Kisha Asa akalala pamoja na baba zake na kuzikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Naye Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Nadab, filho de Jeroboão, começou a reinar sobre Israel no segundo ano de Asa, rei de Judá; e reinou sobre Israel dois anos.
Nadabu mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Asa wa Yuda, naye akatawala Israeli kwa miaka miwili.
26 Ele fez o que era mau aos olhos de Iavé, e caminhou no caminho de seu pai, e em seu pecado com o qual ele fez Israel pecar.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za baba yake na katika dhambi yake, ambayo alisababisha Israeli kuifanya.
27 Baasa, filho de Ahijah, da casa de Issachar, conspirou contra ele; e Baasa golpeou-o em Gibeton, que pertencia aos filisteus; pois Nadabe e todo Israel estavam sitiando Gibeton.
Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya shauri baya dhidi yake, naye akamuua huko Gibethoni, mji wa Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli yote walipokuwa wameuzingira.
28 Even no terceiro ano de Asa, rei de Judá, Baasa o matou e reinou em seu lugar.
Baasha akamuua Nadabu katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, naye Baasha akaingia mahali pake kuwa mfalme.
29 Assim que ele foi rei, ele atingiu toda a casa de Jeroboão. Ele não deixou para Jeroboão ninguém que respirasse, até que o tivesse destruído, segundo o ditado de Javé, que ele falou por seu servo Ahijah, o silonita;
Mara tu alipoanza kutawala, aliua jamaa yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu yeyote aliyekuwa hai, bali aliwaangamiza wote, kulingana na neno la Bwana lililotolewa kupitia kwa mtumishi wake Ahiya Mshiloni,
30 pelos pecados de Jeroboão que ele pecou, e com os quais ele fez Israel pecar, por causa de sua provocação com a qual ele provocou Javé, o Deus de Israel, à ira.
kwa sababu ya dhambi alizokuwa amezitenda Yeroboamu na kusababisha Israeli kuzitenda, tena kwa sababu alimkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli.
31 Agora o resto dos atos de Nadab, e tudo o que ele fez, não estão escritos no livro das crônicas dos reis de Israel?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Nadabu na yote aliyofanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
32 Houve guerra entre Asa e Baasa, rei de Israel, durante todos os seus dias.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli wakati wote wa utawala wao.
33 No terceiro ano de Asa, rei de Judá, Baasa, filho de Ahijah, começou a reinar sobre todo Israel em Tirzah durante vinte e quatro anos.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme wa Israeli yote huko Tirsa, naye akatawala kwa miaka ishirini na minne.
34 Ele fez o que era mau aos olhos de Javé, e caminhou no caminho de Jeroboão, e em seu pecado com o qual ele fez Israel pecar.
Akatenda maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za Yeroboamu na dhambi yake, ambayo alikuwa amesababisha Israeli kuitenda.

< 1 Reis 15 >