< 1 Crônicas 26 >
1 Para as divisões dos porteiros: dos coraítas, Meselemias o filho de Kore, dos filhos de Asafe.
Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
2 Meselemias teve filhos: Zacarias o primogênito, Jediael o segundo, Zebadiah o terceiro, Jathniel o quarto,
Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
3 Elam o quinto, Jehohanan o sexto, e Eliehoenai o sétimo.
Elamu wa tano Yehohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
4 Obed-Edom teve filhos: Semaías o primogênito, Jehozabad o segundo, Joah o terceiro, Sacar o quarto, Nethanel o quinto,
Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
5 Ammiel o sexto, Issachar o sétimo, e Peullethai o oitavo; pois Deus o abençoou.
Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
6 Nasceram também filhos de Semaías, seu filho, que governou a casa de seu pai; pois eram homens poderosos e de valor.
Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
7 Os filhos de Semaías: Othni, Rephael, Obed e Elzabad, cujos parentes eram homens valentes, Elihu e Semaquias.
Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
8 Todos estes eram dos filhos de Obede-Edom com seus filhos e seus irmãos, homens capazes e em força para o serviço: sessenta e dois de Obede-Edom.
Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
9 Meshelemias tinha filhos e irmãos, dezoito homens corajosos.
Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
10 Também Hosah, dos filhos de Merari, teve filhos: Shimri o chefe (pois embora não fosse o primogênito, seu pai o fez chefe),
Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
11 Hilkiah o segundo, Tebalia o terceiro, e Zacarias o quarto. Todos os filhos e irmãos de Hosa eram treze.
Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.
12 Destes foram as divisões dos porteiros, até mesmo dos chefes, tendo escritórios como seus irmãos, para ministrar na casa de Yahweh.
Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
13 Eles lançam sorte, tanto os pequenos quanto os grandes, de acordo com as casas de seus pais, para cada portão.
Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
14 O lote para o leste caiu para Shelemiah. Então, para Zacarias, seu filho, um sábio conselheiro, eles lançaram a sorte; e sua sorte saiu para o norte.
Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
15 Para Obed-Edom em direção ao sul; e para seus filhos o armazém.
Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
16 Para Shuppim e Hosah para o oeste, junto ao portão de Shallecheth, na estrada que sobe, sentinela oposta à sentinela.
Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa. Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:
17 Para o leste eram seis Levitas, para o norte quatro por dia, para o sul quatro por dia, e para o armazém dois e dois.
Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
18 For Parbar para oeste, quatro na estrada, e dois em Parbar.
Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
19 Estas eram as divisões dos porteiros; dos filhos dos coraítas, e dos filhos de Merari.
Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
20 Dos Levitas, Ahijah estava sobre os tesouros da casa de Deus e sobre os tesouros das coisas dedicadas.
Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
21 Os filhos de Ladan, os filhos dos gershonitas pertencentes a Ladan, os chefes de família dos pais pertencentes a Ladan, o gershonita: Jehieli.
Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
22 Os filhos de Jehieli: Zetham, e Joel, seu irmão, sobre os tesouros da casa de Yahweh.
wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.
23 Of os Amramitas, dos Izharitas, dos Hebronitas, dos Uzzielitas:
Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:
24 Shebuel, o filho de Gershom, o filho de Moisés, era o soberano sobre os tesouros.
Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
25 Seus irmãos: de Eliezer, Reabias seu filho, e Jesaías seu filho, e Jorão seu filho, e Zichri seu filho, e Shelomoth seu filho.
Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
26 Este Shelomoth e seus irmãos estavam sobre todos os tesouros das coisas dedicadas, que David, o rei, e os chefes de família dos pais, os capitães de milhares e centenas, e os capitães do exército, tinham dedicado.
Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
27 Eles dedicaram parte dos saques ganhos em batalhas para reparar a casa de Iavé.
Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana.
28 Tudo o que Samuel, o vidente, Saul, filho de Kish, Abner, filho de Ner, e Joab, filho de Zeruiah, tinham dedicado, quem quer que tivesse dedicado alguma coisa, estava sob a mão de Shelomoth e de seus irmãos.
Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
29 Dos Izharitas, Chenaniah e seus filhos foram nomeados para os negócios externos sobre Israel, para oficiais e juízes.
Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
30 Dos hebronitas, Hasabias e seus irmãos, mil e setecentos homens de valor, tiveram a supervisão de Israel além do Jordão para o oeste, para todos os negócios de Yahweh e para o serviço do rei.
Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme.
31 Dos hebronitas, Jerijah era o chefe dos hebronitas, de acordo com suas gerações, pelas famílias de seus pais. Eles foram procurados no quadragésimo ano do reinado de Davi, e homens poderosos de valor foram encontrados entre eles em Jazer de Gilead.
Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
32 Seus parentes, homens de valor, eram dois mil e setecentos, chefes de família dos pais, que o rei Davi nomeou supervisores sobre os rubenitas, os gaditas, e a meia tribo dos manassitas, para cada assunto relativo a Deus e para os assuntos do rei.
Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.