< 1 Reis 12 >

1 Rehoboam foi a Shechem, pois todo Israel tinha vindo a Shechem para torná-lo rei.
Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
2 Quando Jeroboão, filho de Nebat, soube disso (pois ele ainda estava no Egito, onde havia fugido da presença do rei Salomão, e Jeroboão vivia no Egito;
Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
3 e eles o enviaram e o chamaram), Jeroboão e toda a assembléia de Israel vieram, e falaram com Roboão, dizendo:
Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
4 “Seu pai dificultou nosso jugo. Agora, portanto, torne o duro serviço de seu pai, e seu pesado jugo que ele nos colocou, mais leve, e nós o serviremos”.
“Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
5 Ele disse a eles: “Parta por três dias, depois volte para mim”. Assim, o povo partiu.
Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
6 O rei Rehoboam aconselhou-se com os anciãos que tinham estado perante Salomão, seu pai, enquanto ele ainda vivia, dizendo: “Que conselho você me dá para responder a essas pessoas?
Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
7 Eles responderam: “Se você for um servo deste povo hoje, e os servir, e lhes responder com boas palavras, então eles serão seus servos para sempre”.
Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
8 Mas ele abandonou o conselho dos velhos que lhe haviam dado, e se aconselhou com os jovens que haviam crescido com ele, que estavam diante dele.
Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
9 Ele lhes disse: “Que conselho vocês dão, para que possamos responder a essas pessoas que falaram comigo, dizendo: 'Faça o jugo que seu pai nos pôs mais leve'”.
Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
10 Os jovens que tinham crescido com ele lhe disseram: “Diga a essas pessoas que falaram com você, dizendo: 'Seu pai tornou nosso jugo pesado, mas torne-o mais leve para nós' - diga-lhes: 'Meu dedo mindinho é mais grosso que a cintura do meu pai'.
Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
11 Agora meu pai o sobrecarregou com um jugo pesado, mas eu o acrescentarei ao seu jugo. Meu pai te castigou com chicotes, mas eu te castigarei com escorpiões””.
Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.’”
12 Então Jeroboão e todo o povo vieram a Rehoboam no terceiro dia, como pediu o rei, dizendo: “Venha até mim novamente no terceiro dia”.
Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
13 O rei respondeu ao povo grosso modo, e abandonou o conselho dos anciãos que lhe haviam dado,
Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
14 e falou-lhes de acordo com o conselho dos jovens, dizendo: “Meu pai fez pesado o seu jugo, mas eu acrescentarei ao seu jugo”. Meu pai te castigou com chicotes, mas eu te castigarei com escorpiões”.
akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
15 Então o rei não deu ouvidos ao povo; pois foi uma coisa trazida por Javé, para que ele pudesse estabelecer sua palavra, que Javé falou por Ahijah, o xilonita, a Jeroboão, filho de Nebat.
Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Bwana, ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
16 Quando todo Israel viu que o rei não os ouvia, o povo respondeu ao rei, dizendo: “Que porção temos nós em Davi? Não temos uma herança no filho de Jessé. Às suas tendas, Israel! Agora cuide da sua própria casa, David”. Então Israel partiu para as suas tendas.
Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli! Angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
17 Mas quanto às crianças de Israel que viviam nas cidades de Judá, Rehoboam reinava sobre elas.
Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
18 Então o rei Roboão enviou Adoram, que estava sobre os homens sujeitos a trabalhos forçados; e todo Israel o apedrejou até a morte com pedras. O rei Roboão apressou-se a subir para sua carruagem, para fugir para Jerusalém.
Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
19 Então Israel se rebelou contra a casa de Davi até os dias de hoje.
Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.
20 Quando todo Israel ouviu que Jeroboão havia voltado, eles o enviaram e o chamaram para a congregação, e o fizeram rei sobre todo Israel. Não houve ninguém que seguisse a casa de Davi, exceto apenas a tribo de Judá.
Waisraeli wote waliposikia kwamba Yeroboamu amerudi, wakatuma watu na kumwita kwenye kusanyiko na kumfanya mfalme juu ya Israeli yote. Ni kabila la Yuda peke yake lililobaki kuwa tiifu kwa nyumba ya Daudi.
21 Quando Roboão chegou a Jerusalém, ele reuniu toda a casa de Judá e a tribo de Benjamim, cento e oitenta mil homens escolhidos que eram guerreiros, para lutar contra a casa de Israel, para trazer novamente o reino a Roboão, filho de Salomão.
Ikawa Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini, wanaume wapiganaji 180,000, kufanya vita dhidi ya nyumba ya Israeli na kuurudisha tena ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Solomoni.
22 Mas a palavra de Deus veio a Semaías, o homem de Deus, dizendo:
Lakini neno hili la Mungu likamjia Shemaya mtu wa Mungu:
23 “Fala a Roboão, filho de Salomão, rei de Judá, e a toda a casa de Judá e Benjamim, e ao resto do povo, dizendo:
“Mwambie Rehoboamu mwana wa Solomoni mfalme wa Yuda, na nyumba yote ya Yuda na Benyamini, na watu wengine wote,
24 'Yahweh diz: “Não subirá nem lutará contra seus irmãos, os filhos de Israel. Todos retornarão à sua casa; pois isto é de mim””. Então eles ouviram a palavra de Javé, voltaram e seguiram seu caminho, de acordo com a palavra de Javé.
‘Hili ndilo asemalo Bwana: Msipande kupigana dhidi ya ndugu zenu, Waisraeli. Nendeni nyumbani, kila mmoja wenu, kwa kuwa hili nimelitenda mimi.’” Kwa hiyo wakalitii neno la Bwana na kurudi nyumbani, kama Bwana alivyokuwa ameagiza.
25 Então Jeroboam construiu Shechem na região montanhosa de Ephraim, e viveu nela; e de lá saiu e construiu Penuel.
Kisha Yeroboamu akajenga Shekemu akaizungushia ngome katika nchi ya vilima ya Efraimu na akaishi huko. Akatoka huko, akaenda akajenga Penueli.
26 Jeroboão disse em seu coração: “Agora o reino voltará à casa de Davi”.
Yeroboamu akawaza moyoni mwake, “Sasa inawezekana ufalme ukarudi katika nyumba ya Daudi.
27 Se este povo subir para oferecer sacrifícios na casa de Iavé em Jerusalém, então o coração deste povo voltará novamente para seu senhor, até mesmo para Roboão rei de Judá; e me matarão, e voltarão para Roboão rei de Judá”.
Kama watu hawa watapanda kwenda kutoa dhabihu katika Hekalu la Bwana huko Yerusalemu, mioyo yao itamrudia bwana wao, Rehoboamu mfalme wa Yuda. Wataniua mimi na kurudi kwa Mfalme Rehoboamu.”
28 Então o rei tomou conselho, e fez dois bezerros de ouro; e disse-lhes: “É demais para vocês subirem a Jerusalém. Olhai e vede vossos deuses, Israel, que vos fizeram subir da terra do Egito”!
Baada ya kutafuta shauri, mfalme akatengeneza ndama wawili wa dhahabu. Akawaambia watu, “Ni gharama kubwa kwenu kukwea kwenda Yerusalemu. Hii hapa miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
29 Ele pôs um em Betel, e o outro em Dan.
Ndama mmoja akamweka Betheli na mwingine Dani.
30 Esta coisa se tornou um pecado, pois o povo chegou até Dan para adorar antes daquele que lá estava.
Nalo jambo hili likawa dhambi, watu wakawa wanaenda hadi Dani kumwabudu huyo aliyewekwa huko.
31 Ele fez casas de lugares altos, e fez sacerdotes entre todo o povo, que não eram dos filhos de Levi.
Yeroboamu akajenga madhabahu mahali pa juu pa kuabudia miungu na kuwateua makuhani kutoka watu wa aina zote, ijapokuwa hawakuwa Walawi.
32 Jeroboão ordenou uma festa no oitavo mês, no décimo quinto dia do mês, como a festa que está em Judá, e subiu ao altar. Ele o fez em Betel, sacrificando-se aos bezerros que havia feito, e colocou em Betel os sacerdotes dos lugares altos que havia feito.
Pia Yeroboamu akaweka sikukuu katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, kama sikukuu iliyokuwa ikifanyika huko Yuda, na akatoa dhabihu juu ya madhabahu. Akafanya hivyo huko Betheli akitoa dhabihu kwa ndama alizotengeneza. Huko Betheli akawaweka makuhani, na pia katika sehemu za juu za kuabudia miungu alizozitengeneza.
33 Ele subiu ao altar que havia feito em Betel no décimo quinto dia do oitavo mês, mesmo no mês que ele havia planejado de seu próprio coração; e ordenou uma festa para os filhos de Israel, e subiu ao altar para queimar incenso.
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouchagua mwenyewe, alitoa dhabihu juu ya madhabahu aliyokuwa amejenga huko Betheli. Kwa hiyo akaweka sikukuu kwa ajili ya Waisraeli na akapanda madhabahuni kutoa sadaka.

< 1 Reis 12 >